Notification
Tidak ada notifikasi baru.

SORRY MADAM (42)

SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
ILIPOISHIA...
“Mungu wangu PCB wewe....Mbona unaonekana kama HKL?”
“Hahaa PCB halisi...Aafu mbona ndege leo imetua kwenye uwanja wa Maputo international airport imekuwaje kutokana tumetua Mozambique?”

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
“Ndege ilipata itilafu kwa watu kama sisi tunao jua ndio tumegundua hilo ila ukiwa ni mgeni huwezi kujua kama ndege imeshindwa kuendelea na safari”
“Sasa si wangetulipa fidia kwa kwa abiria inakuwaje ndege inakuwa haina uwezo wa kumaliza msafara wake?”
“Mimi niliamua tuondoke kutokana wewe umeseme unahitaji kumuona mama yako ila kwa walio baki wakisubiria ndege kutengenezwa watakuwa wamelipwa fidia na kama siku ukiondoka utakwenda kupanda ndege uwanja wa kimataifa wa Cape town”
“Sawa”

Safari ya kwenda hospitalini haikuchukua muda sana hii nikutokana na wingi wa barabara nyingi zinazo punguza msongamano wa magari.Tukafia hospitalini na moja kwa maja Emmy akaenda kwenye katabu kinacho onyesha orodha ya wagonjwa waliopo hapa hospitalini na nikamtajia jina la mama kishha akatumi kama dakika tano kulitafuta na akalipata

“Kumbe mama yako ni waziri?”
“Ndio”
“Twende ukamuone”
“Moja kwa moja tukealekea kwenye chumba alicho lazwa mama na kabla hatujaingia nikamkuta askari mmoja akiwa amesimama nje ya chumba alicho lazwa mama
“Hamuruhusiwi kuingia humu ndani nyinyi ni kina nani na munahitaji nini?”
“Mimi naitwa Dokta Emmy Samson na mfanyakazi wa hii hospitali”
“Naomba kitambulisho chako”

Emmy akatoa kitambulisho chake na kumpa askari aliye simama mlangoni na akakisoma kwa muda kisha akamrushu Emmy kuingia ndani na mimi nikataka kuingia ndani ila akanizuia kuingia
“Na wewe ni nani?”
“Mimi ni mtoto wa huyo mama huko ndani?”
“Mbona hatuna maelezo ya aina yoyote kuhusiana kama mgonjwa ana mtoto?”
“Mimi ni mwanaye unadhani nitafunga safari kutoka Tanzania hadi hapa nije kujipendekeza kwa mama yangu?”

Nilizungumza kwa hasira kiasi kwamba watu walipo karibu na eneo la mlango wa kuingia kwenye chumba alicho lazwa wakaanza kunishangaa
“Eddy kuwa mpole ngoja nikamuone mama”
“Kijana ninakuoma usimame mbali na hili enoa la sivyo nitakuitia walinzi waje wakutoe”
“Eddy tafadhali nakuomba uwe mpole nitazungumza na mama na utamuona tu”

Nijaitahidi kutulia hasira zangu na kusimama pembeni kidogo na chumba alicho lazwa mama huku sura yangu ni kiwa nimeikunja.Emmy akaingia ndani ya chumba na baada ya muda akatoka na kumnong’oneza askari kisha kwa ishara Emmy akaniita na nikanyanyuka kwa haraka hadi sehemu waliyo simama kisha askari akaniruhusu kuingia ndani.Macho yangu yakatizamana na mama ambaye kwa muonekana hali yake sio nzuri sana japo nimemkuta amaekaa kitako kwa mwendo wa haraka nikamfwata mama na kumkumbatia huku machozi yakinimwagika

Tukabaki tumekumbatiana na mama ndani ya dakika kadhaa kisha nikamuachia na kuiona sura yake ikiwa imelowana kwa machozi mengi,Mama akanishika mashavuni na kunibusu kwenye paji la uso huku akinichunguza sehemu mbali mbali za mwili mwangu na kunifanya nizidi kububujikwa na machozi
“Eddy ni nini kilicho kupata mwanagu?”

Mama aliniuliza huku akiwa anabubujikwa na machozi kiasi kwamba nikashindwa kulijibu swali lake hadi ndani ya dakika tano ndipo nikaanza kumuadisia kila kitu kilicho tokea na jinsi baba alivyo nifanyia kiasi kwamb hadi ninamalizia nikamshuhudia Emmy akiinama chini huku akitokwa na machozi.
“Eddy mwanagu nakuomba unisamehe”
“Nikusamehena nini mama?”
“Eddy najua siku zote ulikuwa unahitaji kujua ukweli juu ya baba yako na mimi nikawa nimekuficha ila....”
“Mama nimesha lijua hilo kuwa pacha wa baba ndio baba yangu”
“Nani amekuambia hivyo?”
“Mama dunia haina siri tena hili swala nimeambia na mtu baki kabisa tena ni muandishi wa habari”
“Basi Eddy tuliache hilo mwanagu kwa maana unazidi kunipa uchungua katika hilo”

Ikanibidi nibadilishe mada ya kuzungu na kuzungumza na kuanza kupiga story za kupoteza mawazo hadi mama na Emmy wakaanza kucheka ila sikumuambia mama kuhusiana na swala la shule yetu kuingia kwenye matatizo.
“Emmy hapa ni wapi kwenye choo?”
“Ukitoka hapo nje mkono wako wa kushoto utaona milango miwili imeandikwa toilet”
“Ahaa powa”

Nikatoka nje na kumkuta askari akiwa amesimama mbali kidogo na chumba akizungumza na simu akionekana akiwa na mazungumzo ya siri ikanibidi kulitega sikio langu kwa umakini kusikiliza ni kitu gani anacho kizungumza
“Ndii si nimrefu kiasi na mwili wake umejazia kidogo?”
“Basi amefika hapa kama lisaa lililo pita”
“Amekuja na mwanamke fulani ambaye hapa ni ndakatari”
“Basi panda ndege uje kwa maana inavyo onekana mipango yote itakwenda kuharibika”
“Sawa Mr Godwin”

Nikajikuta hata hamu ya kwenda kujisaidi haja ndogo ikakata na kabla hajaguka nikaingia ndani huku nikiwa ninawasiwasi hadi mama akanigundua kwa haraka
“Una tatizo gani mwanangu?”
“Mama hivi huju mlinzi mumemtoa wapi?”
“Kwa nini?”
“Wewe nijibu?”
“Huyo amekwa na ubalozi wa Tanzania uliopo hapa nchini”
“Unauhakika kweli ni mwema?”
“Ni mwema kivipi?”
“Au kuna siku ambayo baba alisha wahi kuja hapa”
“Hajawahi kuja hapa na wala hatambui kama nipo hapa”
“Sawa”

Nikatoka nje na kumkuta mlinzi akiwa amesimama kwenye sehemu ambayo tulimkuta kwa mara ya kwanza na akaniangalia kwa jicho la kuiba na mimi moja kwa moja nikaelekea chooni na kumaliza haja yangu kisha nikarudi huku moyoni mwangu nikiwa na wasiwasi kiasi kwamba nikakosa amani kabisa ya kukaa ndani ya chumba alichopo mama na Emmy.
“Emmy nakuomba mara moja nje?”
“Kwema?”
“Kwema tuu wewe ninakuomba”

Emmy akatoka na nikamshika mkono hadi sehemu iliyo tulia ambayo si rahisi kwa askari kuniona
“Hivi tunaweza kumuhamisha mama hospitali?”
“Kwanini?”
“Nijibu kama kuna uwezekano wa mama kuhamishwa hospitali ua hakuna?”
“Uwezekano upo ila ni hatua zahadi yeye kuhamishwa kwenda hspitali nyingine ni ndefu kwa maana hapa ameletwa na serikali ya Tanzania....Ila ni kwanini unahitaji ahamishe kuna nini?”
“Nafsi yangu imekosa amani kabisa juu ya mama kuendelea kuwa katika hospitali hii”
“Wasi wasi wa nini wakati hapa maaskari wamejaa wengi na hakuna mtu atakaye weza kumdhuru mama na mimi leo nitakaa naye siku nzima humu ndani”
“Emmy ninaamini hujui kwa undani hali ya familia yangu pale umesikiliza mamaneno machache wewe mwenyewe umejikuta ukitokwa na machozi sasa sihitaji uweze kulia zaidi ya pale ulivyo kuwa unalia?”
“Kwa nini unakuwa unananificha kwa kitu ambacho wewe unakihisi?”
“Kwa sasa huwezi kunielewa ila utanielewa”

Nikaachana na Emmy na kwenda chumbani kwa mama na kumkuta akiwa anazungumza na madakatari wawili ambao wamejifunga vitambaa vya kijani usini vinavyo fanana na nguo zao walizo zivaa baada ya kuniona mimi wakaniomba nisubiri nje kwa muda.Kusema ukweli nafsi na moyo wangu vikajikuta vikishindwa kuchukua maamuvu ambayo madakatri wameniomba nitoke.Emmy akaingia na akaonekana kuwashangaa madaktari hawa ambao wamejifunga vitambaa jambo ambalo ni tofauti sana kwa madaktari tunao waona kwenye hii hospitali wakiwa wameziacha sura zao wazi
“Nyinyi ni kina nani?”

Madaktari wakatazamana kisha mmoja akajikoholesha kisha akaanza kuzungumza kwa sauti ya kujiamini
“Sisi ni madakatari maalumu tumetumwa na serikali ya Tanzania kuja kuzileta dawa ambazo zinamsaidia muheshimiwa waziri katika kupona”
“Ngoja mumesema kuwa mumetoka wapi?”
“Tanzania?”
“Dawa mumetumwa na nani?”
“Na wizara ya afya”
“Hivi nyinyi kama hizo dawa mungeziona zina faida sana si munge mpa mama yangu tangu siku akiwa yupo Tanzania akiwa anaumwa”
“Hizi dawa kwa hapa hatuna tumeziacha ofisini”
“Basi nendeni mukazilete”

Madakatari wakaanza kubabaika kiasi kwamba sote tukabaki tukiwatazama kwa macho makili na hata walivyo toka hawakuga kiasi kwamba wasiwasi wangu ukaanza kupata jibu kwamba kuna mkono wa baba katika swala hili.
“Mama ninahitaji tuhame hospitalini kwa maana baba anatufwatilia na nisipo angalia ninaweza kufa”
“Kweli mwanangu?”
“Basi ngoja nikaonane na daktari mkuu nitakuja muda sio mrefu”
Emmy akatoka ndani ya chumba na kutucha mimi na mama huku akili yangu ikiwa na kazi ya kupanda nini cha kufanya kuweza kumtorosha mama katika hospitali hii.Baada ya nusu saa Emmy akarudi akiwa ameongozana na daktari mmoja wa kuzungu ambaye ni mtu wa makamo.
“Mama huyu ndio mkuu wangu wa hapa kazini”

Daktari mkuu akaanza kutupa mipango ya kufwata ili tuweze kumuhamisha mama katika hospitali hii jambo ambalo kwa mtazamo linachuku muda mrefu wa siku kama mbili kwani nilazima kibali kiweze kutoka katika serikali ya Tanzania na kipitie katika ubalozi wa Tanzania ndipo mama aweze kuhamishwa
“Basi tutabubiria hadi kesho”
“Mama Hadi kesho una uhakika na kitu unacho kizungumza?”
“Eddy kila kitu kinakwenda kwa mpangilio wa kiserikali na ukisema uende wewe kama wewe itakuwa ni shida kumbuka kuwa mimi serikalini nina mamlaka na ninachukuliwa kama kiongozi kwahiyo nakuomba uwe mvumilivu mwanangu”
“Mama..”
“Eddy nielewe......Sawa daktari nimekuelewa nyinyi fanyeni hizo hatua na mukihitaji msaada wangu tutashirikiana”
“Sawa”

Emmy na daktari mkuu wakatoka nje na kutuacha mimi na mama huku nikiwa ninamipnago mingine ya kuto kumshorikisha mama.Emmy akarudi ndani na kukaa pembeni ya kitanda alicho lala mama
“Eddy unaoenekana wewe ni mbishi sana”
“Huyo mwanangu nimesha mzoa ila ana ugonjwa wa hasira kiasi kwamba akiwa anabishana na mtu huwa hapendi kushindwa”
“Mama achilia na ugonjwa wa hasira ila kuna hatari ipo mbele yako sasa nyinyi endeleni kuniona kuwa mimi sifai”

Tukaendelea kukaa hadi mida ya saa moja usiku nikamuomba Emmy kunielekeza ni wapi ninaweza kupata sehemu yenye benki ya Backryas na akanielekeza na haikuwa mbali sana na sehemu hospitali ilipo
“Niwachukulie chakula gani?”
“Mimi nina chakula changu maalumu huwa ninaletewa na madakatari wa hapa?”
“Emmy?”
“Mimi niletee keki na soda ya kopa ya koka”

Nikatoka na kumkuta askari akiwa anatembea tembea huku na kule akionekana akisubiria kitu fulani kwa hamu
“Hivi zamu yako wewe inabadilika saa ngapi?”
“Nani mimi?”
“Kwani hapa nina ongea na nani?”
“Mimi zamu yangu inabadilika saa nne usiku”
“Ahaa powa”

Nikaachana na askari na kwenda sehemu aliyo nielekeza Emmy na kukuta ATM ya benki ya Backrays na kuchukua pesa kiasi zitakazo nisaidia katika matumizi madogo ya hapa Africa kusini. Nikaingia kwenye mgahawa uliopo karibu na hospitali na kuagizia chakula ambacho nitaweza kukila na nikatafuta sehemu ambayo ninaweza kuuona mlango wa kuingilia katika hospitli na kabla sija letewa chakula nikaona taksi ikiwa imesimama kisha nikamshuhudia baba akishuka ndani ya gari akiwa ameongozana na wanaume wawili na katika taksi nikamuona Sheila akiwa amekaa siti ya nyuma.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Simulizi Sorry Madam Z36
Jiunge kwenye mazungumzo (2)
Maoni 2
  1. Gendo
    22 Machi 2022, 14:00
    Profile
    Gendo
    Gendo
    Said: Story iko sawa kama vp tuendelee 43
    Story iko sawa kama vp tuendelee 43