KUTI KAVU (13) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Ijumaa, 10 Februari 2023

KUTI KAVU (13)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA KUMI NA TATU
ILIPOISHIA...
Lilikuwa ni swali gumu sana kwa Doi, kwa sababu katika maisha yake hakuwahi kulisikia jina hilo la Makeke. Alijaribu kuvuta kumbukumbu zake ni wapi amewahi kulisikia ama kuliona bila mafanikio.

“Makeke?” Doi aliuliza baada ya kushindwa kulitambua jina hilo.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
“Ndiyo, Makeke…yule anayefanya kazi KWITALE ADVOCATES & COMPANY, unajifanya humjui?

“Hapana… simjui”

“Na Dominic je?”

Kutajwa kwa jina Dominic kuliyabadiri mapigo ya moyo wa Doi kwa kasi ya aina yake. Moyo wa Doi ulikuwa ukidunda kama moyo utakao kuchomoka kutoka mahali pake! Taswira ya Dominic Masaka ilimjia akilini mwake, mwili ulimuishia nguvu na kasi yake ya kutembea ikaanza kupungua kwa kila hatua aliyopiga.

Hakudhani kama angeweza kuhimili kumwona Domi baada ya dhuruma kubwa ya pendo aliyomfanyia. Alitamani kukimbia ili arejee kwenye chumba cha mahabusu alikotoka lakini hakuweza, alishindwa kabisa “Hajaja baba wala mama, amekuja Domi!” Doi aliwaza.

“Samahani afande, naomba unirudishe,” Doi alisema.

“Inamaana hutaki kuzungumza na mwanasheria wako?”

Ilimbidi kujikaza kisabuni, Doi aliongoza mpaka chumba cha mazungumzo huku akiwa na wasiwasi na maswali tele. Alipofika mle chumbani Doi, alimtambua Dominic aliyekuwa amekaa akiutazama mlango wa kuingilia ukiwa kama unatokea kwenye kutoka katika vyumba vya mahabusu. Domi alipomuona Doi alitamani kusimama na kumkimbilia lakini Makeke alimzuia.

Doi alifikishwa pale mezani walipo Domi na Makeke, alipofika tu Makeke akaamuru afunguliwe na koplo Mwalo alitii.

“Habari yako Doi?” Makeke alisalimia. Doi aliitika huku macho yake akiwa ameyaelekeza chini kwa aibu, alijibu salamu ile kwa sauti iliyotetemeshwa na kilio kilichosindikizwa na michilizi ya machozi iliyoanzia machoni na kutiririka kupitia mashavuni hadi kidevuni mwake. Pale kidevuni machozi yalijikusanya na kutengeneza tone kubwa ambalo taratibu lilikiacha kidevu na kudondoka kuelekea mezani, kabla tone lile la machozi halijafika mezani, Domi aliliwahi likadondokea kiganjani mwake, kisha akatoa leso na kumfuta machozi yaliyosalia kwenye mashavu ya Doi kwa kutumia leso yake huku akisema, “Usilie Doi… ipo namna,”

Kauli ya Domi ilipenya kwenye masikio ya Doi na kufanya mchomo mkali moyoni akajiona msaliti kwa kijana Domi, kijana aliye na upendo wa kustaajabiwa. Kijana ambaye hakuwa tayari kuliona chozi lake likidondoka chini, ajabu hii!

Je ni lita ngapi za machozi zimemtoka kijana huyu na kumwagika chini? Tena zikimtoka kwa sababu yake! Doi aliumia sana. Akaikumbuka siku ile ya kwanza alipokutana na Domi kwenye daladala, na namna walivyofahamiana. Kumbukumbu za Doi zilienda mbali zaidi, akakumbuka jinsi Domi alivyokuwa akifuatisha mashairi ya wimbo aliokuwa akiusikiliza siku hiyo kupitia simu yake, “… I can be you hero….now I stand by you for rever…’Sauti ya Domi ikifuatisha mashairi hayo ilijirudia kichwani mwa Doi na kufanya mwangwi uliojirudia mara nyingi, mara zisizo na idadi. Ilikuwa ni sauti yenye kumanisha lakini katika hali ya mzaha.

“…naweza kuwa shujaa wako… na sasa nasimama upande wako hata milele…” Akili ya Doi ilipata hangaiko la moyo lililomfanya atamke bila kujua, “Naomba unisamehe Domi”

“Usijali mpenzi wangu nimekusamehe,” alisema Domi huku akijifuta machozi kwa leso ile ile.

Makeke alishuhudia kila jambo lililokuwa likiendelea baina ya wawili hawa ambao ni dhahiri bado walikuwa wakipendana na kuhitajiana, katika kila hatua, “Doi Vioja, naitwa bwana Makeke. Ni wakili kutoka katika kampuni ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY, niko hapa kama wakili wako kwenye kesi unayokabiliana nayo, niko hapa kuhakikisha unapata haki yako kwa mujibu wa sheria. Na huyu hapa ni bwana Dominic Masaka, ni mshirika wangu ambaye nitakua naye bega kwa bega katika swala hili, naye pia anatoka KWITALE ADVOCATES & COMPANY…” Makeke alisita kidogo kisha akayatembeza macho yake kuwatizama Domi na Doi kwa zamu, Domi na Doi wote walikuwa wanalia. Alifikiri kidogo kisha akaendelea… “Bwana Dominic… usiruhusu hisia zikutawale, najua umeumia na kila mtu ameumizwa, hivyo basi, nakuomba uyarudishe mawazo yako kwenye kazi iliyotuleta kwa sababu hatuna muda wa kupoteza.” Mara baada ya kusema hayo alimgeukia Doi, “ok… bibie… kama nilivyosema hapo awali kuwa tupo hapa kuhakikisha unapata haki yako kwa mujibu wa sheria. Uko tayari kutoa ushilikiano?” Makeke aliuliza.

“Ndiyo niko tayari”

“Ok… hivyo basi naomba unieleze kwa uelewa wako ulivyoshiriki katika mkasa huu,” Makeke alisema.

Domi aliyekuwa kimya naye aliongeza, “sheria ina tabia moja Doi, nayo kutenganisha uongo na ukweli ili kuwezesha haki ipatikane, hivyo basi, huna budi kuelezea ukweli ulivyo, ili tujue namna ya kukusaidia.”

Asikwambie mtu, maisha ya jela si mchezo! Na hakuna mwnye uwezo wa kuyavumilia, wanaotumikia vifungo vyao ndani ya magereza hukesha wakiomba nusra ili waweze kuachiwa. Hivyo Doi hakuwa na namna isipokuwa kutoa ushirikiano uliohitajika ili kama itawezekana aondokane na maisha ya gerezani maisha ambayohayavumiliki hata kidogo, Doi akaanza kwa kusema, “Kusema ukweli kabisa, mimi sihusiki na wala sijui lolote kuhusiana na hayo madawa niliyokutwa nayo.”

“Ilikuwaje yakakutwa kwenye mizigo yako?” Makeke aliuliza baada ya kuwa ameandika pembeni, mara Doi alipomaliza kutoa maelezo ya kwanza.

“Sijui ikuwaje kuwaje mpaka yakawa kwenye mizigo yangu.”

“Iliwezekanaje mizigo yako iwe na vitu usivyovifahamu, kwani kuna mtu mlikuwa mnashea nae begi?” Makeke aliuliza.

Domi aliandika pembeni, kisha akauliza, “Kwani wakati unapanga mizigo yako, kwa maana ya vitu vilivyokuwa kwenye begi na mkoba ambamo madawa yamekutwa, mlikuwa pamoja na nani?”

Makeke alitikisa kichwa kama ishara ya kukubaliana na swali alilouliza Domi, akaandika pembeni kisha akatega sikio ili kusikiliza majibu yatakayotolewa na Doi.

“Mizigo yote ya ndani ya begi na mkoba niliipanga nikiwa pekee yangu,” Domi aliandika, kisha akamgeukia Makeke ambaye bila kuchelewa aliuliza swali linguine kwa Doi, “…. Labda hayo mabegi pamoja na mkoba vilikuwa chini ya miliki ya nani kabla hujaanza kupanga mizigo yako,”

“Begi na mkoba vilikuwa ni vipya,”

“Ni nani uliyemtuma akanunue au ulienda mwenyewe? Na vilinunuliwa duka gani?” Domi aliuliza. Maswali yalikuwa ya moto kiasi cha kumchosha Doi kichwa, hali ya kulia ilipungua na hatimaye kuisha kabisa akaielekeza akili yake katika kufikiri zaidi juu ya maswali aliyokuwa akikabiliana nayo kutoka kwa bwana Makeke na Domi.

“Begi na mkoba vililetwa tu, kwa sababu mimi sikuwa na uchaguzi wa aina wala ukubwa wa begi kwa ajili ya safari, hivyo baada ya kuwa vimeletwa nilichofanya ni kuvipokea tu.”

“Ni nani aliyeleta?” Makeke aliuliza. Swali la ni nani aliyeleta begi na mkoba lilimuwia gumu Doi katika kulijibu, wakati bado anafikiria namna ya kulijibu, Domi akaongeza, “Labda kabla hujajibu hilo swali, itakuwa vyema kama majibu yake yataambatanishwa na majibu ya swali hili; tiketi yako pamoja na pass vinaonyesha kuwa ulikuwa unaelekea Ufaransa, sio?”

“Ndiyo,”

“Vizuri sana, kwa hiyo Ufaransa ndiyo ingekuwa mwisho wa safari yako, au ungeendelea baada ya pale, na lengo la safari yako nchini Ufaransa lilikuwa ni lipi na ulikuwa peke yako au na mtu mwingine?”

Swali hili pia lilikuwa kama mwiba akilini na moyoni kwa Doi, alijaribu kufikiri ili apate majibu mwafaka dhidi ya maswali husika. Alikuna kichwa mara kadhaa kabla ya kujibu kisha akasema, “Begi na mkoba vililetwa na Damian, katika safari ya kutoka hapa Tanzania hadi Ufaransa ningekuwa peke yangu. Lakini mara baada ya kufika Ufaransa ningepokelewa na Damiani. Alinieleza kuwa; safari ya Ufaransa ni kwa ajili ya mapumziko tu, na baadae tungerudi nyumbani,”

“Domi alinieleza kuwa siku ulipoondoka nyumbani ulimwachia barua pamoja na dola za Kimarekani, si sivyo?” kila swali alilokuwa akikabiliana nalo Doi lilikuwa la moto, hili pia kama yalivyo mengine yaliyotangulia lilikuwa kama msumari wa moto kichwani kwa Doi. Licha ya swali lenyewe kutaka jibu jepesi, lakini utoaji wa jibu ulihitaji ujasiri ambao Doi hakuwa nao. Hakuwa na jinsi isipokuwa kujibu maswali yote kwa ufasaha ili aweze kujinasua kutoka katika kuti kavu alilopo, alijibu, “Ndiyo.”

“Bila shaka pesa hizo ulipewa na Damiani?”

“Ndiyo,” Doi alijibu.

“Alishawahi kukueleza kuwa anajishughulisha na nini?”

Doi alifikiri kidogo, kisha akajaribu kuvuta kumbukumbu kama alishawahi kuambiwa na Damian juu ya shughuli anazofanya. Alijitahidi kukumbuka bila mafanikio. Hatimaye kumbukumbu zake zikamrudisha siku kadhaa nyuma.

Ilikuwa siku ya Jumanne, siku ambayo Doi alikuwa nyumbani kama kawaida yake baada ya Domi kuondoka kuelekea kwenye mihangaiko yake ya kila siku. Doi alikuwa akijisomea moja ya miswada aliyoiandaa Domi kwa ajili ya kuchapa vitabu endapo angefaikiwa kupata ufadhili. Alikuwa amekolea baada ya kuwa amening’inizwa kwenye uzi wa taharuki iliyojengwa vyema kwa ukufu wa maneno yaliyounganishwa barabara na kufanya hadithi aliyokuwa akiisoma kuukonga moyo wa yeyote ambaye angethubutu kuanza kuisoma. Ilikuwa ni hadithi ile inayoitwa, ‘KWENYE SIKU YANGU YA KUZALIWA’ ni hadithi ambayo ilimsahaulisha Doi makali ya njaa yaliyokuwa yakimwandama kwa kutokula tangu asubuhi.

Akiwa amezama kabisa kwenye ukufu wa maneno yanayosimulia visa vya kusisimua baina ya msichana anayeitwa Wayeka na mpenzi wake Kitiheka, ambao ni wahusika wa hadithi hiyo ya ‘Kwenye siku yangu ya kuzaliwa’ Doi alishituliwa na sauti za mlango uliokuwa ukigongwa.

“Ngo… ngo… ngo….”

Hakutaka kabisa kuondolewa kwenye uhondo aliokuwa akiupata kutoka kwenye hadithi hiyo iliyoandikwa na mpenzi wake lakini hakuwa jinsi. Sauti za mlango unaogongwa ziliendelea kumpa kero iliyomsababishia kupatwa na chukizo dhidi ya aliyekuwa anagonga mlango licha ya kutomjua ni nani.

Hakuwa na budi kusema, “karibu”, huku akijiinua kivivu kutoka kitandani alipokuwa amekaa akisoma kitabu chake, alienda mpaka mlangoni akaufungua mlango. Alikuwa ni Zai… Zainabu Mpotoshi, shoga yake wa siku nyingi ambaye sasa ni jirani yake baada ya kuwa amehamia nyumbani kwa Domi.

“Karibu shosti… karibu ndani” Doi alikaribisha.

“Ahsante shosti mwenzio nimegonga kweli…. Mpaka nikahisi labda haupo. Ulikuwa umelala?’

“Aku, nilikuwa nimemezwa na ufundi wa shemejio hapa,” alisema Doi huku akiushika ule muswada kumuonyesha Zai ambaye hakujishughulisha nao.

Baada ya salamu na mazungumzo mafupi baina yao hatimaye Zai alimweleza Doi shida yake.

“Shosti…. Mi sina mengi naomba tu unisindikize Uchumi Supermarket, kuna mtu nataka kukutana naye pale. Naomba unisindikize shoga, jipale nakusubiri.”

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni