SEHEMU YA THEMANINI
ILIPOISHIA...
“mke wangu saa hizi, saa kumi na mbili na nusu, nitalala nini?”
Phidaya akajifunika kwashuka gubigubi, kwa jinsi ujauzito wa mke wangu ulipo fikia, unampelekesha kama mtoto mdogo kwani kila analo lifanya nikituko kwangu.
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Asubuhi namapema nikakutana na john kwenye mgahawa uliopo chini ya hoteli hii, akaanza kuniadisia kila kitu amcho kilitokea kwapindi kizima nilipokuwa sipo nchini tanzania
“mama, yupo salama kabisa na nijuzi kati tu, hapa nilikuwa naye kwenye ndege yetu inayo elekea tanzania, alikuja huku kwa mambo yake binafsi”
“ehee ilikuwaje?”
“siku ambayo ilikuwa ni graduation(mahafali) yakumaliza kidato cha sita ndipo, siku ambayo nilikutana na mama wakati wausiku.Ile siku nakumbuka ilikuwa nijumamosi, wakati wausiku nilikuwa na demu mmoja sidhani kama utakuwa unamfahamu”
“alikuwa ni mwanafunzi?”
“ndio, anaitwa catherina?”
“simkumbuki”
“nahisi alihamia kipindi wewe, umeshaondoka, kama unavyojua mwanangu maisha ya shule, tuliamua usiku kwenda sehemu yakujificha kule msituni, ambapo tulianza, kufanya yetu kwenye kichaka”
“mmmm, hukuwa na pesa ya chumba nini?”
“ahaaa hoteli zote zilijaa wageni, waliokuja kwenye sherehe, kipindi tunafanya yetu, kwa mbali tulianza kusikia vishindo vya watu wakitembea kwenye eneo tulilopo, ikatulazimu kukatisha mautamu yetu, nakujikuta tukijificha kwenye kichaka chetu”
“tuliwashuhudia watu hao wakiitupa miili ya watu wawili, huku wote wakibishana nakudai kwamba watu hao tayari wameshafariki, walipo watupa, wakaondoka zao na kutuacha sisi, tukiwa tunatetemeka”
“sasa mulikuwa munatetemeka nini?”
“weee, eddy wewe unazungumza tuu, kukutana na watu kama wale si kitu kidogo, mbona catherina alijikojolea kwa woga”
“dooooo” nilijikuta nikicheka
“sijui hata ujasiri niliupatia wapi, nikajikuta nikipiga hatua za kwenda kutazama sehemu walipo tupwa watu wale, japo catherina alikuwa na wasiwasi, kufika ile sehemu, nikastukia kuona mmoja wao akistuka na kutoa ukelee, kumcheki vizuri wapili naye nikagundua kwamba yupo hai, ambaye ni mama yako, ila miili yao ilikuwa imedhohofika sana, tena sana, ilinilazimu kwenda kumuomba, lucas gari lao”
“lucas nani?”
“lucas martin, tuye jamaa wa hkl aliyekuwa anajisikia sana”
“ahaaa nimemkumbuka”
“alikuwa anatembeala na gari ya baba yake, aliyokuja nayo kwenye mahafali, basi tuliwapeleka kwa bibi yangu aliyepo pale pela arusha yeye ni nesi, ila nilifanya nisiri sana watu wasijue kutokana mazingira tuliyo wapata, yalikuwa nihatarishi sana.Bibi yangu alianza kuwafanyia matibabu hadi afya zao zikawa salama”
“huyo mtu wapili alikuwa ni nani?”
“ni sheila, ambaye kwa sasa, anaishi kwa mama”
“ahaa sasa ilikuwaje kwa mzee godwin”
“sasa hapo ndipo nilipopata kujua kwamba, mchongo wote wakutekwa kwa mama yako, aliyesababisha kutekwa kwake ni mzee godwin ambaye kwa sasa, ananyea debe gerezani”
Habari aliyo nipa john, ikajenga furaha iliyojawa nashauku yakutaka kutaka kumuona mama yangu,
“kwenye ndege umesha ajiriwa au bado?”
“ndio ninamalizia mafunzo,”
“kwa nini umekuwa muuhudumu wa ndege wakati, mipango yetu ilikuwa ni kuwa madaktari bingwa?”
“kaka, pcb mbaya mwanangu, nilizungusha”
“ulizungusha…..!!?”
“ndio ndugu yangu, nilipata zero, ila sijutii sana kwani muda mwingi niliutumia sana na catherina”
“na huyo catherina alipata ngapi?”
“ahaaa naye pia alizungusha, japo alikuwa hkl, ila alizungusha”
“poleni sana”
“asate, eheee na wewe umemtolea wapi huyu bibie muarabu si muarabu, mzungu si mzungu?”
Nikaanza, kumuadisia john mkasa mzima wa maisha niliyo pitia kuanzia siku nilipokuwa nikitafutwa tanzania na kukimbilia nchini kenya ambapo ndipo, safari yangu yakwenda nchini iraq ilipo anza, nikamuelezea jinsi nilivyokutana na phidaya, na alivyokuwa msaada mkubwa sana kwenye masha yangu
“ninampenda sana phidaya”
“unauhakika?”
“ndio, asilimia mia”
“mmmmm ni yule eddy ninaye mjua mimi, au kwa maana wewe ulikuwa mzee wa gologolo”
“hahaaaa, nimkekuwa mtu wangu, hapa nipo kwenye majukumu yakuitwa baba”
“safi ndugu yangu, ila nakutobolea siri moja?”
“siri gani?”
“sheila anakupenda sana, na hapa yupo anakusubiria wewe”
“mmmmm,”
Nilijikuta nikiguna, huku mapigo yamoyo yakianza kunienda mbio, mwili mzima ukaanza kusisimka, na nywele kichwani zikaanza, kunisisimka, jambo ambalo kwenye maisha yangu halikuwahi kutokea siku hata moja.Nikasimama haraka huku akilini mwangu nikmfikiria phidaya
“eddy unakwenda wapi?”
“chumbani”
Nilizungumza huku nikizidi kupiga hatua za haraka, nikaingia kwenye lifti pamoja na john, ambaye alikuwa akinifwata kwa nyuma, ikasimama kwenye ghorofa ya tatu, kama jinsi nilivyo minya batani ya ghorofa hii ambayo niyatatu, nikaanza kukimbia kuelekea chumbani kwangu, nilipo muacha mke wangu akiwa amelala, wasiwasi mwingi ukiwa umenitawala, nikafika kwenye mlango wachumba changu, nikaufungua kwa nguvu, kitu cha kwanza kutazama nikitandani, nikastuka kukuta mke wangu hayupo huku shuka jeupe lililo tandikwa juu yakitanda likiwa limejaa damu nyingi, jambo lilizozidi kustua mimi na john
Nikakimbilia kwenye mlango wa kuingilia bafuni, ila sikufanikiwa kumuona phidaya, joto kali la mwili likaanza kuambatana na woga ambao tangu kuzaliwa kwangu sikuwahi kuupata siku hata moja, nikatizama kila shemu ya chumba hadi chini ya uvungu ila sikumuona mke wangu, machozi kwa mbali yakaanza kunilenga lenga, huku nikijaribu kutafakari ni nini nifanye
“kwani alikuwa humu ndani?”
Nilijikuta nikiachia msunyo mkali, baada ya john kuniuliza swali ambalo jibu analo kichwani mwake, kwani muda nilipokuwa ninatoka nilikuwa nipo mwenyewe, na sote tumekuta damu juu yakitanda iweje aniulize kwamba alikuwepo humu ndani, nikatoka kwa hatua za haraka, huku shati nililo livaa likiwa linavuja jasho jingi, sana
“sasa eddy unakwenda wapi?”
John aliniuliza huku akinifwatwa kwanyuma tukielekea zilipo lifti za ghorofa hili, sikumjibu john chochote kwa maana ninahisi, hatambui nini umuhimu wa mke, isitoshe mke mwenye kiumbe change tumboni, kupotea katika mazingira yakutatanisha, tukaingia kwenye lifti ambayo kuta zake nne zina vioo, nikawa na kazi yakujitazama jinsi macho yangu yanavyo tiririsha machozi yanayotoka pasipo kuwa na kilio, huku wekundu ukiwa umetawala kwenye macho yangu, john akanipa kitambaa chake ili nikisaidie kufuta machozi
“nimepata wazo, hembu twende kwenye chumba cha ulinzi kwa maana humu ndani kuna kamera za ulinzi kila kona”
John alizungumza huku akinitazama usoni, wazo lake kidogo likarudisha ufahamu kwani kitu ninacho kifikiria ni phidaya na kiumbe change, kitarajiwa
“samahani dada”
John alizungumza na muhudumu mmoja kwa kingereza, mara baada ya sisi kutoka kwenye lifti iliyo tufikisha chini kabisa katika eneo tulilokuwepo
“bila samahni?”
“ninaomba kuuliza ni wapi kwenye chumba cha cctv camera”
“kwani kuna tatizo?”
“ndio lipo, kuna dada mmoja, ni mjamzito amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha, mume wake alimuacha chumbani akiwa amelala ila tulipo kwenye hatujamkuta”
“mmmm kuseme ukweli, mimi sijaona dada mjamzito akitoka, labda chakuwasaidia nyinyi, nikuwapeleka kwa meneja na yeye ndio atatoa idhini ya nyinyi kupelekwa kwenye hicho chumba”
“asante dada”
Sikuchangia neon lolote zaidi yakuwasikiliza john na muhudumu jinsi wanavyo zungumza, huku macho yangu yakitazama kila upande wa sehemu tulipo simama, nikastukia nikuvutwa mkono na john ambao tayari walishaanza kuondoka na kuniacha mimi nikiwa nimesimama kama sanamu, lakuongozwa na betrii
“kaka, usijali shemeji atapatikana, ninaimani hawezi kuondoka humu ndani ya hoteli kwa hali ile”
John aliendelea kuzungumza huku tukipiga hatua tukimwafwata dada, huyu kwanyuma, tukaingia kwenye moja ya chumba ambapo macho yangu hayakuwa ngeni kwa mtu aliye kaa kwenye kiti hichi huku akionekana kwamba ndio meneja wa hii hoteli
“meneja kuna, hawa wageni wa…..”
Meneja wake akainua mkono, kwa ishara ya kumkatisha mfanyakazi wake, na meneja wake akapiga hatua za haraka hadi sehemu nilipo simama mimi, huku akiwa ametabasamu usoni mwake, akanikumbatia kwa furaha, hapa ndipo nikapata uhakika kwamba ni mlinzi wa baba, ambaye kuna kipindi alinipeleka kwenye benki, nikatoe pesa kwa ajili ya kununulia siku ila ndipo nilipokutana na sheila baada ya jamaa kumkuta akiminyana na sheila aliyekuwa amechanganyikiwa
“eddy umekuwa mkubwa mdogo wangu”
Jamaa alizungumza huku akitabasamu, na mimi nikajikaza niweke tabasamu lakinafki ili mradi tu nisalimieane naye
“eddy mbona kama umepoteza furaha usoni mwako, unatatizo gani?”
Nikamuelezea jamaa jambo linalonisumbua,bila kupoteza muda akaniomba tuelekea chumba maalumu chenye video nyingi zinazoonyesha maeneo mbalimbali ya hotel, tukaanza kuonyeshwa matukio yaliyo pita muda mchache kwenye eneo la chumba chetu kilipo, tukashuhudia kumuaona mwanake aliye valia baibui lililo mficha sura yake akiingia ndani ya chumba change, muda mchache baada ya mimi kutoka, ndani ya dakika kadhaa akatoka akiwa amembeba mke wangu, kwenye mikono yake huku akiwa amemfunika kwa shuka jeupe, kama mtu aliye uwawa.
“peleka mbele kidogo”
Jamaa alizungumza na kumfanya muongozaji wa video hizi kupeleka picha za video mbele kidogo, ambapo tukamshuhudia mwanamke huyo ambaya hadi sasa, hivi sura yake hatukuiona, akimuingiza mke wangu kwenye gari yawagonjwa na kuondoka naye, pasipo watu kumshuhudia
“ujinga huu, ulipo kuwa unafanyika mulikuwa wapi?”
Jamaa alizungumza huku akimfokea mfanyakazi wake anaye ongoza mitambo ya kamera za ulinzia, mwili mzima ukaanza kunitetemeka na kujikuta nikizidi kuchanganyikiwa pasipo kujua ni kitu gani ambacho, nilimemkosea huyu mwanamke aliye mteka mke wangu, kila mmoja akabaki kimya akimtazama mwenzake asijue nini chakufanya
“sasa hapa itakuwaje?”
John alizungumza na kumfanya jamaa, ambaye hadi sasa hivi jina lake silifahamu kutokana sikuwa na mazoea naye sana kipindi yupo nyumbani kwa baba, akatoa simu yake na kuminya baadhi ya namba na kuiweka simu yake sikioni, akaanza kuzungumza lugha ya kizulu, ambayo kwangu si ngeni sana japo siifahamu.Akamaliza kuzungumza na simu na kututazama
“nimewasiliana na makao makuu ya polisi hapa ‘johannesburg’ na wameniambia wanaanza kulifanyia kazi muda huu”
“sa..Sa umesema wanafanyia kazi?”
Nilizungumza kwa kiwewe kikubwa huku nikimtazama jamaa
“ndio wameshaanza kulifanyia kazi, kwani nimewatajia hadi namba za gari kuhakikisha wanalinasa gari husika”
Jasho halikuacha kunitiririka japo kuwa ndani ya chumba hichi kuna baridi nzuri yajutosha, jamaa akamuomba mtu wake azitume picha za gari na mwanamke hukyo makao makuu ya polisi kupitia mtandao(internet), ili kuzidi kuwarahisishia kazi askari polisi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com