KIBWE NA SAFARI YA AJABU (5)

0
Mtunzi: Sango Kipozi

SEHEMU YA TANO
ILIPOISHIA...
Pamoja na ng’ombe huyo Nyalile alichukua kama gunia mbili za mchele na kuutosa kwenye lile jungu lililokuwa likichemka kwa mchemko wa kelele kubwa za ngurumo pale msituni! Shughuli iliendelea na muda wote lile zimwi lilikuwa likichochea mapande ya miti mikubwa mafigani, kukoleza moto wake ili chakula kichemke vizuri.

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

ENDELEA...
Kitendo kile kilisababisha moto mkubwa sana kuwaka , ulioambatana na moshi mnene, ikawa kama msitu wote ulikuwa unawaka moto!

Pale alipokuwa Kibwe, ukilinganisha ukubwa wa miti iliyomzunguka, alionekana kama kidege kidogo mno. Aliwaza na kukumbuka maneno ya Bunga, kwamba akitaka kuvuka mpaka kuelekea kaskazini ya mbali bila kukamatwa na Nyalile, lazima amliwaze kwa wimbo mzuri utakaomburudisha na kumfurahisha, kwani atakapofanya hivyo lile zimwi litadhani kuwa ni kidege kinachoimba! Vilevile, Bunga alimwambia kuwa lile jicho moja la Nyalile halioni vizuri. Habari yote hiyo ilimpa moyo Kibwe, akahisi kuwa angeweza kufanikiwa kulikwepa zimwi lile, kama akijitahidi kufanya vile alivyaelekezwa na Bunga. Lakini imani yake ilipungua wakati lile zimwi lilipomaliza kupika na kisha kuketi chini ya mti mkubwa, na kuanza kufuta jasho lililotiririka kama mfereji wa maji! Maajabu yale yalimfanya Kibwe aduwae kabisa na hofu yake kuongezeka upya! Hakujua afanye nini! Je, akimbie? Akimbilie wapi na njia ni ile moja tu! au arudi alikotoka walikokuwa wale mazimwi wala ufuta? Aliona kuwa hapana budi afanye alivyoambiwa na Bunga, kwani hakuona njia nyingine!

Hivyo, kwa sauti iliyojaa mawimbi kwa wingi wa hofu, Kibwe alianza kuimba wimbo, kwa maneno yaliyomjia katika mawazo yake wakati ule…..!

Nyaalileee! Nyaalileee, Nyaali… Nyaalileee, Nyaali…… Nyaalileeee! X2

Babu zimwi nipe motooo,

Nyaali Nyaalileee,

Niikapikie waanaanguuu,

Nyaalii Nyalileee,

Niipate viijunguuu namiii,

Nyaali nyaalileee,

Chaa wali naa cha mchuuzi ii,

Nyaali Nyaalileee!

Nyaaliileee! Nyaaliileee! Nyaalii Nyaaliileee! Nyaalii Nyaalileee!

Kibwe alipomaliza wimbo wake ule, alimchungulia zimwi Nyalile, ili atambue hisia zake baada ya kusikia ule wimbo. Alimuona Nyalile akiinua kichwa na kuangalia juu ya lile bonde kwenye miti mingi mirefu alikokuwa yeye Kibwe! Lo! Kijana yule alianza kutetemeka na jasho likazidi kutoka! Ni dhahiri Nyalile hakuona kitu chochote huko, kwanza kwa kuwa Kibwe alikuwa ni mdogo sana na miti iliyomficha ilikuwa ni mikubwa, na pili, jicho moja la Nyalile halikuwa likiona vema! Kibwe akapata faraja kidogo, alipomuona nyalile kiogo kidogo akianza kutabasamu, na hatimae kutoa kicheko cha aina yake na halafu akisema;

“Weee kidege weee! Uko wapi? Wimbo wako ni mzuri sana. Hebu imba tena nisikiye!” Kibwe alizidi kujibanza mitini, akihisi wakati wowote ule, Nyalile angeweza kumuona! Pamoja na hofu yake, Kibwe alijitahidi kurudia kuimba ule wimbo wa Nyalile, ili kumfurahisha. Na halafu lo! Kwa jinsi zimwi alivyofurahia wimbo ule, alikariri maneno katika kiitikio, “Chaa walii naa cha mchuziii, Nyaalii nyaaliileee………!” Na kisha weee! Zimwi Nyalile liliinuka na kujikung’uta, huku likizidi kutabasamu kusikia jina lake likitajwa, na pia likifurahia uzuri wa kiitikio cha wimbo ule. Basi ikawa tena ni:

“Chaa wali na cha mchuchiiii, Nyaalii Nyaaliileee! Chaa walii na cha mchuuchiii, Nyaliii nyaaliileee…….!”

Alipokua akirudia rudia kiitikio hicho, zimwi Nyalile alikuwa akicheza hatua mojamoja, akifuatisha wimbo ule, na kuitikia vile alivyoelewa yeye! Alivyonogewa zaidi, akawa anapiga hatua za haraka haraka na kuendelea na kiitikio chake; na hatimae likatimka mbio huku likiitikia;

“Chaa wali na cha mchuchiiii, Nyaalii Nyaaliileee! Chaa walii na cha mchuuchuuchii, Nyaliii nyaaliileee a!

Moja kwa moja zimwi Nyalile likayoyoma na wimbo wake huku likitimua vumbi na kuangusha miti kwa kuikumba lilipopiga mbio, huku likiimba. Hiloooo! Likayoyoma, msitu na nyika mguu nipe, hadi likafika mbali mno, bila kujielewa, likielekea kusini mwa dunia! Kibwe naye, haraka alishuka bondeni na bila kupoteza muda…… akaanza kupiga mbio bila kusimama, hadi alipovuka ule mpaka uliotofautisha eneo la kule kunako kuchwa jua, ambako ni magharibi ya dunia, na kaskazini ya mbali ya dunia. Kibwe alikuwa akielekea kwa mzee wa busara aliyeelekezwa na Bunga, ili kupata maelekezo kuhusu maendeleo ya safari yake ya ajabu.

MZEE WA BUSARA.

Safari yake ikamfikisha mahali kati ya milima miwili mirefu, kwenye mazingira mazuri sana, yenye mianguko na maporomoko ya maji, mahali palipojaaliwa ardhi iliyorutubika mno. Kule, Kibwe alikuta miti ya matunda ya makomamanga iliyostawi vizuri sana. Aliona ndege wakirukaruka na kuimba kwa furaha juu ya miti hiyo, ambayo chini yake vilipita vijito venye maji safi na ya baridi, vikitokea juu ya milima. Kibwe alifarijika mno na hali ile, hususan baada ya kuona maeneo mengi yaliyoathirika na ukame, na pia yaliyokabiliwa na uwazi uliotokana na mashambulizi ya majabali na ardhi, baada ya kuteketezwa na wala mawe. Alishangaa kuona jinsi sehemu ile ndogo ilivyotofautiana na maeneo yale ya awali!

Mara Kibwe akakumbuka!

“Ahaaaaa! Sijui kwanini nilitaka kusahau! Hapa ndipo Bunga aliposema kuwa nitamkuta mzee wa busara, ili nipate maelezo kuhusu safari yangu! Sijui huyo mzee wa busara ni nani? Lakini nitafahamu baadae, kama kweli hapa ndipo mahali penyewe.” Hata hivyo kwa uchovu na njaa aliyokuwa nayo, kijana yule aliamua kuketi chini ya mkomamanga , akawa anaokota makomamanga yaliyoiva na kudondoka chini, na kuanza kula. Aliendelea kuketi chini ya ule mti akipumzika, ili kupata nguvu mpya. Alikuwa akitafakari kuhusu hatima ya safari yake wakati aliposikia mlio kama wa pikipiki iliyokua ikianza kuondoka! Alihisi kama mlio ule ulikuwa ukitokea chini bondeni hatua chache kutoka alipokuwa ameketi, na alipotafakari kuhusu mlio huo, akahisi kuwa ulikuwa ni kama kikohozi cha jitu kubwa sana! “Sijui ni kitu gani hicho tena?” Kibwe aliwaza, na kwa mara nyingine akaanza kupata hofu. Alianza kujuta kwa nini alikuwa kule mbali mno na wazazi wake, ambao hata hakukumbuka walikokuwa! Hata hivyo, taratibu alinyanyuka na kuanza kuangaza angaza, akisogea bondeni uliposikika ule mlio. Alitaka sana kufahamu ni kitu gani kilichotoa mlio wa labda tuseme….pikipiki? ……Trekta……..?

Kila alipoangaza, hakuona kitu chochote! Alisogea na kuzidi kuchungulia chini bondeni, lakini hakuona kitu licha ya ardhi ya tope jeusi ambalo liliotesha majani marefu, na pia kulikuwepo lundo la kifusi kilichoinuka mithili ya kilima kidogo. Juu ya kilima hicho, Kibwe aliona uyoga pori umestawi vizuri sana. Taratibu alisogea zaidi na kukichungulia kile kilima, kuona kama angeweza kushuka bondeni kwa kurukia juu ya kilima hicho. Kwa hiyo kutoka juu alikokuwa, kijana yule alijirusha na kuangukia juu ya hicho kilima. Hapo aliweza kuangaza vema sehemu zote za bondeni, ingawa bado alishindwa kuona kitu chochote ambacho kingeweza kutoa mlio wa kustusha kama ule aliousikia muda si mrefu uliopita.

Kibwe alishangaa sana, kwani alikuwa na uhakika mkubwa kuwa sauti aliyoisikia ilitokea bondeni.

“Haya sasa ni maajabu makubwa! Hivi ndio kusema kuwa labda huo mlio sikuusikia? Au tuseme haukutokea humu bondeni?” Alijiuliza kwa mshangao mkubwa juu ya muujiza ule wa aina yake. Lakini kabla hajazidi kudadisi, alisitushwa tena na mlio ule usiofahamika, ila safari hii alijikuta akirushwa hadi ng’ambo kabisa juu ya bonde.

“Aaaaaaaaaaaaaaaaghh! Mama yangu weeeeeeeeaaaagh…!” Alilia kwa taharuki wakati alipokuwa akielea hewani kabla ya kuangukia kwenye matawi ya mti, mbali na pale alipokuwa awali.

Kijana aligwaya vibaya sana akiwa ananing’inia juu ya mti kama popo. Alikuwa akitweta na kupumua kwa kasi, huku macho yametoka pima, bila kufahamu kilichomsibu! Halafu, kabla hajatulia vema, kilisikika kitu kama chafya ya nguvu iliyoambatana na upepo mkali kama wa gari moshi likifoka, na hapohapo yeye alizolewa na huo upepo na kujikuta akielea tena hewani, na kisha akatupwa mbali zaidi juu ya bonde kulikokuwa na miti ya mikomamanga, akawa amebanwa na matawi ya mmoja kati ya mikomamanga ile!

Walisindikizwa na raia wa Azarbajan kwa shangwe na hoihoi hadi bandarini, na kule wakaagana kwa upendo mkubwa, na kisha merikebu ikaanza safari nyingine ya ajabu ya Kibwe, kumuokoa Bhaduri binti Sultani Bashar wa Mashariki ya mbali ya dunia!

Merikebu ya Mfalme KashKash iliyoyoma usiku na mchana, na hali ya bahari ilikuwa shwari kabisa, kwa muda wote huo.

“Tuna bahati kubwa, kwani mpaka sasa bado hali ni shwari sana.” Hanga alimwambia mwenzake Kibwe. “Kwa kawaida mimi hutapika sana baharini, lakini leo niko salama kabisa,” Alieleza. Kibwe alimwambia kuwa kwa kuwa bado safari ni ndefu asijiamini sana. Kwa maneno hayo, wote wawili walicheka kwa pamoja. Meli hiyo iliyowabeba vijana hao wawili, wahudumu wakutosha wa meli na manahodha, ilizidi kuyoyoma hadi kufika katikati ya bahari, halafu jambo la ajabu likatokea! Ile meli ilisimama ghafla, kama kwamba ilinasa mahali. Kibwe alipomuuliza nahodha aliyekuwa kwenye usukani ni nini kilichotokea, akajibiwa kuwa hakuelewa ni nini kimeikwamisha meli yao.

“Huenda majani ya mwani yamenasa kwenye pangaboi linalozungusha maji huko chini ya meli,” alisema nahodha. Alipoambiwa hivyo kijana yule alijitolea kwenda kuangalia kule chini ya meli, ingawa wenzake walimzuia sana.

“Ni hatari kwenda peke yako. Labda tufuatane pamoja .” Hanga na baadhi ya wahudumu wa ndani ya meli walimwambia. Ingawa Kibwe alipinga kufuatana nao, lakini wenzake walishikilia tu, hadi yule kijana akakubali waende wote.

Naam, karibu watu wanne walishuka na kuogelea kwenda chini ya ile merikebu, kuangalia hicho kilichonasa kwenye pangaboi la meli yao. Wote waliogelea, na Kibwe alikuwa mbele zaidi, hivyo alitangulia kuwasili pale lilipokuwa hilo pangaboi. Lakini lo! Pangaboi lenyewe lilikuwa limeshikiliwa madhubuti na mtu mmoja mwembamba kupita kiasi, na mrefu kuliko utakavyofikiria! Macho ya mtu yule yalikuwa pembeni mwa sura yake, iliyofanana na chura!

“Ahaa! Kumbe! Tunakutana tena siyo?” Kibwe aliwaza, na bila kupoteza muda, na haraka kama mwendo wa mshale, kijana yule alitoa rungu lililokuwa kwenye mfuko alioubeba mgongoni, na kulirusha kwa nguvu zake zote, kumtupia yule mtu wa ajabu, akilenga ule mkono ulioshikilia lile panga boi! Kwa kishindo kikubwa, lile rungu likamfikia kwenye mkono wake huo, na palepale akaachia lile panga boi, na kama umeme, akapotelea chini kabisa ya bahari!

Naam kwa mara nyingine, Kibwe alikutana na mmoja kati ya jamii ya majini wa bahari, jamaa zake ‘Makatta wa Makattani.’ Wakati hayo yakitokea, wenzake wengine waliokuwa wakija kuangalia chini ya merikebu, walifika na kumkosa yule jini wa bahari kwa sekunde tu!

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)