KUTI KAVU (2) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumatatu, 6 Februari 2023

KUTI KAVU (2)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA...
Akauendea mkoba wake na kutoa bulungutu la noti la dola za kimarekani na kuliweka pale chini ya mto sambamba na ile barua kisha akaichukua picha ya Domi ambayo aliipiga siku ya mahafali yake ya kuhitimu shahada yake ya kwanza, picha ambayo huwekwa kwenye meza iliyoko chumbani mule. Kwenye ile picha Domi alionekana akiwa mwenye furaha kupindukia kwa sababu ya tabasamu mwanana alilokuwa nalo kwenye picha ile.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Doi aliishika ile picha kwa mapenzi mazito, kisha wazi wazi akaia nafsi yake ikimsuta! Machozi yakaongezeka zaidi, akaibusu ile picha na kuitazama tena kwa mara nyingine kisha akairudisha pale ilipokuwa awali. Akaufungua mkoba wake na kutoa leso kwa ajili ya kufutia machozi yaliyoenea mashavuni mwake.

Doi akatoka nje na kuufunga mlango akiwa na mkoba wake begani. Akaanza kupiga hatua za kuondoka, hatua chache kutoka mlangoni Doi aligeuka nyuma na kuutizama tena ule mlango akiwa hana uhakika kama atauona tena kwa siku za karibuni. Doi akageuka na kuendelea na safari yake wakati huo saa ya kwenye simu yake ilionesha saa 6:56 mchana.
****
Gari aina ya marcedes Benzi yenye rangi nyeusi ilikuwa imeegeshwa kando ya barabara ya vumbi, huku muziki mkubwa ukisikika kutoka ndani yake. Damian aliyekuwa ndani ya gari hiyo aliinua mkono wake na kuitazama saa yake ya mkononi, alifanya hivyo mara kadhaa huku akionesha hali ya kuanza kuingiwa na wasiwasi.

Damiana alipunguza sauti ya redio na kubonyeza bonyeza simu yake kisha akaiweka sikioni, “Mtumiaji wa simu unayempigia hapatikani kwa sasa, tafadhali… jaribu tena baadaye.” hiyo ilikuwa ni sauti iliyosikika kutoka kwenye spika ya simu yake, sauti ambayo ilizidi kumchanganya kabisa Damian! Akaiona simu hiyo kuwa haina tena msaada kwake, akaitupa kwenye kiti cha abiria kilichokuwa kushoto kwake.

Damian akaitazama tena saa yake katika hali ya kuhamanika zaidi!

Kupitia kwenye kioo cha pembeni cha gari, kioo cha mkono wake wa kulia, Damian aliona kitu a

mbacho kiliuteka umakini wake! Akayagandisha macho yake kwenye kile kioo na mara pole pole akaanza kuruhusu tabasamu lichukue nafasi usoni pake!

Ni wazi kuwa Damian alikiona kile alichokua akikisubiri kwa muda wote! Alikuwa ni msichana mrefu kiasi, mwenye wembamba wa kawaida, akiwa amevaa miwani myeusi, sambamba na gauni refu lililoyasitiri sawia maungo yake. kifua chake hakikuwa kikubwa sana, kilikuwa ni cha wastani. Kiufupi ni kwamba umbo la mwanamke huyo lilifutuka kwenye mapaja yake kuelekea pembeni kila upande na kumfanya afanane na ile namba iliyo katikati ya saba na tisa, yaani namba nane. Muonekano wake huo ulimfanya aonekane mrembo kupindukia na kuwa kivutio kwa wenye macho yanayoona!

Damian alikuwa akiitambua tabu inayoachwa nyuma na mrembo yule kwa kila aliyemtazama baada ya kuwa amemuachia mgongo. Kwani makalio yake yalikuwa yametuna mithili ya kichuguu. Hili Damian alilijua fika!

Mrembo yule alizidi kusogea kule ilipo gari ambayo Damian alikuwa ndani yake. Tabasam la Damian likazidi kujipambanua zaidi! Na punde si punde mrembo yule akafika! Damian akamfungulia mlango yule mrembo akaingia garini.

“Pole kwa kukuweka, kuna mambo kidogo yalinichukulia muda ndiyo maana nimechelewa. Halikuwa lengo langu..” alijaribu kujitetea yule msichana

“Usijali mpenzi hujachelewa sana” Damian alisema huku akimkumbatia yule mrembo na kuyakatisha maneno yake kwa mabusu motomoto, kisha akasema “Doi mpenzi…..” Damian alisita kidogo huku akimuangalia Doi usoni bila ya kujua aongee nini! Mara ghafla sauti ikamtoka Damian, “Nakupenda Doi..” Damian hakutaka kusubiri jibu kutoka kwa Doi. Aliitekenya gari ambayo nayo ilicheka bila ubishi, akamgeukia Doi akamtizama bila kusema neno kisha akajiweka sawia na kutazama mbele. Polepole akaanza kuipeleka gari ilipo barabara ya lami!

Walipofika kwenye barabara ya Lami, Damian akaipa gari mwendo wakatokomea kuelekea mjini, wakitokea Yombo Buza maeneo ya kiwanja cha Tanesco. Wakati huo ikiwa ni saa 7:12 mchana.
***
Saa 7:00 mchana Dominic alikuwa akimalizia kupanda ngazi za jengo la ATC, jengo ambalo ndani yake kulikuwa na ofisi za kampuni ya mawakili ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

Dominic aliongoza moja kwa moja mpaka mapokezi ambako alimkuta dada wa mapokezi. Yule dada wa mapokezi alimchangamkia sana Dominic!

Baada ya salamu Dominic alijitambulisha, “Samahani dada, mimi naitwa Bwana Dominic Masaka ni…” kabla hajamaliza kauli yake yule dada alidakia akamkatisha kwa kusema, “Ninakukumbuka vizuri sana Bwana Masaka, huna haja ya kujitambulisha, nilikuona hapa siku ile mlipokuja kwenye ya usaili.”

“Ok…. Vizuri sana dada, niko hapa kwa…..”

“Kwa ajili ya kumuona Bwana Makeke” Yule dada alidakia tena na kumuacha hoi Dominic!

Yule dada wa mapokezi alionekana kuwa ni muongeaji sana, na hata kazi yake ya mapokezi ilionekana kumfaa haswa!

“Nenda moja kwa moja mpaka ofisi ya katibu, tayari ana taarifa zako.” Alisema yule dada huku akimuonesha Domi ofisi ya katibu ilipo.

Wakati Domi anaondoka kuelekea ofisi ya katibu, aliisikia sauti ya yule dada akimuita, “Mr Dominic…” Domi akasimama ili kumsikiliza. “My name is Neema” alisema yule dada huku akiachia tabasamu murua!

Dominic aliitikia kwa kichwa huku akiwa na yeye anatabasam, kisha akampungia mkono kuashiria kuwa amemuelewa.

Dominic alienda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya katibu, alipofika walisalimiana na baadaye Dominic alielekezwa kukaa kwenye kiti kilichokuwa mbele ya meza kubwa ya kiofisi iliyokuwa ofisini mule.

“Mimi naitwa Mr Makeke Cosmas, ndiye katibu wa KWITALE ADVOCATES & COMPANY sijui mwenzangu unaitwa nani?” alisema Makeke ambaye kwa muonekano alikuwa ni mtu wa makamo, ambaye umri wake ni kati ya miaka thelasini na saba mpaka arobaini hivi. Alikuwa amevaa suti nadhifu nyeusi sambamba na tai nyekundu kifuani pake. Alikata nywele zake kwa mtindo wa low cut na kuzifanya zionekane fupi na zenye mvuto.

“Mimi naitwa Dominic Masaka, muda mfupi uliopita nilipigiwa simu kuwa ninahitajika hapa ofisini”

“Ok, vizuri sana. Nashukuru kukufahamu Bwana Masaka, karibu sana KWITALE.” Alisema Makeke huku akifunua baadhi ya mafaili yaliyokuwa mezani kwake.

“Ahsante sana Bwana Makeke” Alijibu Dominic.

Baada ya muda mfupi, bwana Makeke alikuwa ameshikilia faili moja mkononi mwake, likiwa limeandikwa ‘Dominic Masaka’ akasimama na kumwambia Dominic amfuate.

Dominic alitii, wakatoka pale na kuingia ndani zaidi ambako walimkuta mtu mwingine.

Ndani ya ofisi walimoingia mlikuwa na vitabu vingi vilivyopangwa kwenye ngazi kwa utaratibu maalum uliovifanya vivutie zaidi.

“Habari za saizi tena bwana Kwitale” Makeke alisalimia na kufanya utambulisho mfupi, “Ninayo furaha kubwa kumtambulisha kwako ndugu Dominic Masaka, na bwana Masaka, huyu ndiye bwana Kwitale mkurugenzi mtendaji wa hii kampuni yetu ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.” Alisema Makeke huku akiwaangalia wote Masaka na Kwitale kwa zamu kila mmoja.

Walipeana mikono na bwana Kwitale akamkaribisha Dominic, “Karibu sana ndugu Dominic, jisikie huru kuwa ndani ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.”

“Ahsante sana bwana Kwitale” Alijibu Dominic kwa utulivu na uwekevu wa hali ya juu.

Makeke na Dominic walikaa kwenye viti vilivyokuwa mbele ya meza kubwa ya kiofisi iliyowatenganisha na bwana Kwitale.

“Bwana Dominic Masaka!” bwana Kwitale ambaye alionekana kuwa amekula chumvi si haba alimuita Dominic kwa ukamilifu wa jina lake.

“Naam, bwana Kwitale.” Dominic aliyekuwa ametulia kimya na kwa umakini aliitika na bwana Kwitale akaendelea, “Tumepitia taarifa zako na tumeridhika nazo, na tukaona ni vema kama tutakuajiri ili uzibe pengo la wakili mmoja ambalo limekuwa wazi kwa muda mrefu. Hivyo nitakuomba uupitie mkataba wetu na kama utaridhika nao uanze kazi mara moja.” Taarifa hii ilipotua masikioni mwa Dominic ilimshtua na kuyabadili mapigo yake ya moyo. Dominic alikuwa kama asiyeamini kile alichokisikia muda mfupi uliopita, akajiona mwenye bahati kwani ametafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio! Na leo hii, muda huu anapata taarifa, tena taarifa kutoka kwa mkurugenzi kuwa anahitajika kuziba nafasi iliyo wazi kwa muda mrefu na tayari amepewa mkataba kwa ajili ya kupitia vipengele vya mkataba huo ili kujiridhisha kabla hajamwaga wino na kuwa mtumishi rasmi wa KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

Dominic alikuwa akipitisha macho kwenye ule mkataba huku mawazo yake yakiwa kwa Doi mpenzi wake, ambaye wamekuwa naye bega kwa bega katika shida na raha bila kujali umasikini alio nao. Domi aliona kuwa muda wa kumvika Doi taji la ushindi ndiyo huu umefika na furaha iliyokuwa imeugubika moyo wa Domi, hakika sijawahi kuimithilisha!

Dominic akaweka sahihi yake kwenye mkataba ule wa ajira na kuwa mwajiriwa rasmi wa kampuni ya wanasheria ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY. Akiwa ameajiriwa kama mwanasheria, taaluma aliyoipenda kuliko zote.

“Eee Mungu ninakushukuru kwa hili kama nilivyokuwa nikikushukuru kwa mengine yote. Naomba Baraka zako na ulinzi wako katika maisha yangu. Amina!” Dominic alikuwa akisali kimya kimya bila kutoa sauti.

Mara baada ya kuwa amemwaga wino kwenye mkataba, Bwana Kwitale alivuta mtoto wa meza na kutoa burungutu la noti za kitanzania zenye thamani ya shilingi laki moja, sambamba na pesa hizo pia Dominic alikabidhiwa hundi ya shilingi milioni mbili, pamoja na funguo za gari. Vitu ambavyo hupewa wafanya kazi wa KWITALE mara tu waajiliwapo ili kuboresha utendaji na ufanisi wao kazini.

“Baada ya wiki moja utapaswa kuhamia kwenye nyumba ambayo kampuni imekupangia. Nakutakia utendaji mwema na unapokuwa KWITALE jisikie uko nyumbani.” Alisema Bwana Kwitale wakati anamkabidhi Dominic vitu hivyo.

Kwa Dominic kila kitu kilikuwa ni kama ndoto! Aliona ameuaga umasikini ghafla mno.

Akawaza sana juu ya kila kinachotokea, alihisi ni kama ndoto na hakutaka kabisa kuishuhudia ndoto hiyo ikiisha na yeye kuurudia umasikini wake uliomtesa kwa muda mrefu!

“Muda wa kutembea kwa miguu kwa kukosa nauli leo umefika kikomo. Mateso ya kushinda na kulala njaa kwa kukosa chakula leo yamefika mwisho. Na ile purukushani na mende kwenye kile kijichumba kibovu leo inahitimishwa, oooh… ahsante Mungu” Dominic aliwaza.

Baadya kukamilisha kila kitu pale ofisni Dominic aliondoka akiwa mwenye furaha sana. Alitamani akifumba macho na kuyafumbua awe tayari ameshafika nyumbani, ili amueleze na kumuonesha kila kitu mpenzi wake.

Dominic aliyetoka nyumbani kwa miguu sasa alikuwa amekumbatia uskani wa gari akiendesha kueleka nyumbani ili kumuwahi mpenzi wake, ambaye alimuacha asubuhi nyumbani bila chakula, zaidi ya unga wa sembe ambao alitakiwa kukoroga uji na kuunywa ili kupunguza makali ya njaa.

Njiani Dominic aliendesha gari kwa kasi, kwa nia na madhumuni ya kuwahi nyumbani na kumpasha mapenzi wake kuwa; matatizo yote yaliyokuwa yakisababishwa na ukosefu wa pesa sasa yametamatishwa, baada ya yeye, yaani Dominic kupata kazi katika kampuni ya mawakili ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni