ROHO MKONONI (14) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumamosi, 9 Julai 2022

ROHO MKONONI (14)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
πŸ“– KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
πŸ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
πŸ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa
Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA KUMI NA NNE
ILIPOISHIA...
...hapo ndipo ilipofuraha ya daktari yeyote ulimwenguni,akampa ishara msaidizi wake,operesheni ikaanza,kwanza kwa kumtolea risasi zote kumi,mwisho maswala ya kitabibu yakafatia,masaa manne wakaitimisha operesheni ile,sasa Butu alilala kitandani akitumia mashine za oxygen hali yake bado ilikuwa mbaya.

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
πŸ‘‰GUSA HAPAπŸ‘ˆ

SASA ENDELEA...
Masaa yakakatika hatimaye Zidu akawasili toka kazini alipoelekea ile mida ya mchana,baada ya kuwasili kwa daktari.

"Vipi kazi imekamilika?!"

Zidu akamuhoji daktari yule huku akiketi sofani.

"Ndiyo mkuu ile miili mitano mfu nimeipandikiza viroba vya unga ulivyo nipatia ila ule mwili mmoja nimeukuta una uhai nimeufanyia operesheni japo hali yake bado mbaya kupona ni kudra za Mungu..."

Zidu akakunja sura,hasira zikampanda.

"Kwani uliambiwa uje utibu hapa au upasue matumbo utie unga ndani yake na kuyashona?!"

"Lakini tahaluma yangu ainitumi kufanya hivyo kwa kiumbe hai!"

Dk Stanley naye akaja juu,.

"Kwa hiyo pakiti moja ujaliweka ndani ya tumbo la mtu?!"

"Yah nimefata maelekezo kama ulivyo nambia kila mwili nitie kiroba kimoja na ndivyo nilivyofanya,kasoro tu kwa huyo kiumbe hai,nimemtoa risasi nikamfanyia opereshen now nimemtundikia dripu na anasaidiwa na mashine za kupumulia".

"Aaah!,comon dk unafanya nini?,ujui yule mtu ana hatari gani kwa taifa ingali akiwa hai,yapaswa ukamuue mara moja na utie hayo madawa katika tumbo lake muda wowote mheshimiwa anawasili sijui tutamjibu nini!?"

"Hapana mkuu utanisamehe bure kazi yangu mimi ainitumi kuua,kwa hilo sitokuwa tayari!".

Daktari akazidi kubishana na Zidu pasina kujua yule ni kiumbe katili kwa kiasi gani,mapigo ya moyo yakazidi kumwenda kasi akazidi kujiuliza yule dokta ni wa aina gani mpaka awe na ujasiri wa kubishana naye?!,kipi kinacho mfanya ajiamini kwa namna ile?,akajikuta akiwaza sasa kutumia nguvu kuiendesha ile kazi hata ikibidi kuua aue kama ato muelewa!,.

"Dokta kama unayapenda maisha yako,naomba fanya kazi nilokuagiza taratibu geuka twende chumbani ukaue yule kiumbe umwekee hiyo pakiti ilobakia hapana muda tena wa kupoteza."

Tofauti na mategemeo yake dk aka achia tabasamu tena lile la madharau,kisha kwa sauti ndogo ila ya kujiamini akageuka...

"Unantisha siyo?,unadhani nina nidhamu ya uoga siyo?!,tandika risasi uzitakazo lakini siwezi badilisha ukweli,siwezi ua kiumbe kilicho hai nilichopoteza muda wangu kukitibu,jasho limenitoka pale labda uue wewe lakini mimi akaa utansamehe tu bure."

Kuongea vile akawa kampa wazo Zidu,kuliko kubishana na kupoteza muda mbona yeye ana weza kwenda na kumuua kwa sekunde chache kwa kumtandika risasi nyingine zisizo na idadi?!

Kwa haraka akageuka na kuelekea chumbani,dokta akimfata nyuma alipofika akafungua mlango bastola mkononi akaielekezea kitandani pale alipo Butu,alijua labda dokta angemzuia ila dokta alibaki tu kumwangalia,taratibu akapeleka kidole chake katika kifyatulio kwa lengo la kuruhusu risasi ichomoke safari hii kwa hali alokuwa nayo Butu sijui kama angepona!..

Sijui kwa kweli.......

Butu anachukuliwa kwa lengo mwili wake ukatumike kubebea na kusafirishia madawa ya kulevya nchi za nje ikiungana na mihili mingine kumi.

Kwa bahati nzuri Dokta ajulikanaye kwa jina la Dokta Stanley anagundua Butu yu mzima haraka sana anamfanyia operesheni ya kumtoa risasi zote kumi kitendo hiki kinazua Sekeseke jipya kwa Zidu,

Anamjia juu daktari.

Maisha ya Inspekta Butu yanakuwa Roho mkononi,mabishano makali yanaendelea mwishoni Zidu mwenyewe ana amua kuzama ndani ya chumba kile akamalize kazi mwenyewe bastola mkononi anaielekeza pale alipo Butu je atammaliza?!....

Kabla ajamtwanga ile Risasi ghafla akasikia sauti nyuma yake.

"Zidu achaaaaa...."

Kisha hatua tena zikipigwa haraka haraka kuja ule upande wao.

Sauti ile aliijua fika,ilikuwa ni ya mheshimiwa Rais,mapigo ya moyo yakaanza kupiga kwa kasi si yeye tu lah hata kwa daktar Stanley naye alitetemeka binafsi aliutambua ukatili wa Raisi wake yule akajua hapo pangenuka tu na si kwake hata kwa Zidu pia ila hata ivyo akujali.

Moyo wake ulisimama katika haki,alikuwa tayari kufa ila si kuua kiumbe kisicho na hatia hiyo kuziwekea tu zile mwili viroba vya madawa moyo wake ulikuwa ukimchuruzika machozi kwa uchungu sembuse kuua?!.

Hapana hakuwa tayari kwa ilo.

Itakavyokuwa na iwe,akawa tayari kupokea lolote lijalo.

Raisi Patrick Bisau akawafikia pale walipo.

" Zidu amna haja ya kumuua huyo kwani inatakiwa miili Kama hii mitano kwa ajili ya kusafirisha mizigo USA hivyo dokta katufanyie mchakato ya miili minne katika hospitali yako dokta Julias atafanya hiyo kazi ya kuiwekea mzigo sawa?!,Zidu hii itangulie uwanja wa ndege kwa Safari ya kuelekea hapo kenya wale wa mama wa msiba si ushaongea nao?!..."

"Ndio mkuu nishawapanga watakuwepo KEIA kuipokea miili Kama ya ndugu zao"

"Very nice kazi nzuri mpigie Isack,Kinampa waje mkaipakie hii miili DIA haraka sana na Isack asafiri nayo wewe utaelekea USA na hii miili mahututi na madokta hawa sawa?!"

"Sawa mkuu"

Zidu akaitika,palepale Raisi aka aga na kuondoka,mzigo wote ulikuwa katika jumba lile la Zidu na kazi ilifanyikia pia palepale.

Baada ya muheshimiwa Bisau kuondoka Zidu na dokta wakatazamana hakuna alotoa neno kwa mwenzake kila mtu akaendea na shughuli yake.

Dokta Silvestar akaelekea mpaka mahali alipo msaidizi wake akampa maelekezo.

"Doto mimi natoka hakikisha usalama wa mgonjwa wangu mpaka hapo dokta Julias atakapowasili badiliko lolote litakalotokea utanijulisha sawa?!"

"Sawa dokta"

Binti yule nesi akaitikia kwa heshima,daktari akatoka zake,tayari kwa kwenda kutekeleza jukumu jipya alilopewa na mkuu wake.

Zidu mapema sana yeye alishaondoka yeye hakuwa na wa kumpa maelekezo pale.
***

SURA YA SITA
UNITED STATES OF AMERICA: WASHINGTON DC
Ndani ya taifa la marekani katika mji mkuu katikati ya jiji katika jengo moja kubwa lenye ghorofa zaidi ya 30 jengo hilo kubwa lilimilikiwa na bilionea alotambulika kwa jina la Mernly Max Arthur.

Ndani ya chumba kimoja juu kabisa ya ghorofa kulikuwa na kikao cha siri ni baada ya taharifa nyeti kutua kwa bilionea huyu Merly kwamba kuna kiasi kikubwa Cha madawa ya kulevya kinaingia nchini kwa njia ya magendo kutoka nchini Tanzania akakumbuka miaka mingi nyuma alishawai kutapeliwa na huyo mwenye mzigo huo kipindi hiko Bisau akiwa mgombea pesa hizo akazitumia kuimarisha chama na kuendeshea kampeni.

Kwa muda mrefu sasa Merly amekuwa akimfatilia Raisi Bisau kwa kusudi la kulipiza kisasi bila mafanikio ila mtafutaji huwa akosi siku hiyo hatimaye habari zikamfikia kuwa watu mzigo unaingizwa na wagonjwa mahututi haraka akaweka kikao kujadili swala Lile.

Alikuwa kavimba kwa hasira,

"Niliapa siku moja kulipiza kisasi kwa kile Bisau alichonitendea na muda ni Sasa sitokuwa na msamaha kwa hili!,alinirudisha nyuma sana Sasa Agent Bray hakikisha unakusanya vijana wako wakakamavu mnawasili uwanjani na ambulance mnawapokea hao wagonjwa Mimi nishawapanga Madison's Hospital ndo walikuwa wawapokee watachelewa kwa dakika tatu nanyi mtazitendea haki kumbuka ni dakika tatu tu..

Agent Bray nakuamini nimekusomesha na Sasa ni mpelelezi unaye tegemewa, na taifa letu la Marekani usije ukaniangusha kwa hili nitampiga huyu fala pigo ambalo hatokaa alisahau katika maisha yake na huu ni mwanzo naapa one day nitahakikisha anakufa na Tanzania inatawaliwa na kiongozi safi Raisi gani anauza madawa ya kulevya?!"

Max Merly aliongea kwa uchungu.

Agent Bray alitabasamu akamtoa khofu mkuu wake kwamba kazi ataifanya Vizuri.

Kwa upande wa Tanzania miili ile mitano ilipasuliwa ikatiwa madawa siku ilofatia ikapakiwa kwenye ndege binafsi Safari ya kuelekea Washngtone Dc ikafatia,wakijua watakaowapokea ni wale walowapanga wao.

Ila kumbe mkuu wa kundi hatari la Mafia nchini Marekani Max Arthur Merly alishamuwekea mtego akimtumia kijana wake jasusi hatari Agent Bray.

Ndani ya ndege kidume Zidu kiliketi pasina wasiwasi madaktari Wawili Stanley na dokta Julias na wasaidizi wao wakizidi kutazama usalama wa wagonjwa wao walolala vitandani pasina ufahamu tena wakitumia mashine za hewa ya Oxygen kupumulia....

Wagonjwa mahututi wanapandikiziwa unga wa madawa ya kulevya katika matumbo yao na kusafirishwa kuelekea nchini Marekani Butu akiwa mmoja happy wakisindikizwa na Zidu kijana katili aliyoko ndani ya usalama wa Taifa nchini Tanzania...

Pia tuliona habari hizi nyeti zinamfikia tajiri Merly Max Arthur mkuu wa mafia nchini Marekani haraka anaitisha kikao cha siri na kazi ile anamwachia kijana wake aitwaye Agent Bray kuhakikisha mzigo ule unafikia kwenye mikono yake je ATAFANIKIWA?!

*UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA WASHNGTONE DULLES*
Ndege binafsi ilomilikiwa na Raisi Bisau ilitua katika kiwanja kikubwa cha ndege Dulles mjini Washngton Dc nchini Marekani.

Kama ilivyo ada mlango ukafunguliwa na machela zilibeba wagonjwa haraka zikashushwa,madaktari maalumu waloandaliwa tayari walisogea kusaidia kupokea wale wagonjwa na kwenda kuwapakia katika magari yao ya wagonjwa.

Walipokamilisha safari sasa ya kutoka uwanjani kuelekea hosptal ikafatia....

Zilikuwa ambulance tatu moja ikipakia wagonjwa wa nne na hizo mbili zilipakia wagonjwa wa tatu wa tatu.

Ambulance ilokuwa mbele kabisa ndiyo alokuwepo Agent Bray kijana aliyekuwa na asili ya 'black America' akiwa ndani ya koti zuri jeupe la kidaktari nywele zake fupi alizichana Vizuri huku kidevu chake akiwa kakipendezesha kwa kuchonga ndevu mtindo wa 'O' macho yake akiyaficha kwa mawani ilomzidishia utanashati shingoni akitupia kipimo maalumu Cha kupimia mapigo ya moyo kiitwacho...........

Kamwe usingeweza kukubali kwamba yule si daktari kwa muonekano tu alokuwa nao tena alionekana Kama daktari mkuu katika jopo lile maalumu waloandaliwa kuja kuwapokea.

Ambulance ya pili walikwepo madaktari wale Wawili Silvester pamoja na Julias masikioni mwao wakiwa na earphone kwa ajili ya mawasiliano maalumu.

Na Ambulance ya mwisho alikwepo Zidu Katili yeye alipiga tisheti ilombana na suruali yake ya jeans na chini akitupia 'simple' Raba alipendeza hakika masikioni mwake alikuwa na 'earphone'alizounganisha na simu yake pembeni yake walikwepo madaktari wale walokuja kuwapokea wote lengo lao kuhakikisha hali za wagonjwa zinakuwa nzuri japo hata wangekufa kwao isingeleta shida yeyote.

Safari iliendelea gari mbili zile zikilifata gari ile ya mbele ambapo ndipo alipokwepo Agent Bray ambaye tayari dereva wake alishajua aneo analopaswa kuwapeleka.

Mbaya Zaidi Zidu akujua ni wapi miili ile inapopelekwa wala ilipo hiyo hospital ya Madison's Hospital ambayo ndio ilotumika kuwapokea wagonjwa mahututi na kuwafanyia upasuaji na kuwatoa hayo madawa kabla ya kusambazwa na mawakala maalumu waloandaliwa,kabla ya miili ile kuwekewa aina nyingine ya madawa na kusafirishwa tena Kama maiti ikitua jijini Dar watu maalumu uipokea kwa majonzi ivyo upita bila kukaguliwa.

Wakati safari ikiendelea ghafla simu ya Zidu ikaita kuangalia ni mheshimiwa Raisi haraka akapokea.

"Mmeenda wapi mbona amuonekani hapo uwanjani?!...."

"Ndo tupo njiani mkuu tushapokelewa?!."

"Unasemaje?!...mbona hapa madaktari kutoka Madison's Hospital wamefika hapo uwanjani awajawakuta."

Zidu akaduwaaa....

"Embu subiri muheshimiwa,...

Akamwangalia moja wa madaktari alokuja kuwapokea Kisha akamtwanga swali.

....Samahani daktari eti tunaelekea hospitali gani?!"

Daktari akageuza shingo kumtazama Zidu,akaachia tabasamu la kumtoa khofu.

"Madison's Hospital"

Daktari yule mmama unayeweza kukadiria miaka yake kwenye thalathini na nane au arobaini akajibu kwa sauti tulivu kisha akageuka kuendelea na shughuli yake.

"Mkuu wala usijali ni Madison's Hospital"

"Hapana umekosea fanya juu chini urudi uwanja wa ndege sasa hivi!,"

Raisi aliongea huku dhahiri alionekana kuwa na wasiwasi,pale pale Zidu akafikiria kuchomoa silaha yake amwelekezee dereva na kumpa amri ageuze gari ile anataka kuingiza mkono mfukoni alishtuka akitazamana na bastola ndogo wale madaktari wakiwa wamezishika Vizuri hapo Zidu akajua kumekucha ya kumepambazuka.

Simama yao,nyuso zao sasa zilibadilika,kwa haraka Zidu akajua wale si madaktari wa kawaida Kama alivyodhani awali.

Wana kingine zaidi ya udaktari.

Haraka akajitahadharisha kabla ya kutahadharishwa kuwa makini.

Akatulia tuli.

"Tulia hivyo hivyo usijiguse hata kujikuna tutausambaratisha ubongo wako..."

Yule dada aliyeonekana kuwa na tabasamu mwanzo aliongea kwa amri akiwa tayari kwa chochote.

"Mikono juu...."

Mwingine akatoa amri,Zidu alitaitika ikabidi atii haraka kijana mwingine akamsogelea na kuichukua silaha Kisha pale pale akapewa amri atoe mkono akachomwa sindano iloenda na fahamu zake....

Msafara ule wa gari za wagonjwa zilizidi kusonga mbele tayari Madamu Mery mwanadada hatari jasusi alisha mdokeza Agent Bray kilichotokea na walivyofanikiwa kumdhibiti Zidu kilaini tu....

USIIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAMπŸ‘‡BONYEZA HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni