Notifications
  • MY DIARY (9)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TISATULIPOISHIA...Basi Dj wangu aliendelea na mautundu yake akaniwekea mambo ya pwani na hapo ndipo uvumilivu ulipomshinda akaja kunibambia na mimi sikuona haja ya kumbania kwa kuwa ni mali zake mwenyewe. Nilizungusha nyonga na kiuno mpaka nikachoka nikajitupa kitandani ili nipumzike. Nafsi yake ilikuwa imeridhika kwani hakutka tena penzi bali alichukua lap top yake na kuanza kunionesha picha na vitu vingine ambavyo vilinipa raha.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (8)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NANETULIPOISHIA...Sijui hata haya maneno yalitoka wapi, fahamu zilinitoka na Ticha aliamua kuninyanyasa maana nilishajikojolea zaidi ya mara tano. Basi na yeye kwa kutafuta mbwembwe alianza yale mambo yao ya katerero, siunajua tena mwalimu John alitokea pande za Bukoba.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinichezea sana na baadaye nilishangaa kukuta jamaa ameshaingiza kunako. Sikujielewa kwa…
  • MY DIARY (7)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SABATULIPOISHIA...Kwaito zilivyonoga uzalendo ulinishinda nikajikuta na mimi nashuka ngazi kuelekea chini sehemu ya kuchezea.Nilizijua kwani shuleni tulikuwa tunazicheza sana hasa kwenye yale madisco yetu ya mwisho wa mwezi.John wangu alibaki juuu akiniangalia jinsi nilivyokuwa nikicheza vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yeye alishindwa kushuka akiofika kile kitu kukaliwa na watu…
  • MY DIARY (6)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SITATULIPOISHIA...Akanambia kuwa wamemwambia wapo East Africa Pub na tayari wamaeshaagiza mkuu wa mbuzi. Mmmmhhhh kusikia mguu wa mbuzi mate yalinijaa mdomoni. Basi kwa harakaharaka nikamwambia naomba niende niende nyumbani nikachukue viwalo vya club kisha nitawakuta hapo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinambia mbona hizo nguo ulizofaa zipo poa tu wewe twende hivyo bhana si upo na…
  • MY DIARY (5)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TANOTULIPOISHIA...Akanisimamisha na kuanza kuiuliza maswali mengi yasiyo na maana huko akionekana kutojiamini. “samahani dada, sijui unaelekea wapi”? Nikamjibu dukani. Akavuta pumzi ndefu na kuniambia ok, nisaidie namba zako za simu. Nikamwangalia juu na chini nikwambaia nimezisahau na simu nimeiacha ndani nikirudi ndani nitakuletea..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Akaishiwa pozi akanambia,…
  • MY DIARY (4)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NNETULIPOISHIA...Uchambuzi huu ulinigusa sana kwani hata mimi nilijihisi kuwa sikuwa na utando huo yaani bikira japo nilikuwa sijawahi kujamiana na mwanaume wa aina yeyote zaidi ya ile michezo ya utotoni ya kula mbakishie baba au ile ya kibabababa na kimamamama. Alianza kunishika mapajani na kunifanya nianze kusisimuka ajabu kwani japo alikuwa ni mwanaume mikono yake likuwa ni milani sana kama ya mtoto wa kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media…
  • MY DIARY (3)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TATUTULIPOISHIA...Nazani sasa unanielewa ninaposema nilikuwa sina ndugu kwani baba yangu hakuwa na ndugu yeyeote zaidi ya marafiki ambao na wao kwa sasa ndio hao wameshagawana mali zote. Nimebaki mimi na dunia yangu hivyo basi nilimwomba rafiki yangu wa kufa na kuzikana kwa jina Joyce anisaidie kunisitiri nyumbani kwao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Likizo ilipoisha tulirusi shuleni na…
  • MY DIARY (2)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA PILITULIPOISHIA...Kwa ufupi japo sitaki kueleza historia yake ila kwa sasa ni shoga na teja. Baba yetu alitupenda sana na alihakikisha tunapata elimu nzuri na bora. Mimi na kaka yangu wote tulisoma International school ya hapo Moshi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baadaye kaka yangu alianza kuvuta bangi kitu ambacho kilimtia hofu baba yangu na kuamua kumpeleka kusoma nje ya nchi.Alikosea sana…
  • MY DIARY (1)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KWANZANilikuwa juu ya jukwaaa nikifanya vitu vyangu ili hali nikijua kabisa watu wote waliokuwa wakinitizama walikuwa wanaumia roho kutokana na mvuto wa umbo langu niliokuwa nao. Nilisikia mijibaba miwili ikiulizana hivi lile wowoo ni la kwake au ni la mchina? Mmoja wao akaropoka “wee kitu original hicho,kwani umemsaahau huyu binti tulishakutana nae kule Arusha mpaka tukambatiza jina la soda kubwa tena ya fanta yaani BAMBUCHA.?” Yeah nimekumbuka alidakia…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (18)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA NANETULIPOISHIA...“Mamaaaaaaaa!” Anna akapiga kelele na kutereza vibaya, miguu yake ikaliacha daraja, Seidon akawahi kukaza mikono na kumzuia, lakini miguu yake tayari ilikuwa imeacha daraja na sasa ikining’inia chini ya daraja. Anna akalia kwa uchungu sana, akijua kuwa mwisho wake sasa umefika.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“Jipe moyo Anna, tumefika mwisho sasa,” Seidon…

WEKA YOTE (17)


JINA: WEKA YOTE
Mwandishi: Gaooh Musah

SEHEMU YA KUMI NA SABA
ILIPOISHIA...
Baada ya kumpoteza porini ndio nimetafuta njia ya nyumbani kisha nilitokea barabarani niliifata mpaka kufika hapa, nako ilinibidi nilale nje tena chini baada ya kujua geti limefungwa ndio asubuhi nimeingia ndani baada ya kusikia mlango umefunguliwa, kufika hapa ndio tunakutana."

TUPATE BURUDANI KIDOGO KISHA TUENDELEE

SASA ENDELEA...
Nilihitimisha uongo wangu, ambao niliupa taswira kama ni ukweli.

"Haaah,pole mwanangu kumbe umepata tabu yote hiyo pole sana"alizidi kunipa pole akionekana amehuzunishwa na tukio lile.
Nilijipongeza kwa kuongea uongo ule uliomfanya shangazi aniamini.
Baada ya maongezi kufika tamati nilingia chumbani nikisubiri chai ninywe, shangazi nae akibaki pale sebuleni.
Nilitoka ndani na kuelekea meza ya chakula na kujilia mikate kadhaa na chai ya maziwa vilivyozidi nipa nguvu.

Siku hiyo ya jumamosi iliisha vizuri tu,nikionekana mpole isivyo kawaida yote ni kuwa na tahadhali juu ya shangazi asijenifukuza.
Muda ukikimbia kama umeme mpaka usiku unafika tunakula kisha nikaekekea chumbani kwangu kulala, nikiutafuta usingizi kila nikiutafuta unakataa kuja, hali iliyopelekea nijitokee tu kutizama runinga.
Nilikuwa peke yangu, natizama tv niko makini mara nashangaa nimekaliwa na neema sikumuona alivyokuja nilishangaa kanikalia na nguo yake ya kulalia iliyoacha wazi mapaja yake hasa upande wa nyuma kutokana na kupandishwa na kitonga alichofungasha............

************************

Nipo nyumbani kwa yule ambaye hata jina lake lilishanitoka kutokana na kutokumuona muda mrefu, Baada ya kumtafuta kwenye simu na kutaka nikamuone, na kweli nikaenda bila kipingamizi mapaka kufika kwake na kuingia alinikaribisha kistaarabu nikaingia kama kwangu kisha alienda moja kwa moja kuniretea kinywaji ambacho nilikipokea kinadhifu kisha nikaanza kukinywa huku tukipiga story nabkucheka dakika kadhaa mlango ulifunguliwa na kuingia mwanaume aliye jazia misuli yake, hapo dada yule alipomuona alishtuka...

alinishangaza nisijue sababu iliyomfanya ashtuke.
"Habari zenu."ilitoka sauti nzito ikitusalimu, ambayo mimi niliitika ila dada yule hakuitika.

"Si nakusalimia mbona huitiki, ahaa kumbe tabia zako kuingiza mabwana zako mimi nisipo kuepo"alisema jamaa yule hapo akanitia woga, kibaya zaidi alikuwa anakuja kule tulipokaa huku mikono yake ikiwa mifukoni.

"Hapana mume wangu, huyu ni mdogo wangu tu"alizidi kumhanya hapo mimi nikiwa sielewi kinachoendeleaa, nilitaka kuamka niondoke baada ya kuona mambo yamekuwa mambo jamaa amejasirika vilivyo.

"Unaenda wapi, unaenda wapi, unaenda wapiii eeh"alinikamata mkono baada ya kutaka kuondoka nilipona moto umewaka, nilikosa cha kujibu baada ya kunidaka mkono huku akinitaka niseme ninapoenda, nikiwa nimezubaa.

"Si nakiuliza eeh"aliongea kwa jazba na kunipiga kelebu juu ya shavu langu.

"Mume wangu usimpige, usimpige"alinitete yule dada ila ikawa kama kachochea moto uliokaribia kuzimika.

"Usiseme malaya wewe, kipi unakosa kwangu mpaka utembee na watoto kama huyu, yani mnafanya kucheka cheka ndani kwangu huku mkishikana shikana."alizidi kusema jamaa yule.
Huku amefura vya kutosha hata uso umeweka mipindo pindo, hakutaka kuniachia kabisa pamoja na kunitandika kelebu juu ya shavu langu.

"Mume wangu huyobni rafiki tu jamani muache usimpige."alizidi kunitetea dada yule.

"Wee, nyamaza ngoja nimuoneshe"alinitisha na kunitandika kofi sasa zito.

"Bro nisamehe kaniita mwenyewe."

"Unasemaje, nyamaza unajua ukimuona anapendeza ndivyo alivyo zaliwa jua ni matunzo, yangu sawa leo nakufundisha"alisema huku akiipekua sarawili yake kuutoa mkanda kisha kunivutia pembeni,Mke wake aliamka kutetea ila nae aliambulia kipigo,na kukaa kando akiangalia tu mchezo.
Alinitight mimi vizuri kisha kunishushia vilivyo mikanda isio na idadi huku akinionya.

"Kaka nisamehe mbona unazidi kuniumiza, nisamehe."

"Nyamaza boya wewe unajua napoteza kiasi gani kumpendezesha mpaka wewe uje kumtumia tu bure, alaah nakupa fundisho"alinikomalia akiwa tayari amesha nisurubu
Na bado hakulizika aliachana na mkanda kisha kuanza kunitupia ngumi,nilijifanya najua kupigana eti nazuia ilikuwa kama kosa alinidaka vyema shingoni kisha ngumi za mbavu kuanza ambazo zilinitoa machozi.
Nakuanza kulalamika yule dada aliamka ilikuja kumzuia asiendelee niumiza lakini aliambulia kofi ambalo lilimpeleka chini sambamba na kudondokea mgongo hadi kutoa ukelele wa maumivu, hakumjali nilipata maumivu ambayo nilishindwa kujitetea kabisa na kipigo kile.

"Utanijua leo kama mkuliya ni nani"Alinishangaza aliposema yeye ninmkuliya hapo nikambuka rafiki yale maneno yankuwa wakulya hawana huruma, sasa nilifikili huyu ataniua hivyi nilichoona hata msamaha sio chochote, aliniamsha pale nilipo anguka chini na kuniegemeza ukutani huku akiendelea kunishushia kipigo bahati mbaya sarawili yake ilikuwa mbioni kumdondoka baada ya kuitoa mkanda hivyo ilimbidi aniachie ilikuizuia sarawili yake, hapo ndio nilipata penyo nilichomoka haraka kuukimbilia mlango kea dhumuni la kutoka nje haraka nikiea mbioni kukimbia kumbe na yeye aliniwahi na kurusha teke lililo nisindikiza nje moja kwa moja nilitaka kudondoka ila nilijizuia haraka nikaondoka mbio mbio na maumivu yangu.

Nilijihisi mwana masumbwi anaekaribia kufika tamati kisha mpinzani wake akiwa sambamba na yeye hapo lazima mbio zizidi, ndivyo ilivyokuwa kwangu nikijiona nimeponyeka chupu chupu mikononi mwa mkuliya neno msamaha asielijua maishani mwake.
Nilipotea eneo lile hatabile nyumba nilikuwa mbali nayo, nikaanza safari ya kuelekea kituo cha karibu cha magari nilipanda baada ya kukuta gari linalo ngoja abiria.
Nikiwa garini nimekaa mwili umechoka kwa kipigo hata vazi langu hasa shati lilikuwa na mikunyo ya mikono aliyokuwa akinikunja.

"Kaka, kaka vipi."iliita sauti ya kike, sikutaka hata kugeuka nikiona itakuwa najisumbua, nilichokuwa nafikilia nikufika nyumbani, dada yule hakukoma kujiita yani kweli Zz"USILOLIJUA SAWA NA USIKU WA GIZA"sikumsikiliza dada yule aliekuwa anaichosha sauti yake kwa kuniita nikisahau msemo wa KUBALI WITO KATAA MANENO"nilimpotezea mpaka gari inasimama kituo ninachoshuka hata ile nataka kushuka alinizidi kuniita ila niliona ananisumbua akili yangu haikuwa pale, nilimfikia konda alietaka tozo lake la nauli hapo ndio nikaingiza mkono mfukon, nilishangazwa mana kulikuwa patupu.

"Oya lete pesa hiyo unatucherewesha"aliongea konda,nilishangaa peke yangu mana pesa ilikuwa mfukoni kisha nisiione, Lilikuwa jambo la ajabu, ila nilikosa jibu baada ya kukumbuka tukio la masaa kadhaa na yule mkulya aliekuwa akionesha umwamba wake mwilini kwangu.
Nikiwa katika harakati za kurudia kuitafuta pesa ikiwa tayari jibu ninalo kuwa pesa haipo.
Nilishangaa shangaa huku konda akilalamika nampotezea muda mpaka akanisaidia kutafuta, ndipo akaja mdada.

"Kaka, mambo pesa zako ulizidondosha kwenye gari nimekuita hukunisikia."ni sauti nadhifu ilimtoka dada yule, alieonekana mpole kupita kiasi hapo nilimshukuru sana ama kweli "USIMDHARAU USIE MJUA."nikidharau aliponiita ila kumbe hakuniitia kibaya,nilimkabidhi konda nauli yake na yule dada kuingia ndani nikimsindukiza kwa macho tu, baada ya gari kujaza abiria likaondoka na mimi kwa woga nikaanza kukipitisha pitisha kwenye vichochoro nisikitane na halaiki ya watu wakanicheka kea muonekano wangu.
Nilitembea dakika kadhaa nikaifikia nyumba yetu, nikaingia haraka haraka kwa makini break ya kwanza ilikuwa mlangoni kuingia sebuleni.
nilipita kwa kunyata baada ya kuwaona Doreen na Careen, wamekaa pale nilichepuka haraka mpaka chumbani kwangu walichosikia ni kubamizwa kwa mlango wangu wa chumbani.

Nilipoingia nikaufunga vizuri.
Na kutulia nikiwa ndani, nikiugulia maumivu ya mwili ambayo wakati huo ndio niliyasikia vizuri kila mahali palipo pitiwa na kipigo palianza kuuma.
Niliona sina cha zaidi ya kulala tu.
Kutokana na kuchoka kwa mwili nikajikuta ninalala muda mrefu sana kiasi kwamba nikapitiliza mpaka saa tatu usiku nikipostuka kwa kung'atwa na mbu.
Hapo ndio nikaamka,moja kwa moja nilitika nje tumbo jepesi halina kitu ndani.

"Haah wewe gao ulikuwa wapi."ni sauti ya kushangaa alionishangalia Neema akiwa na wenzake, katika ile meza ya chakula sikujibu swali lake zaidi ya kusogea pale wa lipo na kukipakulia chakula bila kuongea na mtu nikionekana mnyonge.

"Gao unanini mbona umechoka hivyo."aliuliza mmoja wao ambaye sijaangaika kumjua ni nani, zaidi ya kuendelea upakuzi kisha nilipomaliza nikaanza kula, Nilihitimisha ulaji ndipo nikanyanyua kinywa kuongea.

"Nimechoka leo nilikuwa nimelala, careen naomba unifulie kesho shule."nilitoa agizo.

"nishafua tayari, gao nimepiga nitazipiga pas pia."alisema careen,hapobnikashikuru na kurudi chumbani kujiandaa kwa ajili ya kuelekea bafuni kuoga, sikuongea na wakina neema wala Ester alievuta mdomo pale aliponiona nilijua fika ni kutokana na kugoma kumpa alichotaka.
Nilivaa taulo na kuingia bafuni nilipooga haraka haraka, ili kuwahi kulala mwili hauna nguvu.
Nilipomaliza kuoga nikawahi ndani kulala hata shangazi sikukumbuka kuuliza kama yupo, sikuwa na muda huo zaidi ya kujisikiliza maumivu tu.
NIlipo ingia ndani kwangu nilijikuta narukia kitanda kivivu kama mzigo wa viazi uliotupwa chini baada ya mbebaji kuchoka kuubeba.
Nilijisindikiza na mikono kidha hapo hapo, usingizi ukanijaa nililala kabisa, kikapita kimya kirefu nikikoroma tu.

Mpaka kunakucha siku hiyo ilikuwa tofauti kutokana Ester kutokuniamshabikiwabkawaida yake ni kuniamsha, nilijua kisirani chake hata siku mfikilia sana nikaamka na kujianda nguo zangu nilizikuta mezani nikazichukua kisha nikaingia ndani kuzivaa mwishowe safari ya shule ikaanza, nilitembea mita kadhaa bado mwili haupo sawa umechoka choka niliingia tayari shule baada ya kufika.
Tulihesabiwa na kwenda kwenye maeneo yetu ya usafi sikukutana n frank wakati huo, sijamuona nilijua hakufika bado hivyo niliendelea na usafi mpaka kengere ya paredi ikagongwa kisha tulipo kaa paredi tukaruhusiwa kuingia darasani huko ndio ilikiwa kasheshe mana nilielekea chooni au lugha nyengine msalani, nilipopita kule nyuma nilishangaa Grace kunifata na kunikumbata huku akilia kabisa tena alivyonikumbata baadhi ya machozi yalinidodea kifuani hata nilipojaribu kumuliza amepatwa na nini aliendelea kulia tu...............

Kitendo kilebkilinishangaza vya kutosha na kushindwa kupata tafasiri kamili ya kilio cha Grace.

"Grace unalia nini naomba unambie jamani,kipi kinakuliza."

"Gao acha tu yani sijui wanaume mpewe nini,aah najuta"alisema grace hapo kidogo picha ilinijia,na kujua fika ni mapenzi hayo ndio yanamsumbua japo sijajua kwa kina tatizo lake ila nilihisi tu kutokana na maneno yake.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

ENJOY WAKATI UKISUBIRI MUENDELEZO, SUBSCRIBE KAMA HAUJAJIUNGA NA CHANNEL YETU

Subscribe channel hizi ili usipitwe na video za Vichekesho


28 Simulizi Weka Yote
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni