SORRY MADAM (85)

0
SEHEMU YA THEMANINI NA TANO
ILIPOISHIA...
Sauti ya victoria ilisikika, alizungumza kwa dhara kubwa sana.Sikutaka kumjibu chochote, nikaikata simu, na kuingia kwenye mtandano wa goole, nika ‘download’, apps inayoitwa google map pamoja na ‘mobile location tracker’, inayo saidia kujua ni wapi namba ya simu iliyo pigwa inapatikana.

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Nikaiingiza namba ya simu iliyo nipigia, kitendo cha dakika moja nikafanikiwa kuletewa alama inayo onyesha ni wapi namba hiyo ya simu ipo na kuna umbali gani kutoka hadi sehemu nilipo.Nikatoka nje ya kupanda pikipiki yangu, na kuondoka kwa kasi, huku nikifwata jinsi simu inavyo nielekeza sehemu ninapoweza kuwapata john na victoria

Ndani ya nusu saa nikawa nimefika kwenye moja ya mtaa, wenye watu wengi wanao onekana ni wavuta bangi, na sehemu niliyo simama pembeni kuna kundi la vijana walio choka choka na maisha, huku mmoja akiwa aimeishika simu ambayo alitumia john kunipigia, nikashuka kwenye pikipiki kwa kujiamini sana hadi sehemu walipo simama.

Nikawasalimia ila hapakuwa na aliye ijibu salamu yangu, nikagusa bega aliye ishika simu akageuka, huku sura yake akiwa aimeikunja, akavuta fumba kubwa la msokoto wake wa bangi, kisha taratibu akaupulizia usoni mwangu, kitendo chake kikanipandisha hasira dhidi yake, nikampiga kidoti na sehemu za siri na kumfanya atoe ukelele, wezake wakataka kuingialia huku wakichomoa visu vyao, nikatoa bastola, nikawaelekezea moja baada ya mwengine akaanza kuondoka kwa kukimbia, akijaribu kuyaokoa maisha yake, nikabaki na mwenye simu
“nani kakupatia hii simu?”
“ehhheee?”

Nikamzaba kofi la shavu, hadi nikahisi na mimi maumivu makali kwenye kiganja change, kutokana nakutumia nguvu nyingi, jamba lililo sababisha vidole vyangu kujitokeza kwenye shavu la jamaa huyu

“ni dada mmoja hiviii”
Jamaa alizungumza huku akilia, kama mtoto mdogo
“huyo dada yupo wapi?”
“sijui mimi”

Nikaikoki bastola yangu, na kuisokomeza mdomomi mwake, macho yangu yaliyo jaa asira yakazidi kumtazama jamaa huyu, ambaye mwanzoni alijihisi ni mbabe sana

“na..Ongea….”
Nikaichomoa bastola yangu mdomoni, ili kumpa nafasi ya kuzungumza

“alimpa mtoto mmoja hivi, nikampokonya na kuichukua mimi”
Jamaa aliendelea kuzungumza huku akimwagikwa na machozi mengi
“unanidanganya….?”
“kweli, ila nawafahamu wale”
“wanapatikana wapi?”
“kuna godauni moja lipo hapo mbele, ndipo zilipo biashara zao”
“twende unipeleke”

Nikaiacha pikipiki, tukaanza kutembea kwa miguu kuelekea lilipo godauni analo lizungumzia jamaa, hapakuwa mbali sana, tukafika kwenye moja ya jengo kubwa lenye  geti kubwa

“simama na ugonge”

Jamaa akasimama na kuaza kugonga, mimi nikasimam pembeni kodogo, huku nikiwa nimejificha.Geti likaanza kufunguliwa kwenda juu, akachungulia mlinzi mmoja mwenye bunduki mkononi mwake, sikutaka kuuliza zaidi ya kufyatua risasi iliyo tua kichwani mwa mlizi huyo, jamaa niliye kuja naye akaanguka chini kwa presha, nikaingia ndani ya godauni hili, lenye maboksi mengi, walinzi waliopo humu ndani wakanza kunishambulia kwa risasi, zilizo nikosa kutokana na kujificha kwenye nguzo moja,

“stop fireee”

Niliisikia sauti ya victoria ikiwaamrisha watu wake kuacha kupiga risasi, nikashusha pumzi nyingi huku nikilishuhudia geti likishushwa chini na kufungwa

“eddy natambua kwamba ni wewe, hapo ulipo ninahesabu hadi tatu ninaomba ujitokeze”

Victoria alizungumza kwa sauti ya juu, niliyo isikia vizuri masikioni mwangu

“mojaaaaaaa,”

Nikashusha pumzi nyingi, huku nikichungulia kuona sehemu alipo, sikuamini macho yangu baada ya kumuona john akiwa amemshika phidaya, anaye lia, huku akiwa amemuwekea bastola ya kichwa

“mbiliiiiiiiiiii”
Nikamtazama mke wangu aliye pauka sana uso wake, nikamtazama tumboni mwake na kukuta tumbo lake lipo vilevile, ikiashiria bado ni mjamzito

“ta……….”

Nikajitokeza kwenye nguzo niliyo jificha, walinzi kama hamsini, bunduki zao zote zikawa zimeelekea kwangu, nikaanza kutembea kuelekea katika sehemu walipo simama john, phidaya na victori, huku bastola yangu ikiwa mkononi mwangu

“eddy mume wangu”

Phidaya akataka kunifwata, ila john akamshika nywele zake na kumvuta kwa nyuma, hadi akatoa ukelele akijaribu kuzishika nywele zake, john akaachia tabasamu pana usoni mwake, taratibu akianza kulishika tumbo la mke wangu.

“eddy, umepata mke nzuri sana”

Victoria alizungumza kwa sauti ya dharau, john akamkumbatia phidaya kwa nyuma, kitendo kilicho anza kunikasirisha, mikono ya john ikashuka taratibu hadi kwenye sehemu za siri za phidaya, akaanza kumlazimisha kulifunua dera(gauni) lake, ili aizishike sehemu za siri za phidaya, sikuvumilia kitendo cha john kumfanyia mke wangu unyama kama huo, nikaminya traiga ya bastola yangu, kwa bahati mbaya nikakuta bastola imeisha risasi, nikastukia nikipiga goti moja chini, huku damu zikianza kuvuja kwenye paja la mguu wangu wa kulia ulio pigwa risasi na john, aliye onekana kukasirishwa na kitendo change cha kujaribu kumuua

“baby usimuue sasa hivi, bado hukumu yake”

Victoria alizungumza huku akimtazama john aliye fura kwa hasira  nyingi, akitaka animalizie kunipiga risasi nyingine.Geti likafunguliwa, yakaingia magari manne aina ya bmw, zinazo fanana rangi, ambayo ni nyeusi yakasimama nyuma yangu, wakashuka wanaume nane walio valia suti nyeusi pamoja na miwani, maumivu ya mguu yakazidi kuniandama, huku kilio cha mke wangu, kikizidi kuniumiza.

Akashuka mwanamke mmoja aliye valia suti yeusi, pamoja na kofia kubwa nyeusi, huku macho yake akiwa ameyafunika na miwani yeusi, nywele zake ndefu, zikiwa zimeufunika uso wake, akanipita na kusimama sehemu alipo simama victoria, wakakumbatiana kwa furaha, kisha akaelekea sehemu alipo simama john, akamkumbatia huku wakizungumza chini chini.
Akageuka nyuma na kunitazama mimi, taratibu akavua miwani yake, akafwatia kofia lake kubwa, taratibu nywele zake akazisogeza pembeni, nikabaki nikistuka baada ya macho yangu kutazamana na macho ya madam mery.Mwalimu aliyekuwa mpenzi wangu kipindi ninasoma

”mambo eddy”

Alinisalimia huku akitabasamu, akpiga hatua za taratibu na kusimama mbele yangu, taratibu akachuchumaa, kidole chake kimoja akakiweka chini ya kidevu changu, kisha akazilete lipsi zangu karibu, akihitaji kunibusu, nikausogeza mdomo wangu pembeni, ila akanishika kwa nguvu na kuninyonya midomo yangu kwa kutumia nguvu, jambo lilizidi kumliza phidaya mke wangu, madam mery akaniachia na kusimama

“mmmmmm ladha yako ya mate, imezidi kuwa tamu, baby wangu.Au huyu mwanamke wako wa kiarabu ameiongezea?”

Alizungumza kwa dharau, akamfwata phidaya, nikastukia kumuona phidaya akimzaba kofi la shavu madam mery, huku akisindikiza kofi hilo kwa mate yaliyo tua usoni mwa madama mery, aliye anza kuchecheka kwa dharau.Madam mery akampiga ngwala phidaya, na kumfanya aangukie mgongo, na kutoa ukelele mkali wa maumivu, mguu mmoja wa madam mery ukatua kifuani kwa phidaya, madam mery akanyoosha mkono, wake wa kulia akiomba kitu.Mlinzi wake mmoja akampa bastola, iliyo tengenezwa kwa dhahabu tupu.Akaikoki tayari kwa kumfyatulia mke wangu risasi

“mery tafadhali ninakuomba usimuue mke wangu”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika kwa uchungu mwingi, phidaya akawa na kazi ya kulia huku akimuomba mungu wake, amlaze mahali pema peponi

“please sorry madam, don’t kill my wife…..Kama mtu wa kumuua ni mimi na si yeye”(tafadali bibie, ninakuomba usimuue mke wangu………)

Niliendelea kuzungumza huku machozi yakinimwagika kwa wingi usoni mwangu, madam mery akanitazama kwa macho makili kisha akmachia phidaya, na kurudi nilipo simama mimi.

“eddy, mimi ni mwanamke katili sana, ulikuwa hujui ni jinsi gani ninavyo mpenda derick, ulimuua kinyama sana.Ulimkatakata kama kuku, na kumbanika.Wewe ni binadamu wa aina gani eheee? Unajua ni uchungu gani nilio upata juu ya kifo cha mume wangu wa ndoa derick”

Madam mery alizungumza kwa uchungu mwingi, huku aknitazama kwa macho makali sana, akanipiga teke la kifua, lililo niangusha chini, kwakutumia kitu chake chenye ncha kali ya kisigino, akanikanyaga kwenye jeraha langu na kuzidi kunipa maumivu pamoja na uchungu.Madam mery akamngong’oneza victoria, ambaye naye alimuuta mtu wake mmoja aliye ondoka katika eneo hili.

“eddy nilikupenda ila siwezi kukuacha mzima hata kidogo”

Madam mery aliendelea kuzungumza huku mara kadha akiniminya kwenye jeraha langu la risasi, meza kubwa ikaletwa na watu wa vitoria, wakaninyanyua na kuniweka juu ya meza hiyo, wakanifunga kamba kwene kila mkono na ziichanua, huku watu wawili wakiwa wanazivuta kamba hizo, kila mmoja upande wake.Wengine wawili wakaifunga miguu yangu na kila mmoja akaivuta upande wake.

Jamaa mmojaa akamkabidhi madama mery upanga wenye kumeremeta kwa rangi yake, madama mery akapiga hatua hadi kwenye meza niliyo lazwa mimi, akanitazama kwa macho ya dharau

“nafanya hii, kwa ajili yakulipiza kisasi cha mume wangu”

“ngoja kwanza, nipo tayari kufa, ila ninakuomba usimuue mke wangu”

Nilizungumza kwa ujasiri, nikiwa nipo tayari kwa kufa, madam mery akalinyanyua panga lake juu, akalishusha kwa kasi kwenye mkono wangu wa kulia

Nikatoa ukulele mkali, ulio mfanya madam Mery kusitisha zoezi lake kuukata mkono wangu, panga lake likiwa limesimama sentimita chache kutoka ulipo mkono wangu
“Madam, ninakuomba unisamee”
Nilizungumza huku machozi yakiendelea kunimwagika usoni mwangu, madam Mery akanitazama kwa macho ya hasira yaliyo jaa ukatili mkubwa, akawatazama Victoria na John ambao macho yao yote yalikuwa kwetu

“Natambua kwamba mimi nimkosaji sana kwako, ninastahili kufa mbele yako, ila si mbele ya macho ya mke wangu.Mtazame jinsi alivyo katika hali yake.Mule ndani amebeba kiumbe kama ulicho kuwa umekibeba wewe, miezi tisa, na Derick akakiangamiza mbele yetu.Yule ni mwanamke mwenzako ambaye anauchungu kama wewe”
Nilizungumza huku machozi yakiendelea kunimwagilka usoni mwangu, madam Mery kwa mbali machozi yakaanza kumlenga lenga, macho yake yamebadilika rangi na kuwa mekundu kiasi huku sura yake ikiwa imejaa mikunjo kwenye paji lake la uso akinitazama kwa uchungu sana

“Mery mimi pia ni binadamu, kumbuka ni mambo mangapi tuliyafanya tukiwa pamoja, vuta kumbukumbu ni vitu vingapi tulishiriki tukiwa pamoja, Eheeee, leo hii unataka kuimwaga damu yangu, leo hii unataka kunisulubu kikatili, le……..”
“Eddy STOP TALKING”(Eddy nyamazakuzungumza)

Madam Merry alizungumza kwa sauti ya juu, yenye uchungu ndani yake.Akalitupa chini panga lake alilokuwa amelishika.Machozi mengi yakaanza kumbubujika usoni mwake, John na Vivtoria wakabaki wakimtazama madam Mery, ambaye taratibu alianza kupiga hatua za kuelekea kwenye gari lake alilo kuja nalo


USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)