Mtunzi: Hussein O Molito
SEHEMU YA SITA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“toa loud speaker bwana.”
Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.
“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
ENDELEA...
“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.
“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya upole.
“sasa?” aliongeza Balqis
“najisikia vibaya mnavyonitenga.” Aliongea Karimu kinyonge.
“basi poa, unakaribishwa kwenye maongezi yetu.” Aliongea Balqis na kuachia kicheko kidogo.
“hivi utakua na nafasi wiki hii?” aliuliza Karimu baada ya kupata nafasi ya kuongea na Balqis.
“yap… kwanini umeniuliza hivyo?” aliongea Balqis na kumpa nafasi Karimu ya kuongea dhumuni lake.
“tuna safari kesho ya kuelekea kwenye visiwa vya Comoro, tutakaa wiki nzima tukila raha huko. So kama una muda ni vizuri ukajiunga na sisi hiyo kesho.” Aliongea Karimu huku akionyesha msisitizo wa kile alichokiongea.
“ Sharji atakuwepo?” aliuliza Balqis na kumfanya Sharji aliyekuwa kimya wakati wote kushtuka na kujibu haraka.
“mimi ndio kinara wa hiyo safari.” Aliongea Sharji na kufanya wote watatu kucheka.
“kwakua Sharji atakuwepo basi nitakuja, mchango ni kiasi gani.” Aliongea Balqis na kuwafanya Karimu na Sharji kuangaliana.
“hakuna mchango mama, tunaenda kama camp kula bata maeneo hayo waki nzima.”
Aliongea Karimu na kumfanya Balqis kucheka.
“poa, tutaonana kesho asubuhi.” Aliongea Balqis na kukata Simu.
Maongezi yao yaliishia kwa furaha upande wao. Hasa kwa Karimu ambaye alikua ana hamu kubwa ya kumuona kutokana na sifa alizotajiwa.
Kiza kilipoanza kuingia, watu wapatao kumi waliingia mule ndani. Walijigawa wasichana watano na wavulana watano. Walibeba mabegi yao kuashiria kuwa safari imeiva.
Walipokelewa vizuri na wenyeji wao Karimu na mdogo wake Sharji.
Vitu vilivyokua ndani vililetwa mbele. Makreti ya bia na pombe kali yalisogezwa tayari kwa part ndogo.
Dakika kumi baadae lilikuja gari likiwa na wafanyakazi wanne walioshuka na majiko ya kuchomea nyama.
Mziki mkubwa ulifunguliwa na watu wakaanza kuselebuka pale kati huku wakijisevia vinywaji na nyama choma za kila aina zilizokuwa zikichomwa bila idadi.
Ilipotimia saa tano usiku. Sharji uzalendo ulimshinda kutokana na kutozoea makelele. Aliaga na kwenda chumbani kwake kulala.
Mawazo juu ya safari aliyokua anaisubiri kwa hamu yalimfanya kukosa usingizi kwa muda mrefu. Baada ya masaa kadhaa, usingizi mzito ukamchukua na kushtushwa na Alarm yake iliyokua ikilia kwa nguvu. Aliamka na kuchungulia nje. Aliona jua la asubuhi likipanda taratibu.
Aliamka na kuchukua mswaki na kuelekea bafuni. Baada ya kuoga, akaliendea kabati na kutoa nguo alizopanga kuvaa siku ile.
Alisogea sebuleni na kuwakuta wale wasafiri wenzake wakiwa wanapata kifungua kinywa huku wakipiga stori zao huku wakicheka kila dakika.
Aliungana nao na kunywa chai, baada ya hapo waliamua kutoka nje tayari kwa safari.
“umeshapata?”
Aliuliza mmoja kati ya wale wasafiri baada ya kumuona Karimu akirudi na gari lake.
“anakuja nayo muda sio mrefu.” Alijibu Karimu.
Dakika tano baadae, iliingia coster moja matata na wote wakatabasamu baada ya kuiona.
“mpigie Balqis ili tujue kama anaenda au alikua anazingua.” Aliongea Karimu baada ya kuona kila kitu kipo tayari kwa ajili ya safari.
“poa.”
Alijibu Sharji na kuchukua simu yake na kuanza kuitafuta namba ya Balqis. Kabla hajabonyeza kitufe cha kupigia, inaingia marcides benz matata yenye rangi ya silver.
Watu wote wakatoa macho baada ya kumuona mwanadada mrembo wa kiarabu mwenye nywele zilizowekwa brich na kuwa kama za kizungu akishuka kwenye ile benzi kwa madaha.. Alivaa gauni refu jekundu lenye mpasuo hadi kwenye mapaja yake.
Karimu alipagawa kupita wote na kubaki ameachama kwa jinsi yule dada alivyokuwa mzuri. Mwendo wa kimiss ndio uliowafanya watu wote kuzihesabu hatua zake mpaka alipowafikia. Balqis aliwasalimia wote kwa kuwashika mikono. Alipofika kwa Karimu, alitumia dakika nzima kusimama kwakua tu karimu aliganda na mkono wake bila kumuachia. Alijitahidi kuutoa mkono wake na kuendelea kuwasalimia wengine kwa style hiyo hiyo.
Alipofika kwa Sharji, aliachia tabasamu na kumkumbatia. Harufu nzuri ya marashi aliyojipulizia Balqis ilipenya vizuri kwenye pua za Sharji.
“tunaweza kuondoka sasa.” Aliongea Karimu na wote wakaingia kwenye ile coster.
Siti aliyokaa Sharji ndio siti aliyokaa Balqis. Muda wote Balqis alikua anatabasamu na kujisika raha kukaa karibu na Sharji ambaye kimtazamo ni mdogo kwake. Na hata kama wakiwa wanatoka kimapenzi basi jamii ingemshangaa.
Walifika feri ambapo bati yao ya kukodi ilikua inawasubiria.
Waliingia kwenye ile boti kubwa iliyokuwa na floor moja. Ilikua na vyumba vya kulala sita na ukumbi mkubwa uliokuwa na viti juu kabisa ya boti ile.
Ukubwa wa boti ile ulifanana na meli ndogo lakini yenyewe ilitengenezwa kwa ajili ya safari za kifamilia au kampuni.
Kila chumba waliamua walale watatu watatu na na kikapatikana chumba kimoja ambacho kwa heshima na hadhi ya Balqis basi walimpa alale peke yake.
Nahodha waliyepewa alianza kukiondoa chombo taratibu na kuanza safari yao.
Masaa matatu baadae, tayari walikua wameshafika mbali sana na hakuna aliyekua anapaona nchi kavu tena. Kwakua walienda na music systerm, basi hawakuwa na budi kuweka miziki kwa sauti kubwa na kuanza kucheza huku wakipata vinywaji waliivyopanda navyo.
Wakati boti inaendelea kukata mawimbi, mara ghafla injini ikasimama.
“vipi tena?”
Yalikua maswali yanayojirudia kwa kila mmoja wao akimuuliza nahodha.
“hata mimi sijui. Maana nimeangalia kila kitu kipo sawa. Sasa sijui kwa nini imezima.” Aliongea nahodha wa boti hiyo baada ya kuikagua boti yake.
“sasa tutafanyaje?” aliuliza Karim.
“nitafanya mawasiliano na kampuni yetu ili walete boti nyingine, hakuna jinsi.” Aliongea nahodha na hoja yake ikapitishwa na kila mtu.
Taarifa hizo ziliwafanya waache kucheza mziki na wote wakatulia tulii kungoja hatua zinazo fuata.
Sharji alijiona anamkosi kwa kua ilikua ni mara yake ya kwanza kupanda chombo cha majini na ndio matatizo yanatokea.
Wakati wote toka wanaingia kwenye ile boti, Balqis alikua habanduki kwa Sharji. Hali iliyowafanya wanaume wengine kumuonea donge Sharji kukumbatiwa vile na mtoto mzuri kama yule.
Karim ndio kabisa, alikua anaumia ndani kwa ndani kwakua alishaanza kumuhusudu. Pia aliamini kua mdogo wake hamuwezi yule dada kwakua alikua mkubwa kwake, basi ni njia pekee ya kumyang`anya mdogo wake na kuwa naye yeye.
--
Masaa matatu yanapita bila matokeo yoyote yanayoridhisha. Uvumilivu unamshinda Karimu na kumfanya amfuate nahodha aliyekua kwenye chumba chake akihangaika kutafuta mawasiliano.
“mbona sielewi na hutupi information yoyote?” aliongea Karimu kwa hasira.
“eneo hili halina network kabisa… nimejaribu kupiga wapi, hakuna kitu.”
Aliongea yule nahodha na kumfanya karimu ashushe pumzi ndefu na kuangalia chini. Aliponyanyua kichwa chake, sura ilikua imeondoa makunyanzi ya hasira na kuwa ya upole.
“sasa tutafanyaje?” aliuliza Karim kwa sauti ya upole.
“hatuna jinsi, zaidi tusubiri meli zitakazopita ili itupe msaada wa kuturudisha nchi kavu.” Aliongea yule nahodha na kumfanya Karimu atoke nje.
“jamani hakuna kinachoendelea hapa, tunachokisubiri ni meli au boti yoyote ipite ndio tuombe msaada wa kuturudisha nchi kavu.”
Aliongea Karimu na wote wakawa hawana jinsi zaidi ya kukubaliana na matokeo.
Masaa yalizidi kukatika hadi kufikia saa kumi jioni ambapo walikula chakula walichokibeba na kuamua kusubiri labda kuna meli yoyote itakayo pita mida hiyo.
Mpaka kiza kinaingia hakuna chombo chochote kilichopita. Wakakaa macho mpaka ilipotimia saa tano usiku.
“jamani twendeni tukalale tu.” Alishauri Karimu baada ya kuchoka kusubiria.
“sasa tutaendaje kulala wakati meli nyingi huwa zinapita usiku?.. tuvumilieni japo ifike saa saba au saa nane ndio tufikie hayo maamuzi.” Alishauri Balqis
“hata mimi naona tuvute muda kidogo.” Sharji alionyesha kuungana na Balqis.
Wazo la Balqis lilipita kwa kukubaliana kuvuta muda angalau ifike saa nane. Upepo uliendelea kuvuma kwa kasi huku watu wengi wakiwa kwenye nyuso za uoga kutokana na mazingira ya baharini yanavyotisha usiku.
Hatimaye saa nane usiku iliwakutia pale pale bila chombo chochote cha majini kupita. Hapo wakaamua kwenda kulala na kusubiri kesho yake.
“unaonaje ukilala na mimi Sharji, mwenzio naogopa kulala peke yangu.” Aliongea Balqis kwa sauti ya chini iliyosikika na Sharji peke yake kwakua alikua nae karibu.
Sharji alifikiria kwa muda bila kujibu kitu kisha akamuonyeshea Barqis ishara ya kukubali kwa kumuonyeshea dole gumba.
Sharji aliingia kwenye chumba alichopangiwa kulala na kaka yake, lakini baada ya muda aliamka na kumuacha mtu aliyekua analala naye na kwenda kwenye chumba cha Balqis.
Aligonga mlango na kufunguliwa . alipoingia ndani, alishangaa kukutana na harufu nzuri ya marashi aliyokuwa akiisikia toka jana yake kwenye gari.
Macho yake yalipata taharuki baada ya kumuona Balqis kwenye night dress nyepesi iliyoonyesha kila kitu kilichomo ndani. Hisia kali za kutamani kufanya mapenzi zikaingia fasta kichwani mwake. Na hata alipokaribishwa kitandani, alipanda haraka na kuchojoa nguo zake zote na kubaki na Boxer.
Kwa madaha na maringo ya ajabu, Balqis alianza kuivua ile night dress na kubaki na nguo ya ndani tu aina ya bikini huku maziwa yake yaliyosimama vizuri yakionekana dhahiri kwenye macho ya Sharji.
Ilikua zaidi ya utamu wa kawaida aliokuwa akiusikia Sharji baada ya kupata vitu adimu vilivyomzidi umri kutoka kwa Balqis aliyeamua kumpa penzi dogo huyo usiku ule.
Game kali iliishia kwa kila mmoja kuchoka na kulala kwa muda usiojulikana.
“mtafuteni Sharji yupo wapi jamani, mbona hafungui mlango?” aliongea Karimu baada ya kugonga mlango sana katika chumba alichokua amempangia kulala mdogo wake na jamaa mmoja kati ya wale aliowaalika.
“mgongeeni na Balqis basi aamke.” Aliongea Karim na kuonyesha hali ya kuchanganyikiwa kidogo.
Mlango wa Balqis uligongwa mara kadhaa bila majibu. Na baadae kelele za mlango ziliwaamsha Sharji na Balqis kutoka kwenye usingizi mzito uliochangiwa na uchovu wa mechi kali waliocheza usiku wa kuamkia siku hiyo.
“kha!!!!”
Ulikua mshangao mkubwa kwa watu karibu wote baada ya kumuona Sharji akiwa na taulo akitoka chumbani kwa Balqis.
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU IJAYO