ROHO MKONONI (12) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumamosi, 9 Julai 2022

ROHO MKONONI (12)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
πŸ“– KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
πŸ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
πŸ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa
Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA KUMI NA MBILI
ILIPOISHIA...
Anategeshewa madawa ya kulevya anakamatwa anahukumiwa na kuswekwa lupango,mbaya zaidi anaingizwa ndanh ya selo ijulikanayo kama lango la jehannamu,hakuna historia ya kuingia huko na kutoka ukiwa hai naye anajikuta katika mateso makali je atasalimika kweli?! Tusonge kuzidi kuburudika zaidi!

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
πŸ‘‰GUSA HAPAπŸ‘ˆ

SASA ENDELEA...
Kiza kilitanda ndani ya macho yake,kumbukumbu kwa mbali zikaanza kumjia!.

Akajaribu kufumbua macho yake, yalikuwa mazito kana kwamba yakigoma kufumbuka ila hatimaye yakafumbuka.

Akajaribu kuvuta kumbukumbu ni wapi hapo alipo,kumbukumbu azikumsapoti,zikagoma kabisa,ila alijua muda ule ni usiku kutokana na kiza kizito,kichwa kilikuwa kizito kwa maumivu makali.

Akatuliza akili!,hapo hapo sasa ndipo kumbukumbu zilipoanza kumrejea maumivu makali ya kausweka moyo wake,akataka kujaribu kusimama pale alipojilaza akashindwa,akatamani hata kukaa pia kwake ikawa ngumu.

Akang'amua hata mwili wake pia umekufa ganzi.

Hapo ndo akachoka kabisa!

Akujua amelala kwa muda gani pale,tumbo liliunguruma kwa njaa angekula nini na uwezo wa kutafuta kwa kipindi hicho kigumu cha kutumikia adhabu alopewa na nchi yake!

Maumivu ya kichwa yalizidi kumgonga,kizunguzungu kikali kikamvaa,ganzi aloipata ilimsaidia kwani hakusikia maumivu ya kung'atwa na siafu wala panya,ikabidi aendelee kulala akiwa kakata tamaa kabisa! na alitamani kufa kwenda kuungana na familia yake kuliko mateso yale mpaka muda ule akujua anapambana na kina nani!,ila alijua ni mtandao mkubwa na ni watu wenye uwezo mkubwa kumzidi hata yeye.
***
Katika jumba moja la kifahari la Zidu alitumihalo kufanyia baadhi ya mikutano yake ya siri,kuhifadhia pia mateka wake,juu ya ghorofa ya tatu katika varanda ya nje kwenye makochi walikaa watu wa tatu,kilikuwa ni kikao cha siri,Zidu akitoa mrejesho wa kazi yake kwa mheshimiwa Raisi na waziri mkuu wake.

"Yule kijana kwa sasa yupo magereza na nimeshaongea na mkuu wa gereza lile mtu yule afe tena kwa mateso makali!"

Walimpongeza sana Zidu kwa kazi aloifanya,alipo yeye hapakuwa na kinachoharibika,waliendelea na maongezi yao wafanyakazi wa jumba lile waka wa andalia chakula wakala hatimaye wakaaga!.
***

BAADA YA MASAA 24: NDANI YA OFISI YA MKUU WA MAGEREZA
Mkuu wa gereza la Segerea Dunga aliketi katika kiti chake,macho yake yakiwa katika kompyuta yake,mdomoni kulijaa mabuyu alokuwa akiyatafuna na mbegu kuziweka kwenye meza yake,buyu hizo alichukua katika kakopo kadogo!,ambapo alikanunua kakiwa kamejaa na sasa ndo alikuwa anamalizia,macho yake yalidondokea katika saa ilokwepo ukutani hapo ofisini kwake akatabasamu,zilisalia dakika kumi kukamilika kwa masaa 24 toka kuletwa kwa Butu pale,akashika mkonga wa simu yake na kuweka masikioni akabonyeza namba kadhaa simu ikaita!

"Naam afande"

Upande wa pili ukaitika kwa sauti nyororo ya kike,

"Niitie askari yeyote hapo mapokezi"

"Sawa afande,.." Binti yule akajibu na kukata simu

"Mudy unaitwa ofisini kwa mkuu"

Pale pale binti akamlenga mtu alomtaka yeye,na kijana huyo binti alo mpendekeza akijua bosi ka muhitaji akajinyanyua na kuelekea ofisini kwa mkuu wake!.

"Kusanya hizi mbegu ukazitupe kwenye dustbeen hapo nje uje hapa!"

Kijana yule akazikusanya zile mbegu bosi wake alizokula na kwenda kuzitupa kisha akarejea kwa mkuu wake!.

"Nenda kamtoe yule mfu lango la jehannamu kama ni Maiti mwacheni aozee huko,ila kama ni mzima mkamtupe triple c tumeelewana?!"

"Ndiyo mkuu"

Yule askari alijibu huku akionesga wasiwas wa waziwazi usoni mwake,aliushangaa ukatili wa mkuu wake ila kwa kuwa tayari ilikuwa ni amri ilikuwa lazima akaitelekeze.

Akawashtua maaskari wenzake, wakaelekea lango la jehannamu wote walijua wangekuta maiti kwani mtu yule toka awekwe kule akula chochote.kunywa wala kuonja,tena akiwa ndani ya mateso makali!

Leo wamkute hai?!

Aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu bado maisha yake yapo hatarini,ndani ya masaa 24 anafungiwa ndani ya chumba kijulikanacho Kama lango la jehannamo huko apewi chakula, anakutana na wadudu wa uchungu wa kila aina,baada ya masaa 24 kuna mtu anatumwa na mkuu wa magereza akamfate,akimkuta hai apelekwe triple c,akikutwa maiti aachwe tu huko huko,kijana yule alotumwa akifatwa na wenzake wanaenda mpaka kwenye selo ile wanafungua mlango na kuchungulia wana cho ona kinawashtua je wameona nini?!

vijana wale wakafika,mmoja akachuchumaa na kufungua kale ka mlango kisha akamulika kwa kutumia tochi iliyokuwepo mkononi mwake,akuamini alichokiona,Butu alikuwa kakaa kitako tena akionekana mwingi wa mawazo,.

"Yupo hai,haya toka haraka"

Askar yule aliwa ambia wenzake muda huo huo akimpa ishara Butu atoke kule,Butu alisimama,akajitahidi kupiga hatua akaenda chini,mwili wote bado ulimuuma na tena ulikosa nguvu ikabidi atambae alipotoka akanyanyuka wakamsaidia kumshika mpaka selo,wote walimuonea huruma ila ndo ilikuwa amna namna,walimfikisha katika selo triple c,lango likafunguliwa akasukumiwa ndani!.

Wafungwa wakampokea kwa furaha akiongozwa na nyapara alokwisha pewa kazi na mkuu wa gereza kumtesa kijana yule ikiwezekana hata kumuua amuue tu.

Kabla akijafanyika chochote kengele ya msosi ikagongwa wote wakatoka, Butu akijitahidi kutembea kwa kushika ukuta asidondoke,naye akachukua sagani yake na kujipanga katika msitari,hatimaye zamu yake ikafika naye akawekewa chakula.

Mpaka muda huo hapakuwa na mfungwa alotaka urafiki na yeye,wengi wakisema hakuna urafiki kati ya askar na mfungwa.

"Chezo yule fala si ndo alinikamataga akanipiga sana na kunisweka rumande,akasimama mahakamani kama shahidi mi nikafungwa sasa leo kaingia kwenye kumi na nane zangu ataisoma namba"

Ilisikika sauti ya mfungwa mmoja ikimnong'oneza mwenzake,na palepale akampa sahani yake amshikie taratibu akamfata Butu pale alipo!

"Hoya we fala unanikumbuka!, ulipokuwa kitengo ukajiona afisa utopatwa na matatizo leo umeingia kwenye 18 zangu utaupenda utawala!"

Mfungwa yule alokuwa na namba 15 katika ovaroli lake akaongea kwa kiburi,ila kwa jeuri Butu akawa anakula,alijua mambo kama haya yatajitokeza ivyo alijua jinsi ya kukabiliana nayo,alowatia kule ndani ni wengi hivyo alijua visasi ni vya kutosha,bila uwoga,bila kumtazama usoni yeye akaendelea kula,jamaa akazidi kukasirika.

"Yani wewe boya naongea na wewe nawe waendelea kula nadhani ujanijua vizuri wewe".

Mtu yule akapiga hatua kadhaa na kumfikia Butu akamnyang'anya ile sahani ilikuwa kosa,ndani ya masaa 24 ajala,akajikuta hasira zikimpanda nguvu zikamjia akajiinua akapiga hatua ya kwanza hatua ya pili akamdaka kijana yule namba 15 kola ya ovaroli lake akamgeuza na kumzawadia ngumi moja ya usoni,jamaa akaachia chakula,butu akakidaka.

"Weweeeeee!, tena na usije ukajaribu tena kuingia katika vita yangu sitosita kukuua,usije ukajaribu tena mpumbavu wewe"

Butu alimpa onyo huku akimbana mdomo tena kwa nguvu,alipo maliza akamsukumia kule,akageuka sahani yake mkononi akarejea alipokuwa ameketi awali.

Tukio lile Nyapara Manzua aliliona,hapo akatambua ukorofi wa mtu yule!.

Si goigoi kama alivyodhani,baada ya chakula wakarudishwa katika selo zao.

Butu alienda akatafuta eneo akaketi,akaegemea ukuta,akaji inamia akiyapa nafasi mawazo kukiandama kichwa chake.tayari alishaua viumbe visivyo na hatia,na siyo ivyo tu amejikuta akiwa gerezani kwa kosa ambalo akulifanya,wakati akiendelea kuwaza si ndo Manzu akazama ndani,kwanza alishtuka kumkuta Butu kakaa sehemu yake kwake ikawa kashapata sababu,akamfata akiwa mwingi wa jazba.

"We kijana nani kakuruhusu ukae hapo nadhani ujataka kumjua Manzu ni nani sasa leo utanijua vizuri."

Manzua akapayuka kwa hasira huku akipiga hatua ndefu kumfata pale alipo,Inspekta Butu akanyanyua kichwa chake,akawa tayari kumsubiria mtu yule kweli Manzua alifika,akanyanyua mkono wake aloukunja ngumi akiupeleka alipo Butu,kijana akakinga mkono wake mkono wa Manzu ukapiga mkono wa Butu,ndani ya sekunde ile ile Butu akajinyanyua na kukaa tayari,Manzu akapiga hatua tatu ndefu za chapchap nyuma,akaunyanyua mguu wake kwa uwepesi kumuendea Butu,ila kijana akawa tayari kashaliona lile teke akalipangua kwa mkono wake,sambamba na kurusha konde zito shavuni kwa Manzua likampata sawia,manzu aka achia mguno wa maumivu,ila akajikaza akataka kujaribu kuirudisha usoni Butu akainama ngumi mbili zikapiga hewa wakati alipoji inua akarusha konde jingine la tumbo Manzu chini...

Wakati hayo yakiendelea wafungwa walikuwa wakishangilia kupigwa kwa manzu,aliwaonea sana,si wafungwa pekee hata maaskari nje walichungulia wakifurahia kitendo kile.

Kila pigo Manzu alilopiga aliambulia maumivu,mdogo wote ulitapakaa damu...kelele za ua,ua,ua,ua zilizagaa,

"Wote kimyaaa..."

Ghafla sauti kali tena ya amri ikasikika kutoka nje ya selo ile kubwa ya wa babe triple c,wengi waliijua sauti ile aikuwa ya mwingine zaidi ya ya mkuu wa gereza lile Gerald Dunga.

"Umefanya kosa sana kumpiga nyapara wako ni kama umenipiga mimi,sasa hukumu yako ni hapa hapa iwe fundisho kwa wengine"

Dunga aliongea kwa ukali akachomoa bastola yake ndogo na kumuelekezea Butu,akipanga amtandike na kumuulia palepale kama alivyoambiwa na mkurugenzi wa usalama wa taifa mr Zidu kite.akaikoki bastola tayari kuiruhusu kuchomoka,Butu alibaki katika bumbuwazi kutokuamini kile kinachotokea,kupata adhabu ya kifo kisa kosa la kupigana?!,hakika jambo hili lilimshangaza sana...

Sasa kidole cha pili baada ya dole gumba cha Dunga,kikawa kinaenda kushika kinasulio,kuruhusu risasi kuchomoka.

Majanga!.

Sekeseke la hatari bado lina ya andama Maisha ya alokuwa Inspekta wa jeshi la polisi John Butu, baada ya kusalimika ndani ya lango la jehannamu anapelekwa katika selo ijulikanayo kwa jina la trple c,huko anakutana na nyapala Manzua,nyapala alopewa kazi ya kumtesa Butu ikiwezekana kumuua kabisa,kazi inakuwa ngumu kwa Manzu hatimaye anapigwa yeye,kitendo cha kupigwa kinawafurahisha wafungwa na hata maaskari pia kwani wengi walimchukia Nyapara yule,je nini kitaendelea?!,tusonge katika hatua inayofuata...

Kabla Mkuu wa Magereza Dunga ajaruhusu risasi kutoka katika bastola yake,ghafla ikasikika sauti nyuma.

"Hapana mkuu usifanye ivyo!.."

Ikabidi mkuu yule wa gereza ageuke nyuma,macho yake yakatua kwa kijana mdogo alokuwa ndani ya sare nadhifu za jeshi la magereza,mabegani kwake akiwa na nyota mbili akipishana naye kwa nyota moja tu yeye alikuwa na cheo cha kapteni akimiliki nyota tatu.

Usoni mwa kijana yule alipambwa na tabasamu jepesi,akamfikia Kapteni Dunga bado tabasamu likipamba mdomo wake.

"Unataka kuniambia nini Luteni?!"

Dunga akaongea kishari mkono wake wenye silaha ukiwa una angalia chini,kijana yule alojulikana kwa jina la Luteni Johnson Mamba ndo alikuwa msaidizi wake,alimfikia akamshika mkono na kumkokota mpaka nje.

USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAMπŸ‘‡BONYEZA HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni