SHEREHE KUZIMU (10)

Zephiline F Ezekiel
0
Mtunzi: Frank Silaa

SEHEMU YA KUMI
ILIPOISHIA...
Baada ya Vivian kuona kwamba mama yake amekataa kubadili mawazo yake aliamua kuondoka na kurudi nyumbani kwake huku akiwa na msongo mwingi wa mawazo. Siku zilizidi kusonga mwili wa Vivian ulizidi kudhoofu kutokana na mawazo. Alikonda sana hadi majirani wakawa wanashangaa kwanini alipungua ghafla wakati alikuwa na mwili mzuri wa kunawiri.

KAMA SIMULIZI HII UNASOMEA NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI KUPATA VIPANDE VYOTE KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA NAYO...
Ukweli ni kwamba Vivian furaha iliyokuwa imepotea ndani ya moyo wake ilisababisha akose hamu ya kula na pia hamu ya kunywa ilitoweka vilevile. Hakuona furaha ya kuishi tena hapa duniani, alitamani kufa ili aweze kukwepa majaribu mazito aliyokuwa anapitia. Mume wake ambae ndie alikuwa furaha yake nae hakuwa hata na chembe ya furaha moyoni mwake. Muda mwingi walikuwa ni watu wa huzuni.

Nelson alipata wazo la kuuza nyumba waliyokuwa wanaishi akiamini kwamba pengine ndiyo iliyokuwa chanzo cha matatizo. Vivian hakulipokea suala la kuuza nyumba kwa furaha hata kidogo kwasababu alijua nyumba haikuwa na tatizo lolote isipokuwa mama yake mzazi. Alijaribu kumshawishi mume wake ili wasiweze kuuza ile nyumba lakini Nelson aligoma kumwelewa kabisa. Kwahiyo nyumba ilitafutiwa madalali na kuuzwa harakaharaka. Jamii iliyokuwa inamzunguka Nelson ilimshangaa sana kwa uamuzi wa kuamua kuuza nyumba chapuchapu tena kwa bei rahisi. Hakuwa na namna kwasababu alikuwa amechoshwa na ndoto mbaya za kila mara.

Mjomba yake pamoja na mama yake walipata taharifa za kuuzwa kwa nyumba ya kijana wao lakini hawakuwa na namna ya kuzuia kwasababu walikuwa wanafahamu matatizo yaliyokuwa yanamsumbua. Kwahiyo walikaa kimya wakiamini kwamba huwenda ni kweli nyumba ile ilikuwa na matatizo kwasababu wao wenyewe walishindwa kuelewa tatizo lipo wapi. Baada ya nyumba kuuzwa walinunua nyumba nyingine maeneo ya ‘Kijenge mwanama.’ Ila kibaya zaidi walipohamia katika nyumba ya pili katika eneo la mbali na pale walipokuwa wanaishi awali, mambo ndio yakazidi kuwa mabaya, njozi mbaya za kutisha ndio zilichachamaa. Ilifika pabaya Nelson akawa anaandamwa na ndoto yupo ndani ya jeneza anazikwa huku mke wake pamoja na ndugu zake wakimlilia sana.

Nelson alihisi kuwa anakufa kwasababu ndoto zote za kutisha alizokuwa anaota mara kwa mara huwa zilikuwa zinatimia, kwahiyo alijua moja kwa moja habari yake ndio inakwisha. Chakushangaza ni kwamba ndoto hiyo ya kuzikwa aliiota kwa mara tatu mfululizo. Alipoteza matumaini ya kuishi kabisa, hakujua cha kufanya ni kitu gani ili aweze kunusuru roho yake. Hadi kufikia muda ule alikuwa hajawai kumweleza rafiki yake hata mmoja kuhusu magumu aliyokuwa anapitia katika maisha yake. Lakini kutokana na paniki aliyoipata kutokana na ndoto ya mauti iliyokuwa inamwandama kila mara aliamua amshirikishe rafiki yake Lucas ili aweze kupata mchango wa mawazo.

Kwahiyo baada ya Nelson kufika kazini kwake siku moja aliamua kumwita rafiki yake ofisini kwake ili aweze kumshirikisha jambo lile. Alimpigia simu ya mezani na kumuomba afike ofisini kwake mara moja. Lucas alimkubalia na kumuahidi kwamba atakwenda baada ya dakika kumi na tato kwasababu kuna barua pepe (email) za wateja alikuwa anazijibu. Baada ya muda Lucas alifika katika ofisi ya Nelson ili aweze kumsikiliza. Wakati walipokuwa wakisalimiana simu ya mkononi ya Nelson iliita, na kusababisha aipokee kwanza ndipo afanye mazungumzo na rafiki yake.

“Haloo.” Sauti ya kiume ilisikikaa upande wa pili.

“Yes hello!” Nelson aliitika.

“Naongea na mzazi wa Mainard.” Sauti ya mtu ambae hakuwa amejitambulisha iliendelea kusikika upande wa pili.

“Naam!”

“Habari yako.”

“Njema tu.”

“Unaongea na mwalimu Peter, mkuu wa shule ya St Lucas’s nusery and primary school.”

“Sawa”

“Nimekupigia simu kukujuza kwamba mwanao amedondoka ghafla darasani na kupoteza fahamu kwahiyo tumemuwaisha hospitali ya Father babu.”

Asante kwa taharifa, nitafika hospitali baada ya muda mfupi.” Nelson alizungumza kwa ujasiri lakini habari zile zilimshtua sana.

Maongezi ya Nelson na rafiki yake yalishindwa kufanyika kutokana na matatizo yaliyokuwa yamejitokeza kwahiyo alimuomba wazungumze kwa wakati mwingine kusudi aweze kuwahi hospitali kuangalia maendeleo ya mwanae. Alipanda kwenye gari lake baada ya kuomba ruhusa kazini na kuondoka kuelekea hospitali. Alipofika kwenye geti la hospitali ya Father babu alipishana na gari la wagonjwa likitoka. Alifika mapokezi na kujieleza kwamba ndie mzazi wa mwanafunzi aliyefikishwa hospitali hapo kutokea shule ya St Lucas academy.

Alijulishwa kwamba mwanae kaamishiwa hospitali ya rufaa ya mount Meru baada ya hali yake kuonekana kuendelea kuwa mbaya. Nelson alihisi kuchanganyikiwa kwasababu hakufahamu mwanae alikuwa amekubwa na tatizo gani. Alimuaga dada aliekuwa mapokezi na kuanza kutoka kuelekea kwenye gari lake ili aweze kuwahi hospitali aliyopelekwa mwanane. Wakati alipokuwa anafungua mlango wa gari lake alisikia sauti iliyokuwa inatokea nyuma yake ikimwita.

“Nelson! Nelson!”

Aligeuza shingo yake na kukutana uso kwa uso na kijana ambae amevalia sare za daktari. Kumbukumbu zilimjia kwamba mtu aliekuwa anamwita alisomaga nae katika shule ya sekondari Ilboru miaka kadhaa iliyopita.

“Habari za masiku Edward.” Nelson alisalimia.

“Nzuri tu kaka! Unaonekana unamawazo sana yani nimekuita karibu mara nane lakini husikii.”

“Acha tu aisee, kichwa changu kinamawazo mengi sana.”

“Mawazo ya nini tena ndugu yangu.” daktari aliuliza.

“Nimekuja kumwangalia mtoto wangu aliyefikishwa hospitalini hapa leo asubuhi lakini nimepata taharifa kwamba amehamishiwa hospitali ya Mount meru baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya.”

“Mwanao ndie yule wa St Lucas academy?”

“Ndio.”

“Daah! Pole sana kwasababu mimi ndie niliyempokea mtoto huyo na kuruhusu pia aamishwe hospitali baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya. Ila usijali atapona.” Daktari alizungumza na kuishia kumtia moyo Nelson asikate tamaa.

“Kwani umebaini anasumbuliwa na nini?”

“Mwanao anasumbuliwa na tatizo la kuishiwa damu. Kasi ya kuishiwa damu katika mwili wake nimeufananisha na ugonjwa mmoja kitaalamu unaitwa ‘Anemia’ ambao hutokea pale ambapo seli nyekundu za damu zinakuwa hazizalishwi katika kiwango kinachohitajika. Jopo la madaktari katika hospitali yetu tumejaribu kumfanyia uchunguzi ili tuweze kufahamu sababu iliyokuwa inapelekea yeye kuishiwa damu kwa kiwango kikubwa namna ile lakini kwa bahati mbaya tumeshindwa kwasababu vipimo vyote tulivyomfanyia vilionyesha yupo sawa ingawa uhitaji wa damu upo palepale.” Jambo hilo limetushangaza sana na ndipo tukaamua kumuhamisha hospitali.” Daktari alizungumza kwa kirefu zaidi kuweza kumuelewesha bwana Nelson.

Maneno yale yalisababisha Nelson ahisi kuishiwa nguvu kwasababu alijua kwamba kama ugonjwa unaomsumbua mwanae umeshindwa kubainika inamana bado ni yale mauzauza yanaendelea katika familia yake. Baada ya mazungumzo hayo Nelson alimshukuru daktari yule halafu akawasha gari lake akaelekea hospitali ya Mount Meru.

Baada ya dakika 15 aliliegesha gari lake katika maegesho ya hospitali. Aliteremka harakaharaka na kwenda mapokezi kupata utaratibu wa wodi aliyofikia mwanae Mainard.

“Mwanao anaitwa nani?” muhudumu wa mapokezi alimuuliza Nelson swali.

“Mainard Nelson, amehamishiwa hapa muda mfupi uliopita kutoka hospitali ya Father Babu.”

“Usijali!” muudumu alijibu wakati anaingiza taharifa zile katika kompyuta iliyokuwa mbele yake. Baada ya sekunde chache alimweleza kwamba.

“Mainard Nelson amelazwa wodi namba 107, ghorofa ya tatu, wodi ya wagonjwa mahututi” Muudumu alimpa Nelson maelekezo ya kufika wodini.

Nelson alifuata maelekezo na kufanikiwa kufika katika wodi aliyokuwa ameelekezwa, lakini mlangoni alikutana na kibao kilichoandikwa ‘Intensive care unite’ ICU.(chumba cha uwangalizi maalumu) Alikaa nje ya wodi kwa muda kama wa dakika kumi ambapo alitoka daktari mmoja. Nelson alijitambulisha kwa daktari yule ili aweze kufahamu hali ya mwanae kwa wakati ule ilikuwa inaendelea vipi.

“Tumemfanyia uchunguzi wa kiafya mwanao lakini tumeshindwa kubaini tatizo halisi linalopelekea kuishiwa na damu kwa kasi kubwa. ila tunaendelea na uchunguzi zaidi ili tuweze kubaini tatizo.

“Vipi daktari, mwanangu atapona kweli?” Nelson alizungumza huku akijifuta machozi yaliyoanza kumdondoka baada ya kushindwa kujizuia.

“Usijali, atapona.” Daktari alimtia moyo Nelson.

“Vipi ninaweza kuingia kumuona kwa sasa?”

“Hapana kwa sasa haitawezekana kwasababu yupo chini ya uwangalizi maalumu.”Daktari alimjibu Nelson.

Nelson aliamua kurudi nyumbani ambapo alifika na kumjulisha mke wake matatizo yaliyokuwa yamemkumba mtoto wao. Vivian aliangua kilio utafikiri taharifa alizopewa ni za kifo cha mwanae. Alijua kwamba mama yake ndio alikuwa anayafanya yale kama njia ya kumkomesha baada ya kukataa kupokea uchawi. Matumaini yake yalipotea kabisa baada ya kusikia kwamba mwanae anasumbuliwa na tatizo la kuishiwa damu, mbaya zaidi madaktari wameshindwa kubaini sababu iliyokuwa inapelekea mtoto kuishiwa damu. Wakati Nelson alipokuwa anambembeleza mke wake alipokea simu kutoka kwa Lucas ambae alikuwa anamuuliza maendeleo ya mtoto aliekwenda kumwangalia hospitali. Nelson aliona asimweleze kwa njia ya simu aliamua kumwomba wakutane jioni ya siku hiyo ili waweze kuzungumza zaidi.

Ilipofika mida ya saa kumi na moja jioni Nelson alikutana na Lucas katika baa moja inayojulikana kwa jina la I.Q bar iliyopo Kijenge mwanama. Nelson alimweleza rafiki yake matatizo yaliyokuwa yanamsumbua, pamoja na hali ya mwanae hospitali. Lucas alisikitika sana baada ya kusikia mikasa aliyokuwa anaelezwa na rafiki yake. Mwishowe alimshauri waende kwa mganga kutafuta suluhisho la matatizo. Nelson alionekana kuwa mbishi sana baada ya kuambiwa mambo ya kwa mganga kwasababu hakuwahi kwenda hata siku moja na pia isitoshe haamini kabisa mambo ya waganga.

Ila alipokumbuka hali ya mwanae hospitali na isitoshe madaktari wameshindwa kubaini sababu ya mtoto kuishiwa damu, aliona wazo la kwenda kwa mganga alilodokezwa na rafiki yake lilikuwa na tija sana kwake. Kwahiyo aliamua kukubaliana na wazo la kwenda kwa mganga kesho yake asubuhi na mapema. Nelson aliagana na Lucas na kila mmoja alikwenda nyumbani kwake. Nelson alipofika kwake alimshirikisha mke wake wazo alilokuwa amelipata kutoka kwa Lucas. Vivian hakuonyesha kupinga kwasababu alikuwa anahitaji mtoto wake aweze kupona kwahiyo alimruhusu kwa moyo mmoja aende kwa mganga. Palipokucha Vivian yeye alielekea hospitali na Nelson alikwenda kukutana na rafiki yake ili waweze kwenda walipokuwa wamekubaliana.

***********

Baada ya Nelson kukutana na rafiki yake walianza safari ya kuelekea kwa mganga.

USIKOSE SEHEMU IJAYO

Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Share App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)