Notifications
  • MWALIMU MKUU (6)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA SITAILIPOISHIA...Hatimae rameki alipata nafuu alizinduka Mama ake alifurahi kumuona mwanae akiwa amepata fahamu“””Eeeee mungu kweli umesikia kilio changu asante sana(uku alifurahi)pole mwanangu””IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“”Asante mama”alijibu ramekiMama rameki na mama loly walirudi nyumbani kumchukulia rameki chakula kwani tangu asubui akupata mlo.*********Upande wa bi sani alifurahi…
  • MWALIMU MKUU (5)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA TANOILIPOISHIA...Mama roly alivyosikia rameki anataka kumwaga alimtema yule nyoka na kumficha pangoni mwake, rameki alimpambu mama roli kwa kasi ya ajabu kama ndege ya vita ikimbiavyo angani“Ramekiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!! tombaaaa”rameki na mama roli walipiga madafu kama manne “heeee rameki siamini???!!”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwannn??”rameki aliuliza“DUDU LOTE HILI…
  • MWALIMU MKUU (4)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA NNEILIPOISHIA...Mwalimu mkuu alistuka kuguswa na kitu kwenye makalio yake alijua rameki atakuwa kaweka mzigo nyuma yake rameki alivyoona ajakaa vizuri alisogea ili akae vizuri mwalimu mkuu alistuka kitu kama tango kikimgusa tena alipitisha mkono ili aone nn alistuka “MUNGU WANGUU”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Rameki alistuka mwalimu mkuu alivyoshika tango lake akapaza sauti“AAAAAA MWALIMU…
  • MWALIMU MKUU (3)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA TATUILIPOISHIA...chausiku alishangaa kuziona zile sale “JAMANI NANI KAKUPA MWANANGUU??!!”aliuliza chausiku kwa mshangao“Kaka juma”alijibu ramekiIKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“Oooh juma jamani mungu akubariki ooooh asante mungu”alitamka mama rameck uku akinua mikono juuRameck alizijalibu zile nguo hakika alipendeza sana adi mama ake alimfagilia kwa vigeregere “jamani juma mungu akuwekee…
  • MWALIMU MKUU (2)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA MBILIILIPOISHIA...“MUNGU WANGU YULE SI MZEE ALINANI???!!!”aliuliza chausiku kwa mshangao chausiku alimuangaria mzee alinani ambae amepoteza furaha yake ya kusomaMzee alinani alikuwa anakuja kuangaria bishala zake pale sokoni kwa kina chausiku.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Mzee alinani alistuka kumuona chausiku alikwepesha macho yake kwa aibu alitoka kwenye soko lile, chausiku alimpitia…
  • MWALIMU MKUU (1)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA KWANZA“MAMA USIFE MAMA NITAISHI VP NA HII MIMBA MAMA”ilikuwa ni sauti ya mdada aitwae chausiku akimwambia mama ake asifee bado anamtegemea mama ake na mimba yakee“CHAUSIKU MWANANGU NAJUA MIMI NDIYO TEGEMEZI LAKOO NILIPAMBANA NA KILIMO ILI USOMEE LAKINI UMECHEZEA SHIRINGI CHOONI MWANANGU UMESHIKA MIMBA BADO MWAKA MMOJA TUU UMALIZE LAKINI NDO IVYO MWANANGU MIMBA NDO ISHAINGIA SINA BUDI KUKUFUKUZA INGALI UKO MOYONI MWANGU NAKUPENDA MWANANGU CHAUSIKUU ILA…
  • THE NIGHTMARE (9)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TISAILIPOISHIA...“mmenifananisha, mimi ndio kwanza naigia ofisini mida hii.” Aliongea yule afande na kuigia kituoni.“sasa aliyekuwa anatuhoji ni nani kama sio huyo?”Alijikuta anajiuliza mwenyewe swali lililompa utata mkubwa kichwani mwake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wakati wakiwa hawajui hili wala lile, walishangaa kuona maaskari wakijazana pale na ambulance ikafika…
  • THE NIGHTMARE (8)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NANEILIPOISHIA...Walipofika feri, walipewa nahodha mwingine tofauti na yule aliyemuota na boti ilikuwa ndogo tu ya kawaida tofauti na ile aliyoiota.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Sharji alijikuta anapiga makelele baada ya kumuona Balqis akiwa amejaa damu mdomoni huku ametoa makucha yake akimfata kwa nia ya kumdhuru.“AAAAAAAAAAAGH”Sharji alipiga kelele na kukurupuka.…
  • THE NIGHTMARE (7)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SABAILIPOISHIA...“kha!!!!”Ulikua mshangao mkubwa kwa watu karibu wote baada ya kumuona Sharji akiwa na taulo akitoka chumbani kwa Balqis.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wengine walicheka na kaka yake alionekana kutoifurahia hali ile.“sasa wewe unatutia wasi wasi bure, si ungesema tu kama unaenda kulala kwa huyu dada?” aliongea kaka yake na kukirudia kile chumba alichompangia…
  • THE NIGHTMARE (6)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SITAILIPOISHIA...“toa loud speaker bwana.”Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya…

BIKRA YANGU (37)

Mwandishi: Emmanuel F. Kway

SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
ILIPOISHIA...
Mzee Mwasha aliserereka mpaka chini akitumia mgongo wake hapo ukutani asubuhi ya saa kumi na mbili ni baada tu ya kusikia taarifa mbaya kutoka hospitalini hapo kuwa mwanae Enock alikuwa ndani ya chumba maututi ambacho kiliwaka moto usiku wa kuamkia jana yake,

SASA ENDELEA...
Hakukua na haja ya kubisha sababu hata yeye aliona chumba hiko jinsi kilivyokua cheusi kimejaa masizi, moyo ulimpasuka na kuanza kulia kwa sauti kubwa sana, lakini ndani ya moyo wake alikua amejawa na furaha sana na kuona njia aliyo tumia ya kuwa tuma watu wake warushe dumu la petrol na moto usiku wa jana baada ya njia zote kugonga mwamba sasa hiyo ime fanikiwa na sasa ataweza kuishi kwa amani sana,

Madaktari walikuja pembeni yake na kumtuliza huku wakimfariji.

Hakuna alicho fanya zaidi ya kuwapigia simu ndugu jamaa na marafiki ili kuanza taratibu na vikao vya msiba wa Enock ,

Alim-maliza mwanae kipenzi alishamuua tayari kwa njia ya moto, sasa ili baki kazi nyingine ya kuwatafuta Sabrina na Catherine, kazi hiyo ilikua ni ndogo sana kwake, kuwa tafuta watu hao wawili ilikua ni lazima wafe, ivyo ndivyo alivyo jiapiza,

Alitoka hospitalini hapo na kurudi nyumbani kwake ambapo kila mtu aliye muona alimuonea huruma hasa baada ya kupotelewa na mtoto wake pamoja na mke wake kwa muda wa kipindi kifupi sana,!

“jamani moto! moto! moto!”

Ilisikika sauti ya muuguzi wa kike majira ya usiku ndani ya hospitali ya jeshi la LUGALO ikipiga kelele kwa mbali huku akikimbia sehemu ya tukio.

Watu wote walitizama eneo hilo nakuanza kulikimbilia huku wakipiga kelele za msaada, kweli ulikua ni moto mkubwasana wenye moshi mweusi baada ya kuingia ndani waliona ni chumba kimoja ndicho kinawaka moto huo, hawa kuelewa chanzo hasa kilichosababisha moto wa ghafla kutokea!,

Kengele ya dharura ilipigwa na wagonjwa kuanza kutoka nje mara moja, na wengine kutolewa haraka haraka.

“humu ndani kuna mgonjwa?”

Aliuliza Generali Shedrack akiwa na kombati za jeshi mwilini mwake.

“ndio Yule mgonjwa wa juzi aliyekutwa na sumu mwilini”

“una uhakika yupo?”

“ndio”

“nishikie hizi”

Generali Shedrack alimkabidhi muuguzi wa kike koti lake la jeshi na kuupiga mlango teke kwa nguvu zake zote na kuufanya udondoke mzima mzima,alijitosa ndani ya chumba kilichokua kina waka moto mkubwa ,macho yalikua yame mjaa ukungu alipata shida sana kuona mbele ila ilimbidi tu afanye kile alicho taka kukifanya ilikua ni lazima ayaokoe maisha ya mgonjwa huyo ambaye kwa siku nyingi sana alikua akiwindwa kuuliwa.

Hakuelewa ni kwanini aliamua kumuokoa kijana huyo mdogo ambaye hakustaili kufa kwa kuungua na moto,

Alifika mpaka kitanda alicholazwa Enock na kumuweka begani kisha kuanza kutafuta njia ya kutokea alivyofika mlangoni kutaka kutoka nae alisita na kutokea mlango mwingine wa dharura uliokua kushoto kwake,

Alimfikisha mpaka nje na kumuweka vizuri na kutoka yeye peke yake, watu wote walimshangaa bila kutoka na mgonjwa ambaye alisema anaenda kumuokoa,hakutaka kuongea chochote zaidi ya kutingisha kichwa kuashiria kuwa hakuweza kumuokoa.
“nimeshindwa, kuna moto mkali!”

Alizungumza Generali Shedrack na kuchukua nguo zake kisha haraka haraka bila ya mtu yoyote kumuona alienda mpaka nyuma, alipomuhifadhi Enock na kumuweka begani, alitembea kwa kujificha mpaka ndani ya gari ya jeshi Hammer aliyokua akitembelea.

Alimuweka nyuma yake na kumfunika na kitambaa na kuanza kuondoka taratibu, ndani ya moyo wake alijua kuwa kusema ukweli juu ya uhai wa mwanaume huyo ilimaanisha kumuweka tena mashakani ili bidi tu amuokoe kwa njia hiyo.

Aliondoa gari taratibu na kusimamishwa getini na mlinzi ambaye alikua na mashaka nae usiku huo,
“naomba nika pumzike Joram, kichwa kina niuma wacha nikanywe dawa nitarudi, endelea na lindo”

Alijitetea Generali Shedrack na kuruhusiwa pale pale, aliendesha gari mpaka nyumbani kwake KAWE mwisho alipo kua anaishi yeye na mke wake Vivian ambaye alikua muuguzi wa hospitali ya taifa muhimbili , alimshusha na kumuweka juu ya sofa na kwenda kuufunga mlango.
“huyu ni nani?”
Alihoji mke wake

“nita kuhadithia kila kitu naomba umpe huduma ya kwanza”

Vivian bila kuweka kipingamizi haraka haraka alitafuta madawa na kuanza kumpima na baadae kumuwekea dripu yenye dawa kisha kumchoma sindano,

Hapo ndipo Shedrack alianzakumuelezea kila kitu juu ya kijana huyo alivyokua anawindwa sana, hata mke wake alitingisha kichwa akisikitika sana kusikia habari hizo mbaya!.

“sasa hao watu wanaotaka kumuuwa unawajua?”

Alihoji Vivian

“mimi sijawajui kama nilivyo kwambia, naomba kesho asubuhi sana saa kumi uwashe gari umpeleke Tanga kwa Mama Andunje!”

“kwanini sasa?”

“hapa sio salama, akionekana pia tutakua kwenye matatizo hata mimi nitakua matatizoni mke wangu”
“sawa hakuna neno”

Ilibidi Shedrack atoke nje na kuanzakutengeneza dala dala yake binafsi ambayo ilikua bado ina marekebisho kidogo usiku huo huo,alivyo hakikisha kila kitu kipo sawa alirudi ndani, alimsisitiza sana mke wake kesho asubuhi aweze kusafiri mpaka Tanga kijji cha handeni akamfiche Enock huko na siri hiyo wabaki nayo wawili tu.

Majogoo yaliwika kuashiria kuwa kumekucha teyari na baadae hazana kusikika, alimuamsha mke wake na kumwambia ajiandae haraka haraka ilikua ni lazima aondoke asubuhi sana ya siku hiyo hiyo.

“sasa wewe huendi?”

Aliuliza mke wake

“mimi nikienda watanishtukia, wewe nenda najua upo likizo mimi natakiwa kazini leo hii mke wangu, hakikisha tunawasiliana”

“sawa mume wangu nitafanya ivyo”

“spea zote zipo kwenye gari kuwa makini bara barani ukifika tu nipigie simu”

Baada ya kumaliza mazungumzo yao taratibu walimbeba Enock na kumlaza ndani ya dala dala hiyo na kumfunika kidogo nashuka ,

“safari njema”

Waliagana na dala dala hiyo kuanza kutembea taratibu huku Vivian peke yake akiwa anaendesha,
Alikua makini sana juu ya usukani akiyatoa macho yake mbele. saa mbili za asubuhi alikua kasha fika chalinze hapo hakusimama alizidi kusonga mbele akibadili gia na kuzidi kwenda taratibu hakua na haja ya kukimbiza gari, ilikua ni lazima afike salama mkoani Tanga,

Alishakata kilometa sabini nyuma, sasa zilibaki chache tu afike kijijini HANDENI hii tu ni baada ya kuzungusha gari raundi abauti ya Segera na kuzidi kusonga mbele,

Tangu safari inaanza aliweza kuweka maji mdomoni mwake tu na mara kadhaa aligeuka nyuma kumuangalia Enock aliyelala ambaye haelewi kitu chochote kinachoendelea chini ya jua , alikua ni kama amekufa kabisa.

Aliacha barabara ya lami na sasa kukitafuta kijiji cha Handeni ilisha timu saa tisa alasiri na kupaki gari nje ya nyumba ya Mama Andunje! ,

Mama aliyemlea mume wake hapo kijijini, kwa kuwa alikua anajua ujio wake hakushtuka sana walimpokea na kuanza kumshusha Enock ndani ya gari, nayeye kumpigia simu mume wake kumwambia kuwa amesha fika tayari.

Walimuingiza ndani ya chumba kidogo na bibi mmoja kutokea ambaye aliaminika katika kutibu kwa kutumia dawa za miti shamba,!

Alivyo muangalia hata yeye alisikitishwa alikimbia mpaka kwake na kuleta majani majani na kinu kisha kuchukua na tangawizi na kuanza kuitwanga akichanganya na majani.

“huyu inabidi tumpake hii dawa kwenye unyayo kwanza”

Aliongea Mama Fina akiwa anatwanga dawa zake,

Baada ya zoezi hilo kuisha alianza kumpaka dawa zile kwenye miguu huku akikindamiza kifua cha Enock.

“sasa ivyo si utamuuwa?”

“hapana hapa najaribu kulegeza mapafu yake ili hewa iweze kupita ki urahisi”

Alijibu mama Fina huku akiendelea kumpatia Enock matibabu .

Ukweli aliokua akiutafuta tayari alishaujua sasa kuwa mwanae Natu hakufariki Dunia na walizika mkono, hii baada ya kupima DNA ya mwili uliozikwa hapo Mkoani Kilimanjaro kijiji cha Mwika kupitia chini ya usaidizi wa mpelelezi wa kujitegemea sasha waliweza kujua ukweli wa mambo.!

Hakua na haja ya kubaki nchini Tanzania ilikua ni lazima achukue usafiri mara moja na aanze safari ya kuondoka , utaratibu wa kukata tiketi ulianza mara moja na tayari alipata ndege ya shirika la RWANDAIR inayoondoka jumatano saa moja ya asubuhi.

Alichofanya ni kuweka pesa kwenye akaunti yake tayari ili ziweze kumsaidia huko atakapo enda, alijua kwake kazi iyo ilikua ni ngumu lakini ilikua ni lazima akamuokoe mtoto wake Mdogo Natu aliyeamini kua anapata mateso makali sana.

Hussein Molito,Khalfan Sudi, Sasha Jason na ndugu wengine wa karibu walikua teyari wapo uwanjani hapo saa moja ya asubuhi siku hiyo ya Jumatano wakimuaga Kway huku wakipunga mikono ambaye tayari alikua akiingia ndani ya chumba maalumu ili kuweka silaha yake.

Alivyomaliza taratibu aliweka mabegi yake juu ya kifaa maalumu kinachopeleka mizigo upande wa pili nayeye kupita chini ya kimlango kwa ajili ya ukaguzi wa mashine za kuscani.

Kitendo cha kupita katika mashine iyo ilianza kupiga kelele nyingi sana huku ikiwasha taa zake juu na kumfanya aanze kutetemeka,

sababu mbele yake aliwaona maaskari wakisimama na kukoki mitutu yao, hakuelewa ni kitu gani afanye zaidi ya kuambiwa agande hapo hapo na yupo chini ya ulinzi.

“hana kitu jamani afande, anco samahani vua cheni saa na mkanda wako kama una kitu cha chuma weka hapo kwenye kapu!”

Alizungumza mwanamke mmoja aliyekua pembeni hapo kwenye kompyuta na kumfanya kway arudi nyuma na kuvua vitu alivyoambiwa , na kupita tena bila wasi wasi.

“ahsante”

“safari njema”

Kway alipita bila kuamini hii yote ni kwa sababu ya mawazo aliyokua nayo kichwani mwake na kusahau kuwa haruhusiwi kupita na kitu chochote cha chuma.

Magari maalumu ya kuweka ngazi yalishafika teyari na kuweka ngazi zake kwenye mlango wa ndege ya Shirika la Rwandair, baada ya zoezi hilo kukamilika abiria walianza kupanda ngazi kwa ajili ya safari ya kuondoka.

“karibuni katika shirika la ndege la Rwandair A1050 hakikisha una funga mkanda muda wote wa safari hasa hasa pale taa za mikanda ziwakapo. Rwandaair inaelekea Entebbe kupitia KIA na KIGALI kwa niaba ya captain Michael Mimi naitwa Irenestella”

Sauti hiyo nyororo ya muhudumu wa ndege(air hostress) ilisikika kutoka kwenye kipaza sauti ikijirudia kwa lugha nyingi tofauti .

Ndege taratibu ilianza kutembea na baadae kuchanganya kasi na taratibu matairi ya mbele kuinuka na mengine kufuatia pia kidogo kidogo kuiacha ardhi ya Tanzania ikipaa angani.

“Halloo!”

Kway alivunja ukimnya kwa abiria mwenzake aliyekua ameketi pembeni yake dirishani.

“Hei Mambo?”

Alijibu mwanamke huyo mtu mzima na kumgeukia

“kumbe unazungumza Kiswahili?”

“ya kidogo sana”

“wewe ni raia wa wapi?”

“Uganda, sema nilikua huku kwa muda wa murefu sana sasa nimeamua kurudi Nyumbani kidogo”

“Naitwa Kway!”

“Sandra, naitwa Sandra Katali, unapita Uganda?”

“ndio” alijibu Kway

“kumbe tupo musafari moja”

KWA WATUMIAJI WA APP KUNA MATANGAZO YANATOKEA KWENYE APPLICATION YETU HIVYO UKIYAONA NAOMBA BONYEZA HAPO NDIO UNANIPA SAPOTI MIMI, UKIBONYEZA UNAWEZA KUCANCEL SIO LAZIMA UENDELE ULIKOPELEKWA, KIKUBWA UBONYEZE HATA MARA 2-3 KILA UKIFUNGUA APP YETU

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO

14 Bikra Yangu Simulizi Z14
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni