ROHO MKONONI (10) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Ijumaa, 8 Julai 2022

ROHO MKONONI (10)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
πŸ“– KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
πŸ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
πŸ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa
Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA KUMI
ILIPOISHIA...
Baada ya Butu kutoka tu kichaa yule wa kike alimsindikiza kwa macho baada ya kupotelea mtaa wa pili,akawasiliana na Isack,kisha akanyanyuka,akabeba pochi lake moja chafu na kuelekea kunapo geti,tena alificha uso wake kwa mikono kusudi kamera za pale getini zisinase sura yake.

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
πŸ‘‰GUSA HAPAπŸ‘ˆ

SASA ENDELEA...
Alipofika getini akaingiza moja ya funguo alizokuwa nazo,akafungua na kuzama ndani,alitembea haraka haraka juu ya tails zilizopo chini mpaka katika mlango wa nyumba ya ndani,akaingiza pia funguo,akafungua,ile kuingia akakutana na sebule nzuri,akaifata korido,chumba cha kwanza akasimama akashika kitasa akakizungusha kikamtwii,akazama ndani!

Hiki ndicho kilikuwa chumba cha Butu cha kulalia macho ya kichaa yule yakadondokea katika kabati,kwa hatua za taratibu akalifata,alipolifikia akatia funguo kabati likafunguka...

Kwa sekunde kadhaa akabaki akitumbulia macho ndani ya kabati lile!

Nguo zilikaa shaghalabaghala bila hata kukunjwa,binti kichaa akatingisha kichwa kwa masikitiko,akafungua pochi lake chafu cha ajabu ndani palikuwa na pakiti kibao za unga zilizofungwa kidogo kidogo katika vipakiti wenyewe uhita kete,akavitoa na kuvisukumia chini kabisa ya nguo!.

Baada ya kukamilisha zoezi lake,binti akabeba pochi lake lile chafu akatoka ndani ya chumba kile,akafunga mlango kama alivyoukuta,akaelekea getini akafunga,akatoweka mtaa ule,akiacha hatari kwa Butu!
***
Isack alizidi mfatilia Butu,huku akizidi kuwasiliana na Zidu!

"Naona anaelekea uwanja wa ndege mkuu!"

Akazidi kumjulisha!

"Ahaaa sawa,atakuwa anataka kwenda kuonana na wale watu wetu ngoja niwajulishe watoke pale kabisa,kingine badgal kashafanya yake ivyo akirudi home tu dogo hana uhuru!"

Isack alimuelewa Zidu alimaanisha nini,alimuaga akakata simu!

Safari iliendelea mpaka uwanja wa ndege wa Dia,Isack akapitiliza,kazi yake ilishaisha,maana kama angeendelea kumfatilia lazima Butu angemtilia mashaka na kitu hiki akikutakiwa!.

Butu alizikumbuka sura za wale wafanyakazi wa tano alowakamataga siku chache zilizopita.

Pia sura za wale waletaji wenye vipara zilinasa katika fikra zake.

Alienda mpaka mapokezi akajitambulisha na kutoa kitambulisho chake,akaomba apelekwe ofisi ya mkurugenzi wa uwanja ule akaelekezwa.Butu akaingia ndani ya lift kuelekea uko alipoelekezwa.

Baada ya kufika Mkurugenzi alimkaribisha Vizuri Butu akajitambulisha Kama alivyojitambulisha mapokezi

Mkurugenzi akahitaji kumsikiliza.

Butu akaomba 'list' ya wafanyakazi wote na picha zao,lengo pengine wale watano angewatambua angewabana lazima wangemfungulia kumjua mbaya wake,alitazama picha za wafanyakazi moja baada ya nyingine cha ajabu akumuona hata mmoja!...

"una uhakika hii ndo list ya wafanyakazi wako wote wa hapa earport?!"

Alimpachika swali mkurugenzi ambaye alimjibu ndo hao tu katika listi hakukuwa na wengine Butu akarudia kuwatazama tena,ila hakuona sura hata moja kati ya zile tano alizokuwa akizitafuta!

Maajabu!!!...

Utata!

Mashaka yakaanza kumvaa,hofu kumtanda!,akahitaji kuona list ya wasafiri wote walotua tar 4 ya mwez wa 4 mida ya saa tano akataja na aina ya ndege na namba zake,akapewa faili la siku hiyo akakagua,pia cha ajabu akuona picha kati ya watano wale alowakamata kabla ajaja kuwa achia kwa dhumuni la kuikomboa familia yake!...

Iweje picha zao zisiwepo?!...

Alizikumbuka sura zao fika,ila pale azikwepo!,nani anayemchezea?!, akajikuta akikosa raha,Butu akazidi kuchanganyikiwa akakifata kiti na kuketi!...

Macho yake yalikuwa mekundu,wakati akiwa kaketi pale ghafla simu yake ikaita,haraka akaitoa kucheki ni askari mwenzake Jonathan!,alokuwa akiisimamia kesi yake,haraka akaipokea ile simu...

Kwani alishakata tamaa ya kujua angefanya nini kwa kuwa kila upenyo auonao kuwa utamfikisha kumtambua adui yake unazibwa na kumuacha katika tafakuri kuu.

Ila kupigiwa na Jona kukamtia nguvu pengine alikuwa na habari njema kwake ambazo zingemuwezesha kumjua mbaya wake

Ni ule wakati Jonathan alipoamua kumpigia akapokea...

"kuna jambo nimeligundua tuonane muda huu kivulin bar tupate moja baridi,moja moto tuzungumze"

"Sawa!"

Palepale Butu hakakata pasina kupoteza muda akatoka ndani ya ofisi zile tayar kuianza safari,kivulini Bar.

***
Kamishna uchovu ulimchovya, alikuwa akisinzia ghafla akazinduliwa na mlio wa simu yake akaitazama alishtuka,ni baada ya kuona 'privet no,'

No za aina ile akuzipendaga kabisa ila akaamua kupokea Kama wajibu wake umtumavyo.

"Nurdin naongea sijui ni nani mwenzangu!?"

Kwa sauti ya utulivu,akijitahidi kutoweka mashaka Nurdin akazungumza...

"Nitambue kama raia mwema inatosha!"

Upande wa pili ukajibu kwa kiburi na dharau ya hali ya juu.

"Ok,nikusaidie nini?!"

Nurdin akaongea kwa hasira ni wazi akupendezwa na dharau za mtu yule

"Aliyekuwa askari wako mtihifu anauza madawa ya kulevya, Butu, kayaifadhi katika kabati lake la nguo chumbani,sasa kazi ni juu yako uamue kufatilia au upotezee juu yako mie nshakupa taharifa hiyoo"

Hapo hapo mpigaji akakata simu!

kamishna Nurdin akashusha pumzi ya kuchoka!

Ndiyo!,alichoka kwa lile aliloambiwa!, ila kama mkuu wa polisi akupaswa kupuuza chochote aambiwacho lazima achunguze mshtakiwa ahukumiwe!

Palepale akashika simu yake,tayari kumpigia Jonathan kijana aliyemwamini kati ya vijana wake wote!.

Upande wa pili baada ya Zidu kukata simu akaachia cheko kuna watu wengine alihitaji kuwa taharifu wakaweke mtego nyumbani kwa Butu ili tu akitolewa wasambaze habari zake!

Waandishi wa habari,...

Alijua polisi wangeweza kuficha jambo lile kusudi kutolipaka matope jeshi lile ila kama waandishi wangeliripoti lazima Butu angeishia pabaya.

Akatabasamu tena palepale akaichukua simu yake tayari kwa kuwasiliana nao,awapange.....

Jonathan akiwa katika kikao alimueleza kila kitu Butu,juu ya kutekwa kwa mama yule,ambaye mumewe ndiyo wao waliyo muua!,wakajaribu kuyaunganisha matukio haya mawili wakapata picha!,kwamba Silivestar familia yake ilitekwa baada ya yeye kugundulika ni msaliti,akajitoa muhanga kufa ili familia yake ipate kuwa huru!,ila sasa je Silvestar ilikuwaje mpaka kutoa siri za watu hao?,je walitapeliana?,ni watu gani wanaukaribu gani na Silvestar?!,bado maswali yakawa mengi kwao!,ila ghafla simu ya Jona ikaita...

"Nakuomba wewe na wenzako mje hapa ofisini mara moja kuna dharura imetokea"

Ikabidi kikao kifungwe,haraka Butu akarudi nyumbani kwake pasina kujua kinachoenda kumtokea.

Inspekta Jona na wenzake wakarejea ofisini!

"Bebeni silaha za moto tuelekee katika cruzer haraka twende kwa Butu,maaskari wale sasa wakawa wakishangaa,ila wakatii amri,wakaingia ndani ya gari ya polisi,Jonathan na kamishna Nurdin wakiwa mbele,huku Patrick,Paul na Isack wakiwa nyuma ya bodi,Jona akaliwasha gari tayar kuelekea kwa ins Butu!
***
Butu alikuwa sebuleni mwake akipitia pitia gazeti ghafla akasikia sauti ya ka kengele cha mlango akasimama na kwenda kufungua,alishtuka kumkuta mkuu wake na walokuwa maaskari wenzake!

"Tunahiji kukagua nyumba yako Butu!"

Nurdin alisema,butu alibaki katika mshangao pasina kuelewa nini kinachoendelea,yote yale Zidu aliyaona,katika simu yake maafisa wale wa polisi wakaingia na kuelekea moja kwa moja chumbani!

"Tunakuomba ufungue kabati!"

Butu bila ubishi pasina kujua kipi kinaenda kutokea akaingiza funguo na kufungua kabati,nguo zikaanza kutupwa chini,punde kete zile za madawa zikaanza kutolewa,palepale Butu akawekwa chini ya ulinzi, akavikwa pingu, na kutolewa nje! Cha ajabu nje waandishi walikwepo wa kutosha aikujulikana walitaharifiwa na nani!,picha zikafatia...

Butu akaingizwa kwenye gari safari ya kwenda kituoni ikafatia!,akiwa chini ya ulinzi mkali!

Tena akiwekwa na wale walokuwa chini yake kicheo!...

Walompigia saluti na kumuheshimu....

Sekeseke linaanza kuya andama maisha ya aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu,pasina kujua anategeshewa madawa ya kulevya katika kabati lake chumbani sasa yupo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi ni nini kitakachoendelea?!,

Habari za kukamatwa kwa aliyekuwa afisa wa jeshi la polisi zilizagaa,vyombo vya habari vyote vilielezea,watu mbalimbali waka andamana kushinikiza askari yule kupewa adhabu kali!.

Wakati hayo yakiendelea Mkuu wa polisi Igp Gerald Uwiyo aliketi ofisini kwake,kichwani kwake alikuwa na mawazo sana,alimkubali sana Inspekta Butu alishtushwa na habari alizozipata,hakuziamini kabisa na alijua lazima kuna mchezo kijana yake yule atakuwa kachezewa,si bure,haraka akachukua simu yake na kumtwangia Cp Nurdin,Nurdin alimuelezea kila kitu,toka kupigiwa simu na mtu alojitambulisha kama raia mwema na kumueleza juu ya kuwepo kwa madawa ndani ya kabati la Butu,walipofatilia na kufanikiwa kuyakuta!.

"Mlikagua cctv camera?!"

"Hapana mkuu hatukufanya ivyo!"

"Ndo kosa mlilokosea,haraka sana uchunguzi uanze mara moja wapatikane hao washenzi wanao mchafua huyu kijana wangu!"

"Sawa mkuu!"

"Ok,ntakutafuta acha niongee na mh Waziri naona anantafuta!..."

Palepale Igp Uwiyo akakata mawasiliano na kamishna akampokelea waziri!

"Umeona habari inayoendelea kwenye vyombo vya habari juu ya kijana wako?!"

"Ndiyo mkuu,lakini kwa hisia zangu Butu kasingiziwa awezi kuwa muuzaji kuna mchezo..."

"Usitake kunifanya nika amini kwamba Raisi alikosea kukuteua mkuu wa polisi,kijana wako kakamatwa na ushahidi,kalichafua jeshi zima la polisi bado unataka kumlinda eti ufanyike uchunguzi nina chokuomba toa tamko katika vyombo vya habari kulahani tabia hiyo na pia uhaidi adhabu kali kwa askari huyo masikio ya wananchi wote yapo kusikiliza serikali itachukua hatua gani,narudia tena apewe adhabu kali iwe fundisho kwa watu wengine hii inaonesha hata siri ya kuipoteza familia yake anaijua..."

Igp alishtuka kwa amri ile,lakini ilipaswa aifate japo moyo wake ulimuuma,haraka kama alivyoambiwa akahitisha mkutano wa waandishi wa habari aka laani kitendo kile cha Butu na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa!...

Hakika sasa maisha ya Butu yalikuwa hatarini!

Roho mkononi!!...

Jeshi lilimtenga,marafiki walimtenga,alifikishwa kituoni akatupwa rumande na kesho yake akapelekwa mahakamani...
***
Mahakama ilifurika watu,wengi wakitaka kujua ni nini hatma ya polisi yule aliyekutwa na madawa nyumbani kwake.

Hatimaye akapandishwa kizimbani ,akasomewa shtaka lake la kukutwa na madawa ya kulevya alipoulizwa alikubali kukutwa nayo japo alikana kujishughulisha na uuzaji,alisema wazi aliwekewa kimtego,utetezi wake ukakosa nguvu akahukumiwa miaka 35 na kulipa faini,wengi walifuraishwa na hukumu ile,.

Butu mwenyewe binafsi alishangaa kesi yake ilivyopelekwa haraka haraka mpaka kuhukumiwa kwake,hapakuwa na uchunguzi,wala nini,sasa anaelekea gerezani,hakuwa na ndugu wala familia wa kumpigania,hakuwa na rafiki wala hata mpz wa kumfariji,akaingizwa katika karandinga tayari kwa kwenda kuya anza maisha mapya ya gerezani.

USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAMπŸ‘‡BONYEZA HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni