ROHO MKONONI (15) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumapili, 10 Julai 2022

ROHO MKONONI (15)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
πŸ“– KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
πŸ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
πŸ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa
Mwandishi: Zuberi Maruma

SEHEMU YA KUMI NA TANO
ILIPOISHIA...
Mwingine akatoa amri,Zidu alitaitika ikabidi atii haraka kijana mwingine akamsogelea na kuichukua silaha Kisha pale pale akapewa amri atoe mkono akachomwa sindano iloenda na fahamu zake....

Msafara ule wa gari za wagonjwa zilizidi kusonga mbele tayari Madamu Mery mwanadada hatari jasusi alisha mdokeza Agent Bray kilichotokea na walivyofanikiwa kumdhibiti Zidu kilaini tu....

KABLA HATUJAENDELEA NIOMBE KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media BASI INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI
πŸ‘‰GUSA HAPAπŸ‘ˆ

SASA ENDELEA...
"Congrats comred nilijua sikukosea kukuacha na huyo mtu!"

Agent Bray alimpongeza mwanadada yule,kwa kipindi hiki bilionea Max Arther Merly ndio aliyosadikika kulishika taifa la Marekani na yeye ndo alikuwa mdhamini mkuu wa chama tawala Cha American People 'AP' yeye ndo alopanga Raisi awe nani katika chama chake.

Na toka chama hiko kiingie madarakani Miaka 15 Raisi alimsikiliza yeye,alitumia wapelelezi maalumu na muhimu wa taifa Kama Kina Agent Bray,mwanadada Machachari Merry,na wengineo kwa mambo yake binafsi.

Arthur kazi yake kubwa ni usambazaji wa madawa ya kulevya duniani na kwa kuwa taifa lake lilikuwa kubwa akupata ukinzani wa aina yeyote na alikuwa na mawakala dunia nzima kundi lake likiitwa Mafia gengstar.

Miaka kibao nyuma wakala wake wa Tanzania akiwa ni waziri Patrick Bisau alituma mzigo wa ma bilioni,ghafla katika hali isiyo ya kawaida fedha zilichelewa kurejeshwa baadaye akasikia Bisau kachukua tiketi ya kugombea nafasi ya Uraisi na hata alipo ipata Bisau alimwambia pesa zake anazitumia katika kampeni akishinda Basi atazireuesha mara mbili yani na kiasi kile kile cha riba.

Kwa kuwa chama cha Patrick kilikuwa na nguvu Max alikubaliana naye,Bisau akapiga kampeni pa kuonga akionga mwisho wa siku akashinda tena kwa kishindo.

Kuwa Raisi Patrick kukamtia kiburi,Max alipoitaji hela yake akawa akizungushwa mwisho wa siku akatamkiwa wazi kutopatiwa hizo hela.

Mazoea ni mzigo kuutua ni ngumu , kwa kuwa Bisau alishazoea kazi ile ya magendo aliendelea nayo japo ni kwa usiri sana,kwa muda mrefu alitamani kuuza Marekani ila alishindwa kwa kuhofia mzigo wake kuingia mikononi mwa Max ila kwa kuwa taifa la Marekani soko lake lilikuwa juu akajipa muda wa kutengeneza mazingira.

Siku hiyo alialikwa kugawa vyeti kwa madaktari kadhaaa waliomaliza masomo yao,zoezi la ugawaji vyeti lilipokamilika Raisi akaomba aitiwe mwanafunzi mmoja punde kijana mmoja mchangamfu akaja.

"Ok unaitwa nani?!..."

"Madisoni Shemweta muheshimiwa!"

"Katika udaktari upo katika tahaluma gani?!"

"Upasuaji muheshimiwa Raisi"

Raisi Bisau akatabasamu,ndo mtu alokuwa akimtaka,kijana yule alikuwa ni yatima alolelewa na kusomeshwa na kituo Cha watoto yatima Cha Mkombozi, historia yake ya maisha pia ikamvutia Muheshimiwa Raisi.

"Nataka nikufungulie hospital nchini Marekani privet unaonaje?!"

Kijana yule akuamini ila Raisi alimpanga akapangilika,Madisoni akasafirishwa na kupitia balozi wa Tanzania nchini Marekani akafanyiwa mchakato wa uraia nchini Marekani,hospitali kubwa ilobeba jina lake Madison's Hospital ikajengwa na kuajiri madaktari wengi wakiwa wa Tanzania na wahindi.

Mpango ukakamilika.

Upasuaji ukawa ukifanyika pale watu wakawa wakipachikwa madawa ya kulevya na kusafirishwa Tanzania,hakuna alogundua hili kwa muda mrefu Bisau akawa akifanya kazi kwa uhuru huku Max akichunguza bila mafanikio.

Ila hakuna siri inayodumu milele ya mtu zaidi ya mmoja,siku ya siku Max akagundua siri ile naye kwa siri akakutana na dk Madison akampa fedha na kumpanga ampe Siri tofauti na ivyo angemuua Madison akaingia upepo,pesa akachukua na Siri akaitoa,mpango ukapangwa ukapangika,Max akaandaa vijana wake akiwemo Agent Bray wakawah uwanja wa ndege na kuwapokea kina Zidu baada ya kuondoka tu ndipo dk Madison alipowasili alipokuta wameondoka ndipo akampigia muheshimiwa Raisi Bisau na kumjulisha.

Raisi alichanganyikiwa,naye kwa haraka akampigia Zidu na kumuomba haraka arudi uwanja wa ndege.

Zidu akamuhaidi kufanya hivyo simu ikakatwa.

Zilipita dakika tano,Bisau akapiga tena kabla ya kukutana na sauti 'mteja unayempigia kwa Sasa apatikani tafadhali jaribu tena baadaye'.

Hata alipojaribu tena jibu likawa lile Lile.

Raisi akazidi changanyikiwa, ulikuwa Ni mzigo wa mabilioni...

Wasiwasi wake ulikuwa ni kwa mtu mmoja tu!....

Max Arthur Merly.

Akukosea,punde sms ikaingia katika simu yake haraka akaifungua kutaka kujua imetoka kwa nani.

Namba ilikuwa ni ya nje,

+1 859-962-3177

'Kwa kuwa umekuwa Raisi ukajua umekuwa Mungu wa dunia ukanidhulumu pesa zangu,Vizuri,ila usiangaike kutafuta mzigo wako pamoja na hawa Raia wako vyote kwa Sasa vipo chini yangu hii ni mwanzo rasharasha mvua inakuja....'

Ujumbe ule Raisi aliusoma zaidi ya mara tatu ila aukubadilika akapiga zile namba kabisa lakini pia azikupokelewa

Mwisho kwa hasira akaitupa ile simu na kuipasuapasua.

Ni Hasara kubwa sana aloenda kuipata!...

Hatimaye siri kubwa ilojificha kati ya bilionea mkubwa nchini Marekani Max Arthur Merly na Raisi Patrick Bisau tunaitambua,juu ya bifu lao la muda mrefu hatimaye Max Arthur Merly anafanikiwa kuiteka miili ya watu kumi ikiwa na madawa ya kulevya ndani,Bisau anachanganyikiwa kupata taharifa hizo je unadhani nini kiliendelea?!, Tusonge katika hatua ifuatayo nayo ni....

Haraka sana Raisi Bisau akamtwanga simu waziri mkuu wake Benson Sai na kuhitaji waonane haraka sana ikulu.

Muheshimiwa Sai alijiuliza ni nini kitakuwa kimetokea bila kupata jibu mwishoni akaona aende tu akasikie wito kwani ndo yalipo majibu ya maswali yake.

Dereva wale akampeleka mpaka ikulu,baada ya kusalimiana wakaingia katika chumba maalumu maongezi yakafuata.

Raisi Bisau alimweleza rafiki yake kila kitu kuanzia Madison alipompigia simu na kumtaharifu kutowakuta wagonjwa pale uwanjani,alipompigia Zidu na majibu alompa mpaka naye alipopigiwa simu na Max,hata waziri pia alichoka ila akakumbuka jukumu lake ni kuto kuonesha udhaifu na badala yake kumtia moyo kiongozi wake yule.

"Ni ku haidi tu muheshimiwa Raisi hakuna baya litakalotokea lazima Zidu ataukomboa mzigo wetu ni kijana ninayemwamini usijali kwa hilo muheshimiwa."

"Kwa hiyo kwa sasa yapaswa tufanyaje Sai"

"Tuwe na subira Muheshimiwa."

"Hapana Mimi na wazo."

"Wazo gani?!"

Sai akahoji akionekana kuwa na hamu ya kujua wazo hilo.

"Tumtume kk yeye pekee ndo anauwezo wa kurejesha mzigo pamoja na kumkomboa mumewe."

Kumbukumbu za waziri Sai azikufuta kazi alizowah kufanya Katarina,kumbukumbu zake ziliandikwa toka kuipatia uhuru Kinte,kupambana na mumewe Zidu uhodari wake wakaona wamtumie akauoneshe kwa bilionea yule.

"Haraka Katarina apigiwe simu nionane naye aingie kazini."

Mwisho Raisi akamaliza,waziri Sai akatoka sasa akiwa na matumaini.
**************
Mwili wote ulimsisimka,hatari ilishagonga katika kichwa chake si kawaida ya mume wake huwa akisafiri akifika salama umpigia na kumwambia mume wangu nimefika salama,ila safari hii mpaka muda huu akupigiwa.

Haraka aka amua akanunue vocha akatia katika simu yake akajiunga vifurushi vya nje akaitafuta namba ya mume wake anayoitumia Marekani akaipiga aikupatikana.

Akajaribu laini yake ya Tanzania pia jibu lilikuwa lile lile au simu imeisha chaji?!...

Hapana,alipingana na wazo hilo baada ya kugundua hata ndani ya ndege angeweza kuchajisha,alijua lazima mumewe atakuwa kaingia kwenye matatizo japo akujua Marekani kaenda kwa shughuli gani,pia alielewa mumewe alitumika kiuhalifu mara kibao alishamuomba abadilike bila mafanikio.

Wakati akiwa katika hali ya sintofahamu ghafla simu yake ikaita kuangalia alompigia ni 'privet namba' huku akiwa na wasiwasi akaipokea...

"Ni waziri mkuu Bisau hapa naongea unaitajika Ikulu na muheshimiwa Raisi kuna gari inakuja kukuchukua hapo nyumbani muda huu ivyo haraka sana jiandae ndani ya dk 5 uwe mbele ya Raisi"

Sauti ile ya waziri mkuu ikaitimisha,mwili wote wa Katarina ulimlegea jasho lilimtiririka akajua lazima mumewe kapatwa na matatizo je ni kafa?!,maswali mengi yakatiririka mawazoni,woga ukamtawala ila akajikaza haraka sana akaanza kujiandaa alipomaliza gari ikawasili akapanda Safari ya ikulu ikafatia.

Sasa kilikuwa ni kikao cha watu wa tatu, Raisi Bisau, waziri mkuu Sai na Katarina akiwa kaongezeka, Raisi hakuwa na budi kumsimulia kila kitu Katarina,mwisho akamueleza wazi kuwa kuitwa kwake ni kwa kazi moja tu,hata kuua ikibidi ila aokoe mzigo ikiwezekana na watu wale kumi wakiwa hai au maiti zao.

Akakabidhiwa paspoti na siku ilofatia ndiyo ilipaswa Katarina asafiri kuelekea nchini Marekani.

Kikubwa yeye alichofikiria ni kumkomboa tu mumewe katika mikono ya watu wale hatari.

Ni kazi ngumu itakayo yaweka maisha yake rehani

Roho mkononi!!!

Alilijua hilo, sekeseke analoenda kukumbana nalo alijua si la kawaida!

Ila je angefanyaje?!...

Mafia Ni kundi lililo ogopwa ulimwenguni.

Akaaga akiahidi kuifanya kazi Vizuri,akapewa baraka akatoka,tumaini kwa viongozi wale wa Taifa likarejea upya.
**********
Katika moja ya jumba la kifahari,jumba lenye ghorofa zaidi ya tano ndani pakiwa pamezungushiwa ukuta mkubwa wenye nyaya za shoti kamera za ulinzi na pakiwa na geti tatu zenye walinzi wa kutosha wenye silaha mabegani walojaza risasi.

Geti ya kwanza ikafunguliwa gari zile za wagonjwa zikaingia ndani pakiwa pamejengwa pakajengeka nyumba ndogo ndogo zikiwa pembeni zenye ghorofa moja mbili mpaka tatu yani kalikuwa Kama ka mtaa cha kitajiri gari zile zikaendelea kwenda hatimaye wakaingia geti la pili napo kulikuwa na walinzi maalumu pembeni pakiwa na banda la mbwa walobweka kwa ukali geti likafunguliwa wakaingia katika mtaa wa pili nao aukuwa tofauti na ule mtaa wa kwanza gari zile zikaendelea na safari hatimaye wakakutana na geti la tatu walinzi wakafungua na gari zile zikapita.

Mtaa huu ulikuwa tofauti na mtaa wa kwanza na wa pili mtaa huu ukuta wake ulikuwa mrefu zaidi kupita kuta za mtaa wa kwanza na wa pili pia ndani palionekana Kama pori miti ya matunda ilitawala si maembe machungwa migomba mbele kidogo wakaikuta bustani nzuri mbele ya bustani ile upande wa kushoto palikuwa na bwawa la kuogelea mbele nyuma ya bwawa Lile kulikuwa na jengo kubwa la ghorofa zaidi ya 50 ukitazama juu uoni mwisho wake.

Hili ndo jumba la bilionea Max Arthur Merly lililopo jijini Washngtone dc japo alikuwa na majumba Kama haya zaidi ya hamsini nchini Marekani,yani mitaa yake mwenyewe,pakiwa na hospital zake ndani maduka,masoko kwa kifupi katika mtaa huu wa tatu wa ndani hawakuruhusiwa kutoka nje,.

Japo mitaa hiyo miwili aliipangisha.

'Max Arthur Merly hospital'

Ambulance zilizimama mbele ya jengo ilo miili ile ikashushwa haraka na kuingizwa wodini.

"Haraka ipasuliwe na mizigo itolewa hakikisheni wanakuwa hai"

Agent Bray aliwa ambia madaktari walokuwa bize kuishusha miili ile.

Mwili wa Zidu kwa kuwa yeye alikuwa kalala akapelekwa katika chumba maalumu akafungwa kitandani kwa pingu maalumu akisubiriwa kuzinduka.

Tayari alikuwa ni mateka.....

Mwili wa Inspekta Butu na wenzake upasuaji ukaanza mara moja hali zao bado zilikuwa mbaya....

Merly Max Arthur mafia mwenye mtandao mkubwa hakupata tabu kugundua kutumwa kwa Katarina.

Alipotua tu uwanja wa ndege akaingia mikononi mwa wanausalama na taharifa akapewa.

Akacheka kwa kiburi akista ajabu upumbavu wa Rais Bisau na Mawazo mabovu ya kumtuma Mwanamke

Akaagiza Katarina apelekwe kwake akachanganywa na mateka wale kumi.

BAADA YA MWEZI MMOJA
Hali za mateka wale ziliendelea vizuri walipona kabisa Merly Arthur alishajua cha kufanya akawasiliana na shirika la habari la BBC na kuandaa kipindi Maalumu Cha watu wale kujielezea historia ya maisha yao.

Zidu na Katarina nao ili kuwa hai na mtoto wao Mdogo Sebastian aliyekuwa akademy Nchini humo kutodhuriwa ikawapasa waeleze ukweli wote Zidu akaeleza kutumika na Raisi kumtesa afisa wa Jeshi la Polisi Butu mbinu alizotumia kuiteketeza familia yake.

SEKESEKE likazaliwa nchini Tanzania watu wakaanza kuandamana wakishinikiza Rais Bisau sambamba na Waziri Mkuu wake kujiuzulu,

Jeshi likaingilia Kati kweli Bisau na Waziri Mkuu wakajiuzulu na kushtakiwa katika mahakama ya kimataifa na mwishowe wabaya wote Raisi Waziri Mkuu wake wakafungwa kifungo cha maisha.

Zidu naye alifungwa miaka mitano jela kwa kuwa alikuwa chini ya Rais ilikuwa lazima afate maagizo yake.

Inspekta Butu akarudi Kazini akipandishwa cheo na kuteuliwa mkuu wa Polisi ' IGP ' na Raisi aliyechaguliwa baada ya uchaguzi wa haki na amani ulosimamiwa na Jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sambamba na umoja wa mataifa.

Hakika mafia japo lilikuwa ni kundi baya Ila kisasi chake kikaliletea mwanga Taifa la Tanzania.

Amani sasa ikatawala katika maisha ya Butu alopita yakabaki Kama historia ambayo asingeweza kuisahau katika maisha yake.

Alimshukuru Mungu tu kwa kuwa bado yupo hai tena akiwa mkuu wa Polisi huru katika taifa lake.

MWISHO
KWA KUTUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK, LIKE UKURASA HUU USIPITWE NA SIMULIZI NA MENGINE HUKO FACEBOOK

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE TAZAMA VIDEO HII KAMA MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA

KWA TELEGRAMπŸ‘‡BONYEZA HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni