Notifications
  • THE NIGHTMARE (9)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TISAILIPOISHIA...“mmenifananisha, mimi ndio kwanza naigia ofisini mida hii.” Aliongea yule afande na kuigia kituoni.“sasa aliyekuwa anatuhoji ni nani kama sio huyo?”Alijikuta anajiuliza mwenyewe swali lililompa utata mkubwa kichwani mwake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wakati wakiwa hawajui hili wala lile, walishangaa kuona maaskari wakijazana pale na ambulance ikafika…
  • THE NIGHTMARE (8)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NANEILIPOISHIA...Walipofika feri, walipewa nahodha mwingine tofauti na yule aliyemuota na boti ilikuwa ndogo tu ya kawaida tofauti na ile aliyoiota.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Sharji alijikuta anapiga makelele baada ya kumuona Balqis akiwa amejaa damu mdomoni huku ametoa makucha yake akimfata kwa nia ya kumdhuru.“AAAAAAAAAAAGH”Sharji alipiga kelele na kukurupuka.…
  • THE NIGHTMARE (7)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SABAILIPOISHIA...“kha!!!!”Ulikua mshangao mkubwa kwa watu karibu wote baada ya kumuona Sharji akiwa na taulo akitoka chumbani kwa Balqis.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wengine walicheka na kaka yake alionekana kutoifurahia hali ile.“sasa wewe unatutia wasi wasi bure, si ungesema tu kama unaenda kulala kwa huyu dada?” aliongea kaka yake na kukirudia kile chumba alichompangia…
  • THE NIGHTMARE (6)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SITAILIPOISHIA...“toa loud speaker bwana.”Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya…
  • THE NIGHTMARE (5)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TANOILIPOISHIA...Alijikuta outomatic akijisemea kwa mshangao baada ya kumuona dada mmoja mrembo mwenye asili ya kiarabu akiingia mule ndani. Hakuvaa ushungi kama alivyowazoea kuwaona waarabu wengi ambao alikutana nao. Huyu alivaa suruali ya jeanz nyeusi na juu akiwa na kikoti chake cheusi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Kati kati kulikua na nguo Fulani nyeupe iliyonakshiwa…
  • THE NIGHTMARE (4)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NNEILIPOISHIA...Aliongea Khalidi na kuufungua mkanda wa suruali yake na kuanza kumtandika Karim.“unanipiga mimi?...utaona!”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Aliongea Karim na kuondoka huku analia.*****************************Zilipita wiki mbili bila ya Karim kuonekana nyumbani kwao. Sabra alisikitika kidogo kutokana na kuwapenda sana watoto wake japokuwa huyo mtoto mkubwa hakuwa…
  • Fumanizi la Mchepuko Mwizi😂 | Comedy
    Mume amefuma viatu vya mchepuko wa mke wake mlangoni lakini akakosea kuingia ndani kabla aweke umakini kwenye hivyo viatu mwisho wa siku akaibiwa na vyake😂Hili tukio lazima lichukuchekeshe sana hata kama ulikuwa haujataka kuchekaItazame kisha nipe like na ukinipa maoni kwenye comment nitashukuru sanaUsisahau kubonyeza Subscribe kama haujajiunga na fungua #ChekanaZephiline kupata video zangu zote ambazo zipo mtandaoniNashukuru sana kwa wewe ambaye unanipa nguvu ya kuendelea kuwaletea kazi nzuri…
  • THE NIGHTMARE (3)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TATUILIPOISHIA...Akiwa hewani akikata mawingu kurudi Tanzania, kichwa chake kilikua na mawazo mengi sana juu ya mume wake. Aliikumbuka siku waliyofunga ndoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Pia alijua kwanini mume wake alipendelea kufanya kazi uingereza na yeye kumfungulia ofisi huku huku Tanzania. Hakujua kuwa kazi anayoifanya mumewe ni ile ya kutembea na tajiri mkubwa…
  • THE NIGHTMARE (2)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA PILIILIPOISHIA...Khalidi alishangaa kuitwa na mtu asiyemfahamu. Alitoka na kwenda kumuangalia huyo mtu maana kiukweli hakua na ndugu aishie hapa Dar hata mmoja anayemfahamu..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Alipigwa na butwaa baada ya kumuona Sabra pale.“ahsante mungu.” Aliongea Khalidi baada ya kumuona tu yule binti pale.“pole sasa kaka yangu, nisamahe mie.” Aliongea Sabra kwa…
  • THE NIGHTMARE (1)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA KWANZANi kipindi cha mvua za masika. Upepo mkali, na mvua kubwa iliendelea kunyesha kwa kasi kila kona ya nchi ya Tanzania.Ipo mikoa iliyofurahia mvua hizo kwa kuwa walikua wanaisubiria kwa hamu kwa ajili ya kilimo. Lakini ipo mikoa iliyokua inapata shida kwa uharabifu wa mazingira na mengineyo mengi.Moja ya miko hiyo ni Dar-es-salaam. Watu wanaoishi katika mkoa huo walichukia mvua mfululizo kutokana na sababu mbalimbali. Biashara nyingi…

KUTI KAVU (2)


Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA...
Akauendea mkoba wake na kutoa bulungutu la noti la dola za kimarekani na kuliweka pale chini ya mto sambamba na ile barua kisha akaichukua picha ya Domi ambayo aliipiga siku ya mahafali yake ya kuhitimu shahada yake ya kwanza, picha ambayo huwekwa kwenye meza iliyoko chumbani mule. Kwenye ile picha Domi alionekana akiwa mwenye furaha kupindukia kwa sababu ya tabasamu mwanana alilokuwa nalo kwenye picha ile.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Doi aliishika ile picha kwa mapenzi mazito, kisha wazi wazi akaia nafsi yake ikimsuta! Machozi yakaongezeka zaidi, akaibusu ile picha na kuitazama tena kwa mara nyingine kisha akairudisha pale ilipokuwa awali. Akaufungua mkoba wake na kutoa leso kwa ajili ya kufutia machozi yaliyoenea mashavuni mwake.

Doi akatoka nje na kuufunga mlango akiwa na mkoba wake begani. Akaanza kupiga hatua za kuondoka, hatua chache kutoka mlangoni Doi aligeuka nyuma na kuutizama tena ule mlango akiwa hana uhakika kama atauona tena kwa siku za karibuni. Doi akageuka na kuendelea na safari yake wakati huo saa ya kwenye simu yake ilionesha saa 6:56 mchana.
****
Gari aina ya marcedes Benzi yenye rangi nyeusi ilikuwa imeegeshwa kando ya barabara ya vumbi, huku muziki mkubwa ukisikika kutoka ndani yake. Damian aliyekuwa ndani ya gari hiyo aliinua mkono wake na kuitazama saa yake ya mkononi, alifanya hivyo mara kadhaa huku akionesha hali ya kuanza kuingiwa na wasiwasi.

Damiana alipunguza sauti ya redio na kubonyeza bonyeza simu yake kisha akaiweka sikioni, “Mtumiaji wa simu unayempigia hapatikani kwa sasa, tafadhali… jaribu tena baadaye.” hiyo ilikuwa ni sauti iliyosikika kutoka kwenye spika ya simu yake, sauti ambayo ilizidi kumchanganya kabisa Damian! Akaiona simu hiyo kuwa haina tena msaada kwake, akaitupa kwenye kiti cha abiria kilichokuwa kushoto kwake.

Damian akaitazama tena saa yake katika hali ya kuhamanika zaidi!

Kupitia kwenye kioo cha pembeni cha gari, kioo cha mkono wake wa kulia, Damian aliona kitu a

mbacho kiliuteka umakini wake! Akayagandisha macho yake kwenye kile kioo na mara pole pole akaanza kuruhusu tabasamu lichukue nafasi usoni pake!

Ni wazi kuwa Damian alikiona kile alichokua akikisubiri kwa muda wote! Alikuwa ni msichana mrefu kiasi, mwenye wembamba wa kawaida, akiwa amevaa miwani myeusi, sambamba na gauni refu lililoyasitiri sawia maungo yake. kifua chake hakikuwa kikubwa sana, kilikuwa ni cha wastani. Kiufupi ni kwamba umbo la mwanamke huyo lilifutuka kwenye mapaja yake kuelekea pembeni kila upande na kumfanya afanane na ile namba iliyo katikati ya saba na tisa, yaani namba nane. Muonekano wake huo ulimfanya aonekane mrembo kupindukia na kuwa kivutio kwa wenye macho yanayoona!

Damian alikuwa akiitambua tabu inayoachwa nyuma na mrembo yule kwa kila aliyemtazama baada ya kuwa amemuachia mgongo. Kwani makalio yake yalikuwa yametuna mithili ya kichuguu. Hili Damian alilijua fika!

Mrembo yule alizidi kusogea kule ilipo gari ambayo Damian alikuwa ndani yake. Tabasam la Damian likazidi kujipambanua zaidi! Na punde si punde mrembo yule akafika! Damian akamfungulia mlango yule mrembo akaingia garini.

“Pole kwa kukuweka, kuna mambo kidogo yalinichukulia muda ndiyo maana nimechelewa. Halikuwa lengo langu..” alijaribu kujitetea yule msichana

“Usijali mpenzi hujachelewa sana” Damian alisema huku akimkumbatia yule mrembo na kuyakatisha maneno yake kwa mabusu motomoto, kisha akasema “Doi mpenzi…..” Damian alisita kidogo huku akimuangalia Doi usoni bila ya kujua aongee nini! Mara ghafla sauti ikamtoka Damian, “Nakupenda Doi..” Damian hakutaka kusubiri jibu kutoka kwa Doi. Aliitekenya gari ambayo nayo ilicheka bila ubishi, akamgeukia Doi akamtizama bila kusema neno kisha akajiweka sawia na kutazama mbele. Polepole akaanza kuipeleka gari ilipo barabara ya lami!

Walipofika kwenye barabara ya Lami, Damian akaipa gari mwendo wakatokomea kuelekea mjini, wakitokea Yombo Buza maeneo ya kiwanja cha Tanesco. Wakati huo ikiwa ni saa 7:12 mchana.
***
Saa 7:00 mchana Dominic alikuwa akimalizia kupanda ngazi za jengo la ATC, jengo ambalo ndani yake kulikuwa na ofisi za kampuni ya mawakili ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

Dominic aliongoza moja kwa moja mpaka mapokezi ambako alimkuta dada wa mapokezi. Yule dada wa mapokezi alimchangamkia sana Dominic!

Baada ya salamu Dominic alijitambulisha, “Samahani dada, mimi naitwa Bwana Dominic Masaka ni…” kabla hajamaliza kauli yake yule dada alidakia akamkatisha kwa kusema, “Ninakukumbuka vizuri sana Bwana Masaka, huna haja ya kujitambulisha, nilikuona hapa siku ile mlipokuja kwenye ya usaili.”

“Ok…. Vizuri sana dada, niko hapa kwa…..”

“Kwa ajili ya kumuona Bwana Makeke” Yule dada alidakia tena na kumuacha hoi Dominic!

Yule dada wa mapokezi alionekana kuwa ni muongeaji sana, na hata kazi yake ya mapokezi ilionekana kumfaa haswa!

“Nenda moja kwa moja mpaka ofisi ya katibu, tayari ana taarifa zako.” Alisema yule dada huku akimuonesha Domi ofisi ya katibu ilipo.

Wakati Domi anaondoka kuelekea ofisi ya katibu, aliisikia sauti ya yule dada akimuita, “Mr Dominic…” Domi akasimama ili kumsikiliza. “My name is Neema” alisema yule dada huku akiachia tabasamu murua!

Dominic aliitikia kwa kichwa huku akiwa na yeye anatabasam, kisha akampungia mkono kuashiria kuwa amemuelewa.

Dominic alienda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya katibu, alipofika walisalimiana na baadaye Dominic alielekezwa kukaa kwenye kiti kilichokuwa mbele ya meza kubwa ya kiofisi iliyokuwa ofisini mule.

“Mimi naitwa Mr Makeke Cosmas, ndiye katibu wa KWITALE ADVOCATES & COMPANY sijui mwenzangu unaitwa nani?” alisema Makeke ambaye kwa muonekano alikuwa ni mtu wa makamo, ambaye umri wake ni kati ya miaka thelasini na saba mpaka arobaini hivi. Alikuwa amevaa suti nadhifu nyeusi sambamba na tai nyekundu kifuani pake. Alikata nywele zake kwa mtindo wa low cut na kuzifanya zionekane fupi na zenye mvuto.

“Mimi naitwa Dominic Masaka, muda mfupi uliopita nilipigiwa simu kuwa ninahitajika hapa ofisini”

“Ok, vizuri sana. Nashukuru kukufahamu Bwana Masaka, karibu sana KWITALE.” Alisema Makeke huku akifunua baadhi ya mafaili yaliyokuwa mezani kwake.

“Ahsante sana Bwana Makeke” Alijibu Dominic.

Baada ya muda mfupi, bwana Makeke alikuwa ameshikilia faili moja mkononi mwake, likiwa limeandikwa ‘Dominic Masaka’ akasimama na kumwambia Dominic amfuate.

Dominic alitii, wakatoka pale na kuingia ndani zaidi ambako walimkuta mtu mwingine.

Ndani ya ofisi walimoingia mlikuwa na vitabu vingi vilivyopangwa kwenye ngazi kwa utaratibu maalum uliovifanya vivutie zaidi.

“Habari za saizi tena bwana Kwitale” Makeke alisalimia na kufanya utambulisho mfupi, “Ninayo furaha kubwa kumtambulisha kwako ndugu Dominic Masaka, na bwana Masaka, huyu ndiye bwana Kwitale mkurugenzi mtendaji wa hii kampuni yetu ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.” Alisema Makeke huku akiwaangalia wote Masaka na Kwitale kwa zamu kila mmoja.

Walipeana mikono na bwana Kwitale akamkaribisha Dominic, “Karibu sana ndugu Dominic, jisikie huru kuwa ndani ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.”

“Ahsante sana bwana Kwitale” Alijibu Dominic kwa utulivu na uwekevu wa hali ya juu.

Makeke na Dominic walikaa kwenye viti vilivyokuwa mbele ya meza kubwa ya kiofisi iliyowatenganisha na bwana Kwitale.

“Bwana Dominic Masaka!” bwana Kwitale ambaye alionekana kuwa amekula chumvi si haba alimuita Dominic kwa ukamilifu wa jina lake.

“Naam, bwana Kwitale.” Dominic aliyekuwa ametulia kimya na kwa umakini aliitika na bwana Kwitale akaendelea, “Tumepitia taarifa zako na tumeridhika nazo, na tukaona ni vema kama tutakuajiri ili uzibe pengo la wakili mmoja ambalo limekuwa wazi kwa muda mrefu. Hivyo nitakuomba uupitie mkataba wetu na kama utaridhika nao uanze kazi mara moja.” Taarifa hii ilipotua masikioni mwa Dominic ilimshtua na kuyabadili mapigo yake ya moyo. Dominic alikuwa kama asiyeamini kile alichokisikia muda mfupi uliopita, akajiona mwenye bahati kwani ametafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio! Na leo hii, muda huu anapata taarifa, tena taarifa kutoka kwa mkurugenzi kuwa anahitajika kuziba nafasi iliyo wazi kwa muda mrefu na tayari amepewa mkataba kwa ajili ya kupitia vipengele vya mkataba huo ili kujiridhisha kabla hajamwaga wino na kuwa mtumishi rasmi wa KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

Dominic alikuwa akipitisha macho kwenye ule mkataba huku mawazo yake yakiwa kwa Doi mpenzi wake, ambaye wamekuwa naye bega kwa bega katika shida na raha bila kujali umasikini alio nao. Domi aliona kuwa muda wa kumvika Doi taji la ushindi ndiyo huu umefika na furaha iliyokuwa imeugubika moyo wa Domi, hakika sijawahi kuimithilisha!

Dominic akaweka sahihi yake kwenye mkataba ule wa ajira na kuwa mwajiriwa rasmi wa kampuni ya wanasheria ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY. Akiwa ameajiriwa kama mwanasheria, taaluma aliyoipenda kuliko zote.

“Eee Mungu ninakushukuru kwa hili kama nilivyokuwa nikikushukuru kwa mengine yote. Naomba Baraka zako na ulinzi wako katika maisha yangu. Amina!” Dominic alikuwa akisali kimya kimya bila kutoa sauti.

Mara baada ya kuwa amemwaga wino kwenye mkataba, Bwana Kwitale alivuta mtoto wa meza na kutoa burungutu la noti za kitanzania zenye thamani ya shilingi laki moja, sambamba na pesa hizo pia Dominic alikabidhiwa hundi ya shilingi milioni mbili, pamoja na funguo za gari. Vitu ambavyo hupewa wafanya kazi wa KWITALE mara tu waajiliwapo ili kuboresha utendaji na ufanisi wao kazini.

“Baada ya wiki moja utapaswa kuhamia kwenye nyumba ambayo kampuni imekupangia. Nakutakia utendaji mwema na unapokuwa KWITALE jisikie uko nyumbani.” Alisema Bwana Kwitale wakati anamkabidhi Dominic vitu hivyo.

Kwa Dominic kila kitu kilikuwa ni kama ndoto! Aliona ameuaga umasikini ghafla mno.

Akawaza sana juu ya kila kinachotokea, alihisi ni kama ndoto na hakutaka kabisa kuishuhudia ndoto hiyo ikiisha na yeye kuurudia umasikini wake uliomtesa kwa muda mrefu!

“Muda wa kutembea kwa miguu kwa kukosa nauli leo umefika kikomo. Mateso ya kushinda na kulala njaa kwa kukosa chakula leo yamefika mwisho. Na ile purukushani na mende kwenye kile kijichumba kibovu leo inahitimishwa, oooh… ahsante Mungu” Dominic aliwaza.

Baadya kukamilisha kila kitu pale ofisni Dominic aliondoka akiwa mwenye furaha sana. Alitamani akifumba macho na kuyafumbua awe tayari ameshafika nyumbani, ili amueleze na kumuonesha kila kitu mpenzi wake.

Dominic aliyetoka nyumbani kwa miguu sasa alikuwa amekumbatia uskani wa gari akiendesha kueleka nyumbani ili kumuwahi mpenzi wake, ambaye alimuacha asubuhi nyumbani bila chakula, zaidi ya unga wa sembe ambao alitakiwa kukoroga uji na kuunywa ili kupunguza makali ya njaa.

Njiani Dominic aliendesha gari kwa kasi, kwa nia na madhumuni ya kuwahi nyumbani na kumpasha mapenzi wake kuwa; matatizo yote yaliyokuwa yakisababishwa na ukosefu wa pesa sasa yametamatishwa, baada ya yeye, yaani Dominic kupata kazi katika kampuni ya mawakili ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413
43 Kuti Kavu Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni