KUTI KAVU (10) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Alhamisi, 9 Februari 2023

KUTI KAVU (10)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA KUMI
ILIPOISHIA...
Balaa ambalo kwa jinsi anavyowajua wazazi wake lilikuwa limewazid uwezo mara sabini. Doi alimjua fika baba yake mzee Vioja, mzee aliyeogopa mahakama kuliko njaa! Mtu wa namna hii ni vipi angeweza kumpigania? Alipoyafikilia hayo matumaini yake kuiepa jela yakazidi kupungua nukta baada nukta

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Baada ya Mudi kuondoka kutoka katika nyumba ambayo alimfumania mkewe mtarajiwa Zainabu Mpotoshi na kuwaacha Mapunda na Zai wakiwa katika hali ya sintofahamu. Mudi aliondoka akiwa na msongo wa mawazo huku akiwaraani kabisa wanawake wote kwa sababu ya kile alichofanya Zai.

Aipofika tu nyumbani kwake, kwanza alihakikisha amemwona bi Udaku mtonyaji wake, ambaye kwa msaada wake ameweza kuyagundua madhambi ya Zai akamshukuru. Licha ya kumshukuru bi Udaku kwa hilo, chuki yake kwa wanawake bado haikukoma.

Mudi alimpa bi Udaku kiasi cha pesa kwa ajili ya kulipia pikipiki aliyotumia kumfuatilia Zai tangu Buza mpaka Jeti Corner. Pia alichukua nguo za gharama za Zai, nguo ambazo alizinunua yeye ili mkewe avae apendeze, nguo hizo zote Mudi alizichua akampa bi Udaku kama shukurani kwa kumfunulia ubaya wa mkewe.

Hakuishia hapo, aliamua kubadili kitasa ili Zai akija asiweze kabisa kuingia ndani “Jirani,” Mudi aliita.

“Abee… jirani,”

“Huyu mpuuzi akija tu hapa uniambie, ili tusije tukagongana naye hapa akanihadaa kwa machozi nikamuonea huruma,”

“Sawa jirani, akija tu, nitakufahamisha,” **** Haikupita muda mrefu tangu Mudi aondoke, Mapunda aliingia ndani na kumwamulu Zai avae aondoke, “Ondoka hapa nyumbani usije ukaniletea balaa… kumbe wewe ni mke wa mtu”

“Nisamehe Mapunda, naomba nibaki hapahapa,” alisema Zai huku sauti yake ikitoka kwa tabu kutokana na kwikwi iliyosababishwa na kilio.

“Usinizingue malaya mkubwa wewe …piga bunda, kama udiliki kunidanganya kuwa hujaolewa unafikili kuwa utashindwa kunidanganya kwa mengine? Fanya haraka utoke usije ukanilea balaa jingine hapa.” Zai alivaa nguo zake akaondoka huku akiendelea kulia. Alilia kwasababu ya upuuzi alioufanya, upuuzi wa kumsaliti mpenzi wake Mudi na kuja kutembea na Mapunda.

7
TINA alikuwa amebeba begi dogo aina ya montana ambalo lilikuwa maarufu sana kwa wakati huo. Tina na mama yake walikuwa wakimsindikiza mzee Masaka ambaye alikuwa anasafiri kuelekea Dar es salaam kwa Dominic mtoto wake.

Wote watatu walikuwa na sura ambazo zilionyesha dhahiri kuna uhaba wa furaha baina yao. Furaha ya Tina na mama yake ilisababishwa na jambo ambalo walilitegemea kutokea ndani ya muda mfupi la kuondoka kwa mzee Masaka kwa safari ya kuelekea Dar es salaam.

Wote walijua fika kuwa watagubikwa na upweke baada ya mpendwa wao huyo kuwa amepanda gari, gari ambalo lilikuwa tayari kituoni likiwasubili abiria.

“Baba ukirudi usisahau kuniletea zawadi,” Tina alisema huku akimkabidhi baba yake begi baada ya kuwa wameshafika kituoni. “Nisipokuletea wewe zawadi n’tamletea nani? Usijali nitawaletea wote zawadi.” mzee Masaka alisema kwa sauti ambayo ilizidi kudhihirisha kuwa hana furaha.

“Tena kabla sijasahau, mama Domi umekumbuka kuniwekea kiko kwenye begi?”

“Nhu! Sikumbuki vizuri… ila nadhani kila kitu cha msingi nimekiweka. Lakini baba Domi…” alisita kidogo akamtazama Tina mtoto wao kisha akamwambia, “Tina mwanangu naomba unipe nafasi kidogo nizungumze na baba yako”

Tina alikuwa mwelewa akajisogeza pembeni ili kuwapa nafasi wazazi wake. Baada ya Tina kuwapa nafasi, mama Domi alimgeukia mumewe, akamwambia, “Hivi mume wangu kwani ni lazima kuvuta hayo masigara yako? Hebu tazama unavyoipa sigara kipaumbele…”

Mzee Masaka alikaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akasema, “Nitajitahidi ili niache mke wangu… nipe muda,” baada ya kusema hayo, gari lilipiga honi wakaagana na Tina aliyekuwa pembeni alisogea wakapeana mikono huku wakimtakia safari njema.

Baada ya masaa manne ya safari ndefu mzee Masaka alifika Mwanza majira ya saa 12 jioni tangu saa nane, muda ambao alianza safari yake akitokea Nyamuswa.

Kwa sababu alifika Mwanza kwa kuchelewa, Mzee Masaka aliandaa kwanza utaratibu wa safari kwa kukata tiketi kisha akaenda kulala katika nyumba ya wageni ambayo ilikuwa palepale Nyegezi jirani na kituo cha mabasi yaendayo mikoani.

Akiwa chumbani kwake Mzee Masaka alijipapasa mifukoni, mwishowe akatoa kipande kidogo cha karatasi kutoka kwenye mfuko wa koti alilovaa, alitambua kuwa hicho ndicho kilikuwa kipande cha mwisho cha karatasi alichonacho ukiachana na tiketi ambayo alitakiwa kuitumia kesho kwa safari.

Kuishiwa karatasi hakukumshitua sana kwa sababu; alijiaminisha kuwa kuna kiko ndani ya begi, aliamini hivyo kwa sababu alimsisitiza mkewe amuandalie kila kitu chake cha muhimu kwa safari na kiko kikiwemo.

Mzee Masaka alisokota sigara yake kisha akaiwasha na kuivuta kabla hajapitiwa na usingizi mzito uliomfanya asahau kushusha neti kabla ya kulala.
****
Baada ya kuwa gari alilokuwa amepanda mzee Masaka kuondoka, mama Domi na bintiye walirudi nyumbani ili kuendelea na shughuli nyingine.

Wakiwa nyumbani mama Domi alibaini kuwa hakumuwekea mzee Masaka kiko, hii ilikuwa ni baada ya kuanza kurudisha kabatini baadhi ya vitu ambavyo alivitoa ili kumuandalia mumewe safari. Wakati anamalizia kupanga nguo, mama Domi alikiona kiko cha mumewe na moyo wake ukumpasuka!

“Hee….. hivi hiki kiko sikikuweka! Basi alivyo baba Domi atagomba wee… anaweza akadhani nimefanya makusudi kwa sababu huwa namkataza kuvuta sigara.
****
Mzee Masaka alishituka usingizini majira ya saa 7:15 usiku, chumbani mote palikuwa giza, alipochungulia nje pia alikumbana na giza totoro. Kwa akili ya haraka mzee Masaka aling’amua kuwa umeme umekatika!

Kiu ya sigara ikamvaa mzee Masaka ghafla, alichukua simu yake ndogo ya Nokia akawasha tochi kwa lengo la kumulika ili achukuwe kiko kwenye begi ili avute tumbaku yake. Alitafuta kila pembe ya begi bila mafanikio, akaamua kutoa nguo moja moja ili aone kama anaweza kukiona kiko chake. Alitoa nguo zote kisha akalikung’uta begin a bado kiko hakikuonekana! Akajisemea, “Huyu mama Domi… Si nilimwambia aniwekee kiko ina maana hakunisikia au alifanya makusudi?” mzee Masaka alifura kwa hasira akiwa mule chumbani huku kiu ya sigara ikizidi kumkolea.

Kwa hasira alizokuwa nazo aliamuwa kubonyeza simu yake kwa lengo la kumpigia mkewe angalau apoze hasira zake kwa kumtukana, lakini alipoiweka simu ile sikioni alizidi kuchoka. Sauti kutoka upande wa pili ikamjibu kama inamzomea vile, “Mtumiaji wa simu unayempigia hapatikani kwa sasa… jaribu tena baadae…” baada ya kusikia sauti hiyo mzee Masaka alizidi kufura kwa hasira huku akiachia matusi, “Mpumbavu sana huyu mwanamke…”

Mwani wa sigara ukazidi kumkolea mzee Masaka, alijisachi mfukoni ili kuona kama ana akiba ya karatasi, lakini hakuna alichoambulia zaidi ya tikiti ya basi ambayo alipaswa kuituma kesho kwa ajili ya safari yake ya Dar es salaam pamoja na noti kadhaa ambazo alikuwa nazo kama akiba na tahadhari njiani.

Akaamua kufungua mlango ili aende mapokezi akaonane na mhudumu wa gesti kwa lengo la kumuomba muhudumu huyo kipande cha karatasi ili aweze kusokota tumbaku yake avute.

Alipofika mapokezi aligonga mlango bila mafanikio na matumaini ya kupata kipande cha karatasi yakazidi kufifia. Akarudi chumbani kwake akiwa amefura kwa hasira huku kiu ya tumbaku ikizidi kumkereketa! Alijisachi tena mifukoni lakini majibu hayakubadilika hakuwa na kitu kingine zaidi ya tikiti yake ya safari pamoja na hela za noti, wakati mwani wa sigara ukizidi kumkolea.

Mwani wa sigara ulimfanya mzee Masaka afanye jambo ambalo lilihitaji kuwehuka kwanza ndipo ulifanye. Angefanyaje ikiwa hakuwa na uchaguzi mwingine wa nafuu isipokuwa huo! Mzee Masaka aliamua kuichana tiketi yake ya safari katika vipande viwili, ambapo kimoja aliamua kusokotea tumbaku ili kuikata kiu yake ya sigara iliyokuwa ikimuweka katika wakati mgumu.

Baada ya kuwa amefanikiwa kuikata kiu yake ya tumbaku mzee Masaka alipata usingizi mnono saa 8:00 kamili usiku akalala.
****
Domi alifika nyumbani kwa Makeke dakika kumi na tano mbele baada ya muda aliokuwa ameahidi kupita. Alijitahidi kukimbiza gari lakini hakuweza kufika ndani ya muda alioahidi kwa sababu ya msongamano wa magari aliokutana nao maeneo ya Moroco.

“Karibu bwana Masaka… karibu sana,” alisema Makeke wakati akimkaribisha Domi baada ya kuwa wamesalimiana.

Domi aliingia ndani na moja kwa moja wakaenda kwenye ofisi ndogo iliyoko nyumbani kwa Makene, ofisi ambayo huitumia mara nyingi awapo nyumbani kwa shughuli zake za kiofisi na za binafsi.

Ofisini, Domi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuizungumzia maada iliyowakutanisha pamoja katika siku na muda kama ule ambapo alianza kwa kusema, “Bwana Makeke, hili swala kama nilivyokwambia hapo awali kuwa huyu binti aliyekamatwa na madawa ya kulevya ni mchumba wangu ambaye nimeishi naye kwa zaidi ya miaka miwili…” Domi alisema hayo kisha akaweka kituo na kumtazama usoni bwana Makeke.

Makeke alikuwa akimsikiliza Domi kwa umakini wa hali ya juu. Hivyo baada tu ya Domi kumaliza kuongea, ukimya ulishika hatamu kwa muda wa takribani nusu dakika. Ukimya huo ulishika hatamu kwa sababu Domi alikuwa akitegea Makeke aseme neno baada ya yeye kuwa amekwishaongea, na kwa upande wa pili Makeke alikuwa akitafakali maneno ya Domi pamoja na kujipanga katika namna njema ya kuongea.

Baada ya ukimya kudumu kwa muda huo Makeke aliuvunja kwa kusema, “Nimekusikia na nimekuelewa vizuri bwana Dominic licha ya uvulivuli ninaoupata kwenye historia yako wewe na huyu binti unajua kesi hii inayomkabili, kesi ya madawa ya kulevya ni nzito sana, na kwa mujibu wa sheria za nchi hii yeyote atakaekutwa na hatia katika kesi ya namna hiyo hana budi kupokea adhabu kali kwa mujibu wa sheria.” Makeke aliweka kituo kwenye maelezo yake kisha akamtazama Domi kwa muda kidogo kabla akaendelea, “…. Mr Dominic, labda nikuombe unipe historia ya maisha yako wewe na huyo binti kabla hatujaenda mbali zaidi…. hapo nikiwa na maana uanzie siku ya kwanza tangu ulipokutana naye mpaka alipotoweka,” alisema Makeke.

Domi alishusha pumzi ndefu, akajivuta nyuma akiwa palepale kitini alipokaa, kisha akarudi tena katika mkao wake ule wa awali, lakini kwa namna ya pekee. Aliisimika mikono yake yote miwili juu ya mezza iliyokuwa mbele yake kwa kutumia viwiko vya mikono yake, huku kidevu chake akikiacha kiegemee katika viganja vya mikono yake.

Domi alimtazama Makeke kwa mara nyingne, kisha akaanza kwa kusema, “Yapata miaka miwili na sehemu sasa tangu nimfahamu Doi na kuanza kuishi naye.” Alijiinua kutoka katika mkao wake ule, na safari hii alijiegemeza kwenye mgongo wa kiti halafu akaendelea, “…. Ilikuwa ni wakati ambao nilikuwa mahakama ya mwanzo ya Temeke kwenye mafunzo kwa vitendo. Mara tu baada ya shughuli za mahakama kuisha, nilielekea kwenye kituo cha daladala tayari kuelekea nyumbani kwa mapumziko.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni