
Mtunzi: Davis Nyandindi
SEHEMU YA SABA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Wakaubeba mwili wa Duba na kuupeleka ndani kisha wakamtuma tena yule kijana apelike ile taarifa kwa mfalme.
KAMA SIMULIZI HII UNASOMEA NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI KUPATA VIPANDE VYOTE KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA NAYO...
Kijana akatoka na kuinza safari yake huku akiwa anakimbia na baada ya masaa kadhaa akafanikiwa kufika kwa mfalme na kukuta akiwa na baadhi ya wazee wakiongelea mambo mengi kuhusu kijiji chao. Kabla hata ya salamu yule kijana akaanza kutoa ile taari huku akihema kwa haraka.
KIJANA: mtukufu Mfalme mganga amefariki.
Mfalme pamoja na wale wazee walishtuka maana ile taarifa ilikuwa mbaya kwa upande wao kutokana na umuhimu ambao alikuwa nao Duba kwa kipindi kile.
MFALME: Eeeeeee !!? Amefariki ?
KIJANA: Ndio mtukufu mfalme amefariki.
MFALME: Kwahiyo wewe ulimemkuta ameshafariki au.
Kijana wakati anataka kusimulia mara mzee sube akawasili sehemu ile, ndiupo mfalme akamkatisha yule kijana na kumkaribisha mzee sube na kumpa taarifa ya msiba wa Duba na wakati yeye ndie aliesababisha kifo chake.
MFLME: Karibu sana mzee Wangu .
MZEE SUBE: Ahsante sana mtukufu mfalme.
MFALME: Mzee tumepatwa na tatizo yule mganga ambae tulitegemea atusaidie juu ya lile jambo letu amefarikii.
alipoambiwa hivyo kwa unafiki akajifanya kushtuka na kushanga kama sio yeye aliefanya hilo tukio .
MZEE SUBE: Eeeeee !! Duba amefariki, Tumeangamia.
MFALME: Ndio hivyo mzee sube.
MZEE SUBE: Mh! kwani alikuwa anasumbuliwa na nini mpaka amefariki maana imekuwa ghafla.
MFALME: Hata mim sijui hivi hapa ndio nlikuwa nanimuulza huyu kijina ambae nilimtuma jana akamuite huyo mganga, yeye ndio ameleta hii taarfa za msiba. Haya kijina nambie ilikuwaje.
Akaanza kusimulia huku watu wote wakimsikiliza kwa makini, mda wote mzee sube alikuwa akijifanya kusikitika kuhuzunisha na msiba ule.
KIJNA: Mtukufu mfalme nilipofika nilimkuta yule mzee mzima wa afya tena akitengeneza dawa, nilipomueleza wapi natoka alifurahi sana nikampa ujumbe ulioniagiza, ila yeye akaomba jana nipumzike alafu leo asubuhi tuanze safari ya kuja huku, lakini cha ajabu leo nimeamka nimemkuta nje amekata roho huku damu nyingi ikiwa usoni mwake ususani maeneo ya poani, mdomoni na masikioni.
Aliponyamaza Sube akadakia na kuanza kuongea kabla mfalme ajasema kitu chochote.
MZEE SUBE:Mtukufu mfalme hapo kuna mkono wa mtu ambao unafanya hayo yote tena ni kati yetu sisi wazee maana haiwezekani kila tunachopanga kinaharibika, lazima kuna msaliti kati yetu..
alisema vile ikiwa kama kujisafisha kwa upande wake, wote walikuwapo mahali pale walikubari kile alichokisema mzee Sube na kuamini kabisa kati yao kuna msaliti, Wakiwa kwenye hali ya kuulizana nani msaliti malme akasimama na kuanza kuongea.
MFALME: kweli kabisa ulichokisema mzee sube haiwezekani kila siku mipango yetu ihalibike, sasa ninasema hivi endapo nitamgundua huyo msaliti hukumu ya kifo itakuwa juu yake.
Waliendelea kuongea kwa mda kuhusu lile swala, walipomaliza wale wazee wakaruhusiwa warudi majumbani kwao lakini mzee Sube aliombwa abaki maana mfalme alikuwa anataka kuongea nae. Wazee wote wakaondoka huku wakiulizana nani msaliti, wakati huo maongezi ya mfalme na mzee sube yakaanza.
MFALME:Nimekuambia ubaki kwa sababu katika wazee wote hapa kijijini wewe ndio ninakuamini na kukutegemea, ila kutokana na kile ulichokisema kuna kitu nimekihisi kutoka kwa wale wazee wenzako.
MZEE SUBE: Kitu gani hiko mtukufu mfalme.
MFALME: Katika hawa viongoz wangu kuna mzee mmoja namuhisi kuwa ndie anaetugeuka tunapokuwa tunapanga mambo yetu.
MZEE SUBE: Nani huyo.
Mfalme akamtazama Sube kwa jicho Fulani lililopelekea sube kuogopa na kuhisi labda amejirikana maana hata siku moja mfalme hakuwai kumwangalia kwa jicho kama lile, kisha akaanza kuongea.
MFALME:Nahisi mzee Bugu ndie msaliti.
Sube akashusha pumzi zake taratibu na kuanza kuongea.
MZEE SUBE:Kweli kabisa mtukufu mfalme maana hata mimi nilikuwa ninamuhisi huyo huyo Bugu lakini nilikuwa nashindwa kukuambia niliogopa kuonekana mchonganishi.
MFALME: Kumbe hadi wewe umegundua hilo, sasa tufanyaje.
MZEE SUBE: Kwa kuwa hatuna uhakika bora umtoe uongozi na umpe mtu mwingine unae muamini ili tutakapokuwa tunapanga mambo yeye asiwepo.
Sube alisema hivyo kwa sababu mara kwa mara Bugu alikuwa akipinga maneno yake na kwenda kinyume kabisa na yeye, aliona atamwaribia mambo yake. Mfalme bila kujiuliza wala kutafakari akakubaliana na mzee sube wafanye hivyo.
MFALME: Sawa mzee wangu nimekuelewa na nitafanya hivyo.
Mzee sube akaruhusiwa kuondoka maana walikuwa wamemaliza maongezi, akaenda nyumbani kwake na kumsimulia mke wake kila kitu kilichotea kwa mfale, Bibi sube alifurahi sana na kumpongeza mume wake kwa kazi mzuri aliyoifanya.Badaa ya hapo masaa yalienda na hatimae ile siku ikawa imepita, siku iliyofuata mfalme akaita wale viongozi wote na kufanya nao mkutano wa dharula ambao haukutegemewa na mtu yoyote yule.
MFALME: Nimewaita hapa kuna kitu nataka niwaambie na hiko kitu kinahusu kubadilisha uongozi maana kuna baadhi yenu kwa sasa mme zeeka sana kwahiyo inabidi muwapishe na wenzenu ili nyie mupumzike. Kwahyo leo nimeamua kumtoa uongozi mzee bugu na kumpatia mzee sube.
Mzee sube alishangaa sana kusikia vile maana hakutegemea kama mfalme angempa kile cheo, ndipo akaanza kupiga makofi huku akimshukuru mfalme kwa hatua aliyoichua. wale viongozi wengine baada ya kuona sube akipiga makofi na wao wakajaribisha huku hali ya mshangao ikitawala usoni mwao, maana lile jambo lilikuwa la ghafla na kwa pale kijijinni kwao hakukua na sheria ya mfalme kumtoa mtu uongozi bila kuomba ushauri kutoka kwa wale wazee, lakin kwa upande wa sube furaha ilitawa. Mfalme akaendelea kuongea.
MFALME: kwahiyo kuanzia leo mzee sube atakuwa kiongozi kama nyie wengine.
Kikao kiliendelea kilipoisha na hatimae kikafika tamati ndipo wale wazee wakaondoka na kumuacha sube pamoja na mfalme, wakiwa njiani wakaanza kuwaongelea wawili wale.
KIONGOZI 1: Jamani mwenzenu hata sielewi nini kinaendelea kati ya mzee sube pamoja na mfalme.
KIONGOZ 2: He! Kwahiyo ww ndio umejua leo ?. Sisi wenzako tumeliona hilo tangu zamani sana.
MZEE BUGU: mimi nashangaa kitu kimoja tu. leo mimi na mzee sube naonekana mimi ndio mzee kweli na wakati nimezaliwa nimemkuta mzee sube ndio anajifunza kuongea.
KIONGOZ 1: Bugu pale lazima mzee sube kuna alichokifanya sio bure .
KIONGOZ 2: Hata mimi naona hivyo hivyo, ila hebu tuachane na hizi mada maana sio mzuri.
waliachana na ile mada na kuongea mambo yao mengine na hatimae wakafika makwao. Kwa upande wa vijana wa kile kijiji siku hiyo na wao walifanya kimkutano kidogo wakiongelea kuhusu yule nyoka jinsi gani wafanye ili wafanikiwe kumnasa.
KIJANA 1: Hivi munajua huyu nyoka tusipomfanyia kazi atatumaliza wote.
KIJANA 2: Kweli unachokiongea maana sisi ndio tunaotegemewa hapa kijijini tukiwa kama vijana na sifa ya hiki kijiji chetu kuwa na vijana mashupavu, mashujaa sasa itakuaje tushindwe kummaliza haka kadudu kadogo kabisa.
KIJANA 3: Jamani kuna kitu nilisahau kuwaambia, Juzi nikiwa natoka msituni kuwinda nikapita nyumban kwa mzee sube maana njia ile ndio urahis mimi kufika nyumbani. Sasa wakati napita mbele ya nyumba ya mzee ghafla alinipta nyoka mmoja nakumbuka alikuwa na rangi ya njano kichwani pamoja na mkiani ila sehemu zingine zote alikuwa na rangi ya blue, baada ya nyoka kunipita akaingia kwenye kile kichaka ambacho kipo karibu sana na nyumba ya mzee sube. nikasogea mpaka pale kwenye kichaka ili nimuue yule nyoka ila cha ajabu wala sikumuona bali nilikuta kijisehemu fulani pakiwa pamemwagiwa unga mweupe na mwekundu pamoja na ukili ukiwa katika ule unga wenye rangi. Nikiwa nashangaa ghafla alikuja mzee sube na kunifukuza eneo lile na kuniambia kuwa nisipite tena njia ile .
KIJANA 4: huyu mzee sube atakuwa anajua ukweli kuhusiana na huyu nyoka.
KIJANA 1:Itakuwa kweli ulichokisema maana nilishangaa sana kuona tabibu wa kijiji anakosa dawa ya kutibu sumu ya nyoka alafu mzee sube awe nayo, wakati yule mzee Chala ameudumia sehemu hii kwa mda mrefu na hakuna ugonjwa ambao alikuwa anashindwa kutibu, na ndio maana yule mfalme wa jirani alikuwa anamuhitaji sana kutokana na umahiri wake wakazi.
KIJANA 5: kama ndio hivyo inabidi tuanze kumchunguza huyu mzee maana asijifanye tabibu kumbe anatuchezea akili zetu.
KIJANA 6: Itakuwa vizuri tukifanya hivyo, kwahiyo tutafanyaje ili tumchunguze.
KIJANA 2: Inabidi tuwe tunazunguka zunguka sana pale nyumbani kwake mpaka tufanikiwe kumuona huyo nyoka, kama tukishindwa kumuona mchana tutaenda kumchunguza tena usiku mpaka tupate ukweli wa jambo hili.
Baada ya kukubaliana vile kila mmoja akarudi nyumbani kwao kwa ajili ya kujiandaa na kazi, ilipoika majira ya saa kumi jioni wakakutana na kuanza kupanga njia watakazo zitumia pindi wakifika nyumbani kwa Sube.
KIJNA 1: Jamani huku tuendako tunatakiwa tuwe makini ili tuifanikishe kazi yetu na itapendeza sana kama Mzee sube hatatuona, maana anaweza kutufukuza. Cha msingi kila mtu ajitoe kwa ajili ya kusaidi mbaka.
Walipomaliza wakaianza safari yao na kuishia kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa karibu sana na nyumba ya Sube, ndipo akatumwa kijana mmoja aende kwenye kile kichaka kuangalia kama ataona kitu chochote, ila kabla ajaondoka aliambiwa endapo ataonekana na mzee Sube asirudi tena mule ndani bali atoe ishara, kama amefanikiwa kumuona huyo nyoka au laa kisha aende zake. Kijana akafanya kama alivyo akizwa alitoka mle ndani na kusogea mpaka kwenye kile kichaka na kujifanya anashangaa kitu Fulani, lakini kabla hajaona kitu chochote ghafla mzee Sube akatoka ndani kwake na kumkuta yeye akichakua chakua majiani. Kwa hasira sube aliongea.
MZEE SUBE: Wewe kijana unafanya nini hapo au wewe mwizi eee, ebu toka na ukawaambie wenzako sitaki nimuone mtu akipita shemu hii kwa sababu sio njia.
Kijana baada ya kufukuzwa akatoka bila hata ya kutoa ishara maana Sube alikuwa anaendelea kumuangalia, kwahiyo akaogopa kufanya hivyo asije akagundua kuwa wanamchuguza, wale vijana wengine walishangaa kuona vile lakini hawakuwa na jinsi waliendelea kusubilia labda watoona kitu chochot . Baada ya mda Fulani kupita, nyumbani kwa mzee sube akafika kijana ambae alikuwa ameagizwa kutoka kwa mfalme.
KIJNA: Mzee sube mtukufu mfalme ameniagiza nije nikuite na amesema tufanye haraka maana mke wake wa pili aitwae Mana ameng’atwa na yule nyoka.
USIKOSE SEHEMU IJAYO
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Share App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi