NIFANYE NAMIMI KAKA (12)

0
Mwandishi: Juma Hiza

SEHEMU YA KUMI NA MBILI
ILIPOISHIA...
“Hapana, uko wapi?”
“Niko nyumbani.”
“Mbona ulikuwa hupokei simu yangu?”
“Nilikuwa bize kidogo kwani kuna nini?”
“Kuna kitu nataka kukuambia.”

SASA ENDELEA...
“Niambie Eva.”
“Safi tu! Dick mzima wewe?”
“Mimi mzima hofu kwako.”
“Niko poa.”
“Unauhakika?”
“Ndiyo niko poa kwanini umeniuliza hivyo?”
“Hamna nimeuliza tu! kwani nimefanya kosa?”
“Hapana, uko wapi?”
“Niko nyumbani.”
“Mbona ulikuwa hupokei simu yangu?”
“Nilikuwa bize kidogo kwani kuna nini?”
“Kuna kitu nataka kukuambia.”
“Kitu gani?” nilimtumia ujumbe huu wa kumuuliza huku moyo wangu ukianza kuingiwa na hofu, nilikuwa katika hofu.

Nilianza kuwaza mambo mengi sana lakini kubwa ambalo nilikuwa nikiwaza ni juu ya hicho kitu ambacho alikuwa akitaka kuniambia kwa wakati ule. Ubongo wangu ukatengeneza tukio la haraka. Lilikuwa ni tukio kuhusu taarifa za ujauzito wa Evadia. Kwa kweli moyo wangu uliweza kupasuka sana hasa baada ya kuwaza hayo.

Hofu ilizidi kunitawala moyoni baada ya Evadia kuchelewa kunijibu ujumbe wangu, nilianza kuwaza mambo mengi sana ambayo kwa kweli yalizidi kunifanya hata ile furaha niliyokuwa nayo mwanzo ipotee na wakati huo nilikuwa nashahuku ya kutaka kuona kile ambacho alikuwa akinijibu. Nakumbuka nilikuwa nikizisoma meseji za Helena ambaye na yeye alikuwa akinisumbua, sikutaka kumjibu kwa wakati huo.

Niliamua kumpigia simu Evadia hapa ilikuwa ni baada ya kusubiria jibu bila mafanikio, alipopokea nikaanza kuzungumza naye.

“Kuna nini?” nilimuuliza baada ya kupokea simu, alikuwa kimya, hakuzungumza lolote.
“Evadia!” nilimuita lakini hakuwa akizungumza lolote, alibaki kimya na kuniacha nikizungumza mwenyewe kama mwendawazimu.
“Evadia mbona huongei sasa?” nilimuuliza tena, mara hii aliamua kunijibu.
“Kuna kitu nataka kukuambia,” aliniambia kwa sauti nyororo iliyosindikizwa na mpangilio wa maneno sawia ambayo yalinogeshwa na lafuzi yake nzuri isiyokera kuisikiliza.
“Kitu gani hicho?” nilimuuliza kwa sauti iliyoashiria kuwa na shahuku ya kutaka kufahamu hicho kitu kilichokuwa kinamtatiza.
“Dick unajua tangu siku ile ulipofanya na mimi mapenzi kiukweli hilo tukio nimeshindwa kulifuta kabisa kichwani mwangu, linanitesa sana nashindwa kusahau sijui kwanini?” aliniambia kisha akaniuliza swali la kimtego.

Kwanza ile hofu iliyokuwa imeanza kunitawala iliweza kutoweka, nilivuta pumzi na kuiachia huku moyoni nikianza kuingiwa na furaha, sikutakiwa tena kuogopa kwani kitu nilichokuwa nimeanza kukihisi kuwa kilikuwa kimetokea hakikuwepo kwa wakati ule.
“Kwanini umeshindwa kusahau?” nilimuuliza swali la kimakusudi kabisa.
“Sijui.”
“Nikuulize kitu?”
“Ndiyo niulize.”
“Ila utanijibu kama ninavyotaka?”
“Ndiyo nitakujibu.”
“Kwanza umenisamehe?”
“Ndiyo nimekusamehe.”
“Kwanini sasa uliondoka siku ile ukiwa katika hali ile?”
“Ni hasira Dick ila yameisha usijali kuwa na amani.”
“Sawa yani nilikuwa naishi kwa hofu sana.”
“Hofu ya nini?”
“Ya kukukosea halafu ukizingatia sikupanga kukukosea ni ibilisi tu! alinipitia.”
“Usijali Dick mimi nimekusamehe ila nataka tuonane kuna mambo muhimu nataka kuzungumza na wewe.”
“Mambo gani tena?”
“Usijali wala hakuna tatizo.”
“Nitaamini vipi kama umenitegea mtego je?”
“Hahahaha! Jiamini bhana hakuna tatizo bhana.”
“Sawa kwahiyo unataka tuonane lini?”
“Kesho uko free?”
“Ndiyo.”
“Basi nitakuambia kesho sehemu ya kukutana pamoja na muda.”
“Sawa kwahiyo hakuna tatizo kati yetu?”
“Ndiyo hakuna.”
“Sawa nafurahi kusikia hivyo.”
“Haya usiku mwema Dick.”
“Nawe pia mrembo,” nilimjibu na huo ndiyo ulikuwa mwisho wa mazungumzo yetu.

Niliitazama saa yangu ya mkononi, ilikuwa ikisoma saa nane za usiku, niliendelea kujibu jumbe za watu waliyokuwa wamenitafuta akiwemo Helena msichana ambaye alijirahisha sana kwangu mpaka pale ambapo sikumbuki muda wala dakika ambayo usingizi uliweza kunipitia.

Nilikuwa katika chumba kidogo sana kilichokuwa kina hewa nzito, wakati huo nilikuwa nimepiga magoti huku mikono yangu ikiwa imefungwa nyuma kwa kutumia kamba ngumu pamoja na miguuni. Pembeni yangu alikuwepo mwanamke mmoja ambaye na yeye alikuwa amefungwa kama nilivyokuwa nimefungwa mimi huku akiwa amepiga magoti.

Nilijaribu kumtazama sura yake ajabu sikuweza kumfahamu kabisa, alikuwa ni mwanamke mwenye sura ngeni machoni mwangu, sikumbuki kama niliwahi kumuona hapo kabla katika maisha yangu.

Nilipojaribu kutazama katika chumba kile niliwaona wanaume watatu wakiwa wametuzunguka, walionekana kuwa na hasira kali kupitia nyuso zao zilizokuwa zimejikunja kutokana na hasira waliyokuwa nayo. 

Nilikuwa nikiwatazama katika muonekano wa sura ya huruma lakini wale wanaume hawakuonekana kujali lolote bali ndiyo kwanza walikuwa wakianza kunipiga huku yule mwanamke wakimshika nywele zake na kuanza kuzivuta. Kilikuwa ni kitendo cha dakika chache sana kabla ya kuanza kusema lolote lile kwa wakati ule.
“Wewe ndiyo Dick?” aliniuliza mwanaume mmoja, alikuwa mweusi, sura yake ilikuwa na alama za vidonda ambavyo bado vilikuwa vibichi kabisa, alitisha mno kutazama, mkononi alikuwa amekishikilia rungu kubwa ambalo alikuwa akilipigapiga mkononi mwake huku akinitazama.
“Ndiyo….ni…ni mimi,” nilimjibu kwa sauti iliyochanganyika wasiwasi pamoja na uwoga.
“Mimi naitwa Kiziba a.k.a Mtoaji roho wa kujitolea,” alijitambulisha kisha akaendelea kuzungumza,
“Kwanini unatembea na mke wa mtu?” aliniuliza huku akianza kunizunguka pale chini nilipokuwa nimepiga magoti, wakati huo wale wenzake wawili walikuwa wakinitazama.
“Mke wa mtu?” nilimuuliza huku nikionekana kutofahamu lolote lile ni wazi kuwa kesi ile waliyokuwa wakinishutumu nayo haikuwa ikinihusu hata mara moja, nilihisi kuonewa sana.
“Unaniuliza eti! Mke wa mtu? Ina maana wewe hufahamu kama unatembea na mke wa mtu tena mtu mzito serikalini?”aliniuliza, safari hii alikuwa mbele yangu akinikodolea macho yake makali sana yaliyozidi kuniogopesha kwa kiasi fulani.
“Hapana sifahamu,” nilimjibu huku nikikitikisa kichwa changu kuonyesha msisitizo wa kauli yangu.
“Ati! Unasema hufahamu?” aliniuliza kwa ghadhabu huku akinizaba kibao cha uso, nilipepesuka lakini kama bahati sikuweza kuanguka kwani tayari nilikuwa nimepiga magoti chini, nilihisi kabao chake kikiniachia alama katika shavu langu. Machozi kwa mbali yakaanza kunilengalenga.
“Ndiyo sifahamu,” nilijibu kwa kujiamini kuonyesha kuwa hakukuwa na ukweli katika kile walichokuwa wakinishutumu nacho.
“Una uhakika?”
“Ndiyo nina uhakika asilimia mia moja.”
“Embu mtazame huyu mwanamke,” aliniambia kisha nikapata wasaa wa kuweza kumtazama yule mwanamke. Sura yake ilikuwa ngeni machoni mwangu. Ni kweli katika maisha yangu niliwahi kutembea na wanawake wengi sana na wote nilikuwa nikiwakumbuka lakini sura ya yule mwanamke ilionekana kuwa ngeni machoni mwangu.
“Unamfahamu huyu?” aliniuliza baada ya kuniona nikimtazama yule mwanamke ambaye aliniambia nimtazame.
“Hapana simfahamu,” nilimjibu lakini kabla yule mwanaume hajasema lolote mara nilipokelewa na sauti iliyoambatana na kilio cha yule mwanamke.
“Dick unanikataa unasema hunijui wakati kila siku tunakuwa wote, kwanini usikubali haya yote yakaisha, wametutesa sana, wametupiga lakini bado unakataa kwanini usiwe mkweli?” aliniambia yule mwanamke maneno ambayo yaliambatana na sauti ya kilio, alikuwa akilia machozi ambayo kwa kweli nilikuwa nikiyafananisha na machozi yale ya waigizaji wa bongo movie, hayakunigusa hata kidogo kwani mwanamke mwenyewe ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona.

Kitendo cha kuniambia yale maneno huku akilia kilinifanya nizidi kubaki katika wakati wa maswali nisijue nini nifanye kwa wakati ule kwanza nilikuwa nimefungwa kamba mikononi na miguuni hivyo ilikuwa ni vigumu kuweza kuamua lolote zaidi ya yote niliamua kuwa mpole wa kila kitu kilichokuwa kikiendelea ndani ya kile chumba kilichokuwa na hewa nzito sana.
“Kijana kwahiyo unatufanya sisi watoto wadogo?” aliniuliza yule mwanaume, wakati huo jasho lilikuwa likinitiririka, nilikuwa nimeloa mwili mzima kutona na jasho lililokuwa kininitoka kwa wakati ule. Uwoga ulianza kuniingia na kila nililokuwa natamani kuzungumza juu ya yule mwanamke nilishangaa kinywa changu kikiwa kizito mwisho nikabaki kimya nikisubiri hatma yangu.
“Mbona hujibu sasa au umeona umeshindwa?” alizidi kuniuliza maswali ambayo kwa kweli yalizidi kuniweka katika wakati wa kizungumkuti, sikuwa nafahamu lolote kuhusiana na yule mwanamke ambaye walikuwa wakidai kuwa natembea naye.
“Jamani mimi simfahamu huyu mwanamke kwanza nashangaa mnavyoniambia natembea naye wakati ndiyo mara yangu ya kwanza namuona hapa,” niliwaambia kwa pamoja huku macho yangu yakimaanisha kile ambacho nilikuwa nikikizungumza.
“Dick unanikana, unanikana Dick kwanini lakini unanifanyia hivyo?” aliniuliza yule mwanamke swali ambalo sikuweza kujua natakiwa nimjibu katika mtindo upi. Nilibaki nikimshangaa nisijui ni lipi jibu sahihi la kumjibu.
“Kijana naona unacheza na akili zetu,” aliniambia Kiziba halafu akawatazama wale wenzake kisha akawapa ishara fulani ambayo iliashiria kufanya kitu walichokuwa wamekidhamiria.

Niliwaona wakimsogelea yule mwanamke ambaye hapo mwanzo walidai kuwa ni mke wa mtu kisha wakatoa bastola na bila kuchelesha muda walimpiga kichwani, damu zikaanza kusambaa mahali pale.

Baada ya kuhakikisha wamemuua yule mwanamke sasa waliamua kunigeukia, kimoyomoyo nilikuwa nimeanza kumuomba Mungu Wangu kwani niliamini zilikuwa zimebakia dakika chache za kuweza kuishi hapa duniani, nilihasa kuuhisi mkojo niliubana na kama masihara ukaweza kutoka wenyewe kwa wakati ule, nilijikojolea hapa ni baada ya wale wanaune kunifikia na kisha mmoja wao kuninyooshea Bastola katika paji la uso wangu.
“Sali sala zako za mwisho,” aliniambia kisha kilichofutia mahali hapo ni kuifyatua.

Niliamka katika ndoto hii ya ajabu, nikurupuka huku mapigo yangu ya moyo yakiwa yananienda mbio, sikuamini kama bado nilikuwa hai kwa wakati ule. Kitendo cha kushikiwa bastola tena katika mazingira yale hakika kiliniogopesha sana.

Nilibaki katika taharuki baada ya kufahamu kuwa kile nilichokiona ilikuwa ni ndoto, ndoto ambayo sikujua ilikuwa ina maana gani hasa. Sikutaka kuifatilia sana ile ndoto zaidi ya yote niliishika simu yangu na kutazama saa, ilikuwa ni majira ya saa mbili za asubuhi. Wakati nilipokuwa nimejilaza huku nikijinyoosha ghafla! simu yangu ikawa inaita, nilipoitazama alikuwa ni Evadia.
“Hallo Eva,” nilisema mara baada ya kupokea.
“Niambie Dick umeamka salama?” sauti nyororo ya Evadia kutoka upande wa pili ilinipokea kwa swali ambalo liliniondoa usingizi kabisa.
“Nimeamka salama kabisa,”nilimjibu huku nikijilambalamba lips kwa kutumia ulimi wangu, nilihisi kumtamani tena.
“Sawa basi baadae mida ya jioni tutakutana pale Mlimani City,” aliniambia.
“Kama kwenye saa ngapi?”
“Saa kumi na mbili.”
“Kwa wakati huo wewe utakuwa unatokea wapi?”
“Dukani.”
“Sasa si ungekuja kunipitia jamani?”
“Ok basi ikifika mida hiyo mimi nitakuja hapo kukupitia ila tu naomba uwe tayari sitaki nije hapo halafu nianze kukusubiria sawa?”
“Usijali nitakuwa tayari nakusubiria.”
“Sawa,” alinijibu kisha akakata simu.

Nilianza kuisahau ile ndoto ya kutaka kuuliwa na sasa nikaanza kuifikiria hiyo jioni itakuwaje, kuna muda nilihisi kama masaa yalikuwa yamesimama kwani ndiyo kwanza yalikuwa ni majira ya saa mbili za asubuhi. Niliamua kumtumia ujumbe mfupi Helena kama salamu hapo nakumbuka tayari nilikuwa nimemtumia Precious ujumbe wa asubuhi njema na aliweza kunijibu.

“Poa mzima uko wapi?”aliniuliza Helena kupitia ujumbe mfupi aliyokuwa amenitumia.
“Niko geto hapa.”
“Hutoki?”
“Hapana leo nipo tu nitaandika Chombezo ila jioni ndiyo nitatoka.”
“Utaenda wapi?”
“Kwa marafiki zangu.”
“Anha!”
“Njoo basi.”
“Nije nifanyaje?”
“Unisaidie kufua nguo.”
“Kwanini usimpe mpenzi wako akufulie?”
“Nimpe mpenzi wangu yupi wakati mimi niko na wewe.”
“Mmmh! Wewe muongo unanidanganya.”
“Nakudanganya na nini?”
“Yani ulivyo na mashabiki wengi hivyo katika Machombezo yako ukose mpenzi kweli?”
“Kwahiyo huniamini?”
“Nakuamini Baby.”
“Ila.”
“Hamna.”
“Njoo sasa unisaidie kufua.”
“Basi nakuja si hapo kwa Tumbo?”
“Ndiyo.”
“Haya ngoja basi nimalizie kufanya usafi halafu nije mpenzi.
“Haina shida.”

Kitu cha kushangaza sikuwahi kumtongoza kabisa lakini tayari alikuwa akiniita majina ya kimapenzi, ni wazi kuwa alikuwa akinipenda sana , nililifahamu hilo na sikutaka nililazie damu, nilichoamua kukifanya ni kumuita na siku hiyohiyo nilipanga kusafiri naye kwenda katika mji wa mahaba nigaragaze.

Nilianza kuisahau ile ndoto ya kutaka kuuliwa na sasa nikaanza kuifikiria hiyo jioni itakuwaje, kuna muda nilihisi kama masaa yalikuwa yamesimama kwani ndiyo kwanza yalikuwa ni majira ya saa mbili za asubuhi. Niliamua kumtumia ujumbe mfupi Helena kama salamu hapo nakumbuka tayari nilikuwa nimemtumia Precious ujumbe wa asubuhi njema na aliweza kunijibu.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA KWENYE APPLICATION YETU HIVYO UKIYAONA NAOMBA BONYEZA HAPO NDIO UNANIPA SAPOTI MIMI, UKIBONYEZA UNAWEZA KUCANCEL SIO LAZIMA UENDELE ULIKOPELEKWA, KIKUBWA UBONYEZE HATA MARA 2-3 KILA UKIFUNGUA APP YETU

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)