KUTI KAVU (1) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumatatu, 6 Februari 2023

KUTI KAVU (1)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA KWANZA
MGUU wa kushoto ulipiga hatua ukifuatiwa na ule wa kulia, hatua kwa hatua lengo likiwa ni kufika kule alikokusudia. Bila kujali amechoka kiasi gani, aliendelea kusonga mbele licha ya utitiri wa mawazo uliofurika kichwani mwake.

Viatu vyake aina ya mokasini nyeusi vilivyoanza kuchakaa, suruali yake nyeusi iliyopauka kiasi, na shati jeupe alilovaa, kwa pamoja vilitosha kabisa kudhihirisha hali ngumu ya uchumi aliyonayo kijana Dominic Masaka, au Domi kama wengi walivyolifupisha jina lake.

Domi alikuwa amechomekea vema, na kuonekana maridadi kwa mavazi yake licha ya mpauko uliodhihiri waziwazi kwenye mavazi aliyovaa.

Njaa iliyokuwa ikimfukuta tumboni mwake haikutosha kumkatisha tamaa na badala yake ilimuongezea hasira na kiu ya mafanikio ambayo ilikuwa ikijipambanua wazi wazi usoni pake.

Kijana huyu mrefu wa wastani, mwenye sura jamali alikuwa akikatisha katika mtaa wa Azikiwe maeneo ya Posta mpya, eneo ambalo liko katikati kabisa ya jiji la Dar es salaam.

Dominic alikuwa na mawazo mengi kichwani mwake ila mawili katika hayo ndiyo yaliyoonekana kumchanganya zaidi. Kwanza; ni aina ya maisha anayoishi, maisha ambayo aliona hayaendani kabisa na kiwango cha elimu aliyonayo!

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Kwa msomi kama yeye kuishi maisha anayoyaishi kwa sasa, ni aina ya maisha ambayo hayakumuingia kabisa akilini kijana Domi. “Maisha gani haya!” Domi alilalama.

Kila alipojaribu kutafuta unasaba uliopo baina ya elimu yake na aina ya maisha anayoyaishi, Domi alizidi kuchanganyikiwa kabisa!

Domi hakutaka kabisa kuamini kama kuna wasomi wa kiwango cha elimu yake, ambao wanaishi aina ya maisha anayoishi yeye. Kama wapo na wameiridhia aina hii ya maisha, basi yeye alikuwa kinyume kabisa na fikra zao.

Kwa Dominic, msomi wa kiwango cha elimu yake hakustahili katu kuishi maisha kama anayoyaishi yeye, ndiyo maana kila mahali na kila nukta ya saa Dominic amekuwa akihangaika kutafuta suluhisho la matatizo ya kiuchumi yanayomakabili.

Swala jingine lililoitesa akili ya Domi, ni juu ya mpenzi wake aitwaye Doi. Domi alikuwa akiustaajabia upendo wa Doi kwake, upendo ambao ni wa kupindukia licha ya ugumu wa maisha alio nao!

Doi alikuwa ni mwanamke mwenye mapenzi ya ajabu kwa Domi. Kwa sababu ya mapenzi hayo mazito kwa Domi, Doi aliridhia na kuvumilia kila hali aliyo nayo Domi! Domi aliutafakari sana upendo wa Doi kwake, lakini mfanowe hakuupata.

Ni siku ya tatu sasa, hawali chochote isipokuwa uji wa sembe usiokuwa na hata chembe ya sukari! “Baby, najua unanipenda kama mimi ninavyokupenda, nap engine hata zaid. Lakini hali ya maisha ni kama unavyoiona mpenzi. Unaonaje kama utarudi nyumbani kwanza, halafu nikishaweka mambo sawa nitakuja kukuchua.” Hiyo ilikuwa ni sauti ya Domi akijaribu kumrai mpenzi wake japo kwa shingo upande. Ndiyo ni kwa shingo upande kwa sababu, kwanza yeye kama mwanaume hakustahili kuonesha kuwa amekata tamaa kwenye kuihimili mikikimikiki ya maisha.

Pili, alihofu kauli hiyo isije kutafsiriwa na Doi kuwa ana mpango wa kumtema kijanja, na anautumia ugumu wa maisha kama kigezo ili iwe rahisi kwa Doi kumuelewa.

Kinyume na matarajio yake, Domi alishangazwa na majibu yaliyotolewa na Doi, “Nakupenda Domi, na kwa sababu nimekupenda kwa hiyari yangu toka moyoni, sina budi kuvumilia kila kitu. Usiwe na wasi wasi mpenzi… shida yako ni shida yangu, kwa nini niondoke, eti kwa sababu maisha yamekuwa magumu? Yana mwisho haya mpenzi wangu, cha msingi ni kutokata tamaa...”

Domi hakujua aseme nini na badala yake akawa anatokwa na machozi!

Kwa moyo wa kiume Domi akasema, “Siyo kama nakufukuza mpenzi, usinielewe vibaya… kwa nini uteseke na maisha haya wakati kwenu ungeweza kukipata kila unachokitaka, tofauti na hapa ambapo tunaishi maisha ya kubahatisha….”

“Ni kweli usemayo Domi, ningeweza kupata kila kitu ninachokitaka, lakini wewe siwezi kukupata nikiwa nyumbani kwetu. Niko hapa kwa ajili yako na si kitu kingine…” Alisema Doi na kumkumbatia Domi, “Nakupenda Domi….nakupenda sana” Doi alizidi kusisitiza huku akimtazama Domi kwa macho yaliyojaa huba. Domi alikuwa akiyakumbuka haya wakati yuko barabarani katika mitaa ya katikati kabisa mwa jiji la Dar es salaam.

Njaa ilikuwa ikimwuma lakini alijikaza kwa sababu hakuwa na jinsi. Alitembea mpaka pembeni ya jengo la ATC (Air Tanzania Cooperation) akalitazama lile jengo kwa jicho la matamanio, kisha akaelekea kwa fundi wa kung’arisha viatu aliyekuwa nje ya ya uzio wa jengo lile na kujipumzisha kwenye benchi la huyo mng’arisha viatu.

“Habari kaka” Domi alisalimia na kuitikiwa na yule mngarisha viatu ambaye tayari walikuwa wamekwishazoeana.

“Salama braza, karibu.”

“Ahsante braza, naomba nijipumzishe hapa ofisini kwako kidogo,”

“Hakuna shida, uko huru braza,” Alijibu yule mngarisha viatu huku akiachia tabasamu pana usoni pake.

Domi alikaa pale kimwili tu, na akili yake akaiacha iende safari, iendelee kutafakari juu ya aina

ya maisha anayoishi na mpenzi wake ili kuona ni jinsi gani atayapatia suluisho.

Akiwa kwenye lindi la mawazo, Domi alishtuliwa na mlio wa simu yake ya mkononi. Kwa haraka aliitoa simu mfukoni ili aipokee, lakini kabala hajaipokea aliona ni vema kama atasoma kwenye kioo cha simu ili amjue mpigaji wa simu hiyo. Macho ya Domi yalipotua kwenye kioo cha simu yake ya mkononi moyo wake ukaanza kumwenda mbio! Kwenye kioo hicho cha simu Domi aliliona jina alilolitarajia. Kwa moyo wa matumaini alibonyeza kitufe cha kijani ili kuruhusu mazungumzo na mpigaji wa ile simu, kabla hajafanikiwa kusema “Haloo..” simu yake ikazimika baada ya kuwa imeishiwa nguvu ya betri! Domi alichanganyikiwa baada ya kushuhudia simu yake ikiishiwa nguvu ya betri na kuzimika wakati ambao simu ya muhimu ilikuwa ikiingia.

Kwa haraka Domi hakujua afanye nini! Aliinuka pale kwenye benchi na kusimama wima.

“Vipi braza?” Yule mng’arisha viatu aliuliza.

“Simu yangu kaka!” Domi alijibu na kumuacha yule mng’arisha viatu njia panda kwa kutoa kauli inayoelea, ikabidi aulize tena, “Simu yako imekuwaje kaka?”

“Imeishiwa chaji wakati simu ya muhimu ilikuwa inaingia.”

“Oh… pole sana braza, kama simu yenyewe ni ya muhimu sana kama unavyosema, weka kadi ya simu yako kwenye simu yangu ili ufanye mawasiliano braza.” Alisema yule mng’arisha viatu huku akimpatia Domi simu ili abadilishe kadi ya simu aweze kufanya mawasiliano.

Domi hakujua ashukuru vipi kwa msaada huo! Aliipokea ile simu na kubadiri kadi ya simu kutoka kwenye simu yake kwenda kwenye simu ya mng’arisha viatu.

Wakati ambao Domi alikuwa akibadiri kadi ya simu, akili yake ilikuwa ikikabiliana na wakati mgumu sana. Alijua wazi kuwa simu yake haikuwa na pesa za kutosha kupiga simu! Nini kupiga? Simu yake haikuwa hata na pesa ya kushtua ili apigiwe, na mfukoni hakuwa na hata senti ambayo angeweza kuitumia kununua salio na kupiga simu. Hivyo wakati anafanya mabadiriko hayo, moyoni alikuwa kiomba yule mpigaji apige tena kwa mara nyingine ili aweze kuwasiliana nae.

Mungu si Athumani, kwani mara tu baada ya simu kuwaka, ile namba iliyompigia awali ikawa inapiga tena. Domi akashukuru kwa Mungu wake, akabonyeza kitufe cha kijani ili kuruhusu mawasiliano, “Haloo.. habari za leo?” sauti kutoka upande wa pili ilisikika.

“Salama, habari yako?” Domi alijibu ile salamu na kusalimiana na yule mtu wa upande wa pili ambaye pia alijbu na kuuliza swali, “Samahani ndugu…naongea na Dominic Masaka?”

“Bila shaka, ni mimi hapa ninaeongea” Alijibu Domi kwa utulivu wa hali ya juu kabisa.

“Sawa.. napiga simu kutoka KWITALE ADVOCATES & COMPANY, unaombwa kufika hapa kwenye ofisi zetu zilizoko hapa mitaa ya Posta kwenye jengo la ATC kuanzia saa 7:00 mchana, mpaka saa 9:30(saa tisa na nusu alasiri) na kama hutofanikiwa kufika leo, kampuni inakukaribisha tena kesho kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 9:30 alasiri.”

“Ahsante sana mkuu nimekuelewa” Domi alijibu.

“Ahsante kwa kunielewa, nakutakia mchana mwema.” Ile sauti ya upande wa pili ilihitimisha na kukata simu.

Maelezo yaliyotolewa kwenye simu yalifufua matumaini kwa Dominic, hakujua tena amshukuru vipi yule mngarisha viatu aliyempa simu yake afanyie mawasiliano.

Wakati huo saa yake ya mkononi ilisema ni saa 6:30 mchana. Kwa kuwa muda ulikuwa unaruhusu Domi hakuona sababu ya kusubiri mpaka kesho, wakati hakuna kinachomzuia kwenda leo.

Domi akageuka na kuliangalia lile jengo la ATC ambalo alikaa kwenye benchi kwa kulipa mgongo, kisha akaanza kurekebisha mavazi yake mwilini kwa kulichomeka vizuri shati lake ndani ya suruali, halafu akachukua brashi ya viatu na kuanza kufuta vumbi lilotapakaa kwenye viatu vyake. Na mara baada ya kumaliza alimrudishia yule mng’arisha viatu simu yake huku akishukuru kwa kumwambia, “Ahsante braza, ubarikiwe sana..”

Wakati Domi anaaga kuondoka yule mngarisha viatu akamwambia, “Kila la kheri kaka” Domi akampungia mkono na kuondoka kuelekea kwenye geti lililokuwa hatua chache kutoka alipokuwa huku moyo wake ukimdunda.
****
Sauti ya redio iliendelea kusikika na kukienea chumba kizima! Wimbo uliokuwa ukisikika kutoka kwenye spika za redio ulimfanya Doi atokwe na machozi.

Akiwa ameketi kitandani, mkononi ameshikilia kalamu, na karatasi ikiwa mapajani mwake Doi aliendelea kuandika licha ya machozi yaliyoendelea kumbubujika.

Baada ya kumaliza kuandika Doi aliipitia tena ile barua yake kwa umakini wa hali ya juu, ilhali machozi yakiendelea kusheheni mashavuni mwake. Aliisoma tena na tena huku wimbo wa ‘barua’ ulioimbwa na kikundi cha muziki wa kizazi kipya cha ‘Daz Nundaz’ ukimalizikia katika spika za redio yake.

Kila aliporudia kuisoma barua yake, Doi alishindwa kabisa kuyatofautisha maudhui ya wimbo ule na kile alichokuwa akikifanya kwa wakati huo!


Baada ya kujiridhisha, aliikunja ile barua na kuiweka chini ya mto mahali ambapo alijua fika kuwa ni lazima Domi ataiona. Mara baada ya kufanya hivyo Doi aligeuka nyuma akiwa chumbani mule, na hapo ndipo alipoiona picha waliyopiga na Domi ikiwa ukutani. Ni wazi kuwa picha ile ilikuwa kama inamsuta kwa kile anachokifanya!

Doi akapiga moyo konde na kuishika simu yake ya mkononi, alipotupia macho kwenye kioo cha simu hiyo kwa lengo la kujua muda, Doi alibaini kuwa muda ulikuwa ukielekea ukingoni. Akauendea mkoba wake na kutoa bulungutu la noti la dola za kimarekani na kuliweka pale chini ya mto sambamba na ile barua kisha akaichukua picha ya Domi ambayo aliipiga siku ya mahafali yake ya kuhitimu shahada yake ya kwanza, picha ambayo huwekwa kwenye meza iliyoko chumbani mule. Kwenye ile picha Domi alionekana akiwa mwenye furaha kupindukia kwa sababu ya tabasamu mwanana alilokuwa nalo kwenye picha ile.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni