SORRY MADAM (67)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA SITINI NA SABA
ILIPOISHIA...
Kwa ukubwa wa gari yangu haikuwa shida sana kuzikanyaga pikipiki mbili zilizopo mbele yangu. Nikapata kiupenyo cha kuingia barabarani na cakumshukuru MUNGU, hakuna magari ya foleni ambayo yanaweza kunizuia kuendelea na safari yangu, huku nikiwaacha waendesha pikipiki wakitoa matusi mengi juu yanguNIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Kwa mbali nikaliona gari, walilokuja nalo majambazi likichanja mbuga barabara ya kuelekea mkoani
“Wale ndio majambazi walio piga tukio benki”
Nilizungumza huku nililiinyooshea kidole gari la majambazi aina ya Rangerover.
“Mmmmm”
Dorecy aliguna, huku akinitazama machoni.Nikazidi kukanyaga mafuta na kuzidi kulisogelea majambazi, ambalo nalo linakwenda kwa mwendo wa kasi sana
“Eddy kuwa makini, wasije wakatushambulia”
“Powa”
Sikuona gari yoyote ya polisi inayokuja nyuma yetu, Nikazidi kulifukuzia gari la majambazi na gafla likakunja na kuingia porini
“Eddy nyoosha tuu, tusiwafate”
“Powa”
Nikaachana na gari la majambazi na kuelekea zangu barabara inayokwenda mikoa ya Tanga na Arusha. Kwa mbali nikawaona askari usalama barabarani wakiwa wamesimama
“Eddy punguza mwendo”
“Huoni kama tutakamatwa?”
“Nitazungumza nao mimi”
“Dorecy”
“Fanya hivyo, la sivyo itakuwa ni tatizo kubwa”
“Powa”
Nikapunguza mwendo wa gari, na askari mmoja akatusimamisha, nikalisimamisha gari langu pembeni na askari huyo akaanza kuja kwa mwendo wa umakini, huku akilitazama gari langu.Nikaishika bastola yangu kwa umakini, ila Dorecy akaushika mkono wangu wa kushoto ulio shika bastola
“Tulia”
Dorecy alinizuia kufanya ambacho ninahaji kukifanya, kwa ishara askari akaniomba nifungua kioo cha gari upande nilio kaa mimi, nikatii kama alivyo hitaji mimi kufanya
“Habari yako afande”
Jamaa alianza kunisalimia, nikaachia tabasamu pana ambalo muda wowote ninaweza kulibadilisha
“Salama tuu, kaka”
“Mbona gari yako, mbele kidogo imebonyea?”
“Ahaaa kuna, mjinga alinibamiza kwenye mataa kule”
“Ahaaa, munaelekea wapi?”
“Nakwenda, Tanga mara moja kuna kazi hapo tumeagizwa na RPC”
“Kuna, gari tunaiwinda ya majambazi wamepiga tulio benki, ndio tupo tupo hapa, tunaisubiria”
“Ipoje hiyo gari?”
Polisi akaniwasha simu yake na kunionyesha picha cha gari hilo
“Nimetumiwa Whatsap hii picha”
Dorecy akaitazama picha ya gari ambalo, tulikuwa tumeongozana nalo
“Hii gari tumeongozana nayo”
Dorecy aliropoka na kunifanya nimgeukie na kumtazama kwa macho makali yaliyo jaa mshangao ndani yake
“Imengia wapi?”
Dorecy akaanza kumuelekeza askari gari sehemu ilipo ingia, askari akawajulisha wezake na sisi tukaondoka
“Dorecy umefanya nini?”
“Kwani tatizo lipo wapi?”
“Sio tatizo lipo wapi, wewe inakuwaje unawachomesha watu wa watu katika ishu zao”
“Sio ishu zao, kumbuka hata mimi ni askari”
“Hata kama”
“Sio hata kama, wewe hukuona ni watu wangapi walio uliwa nje ya benki”
“Ila sijapenda hiyo tabia sawa”
“Eddy, kumbuka hata wewe ni muhalifu”
“So”(Sasa)
Nilimjibu Dorecy kwa kifupi, huku nikiwa nimekasirika sana
“Sihitaji hicho kibesi chako”
“Unasemaje wewe?”
“Sihitaji hicho kibesi chako cha kijinga, nitakubadilikia sasa hivi, umenielewa?”
Dorecy alizungumza kwa sauti ya ukali, huku akinitazama kwa hasira.Kwa kona ya jicho la kushoto nikamtazama Dorecy na kugundua hajafunga mkanda, nikaongeza mwendo wa gari, gafla nikafunga breki za kustukisha na kumfanya Dorecy kupiga kichwa kwenye dasbord ya gari.Kwa haraka nikamuwahi kumshika shingo yake na kuiminya kwa nguvu
“Huwa sipendi, ujinga kwenye yangu maisha sawa?”
Niliminya Dorecy shingo yake kwa nguvu, huku nikimtakandamiza kwenye kwenye siti yake.Nikazichomoa bastola zake katika sehemu alipo ziweka, na kuziweka upande wangu.
“Wewe ni nani?”
Nilizumuuliza Dorecy huku nikiendela kuminya kwa nguvu kwenye siti yake aliyo kalia.Dorecy akawa na kazi ya kuushika mkono wangu ulio ishika shingo yake
“Ed...eddy ni...aachi...ee”
“Nitakuua, mwehu wewe”
Nikamuachia Dorecy, akaanza kukohoa huku akihema kwa kasi kwani kwa jinsi nilivyo mkaba ni nusu ya kuyaona mauti
“Upo na mimi, au?”
Nilimuuliza Dorecy na kumfanya aendelee kukohoa, nikabaki nikiwa nimemtazama kwa macho makali kama ya simba dume aliye uliwa mke wake, Dorecy akanitazama kidogo kisha macho yake akayakwepesha tena na macho yangu na kutazama chini huku akiendelea kukohoa.Nikaichukua bastola yangu na kumuelekezea Dorecy ya kichwa huku nikiwa nimeikandamiza kwenye nywele zake, nikamshuhudia Dorecy akitingishika mwili mzima
“Nimekuuliza, upo na mimi au?”
“Nipo na wewe”
Nikaachia msunyo mkali na kuishusha chini bastola yangu na kuwasha gari langu na kuendelea na safari.Hadi ninafika Segera ikanilazimu kusimamisha gari kwani sikujua ni wapi nielekee, kwani Arusha siwezi kwenda kutokana ninatafutwa,
“Mbona umesimamisha gari?”
“Nafikiria kwa kwenda”
Sote tukabaki kimya, kwa wakati huu sikuwa na uwe wa kwenda alipo mama, kwani sijajipanga vizuri na ukatili wa Mzee Godwin ninatambua vizuri sana, na nikienda kichwa kichwa ninaweza kufa nikiwa ninajiona
Twende Tanga”
Dorecy alizungumza
“Unapajua?”
“Ndio, kuna rafiki yangu kule atanisaidia pia kwa hili swala lako”
“Unamuamini?”
“Ndio Eddy”
“Pita basi huku, uendeshe hari kwani mimi sipajui Tanga”
“Sawa”
Dorecy akashuka kwenye gari na mimi nikahamia kwenye siti yake.Akaingia kwenye gari na safari ikaendelea, ila kwa muda wote nipo makini sana na Dorecy kwani anaweza kubasilika wakati wowote ikawa ni tatizo jengine kwangu
“Ulishawahi kufika Tanga?”
Dorecy alizungumza
“Hapana, ndio leo ninakwenda”
“Sawa”
“Kwa nini, umeniuliza hivyo?”
“Hapana, nilihitaji kujua tuu kama ulisha wahi kufika”
Nikamtazama Dorecy kwa umakini, kisha nikashusha pumzi nyingi.Safari ikaendelea huku nikimuomba Mungu, Dorecy asije kuniyumbisha hata kidogo kwenye mpango wangu wa kumuokoa mama yangu, ambaye siamini kabisa kama Mzee Godwin amemuua hadi sasa hivi.Japo ninausingizi mzoto, ulio tokana na uchovu wa hekaheka za jana hadi sasa hivi, sikuweza kabisa kuyaruhusu macho yangu kufumba kwani, litakuwa ni kosa kubwa sana kwangu na sukujua ni kitu gani ambacho Dorecy anakifikiria kichwani kwake kuhusiana na mimi.
Kila ninavyo jizuia kuyafumbua macho yangu, ikafikia kipindi nikajikuta nikishindwa kuvumilia, nikaiminya kidogo siti yangu kwa nyuma na kuiegemea vizuri na kulala, gafla nikamuona Mzee Godwin akiwa amemshika mama yangu na kumuweka juu ya meza kubwa, akaipanua miguu ya mama juu ya meza huku akisaidiana na watu wake, akaanza kumkita misumari, mirefu ya miguuni kisha, akampigilia misumari mingine kwenye viganja vya mikono yake, pembeni yupo Madam Mery na Manka wakishangilia jinsi mama anavyo fanywa
“Muue, kwani hata yeye mwanaye ameniulia mume wangu kikatili sana”
Madam Mery alizungumza huku akishangilia na kupiga makofi akifuahia sana kitendo kinacho endelea.Mama akazidi kulia kwa uchungu, huku damu nyingi zikiwa zinamiminika katika miguu ya viganja vya miguu yake
“Nimekuambia chinja kabisa huyo”
Madam Mery aliendelea kushangilia, Madam Mery akachukua mashine ya kupasulia miti mikubwa na kumkabidhi Mzee Godwin
“Weka dishi la maji chini”
Mzee Godwin alizungumza, Manka akalisogeza dishi la maji chini ya meza na kuliweka vizuri, na damu za mama zinazo toka kwenye mikono yake zikaanza kuingia ndani ya dishi.Mzee Godwin akaanza kuiwasha mashine ya kukatia miti hadi ikawaka, kwa kutumia mashine ya kukatia miti akaanza kuukata mguu wa kulia wa mama, na kuzidi kukizidisha kilio cha mama.Akaendelea kuikata miguu ya mama miguu ya mama.
Hakuishia hapo, kwa kutumia mkasi mdogo akaichana tisheti ya mama na kumuacha kifua wazi, akalishika zima moja la mama, akalinyonya kidogo kisha akachukua kisu kikali alicho kabithiwa na msaadizi wake na kukilikata zima la mama upande wa kulia jambo lilizidi kumuongezea mama uchungu, akaendelea kulia kwa maumivu anayo yapata
“G Niue tu, kuliko kunitesa hivi”
Mama alizungumza kwa sauti iliyo jaa vilio, mzee Godwin na watu wake wakaanza kucheka kwa dharau akiwemo, Manka na Madam Mery.
“Unataka kufa?”
“Bora nife, kuliko kunifanya hivi”
Mzee Godwin akalitupa ziwa la mama alilo likata ndani ya beseni, kisha kwa nguvu akakichoma kisu chake, tumboni mwa mama na kuuanza kumchana hadi utumbo wake ukatoka nje, kwa kutumia mashine ya kukatia miti akakikata kichwa cha mama na kukitenganisha na mwili wake
“Nooo”
Nilizungumza kwa nguvu, huku nikistuka na kujikuta nikiwa ndani ya gari hapa ndip nikagundua ni ndoto kwa kila kitu nilicho kuwa nimekiona juu ya mama yangu, jasho jingi likazidi kunimwagika na kulisababisha shati langu la pilisi kulowa kama nimemwagiwa maji mengi.Nikaendelea kutasikilizia mapigo ya moyo jinsi yanavyo kwenda, huku nikiwa nimetizama chini, nikageuza shingo yangu upande alio kaa Dorecy na sikumku.Nikanyua kichwa kwa haraka huku nikiwa na wasi wasi na kukuta gari ikiwa imesimama nje ya kituo cha polisi kilicho andikwa kwa maandishi makubwa
{KITUO CHA POLISI CHUMBAGENI TANGA}
Nikamuona Dorecy akitoka nje ya kituo, akiwa ameongozana na askari watatu wenye bunduki mikononi mwao, huku akinyoosha kidole sehemu ilipo gari, nikajaribu kufungua mlango ila nikashindwa na polisi nao kwa mwendo wa umakini wakazi kuisogelea gari yangu
Nikazidi kuchanganyikiwa, kwa jinsi askari wanavyo isogelea gari langu kwa umakini.Nikajipapasa mifukoni mwangu sikukiona bastola zangu jambo lililoufanya mwili wangu kupoteza nguvu zote na kubaki nikiwa ninawatizama hadi wanafika kwenye gari.Dorecy akawa wa kwanza kufungua gari na kuingia huku akishusha pumzi
“Jamani, huyu ni shemeji yenu, anaitwa Eddy, Eddy hawa ni rafiki zangu nilikuwa depo so ndio nimepitia hapa kuwaona”
Nguvu zote za mwili zikazidi kudidimia kwani nilidhani kuwa jamaa wamekuja kunikamata kwa makosa niliyo yafanya
“Kaka habari yako?”
Askari mmoja alinisalimia, hata nguvu za kumuitikia sikuwa nazo zaidi ya kukitingisha kiwachwa changu nikimaanisha kwamba nimemuitikia salamu yake
“Unaonekana umechoka mume wangu?”
Dorecy alizungumza huku akinishika kidevu changu
“Yeaah”
Nilijibu kwa upole mwingi
“Kaka, mtunze bwana dada yetu, wewe si unaona jinsi alivyo mchuma wa huakika”
Askari mmoja alizungumza huku akiachia tabasamu usoni mwake
“Musijali kwa hilo”
Niliwajibu, kidogo hali yangu ikaanza kunirejea, hata mapigo ya moyo kidogo yakabadili muelekeo wake na kurudi katika mapigo yake 72 kwa dakika
“Huyu dada yetu kipindi tupo depo, Moshi alihamishwa na kupelekwa JWTZ”
“Kaka, hivi huchezei makofi mawili matatu, kwa maana shosti alikuwa mkorofi huyo”
Sote tukajikuta tulicheka, kwa maana sikutarajia kuwa hawa jamaa muda huu nitakuwa ninacheka nao kwa furaha kiasi hiki
“Hapana jamani, ubabe nimeacha siwezi kumpiga mume wangu, mwenyeni ninampenda kama nini?”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni