SEHEMU YA HAMSINI NA NNE
ILIPOISHIA...
Naomi alishajiona mshindi tayari alitafuta chumba haraka haraka, na baada ya masaa mawili alikua na daktari huyo chumbani, taratibu alitoa nguo yake ya juu na kubaki na sidiria Dokta Simon alishindwa kuelewa.SASA ENDELEA...
“mbona unavua nguo?”
“wewe mwanaume mpaka hapa hujui nataka nini?”
Hapo ndipo Dokta simon alijua nini nia ya Naomi alijikuta tayari ananyonywa mdomo wake huku akishikwa shikwa taratibu juu ya Mashine yake na kufanya itune na kuishiwa nguvu kabisa na kumfanya damu imuende mbio mno, hakuweza kusema lolote zaidi ya kuonesha ushirikiano hata yeye.
Naomi aliifungua zipu ya daktari huyo na kutoa MASHINE kisha kuanza kuilamba taratibu sana kwa ufundi huku akianza kuchezea chezea gololi mbili zilizokua kwa chini, ndani ya dakika mbili tu nguo za dokta zilikua chini zimetupwa hata yeye hakuelewa zilitoka vipi mwilini mwake,
Naomi alikua na kazi moja tu kucheza na filimbi ya Dokta huyo ambaye alikua hoi bin taaban kwa raha
zote na kutamani wakati huo huo mechi ianze. Naomi alivua nguo zake zote na kumpandia kwa juu kisha kujiweka mwenyewe kwenye mashine na kuanza kukatika kwa juu tena taratibu kwa madoido,
Mzee huyo daktari mwenye mvi chache alikamata vizuri kiuno cha binti huyo ambaye aliye kua ni kama binti yake wa kumzaaa lakini hakujali hilo, alishaanza kuhisi raha za ajabu huku akipelekwa puta kwenye mchezo huo wa kikubwa…
“Doktaaaaa!”
Aliitaa Naomi Kwa sauti ya puani huku akiwa anakatika juu yake
“Abe..ee Naaa…m”
“kunaaaaa kaziiii nataka unifanyieeeeee”
“Ipppiii aaaaaaaah?”
“kuna mtu natakaaaa umpotezeeee dunianiiii”
“hapaaaana sitoowezaaaaa”
Hapo hapo Naomi alisitisha kukatika na kutulia huku akimuangalia machoni
“hutaki basi naondoka”
“basi tafadhali binti tuendelee nionee huruma mzee wako, basi nitafanya unachokitaka”
“ukifanya nachokitaka utani faidi sana, ushawahi kula tigo?”
“haaaapana”
“basi nitakupa mpaka nyuma”
“nipee sasa hiivii”
Kweli Naomi hakua na masihala aligeuka na kushika vizuri mashine ya daktari kisha kuiingiza ndani ya shimo la nyuma yaani mlango wa uwani na kuanza kukatika tena…….
Dokta Simon yupo kitandani yupo hoi bin taaban kwa raha na burudani alizokua akizipata kutoka kwa Naomi, katika maisha yake hakuwahi kupewa mapenzi ya aina hiyo kwani alienda mizunguko mitatu kwa masaa machache, ni utundu huo peke yake aliupata kutoka kwa Naomi mwanamke ambaye aliyejitolea rushwa ya ngono ili afanikishe kumuuwa Catherine. Aliamini kuwa mwili wake ni silaha tosha kumpagawisha dokta huyo Mzee, aliyekua na umri uliofanana na baba yake mzazi.
“Vipi turudie tena?”
Aliuliza Naomi akiwa kifuani mwa daktari wote wakiwa watupu wamejifunika na shuka
“mmmh mmmh”
Alikataa kwa kutingisha kichwa akiwa yupo hoi jasho linamtoka.
“mbona hapa bado, ukishanifanyia kazi yangu, utapenda mwenyewe”
“kweli?”
“nakwambia ukweli”
“nina familia ujue, nina mtoto kama wewe, usije ukafanya nikaikimbia familia kisa wewe, sikuwahi kujua kama watoto wa siku hizi mna mambo makubwa kiasi hiki”
“hayo tisa, kumi nataka Catherine umpoteze, naelewa sana maisha yake unayo”
“ndio,”
“sasa fanya ivyo ivyo basi Darling”
“okay”
Naomi alitabasamu kusikia jibu hilo,alishawaza mbeleni kuwa mambo yangemnyookea, watu wa karibu ndugu zake na Enock walivyompa taarifa juu ya Moto mkali kuunguza nyuma aliwajibu kuwa yupo Arusha na muda mfupi angerejea Dar es salaam na ndivyo walivyodhani, hawakuelewa kuwa mwanamke huyo ni simba aliyejifika ngozi ya mwanakondoo.
Siku zilizidi kwenda,na wiki kukatika bado hakuweza kusikia habari yoyote ile ya msiba Wa Catherine kutoka kwa Dokta Simon, hapo ndipo alipoamua kumpigia simu siku hiyo mchana.
“kazi yako siwezi kuifanya,tena ukiendelea kunisumbua nitakushtaki, siwezi kuuwa mimi” Alijibu Dokta simon.
“ha ha ha ha ha ha, nadhani hunijui vizuri, okay sawa tuone mimi nawewe nani zaidi, una mke ana itwa Diana, nina amini una mpenda sana, na unaipenda kazi yako pia”
“usinipigie tena simu Naomi”
“umechelewa”
“una maana gani?”
“nakutumia video uliyokua unanifanya kinyume na maumbile, na itaenda kwa mkeo sasa hivi”
Moyo wa Dokta Simon ulidunda kwa kasi sana kusikia habari izo, akili yake ilimtuma moja kwa moja mpaka kwa familia yake na ukoo wake kwa ujumla jinsi walivyomuheshimu hata serikalini vile vile, alielewa nini maana yake.
“unanana..sema una una nini?”
Alipata kigugumizi cha ghafla.
“ndio ivyo sasa hivi nakutumia”
Kweli ndani ya dakika moja video iliingia kwenye simu kupitia mtandao wa watsap hapo ndipo alishindwa kuamua cha kufanya ilibidi ampigie tena simu Naomi na kukubaliana na lolote analotaka.
“ila naomba baada ya kukufanyia kazi yako hiyo video uifute”
“sitakua na sababu ya kukaa nayo”
Hakua na jinsi zaidi ya kukubali kwenda kushiriki mauaji japo hakupenda hata kidogo, hakua na jisni yoyote ile, alipewa siku mbili tu na Naomi ili afanye kazi hio ya kumuondosha Catherine duniani.
Hali ya Catherine kila kukicha ilizidi kutisha ili kuwa mbaya sana hakuweza kula hata kidogo, alitapika mfululizo na kukonda ghafla madaktari ilibidi wamuwekee ukaribu wa hali ya juu sana kuliko mgonjwa mwingine yoyote yule, baada ya kuchukua vipimo vyake aligundulika kuwa ana ugonjwa Wa typhoid na homa kali mwilini!, hapo hapo akiwa kitandani alianza dozi ya vidonge vya typhoid huku akiwa ametundikiwa dripu aina ya Glucose kwenye mishipa yake ya damu ili kurudisha nguvu zake. kwa upande wa Enock ilikua kinyume yeye hali yake ilizidi kuwa nzuri na kuonesha matumaini, dalili zilionesha kuwa atarudi katika hali yake ya kawaida licha ya yote lakini hakuwa mwenye furaha hata kidogo, habari za Catherine zilimfanya aonekane bado anaumwa, kila siku alikua akitoka wodi lake mpaka kwa Catherine kuangalia hali yake,
Alivyomuona alitamani kulia, Catherine aliongea kwa tabu nyingi sana alimuangalia mtu kwa shida.
“Catherine Mpenzi”
“Ab…ee Dar..ling”
“unajisikiaje na hali?”
“sa..sa nina afadhali ond..oa shaka mpenzi wa..ngu. nikipona tutafunga nd..oa?”
“ndio utakuja kuwa mke wangu unizalie watoto, unakumbuka ahadi yetu?”
“ndi..o naku..mbuka niombee nipone niwe mzi..ma sidhani ka..ma nitapona nahisi nita..kufa sitaki kuf..a Enock uzidi kuniombea!”
“usiseme ivyo Catherine, unamkufuru Mungu. Utapona tu, kama Mungu kaweza kutupigania kutoka kwenye moto hatoshindwa kukupigania, Mungu wetu ni Mwema”
“Ahs…ante Mpe..nzi wangu”
Yalikua ni maneno ya kuuzunisha sana kwa wawili hao, Enock alishindwa kuyazuia machozi yake alitoka nje na kuanza kulia sana,maneno aliyokua akiongea Catherine yalimuogopesha sana hata alivyoangalia hali na maneno aliyokua akiongea yaliendana kabisa hilo hakupinga,alikumbuka mambo mengi yaliyopita katika maisha yao jinsi walivyoteseska mpaka kufikia hapo, ni kweli maisha yao yalijawa na misukosuko mingi sana,
“Enock usilie Mwanangu,”
Mama Catherine alisema na kumfanya Enock apanguse machozi yake harakaharaka akitumia viganja vyake vya mikono.
“hapana Mama nipo sawa, nipo sawa”
“Catherine vipi hali yake?”
“sasa hivi inaridhisha”
Catherine alizidi kupewa huduma na matibabu, kila kukicha madaktari walimtibu kwa uangalifu sana, hali yake taratibu ilianza kurudi kama zamani aliweza hata kutembea na kukaa kitandani mwenyewe, hata yeye alijipa moyo anaenda kupona muda mfupi kutokana na hali aliyokuwa nayo, aliweza kula sasa bila kutapika, afya yake taratibu ilianza kujijenga na mwili kurudi kwa ujumla!,
Ghafla siku hiyo asubuhi baada ya kumaliza kunywa uji alianza kuhisi tumbo lina muuma sana, alivyoenda chooni aliharisha sana,kwa mara ya kwanza alidhani wenda ni mchafuko wa tumbo lakini siku mbili mfululizo aliharisha na kupoteza maji mengi sana mwilini mwake,alikua hakauki chooni, kila mtu aliogopa sana, madaktari walipata tena shughuli za kuanza kumtibu upya, hata wao walishindwa kuelewa ni kitu gani kimemtokea Catherine.
Nywele zake zilianza kubadilika rangi na kuanza kukatika, mwili wote ulipungua tena mara tano yake, walivyo mpima uzito kila mtu alishika mdomo, uzito wake ulipungua kilo ishirini ndani ya siku chache,hazikupita siku mbili alianza kutapika kila kitu na wakati mwingine mpaka damu, alianza kukohoa kikohozi kikavu, Mama yake aliingiwa na wasi wasi mwingi sana alishaelewa nini maana ya dalili izo, alimuomba sana Mungu wake Catherine asiwe ni muathirika wa ugonjwa hatari wa Ukimwi, sababu alijua ni jinsi gani ulivyokua una tesa na hauna tiba, Hata madaktari nao walikua na mashaka juu ya afya ya Catherine, hapo ndipo walipoamua kumuita mama yake mzazi ili waanze taratibu za kumpima damu kubwa.
“Mimi sina tatizo mumpime tu damu yake”
“okay sawa, hakuna tatizo tulikua tuna subiri kauli yako”
Hapo ndipo madaktari walipoanza kuchukua damu kubwa ya Catherine na moja kwa moja kuingia nayo maabara kwa kuiangalia kama ina maambukizi ya virusi vya ukimwi, haikuchukua hata lisaa limoja Mama Catherine aliitwa ndani ya chumba cha daktari ili apewe majibu ya mwanae, mapigo yake ya moyo yalimwenda mbio sana.
“nasikitika kukwambia kuwa mwanao…..!”
Daktari alishindwa kumalizia majibu aliyokua akitaka kuyatoa na kumtuliza Mama Catherine ambaye alikua analia kwa kwikwi.
“kumbe wifi una watoto wakubwa kiasi hiki?”
“aaah sio sana. Lakini umri umeenda pia, huyu ana miaka ishirini na tatu yupo Libia,ana maliza digrii ya udaktari kama baba yake, kuna mwingine mkubwa ameolewa sasa hivi na anakaribia kujifungua”
“hongera, mimi bado hata sijafikiria kuwa na wangu wifi”
“mmh.. lakini bado sijakufahamu vizuri, naomba tufahamiane”
“mimi naitwa Naomi, nafanya kazi na Dokta Simon, ni kama kaka kwangu leo alinialika hapa kwake”
“ooh nashukuru kukufahamu, ndio kwanza anajiandaa yupo chumbani”
“sawa basi atanikuta”
Naomi alishafika nyumbani kwa Dokta Simon akiwa na mke wake ameshika album za picha mbali mbali anaziangalia, mpaka wiki mbili zinapita hakuweza kusikia habari zozote zile juu ya Kifo cha Catherine ilikua ni lazima aweke unoko kwa mke wake na kumuonesha video waliyokua kitandani wanafanya mapenzi na daktari huyo aliyekua anaheshimika sana na familia yake mpaka katika jamii yake kwa ujumla,
Dokta simon alivyotoka chumbani kwake alishtuka sana kuiona sura ya NAOMI akiwa yupo seblen tena yupo na mke wake Diana, alielewa nini maana yake.
“vipi mbona umeshtuka?”
Alihoji mke wake
“hapana nipo sawa naona kuna ugeni”
“Dokta ndio nimekuja sasa”
Alidakia Naomi
“ahaa sawa, twende basi”
“twende wapi?”
“tukamalizie ile kazi ya operesheni”
“hakuna cha kazi yoyote, nimekuja kumwambia mkeo utanifanyia kazi yangu au hunifanyii?”
“kwani kuna nini?”
Diana aliuliza baada ya kuona haelewi kinachoendelea hata yeye aliingiwa na mashaka.
“hakuna kitu mke wangu”
“hapana kuna kitu”
“usimfiche mkeo mwambie ukweli la sivyo nafanya yangu simu hii hapa, utanifanyia kazi yangu hunifanyii?”
“nitaifanya”
“lini?”
“leo hii hii itakua imeisha”
“sawa mimi naenda ila usipoifanya……”
Jasho liliaza kumtoka mwilini mwake na kulowanisha shati alilokua amelivaa japo alikua ametoka kuoga muda mchache uliopita, alikua katika wakati mgumu sana, ilibidi tu achukue maamuzi ya kuuwa ili kuepukana na fedhea atakayoipata siku chache zijazo, bila kuongea chochote Dokta Simon aliingia ndani ya gari mpaka hospitalini, hakua na chaguo lingine zaidi ya kuandaa chupa yenye sumu kali sana na kuiweka ndani ya droo lake akisubiri usiku uingie ili amalize kazi yake.
KWA WATUMIAJI WA APP KUNA MATANGAZO YANATOKEA KWENYE APPLICATION YETU HIVYO UKIYAONA NAOMBA BONYEZA HAPO NDIO UNANIPA SAPOTI MIMI, UKIBONYEZA UNAWEZA KUCANCEL SIO LAZIMA UENDELE ULIKOPELEKWA, KIKUBWA UBONYEZE HATA MARA 2-3 KILA UKIFUNGUA APP YETU
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA