SORRY MADAM (66)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA SITINI NA SITA
ILIPOISHIA...
Nilizungumza huku nikiendea kumwagikwa na machozi mengi, malengo yangu yote niliyo jiwekea kuja kuwa daktari bingwa nchini Tanzania yametoweka kabisa, hapa ndipo nikaanza kuamini kwamba pesa haitimizi malengo ya mtu, kwani tangu nimezaliwa sikuwahi kuishi maisha ya shida kwani baba anapesa na mama ndio tajiri kupindukia, ila kwa sasa ndio wamekuwa maadui sana.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Sikujua baba yangu wa damu anaendeleaje, kwani sikupata hata muda wa kukaa na mama na kumuuliza kuhusiana na baba yangu aliyepo Afrika kusini
Macho yangu, nikaendela kuyakaza kwenye kioo, nikiitazama sura yangu, iliyo jaa dhambi na ukatili ulio mkubwa.Sikupenda kuwa hivi, ila matatizo yakanibidi mimi kuwa hivi
“Mungu, nisamehe, mimi ni mwenye dhambi tena dhambi nyingi.Ila ninaomba nimuue Mzee Godwin tuu.Ili nikifa nife kwa amani”
Nilijikuta nikizungumza maneno haya ambayo sikujua ni kwanini nimeyazungumza, tena kwa sauti ya juu.Nikafungua bomba la maji ya mvua na kuasimama kwa muda chini ya maji haya yanayoendelea kutiririka mwilini mwangu.Mwili wangu umejawa na nongo nyingi sana kwani hata maji ambayo yanaingia kwenye kishimo kidogo cha hapa bafuni yanaonyesha jinsi mwili wangu ulivyo jaa uchafu.Nikaoga na kurudia kupiga mapovu manne ndipo, hali ya uchafu ikaondoka mwilini mwangu.Hata rangi halisi ya mwili wangu ikarejea.Nikamaliza na kurudi chumbani kwangu, nikiwa ninatafuta ni wapi lilipo taulo langu lipo, mlango wa chumbani kwangu ukafunguliwa na Dorecy
“Ahaaa sory Eddy...!!”
“Ahaaa bila samahani”
Nilizungumza huku mikono yangu nikiwa nimeiziba kweye sehemu zangu za siri
“Chakula tayari kule”
“Sawa, ninakuja”
Dorecy akatoka, nikavaa pensi, nikaelekea sebleni na kumkuta akiwa ananisubiria kwenye meza ya chakula
“Mbona, hukula chakula?”
“Nilikuwa ninakusubiria”
“Ohoo, ungeanza tuu”
“Hapana, itakuwa sio tabia nzuri sana kwa yule umpendaye”
“Kweli”
“Ehee, sisi kwetu hatujafundishwa hivyo”
“Sawa”
Nikakaa kwenye kiti, Dorecy akanitengea chakula changu na taratibu tukaanza kula,
“Kipindi nikiwa, Sunday school tulikuwa tunafundishwaga kusali kabla ya kula”
Nilizungumza
“Mulikuwa munafundishwaje?”
“Tulikuwa tunaomba, Ohh loard our father, bleas this food for this day, Welcome Dorecy”(.....baba yetu wa mbinguni, bariki hiki chakula cha leo, karibu Dorecy)
“Hahaaa, Eddy.Sasa mbona leo hujasali?”
“Ahaa weee acha tuu”
Tukaendelea kula huku nikitazamana mara kwa mara na Dorecy, nikanyanyuka na kuzunguka meza hadi alipo kaa Dorecy, nikasimama nyuma yake, mikono yangu nikaiweka mabegani mwake.Nikainama taratibu na kumbusu shavuni
“Dorecy”
“Mmmm”
“Ninakupenda”
Dorecy hakunijibu chochote, taratibu nikaanya kuinyonya shingo yake na kumfanya aanze kujichezesha chezesha kwa hisia.Nikamnyanyua kwenye kiti na kuanza kuinyonya midomo yake, huku nikaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine.Tukajikuta tunazama kwenye dimbwi kubwa la mapenzi huku kila mmoja akijitahidi kumpa mwenzake raha ambayo anastahili kuipata kwenye dimbwi la mapenzi.Tukatumia kama dakika thelathini na nano kuburudishana hadi tunamaliza, tukavikuta vyombo vyote vipo chini huku sisi tukiwa juu ya meza tukitoa pumzi nyingi
Nikambeba Dorecy hadi chumbani kwangu, sote tukaingia bafuni, tukaoga na kurudi chumbani na kujitupa kitandani
“Eddy, unampango gani juu ya mama”
“Nataka nikamkomboe, siamini kama amekufa?”
“Japo sipendi kujua kilicho tokea kwenye familia yako hadi kukafikia huku, ila nakuhaidi tutashirikiana kudfa na kupona”
“Nitashukuru kwa hilo”
“Kingine, itabidi unyoe nywele zako....”
“Ili”
“Uvae zile nguo za askari, la sivyo utakamatwa kirahisi”
“Etii ehee?”
“Hapo hakuna cha Etii, inabidi iwe hivyo”
“Sawa, tutafanya asubuhi”
Kutokana na kuchoka kila mmoja akajilaza na usingizi mwingi ukanipitia,Nikawa wa kwanza kuamka nikaingia bafuni na kuoga, nikamuamsha Dorecy naye akaingia bafuni na kuoga.Nikachukua mashine ya umeme ya kunyolea na kumkabidhi Dorecy, akaanza kuninyoa nywele zangu zote na kunifanya nibadilike sana.
“Dory, nataka twende bank mara moja”
“Tukafanyaje?’
“Kuna ishu nakwenda kuiuzia benki”
“Benki gani?”
“CNB”
“Sawa, ila tumia hizo nguo za polisi”
“Powa”
Nikavaa, nguo za polisi,aliye chapwa na Dorecy, zikanitosha vizuri, nikazunguka lilipo gari la polisi nilipo liacha na kuchukua kofia moja ambayo ipo ndani ya gari, nikarudi sebleni na kuvaa viatu vya kiaskari
“Kama polisi kweli vile”
“Umeona eheee”
“Eddy una picha ndogo”
“Ya nini?”
“Kuna kitambulisho nataka nifoji hapa”
Nikaingia chumbani kwangu na kutoa picha ndogo ya na kukabidhi Dorecy, akaanza kazi ya kufoji kitambulisho kimoja cha polisi.Nikachukua bastola moja na kuichomeka kwenye viatu na kuifunika na sruali, nikachukua bastola nyingine na kuichomeka kiunoni.Nikavaa jaketi la kuzuia risasi, Dorecy naye akawa amemaliza kuvaa nguo zake, Nikaingia ndani kwangu na kuchukua begi lenye madini, nikaingia chumbani kwa mama na kuchukua funguo ya gari lake aina ya VX V8 na kutoka navyo nje
“Una endesha, niendeshe”
Nilimuuliza Dorecy
“Wewe endesha, huu mji wenu mimi siuelewi kabisa”
Tukaingia ndani ya gari na kuondoka nimasisitizia mlinzi asiruhusu mtu kuingia ndani ya nyumba yetu.
“Nimemaliza kukitengeneza kitambulisho chako”
Dorecy akanikabidhi kitambulisho changu, chenye jina la Edward Kilonzo, ni jina la askari aliye tandikwa bakora na Dorecy.Tukafika benk, kabla sijashuka Dorecy akanibusu shavuni.
“Ninakupenda Eddy wangu”
“Na mimi pia”
“Kwani humo ndani ya begi kuna nini?”
“Nitakuambia nikirudi”
Nikatazama mazingira yote ya benki na kuona yapo salama, nikashuka kwenye gari huku nikiwa na kibegi na kuanza kupiga hatua za kuelekea ulipo mlango wa benki, huku amcho yangu yakiwa makini sana.Nikafika hadi kwa muhudumu pasipo askari wa mlangoni kunigundua
“Dada habari yako?”
“Salama”
“Meneja nitamuona wapi?”
“Una mawasiliano naye?’
“Hapana ila, ninaujumbe kutoka kwa bosi wangu.Kuna huu mzigo nimeagizwa nimkabidhi yeye”
“Unalijua jina la meneja?”
“Ndio, anaitwa bwana Turma”
“Basi twende, nikupeleke ofisini kwake”
“Asante”
Tukaingia kwenye lifti na kupandisha gorofa ya kwanza, nikaingia ofisini mwa Bwana Turma ambaye ni rafiki mkubwa wa mama, na mimi ananifahamu vizuri sana.Kwa bahati nzuri nikamkuta hana mtu anaye zungumza naye
“Meneja unamgeni”
“Muambie aingie”
Muhudumu akaniruhusu kuingia ndani ya ofisi, kisha yeye akaondoka, nikaivua kofia yangu na kumfanya bwana Turma kutabasamu baada ya kuniona
“Eddy, umekuwa askari?”
Aliniuliza huku akicheka
“Hapana mjomba”
“Ila?”
“Ahaa vijimambo tu,”
“Ila ninasikia unatafutwa na polisi”
“Ndio, ila mjomba ninaomba msaada wako”
“Msaada gani?”
“Kuna haya madini, yanadhamani kubwa sana.Ninaomba niwauzie nyinyi kama benki na pesa yangu muiweke humu ndani, ipo siku MUNGU akibariki, mimi au mwangu anaweza akasaidiwa na hiyo pesa”
Bwana Turma akaniangalia kwa macho ya umakini, akaniomba nimuonyeshe hayo madini.Nikamfungulia begi na kumuwekea, kibegi juu ya meza.Akabaki akishangaa
“Umeyatoa wapi?”
“Hii ni mali ya mama, ninakuomba sana uniwekee”
“Wewe ulikuwa unayauza kwa kiasi gani?”
“Bilioni moja na nusu shilingi”
“Mbona nyingi sana”
“Hata haya madini, yanadhamani kubwa sana.Nikisema niuze kwa masonara si chini ya bilioni tano”
“Sawa mjomba nimekuelewa, ngoja nikawaite wahasibu na wanasheria wa benki tuwez kufanya biashara”
“Sawa mjomba”
Bwana Turma akatoka nje ya ofisi yake na kuniacha nikiwa ndani, nikakaa zaidi ya dakika kumi na tano, sikumuona bwana Turma kutokea, nikaanza kupata wasiwasi, labda amekwenda kuwaita askari.Nikanyanyuka na kukifunga kibegi changu, nikatizama kwenye kioo cha computer yake, iliyopo juu ya meza yake, kilicho gawanyika katika vipande sita vya picha za video za kamera za ulinzi na kuona gari aina ya Rangerover ikisimama kwa kasi nje ya Benki na wakashuka wasichana watano walio valia mavazi meusi huku wakiwa na bunduki mikonini mwao.Wakanza kuwashambulia askari huku walili wakiingia ndani ya benki na kuanza kuwashambulia askari na kuwaamrisha watu wote kulala chini.Nikamuona wakimuamrisha bwana Turma kuingia kwenye chumba ambacho ndicho wanahifadhia pesa
Japo ninaroho kidogo ya kikatili, ila kwa jinsi risasi zinavyo ngurumishwa nje na majambazi hawa, sikuthubutu hata kujaribu kutoka ndani ya chumba.Bastola yangu nikaishika vizuri kwa umakini huku macho yangu yakitazama kwenye kioo cha computer iliyopo juu ya meza.Nikawashuhudia wasichana wawili wakimuamrisha bwana Turma kuingia ndani ya chumba ambacho ni chakuhifadhia pesa.Wakaendela kuingiza pesa kwenye mifuko yao, nikamuona msichana mwengine akiingia akiwa na bunduki.Sikusikia kitu anacho kizungumza.Nikaanza kusangaa baada yakuwaona watu wakivuliwa nguo na kupangwa mstari katika mlango wa kutokea nje
“Wanataka kufanya nini hawa?”
Nilijiuliza swali ambalo jibu lake nikalipata baada ya kuona watu wakitolewa nje wakiwa uchi pasipo kuwa na nguo hata moja kwenye miili yao.Wasichana wakajichanganya kwenye kundi kubwa la watu wanaotoka wakiwa, wanakimbia.Nikaitumia nafasi hiyo na mimi kutoka ndani ya chumba huku kibeki changu nikiwa nimekifunga vizuri na kukishika kwenye mkono wangu wa kushoto huku mkono wangu wa kulia nikiwa nimeishika bastola yangu.Nikajichanganya kwenye watu na kukimbilia lilipo gari letu,Nikamkuta Dorecy akiwa amejiinamia kwenye gari, nikafungua mlango wa gari na kuingia ndani
“Eddy vipi huko?”
“Tuondoke, sikwema huku”
Nikawasha gari na kuliingiza barabarani kwa kasi ya hali ya juu,
“Eddy tunaelekea wapi?”
Dorecy aliniuliza huku akinitazama kwa macho makali, sikulijibu swali lake zaidi ya kuongeza mwendo kasi wa gari langu.Nikafika maeneo ya mataa na kukuta msongamano wa magari mengi yakiwa katika foleni
“Shiitii”
Nilizungumza huku nikiitizama gari ndogo ya polisi inayokuja nyuma yangu kwa kasi, wakionekana kunifwatilia mimi.Kutokana nyuma yangu hakuna gari, nikairudisha nyuma gari yangu, na kuingia barabara ya pili inayopitwa na watembea kwa miguu, Kazi yangu ikawa ni kupiga honi, huku nikiwa makini katika uendeshaji wangu.Watu wengi wakawa na kazi ya kulikwepa gari langu huku wengine wakijirusha kwenye mitaro kuepuka kifo
“Eddy angalia mbelee”
Dorecy alizungumza kwa sauti kubwa, kwani kuku gari la abiria linakuja mbele yetu kwa mwendo wa kasi, Kwa haraka sana nikakunja kushoto na kuzibaniza pikipiki za waendesha bodaboda zililozo pangwa barabarani wakisubiria wateja, kwa kupitia kioo cha pembeni, nikalishuhudia gari la abiria lilipoteza muelekeo na kuyakuma magari mengine na kusababisha ajali mbaya. Kwa ukubwa wa gari yangu haikuwa shida sana kuzikanyaga pikipiki mbili zilizopo mbele yangu.Nikapata kiupenyo cha kuingia barabarani na cakumshukuru MUNGU, hakuna magari ya foleni ambayo yanaweza kunizuia kuendelea na safari yangu, huku nikiwaacha waendesha pikipiki wakitoa matusi mengi juu yangu
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni