KUTI KAVU (14) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Ijumaa, 10 Februari 2023

KUTI KAVU (14)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA KUMI NA NNE
ILIPOISHIA...
Baada ya salamu na mazungumzo mafupi baina yao hatimaye Zai alimweleza Doi shida yake.

“Shosti…. Mi sina mengi naomba tu unisindikize Uchumi Supermarket, kuna mtu nataka kukutana naye pale. Naomba unisindikize shoga, jipale nakusubiri.”

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
“Jamani Zai… mwenzio nilikuwa nasoma hadithi hapa umenikatisha uhondo wangu, nivumilie basi nijiandae.”

Saa moja baadaye Zai na Doi walikuwa kwenye viwanja vya ‘Quality Centre’, mahali ambapo lipo duka la Uchumi Supermarket.

Zai alikwenda pale kwa minajili ya kuonana na hawala yake ambaye alimwambia waonane ili amfanyie shopping ya vitu ambayo Zai aliomba anunuliwe na hawala yake huyo. Hawala yake Zai alijitambulisha kwake kuwa anaitwa Marcus japo jina lake halisi halikuwa hilo, alikuja na swahiba yake ambaye alitambulishwa kuwa anaitwa Damian.

Damian alipomuona Doi alivutika naye akamtumia Zai kumkuadia baada ya yeye kutopata ushirikiano kutoka kwa Doi kwa namna aliyoitarajia. Hivyo baada ya shughuli ya pale ‘Quality Centre’ Zai na Doi walilejea nyumbani, wakati Zai akielekea kwake alipokuwa akiishi na Mudi, Doi alielekea kwake mahali walipoishi yeye na Domi, siku hiyo ikaisha.

Siku iliyofuata majira yaleyale kama ya siku iliyopita Zai aliwasiri nyumbani kwa Doi ambako kama ilivyo ada alimkuta akipitisha wakati kwa kufunua kurasa baada ya kurasa za hadithi iliyoukonga moyo wake, hadithi ya, “kwenye siku yangu ya kuzaliwa”

“Shoga we nawee…. huchoki? Kila nikija hapa kwako wewe na hicho kitabu… kitabu na wewe utadhani umerogwa!”

“Mh! Shosti mdomo huo… mdomo huo...”

“Basi yaishe bibi weee… sikujia hayo…”

“Haya sasa yaseme yaliyokuleta,”

“ We ni wangu shosti, lazima nije nikujulie hali. Vipi bukheri?”

“Mi bukheri shosti”

“Mi bukheri shosti,” Zai aliigiza sauti ya Doi kwa kubana pua, “Eti bukheri?” alisema Zai. “Tuacchane na hayo” aliendelea, “Mi ni mzuri shosti ila kwako sitii maguu,”

“Umeanza mambo yako,”

“Lazima niseme shosti kama umenizidi… umenizidi tu, watu si wanaona wenyewe ila unajichakaza Doi, unajichakaza..”

“Najichakaza kivipi,” Doi alihoji.

“Doi…. unadhani wewe ni wa kusuka mabutu na ukifumua tu mabutu, basi unasuka twende kilioni. Unadhani wewe ni wa kufunga kiremba muda wote utadhani bibi wa kinyamwezi aliyeko Tabora wakati uko Dar?” Zai alisema.

“Yametoka wapi hayo tena shoga?”

“Hapana Doi wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu, nadhani unakumbuka kuwa nilirudia darasa ili nisome darasa moja na wewe, hivyo siwezi kuvumilia kuona unachakaa kiasi hiki! Napenda kuona unasuka sangita na ukifumua tu unaweka relaxer au bonding kabisa!”

Maneno ya zai yalimchanganya Doi kiasi cha kushindwa kuelewa ni nini hasa alichokimaanisha. Aliyatafakali sana maneno yale lakini jibu halikuwa tayari kuungana naye. Ikambidi kumuuliza shoga yake, “Sijakuelewa Zai”

“Hivi ni nini kinakufanya ung’ang’anie maisha ya namna hii? Maisha yanayozidi kukuchakaza siku hadi siku… Sikiliza Doi, najua unampenda Domi… ila haina maana kuwa kila unayempenda ni lazima uishi naye….”

“Zai ishia hapohapo… najua unalotaka kusema, naomba uniache na Domi wangu,” alisema Doi huku akiwa ameunyoosha mkono wake mithili ya askari wa uslama barabarani asimamishaye kuelekea kwa shoga yake.

“Tatizo lako ni kujifanya mjuzi wa kila jambo, mi sijasema umuache Domi”

“Kumbe je?”

“Fanya kitu ambacho kitakusaidia wewe halikadhalika pia Domi, najua Domi ni msomi… tena msomi wa chuo kikuu, lakini kama unavyojua nchi hii bila kutoa kitu hupati kitu… nakusudia kusema kuwa ili Domi apate kazi ni lazima atoe hongo. Hivyo kwa maisha haya hiyo hongo itatoka wapi?”

“Kwa hiyo afanyeje sasa?”

“Hilo ni swali zuri sana. Jana wakati tupo na Marcus pale ‘Quality Centre’, alikuwepo pia rafiki yake, si unamkumbuka?”

Doialitikia kwa kichwa kuwa anakumbuka na Zai akaendelea, “…basi jamaa ana pesa balaa…. mbuzi haruki! Ni mtu na pesa zake anaomba kesho mkutane naye…”

“Muda umeisha naomba nimrudishe Doi chumbani kwake,” sauti ya afande Mwalo ilimgutua Doi kutoka kwenye lindi hilo la mawazo.

Domi na Makeke waliagana na Doi huku wakiahidi kurudi tena. Walitoka mpaka nje ya gereza, lakini kabla hawajalifikia gari walilokuwa wamekuja nalo walikutana na Mzee Vioja akiwa sanjari na mkewe, mama Doi.

Walisalimiana kisha Domi aliwatambulisha kwa bwana makeke, akimuelezea kuwa ndiye wakili watakaye kuwa naye bega kwa bega kwenye kesi ya Doi.

Baada ya utambulisho huo Domi aliwaomba wakasalimiane na mzee Masaka ambaye aliachwa ndani ya gari akiwasubiri wakati wao wameenda kuzungumza na Doi.

Mzee Vioja na mkewe hawakuwa na pingamizi, walienda mpaka kwenye gari wakasalimiana na mzee Masaka ambaye pia alifurahi baada ya kutambulishwa kwao. ****

Mzee Masaka aliamka asubuhi huku akilalamika kuumwa kikohozi pamoja na maumivu makali ya kifua kwa ndani.

“Koh… koh… koh..” alizidi kukohoa mzee Masaka mbele ya Domi ambaye alikwenda chumbani kwake kumsalimia kabla hajaenda kazini.

“Nimekohoa usiku kucha na kila nikikohoa nahisi maumivu ndani ya kifua”

Domi alimuhurumia baba yake,v“Pole sana baba, inabidi twende hospitali upate vipimo ikibidi upate matibabu,” Domi alimrai baba yake.

Rai ya Domi kwa baba yake ilipokelewa bila pingamizi. Mzee Masaka alijianda na alipokuwa tayari walielekea hospitali.

Njiani Mzee Masaka aliendelea kukohoa na maumivu ndani ya kifua yalizidi kupamba moto sanjari na maumivu ya koo yaliyokuwa yakimpa wakati mgumu kila alipojaribu kumeza mate.

Baada ya muda wa takribani saa moja hivi, Dominic na Mzee Masaka waliwasili hospitalini kwa ajili ya kumuona daktari. Mzee Masaka alimweleza Daktari namna anavyojisikia mwilini mwake. Na mara baada ya kutoa maelezo yaliyokuwa yakisikilizwa kwa makini ya hali ya juu na daktari, Daktari alimuuliza, “Unavuta tumbaku?”

“Ndiyo dokta navuta” Mzee Masaka alijibu swali la daktari bila kuumauma maneno.

Mara baada ya jibu hilo Daktri alitambua kuwa tatizo la Mzee Masaka limechangiwa kwa kiasi kikubwa na matumizi ya tumbaku. Aliuhisi ugonjwa wa mzee Masaka kupitia maelezo yake lakini hakutaka kumuanzishia matibabu kabla ya kumfanyia uchunguzi wa kina. Hivyo baada ya maelezo mzee Masaka alifanyiwa vipimo ambavyo vilitoa majibu yaliyomshangaza hata Daktari. Mzee Masaka alikuwa mgonjwa, alikutwa na maambukizi ya saratani ya mapafu ambayo kwa mujibu wa Daktari ilisababishwa na matumizi ya tumbaku.
****
Mzee Masaka alianza kutumia tumbaku miaka mingi iliyopita wakati ambao alikuwa ni mwanafunzi wa shule ya msingi Bukama. Alianza kwa kuokota kipande cha sigara kilichoachwa na mjomba wake ambaye walikuwa wakilala naye chumba kimoja wakati huo. Baada ya kuvuta kipande hicho cha sigara, siku iliyofuata alirudia tena kwa kuvuta kipande alichokiokota nje, bila shaka nacho kilitupwa na mjomba wake.

Tabia yake ya kuokota vipande vya sigara na kuvivuta ilipamba moto na hata kufikia hatua ya kuanza kuiba sigara za mjomba wake ambaye alikuwa na tabia ya kununua pakiti nzima kwa sababu ya kukubuhu katika uvutaji. Uvutaji wa sigara ulimkolea Masaka kiasi cha kupatwa na tabu isiyoelezeka pindi akosapo sigara. Alivumilia kwa muda na mwani ulipomzidia Masaka alianza udokozi wa vijisenti vya baba yake ili tu akaikate kiu yake.

Hakuna aliyefahamu kwa wakati huo kama Masaka anavuta sigara, hata baba yake hakuwa na habari licha ya pesa zake zilizoibwa kutumika kugharamia starehe hiyo haramu. Angejuaje wakati muda mwingi alikuwa ‘bwii’? Hivyo kila senti yake iliyopungua aliijumuisha katika matumizi yake ya kilabuni alipokuwa akienda kila baada ya kazi.

Alipohitimu darasa la saba, mzee Masaka hakuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari. Akalazimika kukiacha kijiji akaelekea mjini Bunda ambapo alibahatika kupata kibarua kwenye kampuni inayojishughulisha na ukamuaji wa mafuta ya mbegu za pamba.
****
“Mzee wangu kwa mujibu wa vipimo inaonekanaa kuwa una tatizo la koo pamoja na mapafu” Daktari alifafanua, “Tatizo hili kwa kiasi kikubwa husababishwa na matumizi ya tumbaku ya muda mrefu…” Maelezo ya Daktari yalimchanganya kabisa mzee masaka kiasi cha kumfanya adondoshe chozi. Taswira ya mkewe, mama Domi ilimjia sambamba na sauti iliyokuwa ikimnung’unikia kwa tabia yake ya uvutaji wa tumbaku. Akajilaumu kwa kutokuwa msikivu kwa mkewe na akailaani ile siku ya kwanza alipovuta tumbaku kwa mara ya kwanza. Mzee Masaka alilia!

Majibu hayo ya Daktari yalipokelewa pia kwa masikitiko makubwa na Domi, ambaye hakuwa na jinsi isipokuwa kumchukua baba yake na kumrudisha nyumbani huku wakisubiri tarehe nyingine ya kurudi tena hospitali kwa ajili ya kliniki kama daktari alivyoshauri.
****
Siku moja Domi akiwa ofisini kwake, aliingia Neema akiwa na bahasha mkononi. Kama kawaida yake alimtania kidogo Domi kisha akamkabidhi barua yake. “Hii ni barua yako… kama itakuwa ni ya nyongeza ya mshahara, usisite kunigawia japo kidogo,” mara baada ya kuyasema hayo aliondoka.

Domi aliipokea ile barua na kuifungua, hakuamini alichokiona! Ilikuwa ni barua ya majibu ya ombi lake la kudhaminiwa katika uchapaji wa hadithi yake. Barua iliyomtaka afike kwenye ofisi za kampuni ya ‘UBUNIFU WETU’ kwa lengo la kusaini mkataba wa uchapishaji wa kazi zake.

9
KESI ya Doi iliunguruma kwa muda wa miezi miwili huku bwana Makeke sambamba na Dominic wakijitahidi kwa kila hali kumtetea kwa mujibu wa sheria. Kisicho riziki hakiliki, kesi iliisha kwa Doi kuhukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatwa na hatia.

Ilikuwa ni huzuni ya hali ya juu kwa Domi pamoja na wazazi wa Doi ambao walihudhuria mahakamani kila kesi ilipotajwa. Rufaa ilikuwa wazi lakini hata ilipokatwa kesi iliunguruma tena na kuisha bila kubadili hukumu ya awali. Doi alilia sana na Domi alilia naye, lakini ukweli haukubadilika.

Doi akayaanza maisha mapya akiwa ndani ya sare za magereza, akiwa kama mfungwa mwenye namba P2832.

Siku hiyo hiyo Domi aliporudi nyumbani, aliufungua mkoba wake na kuitoa ile barua aliyoandikiwa na Doi, barua ambayo alikuwa akitembea nayomuda wote kila mahli alipoenda. Baada ya kuifungua Domi aliisoma ile barua ambayo ni barua chungu katika barua zote alizowahi kuandikiwa;

“Kwako mpenzi Domi, natambua fika kuwa unajua nakupenda na ndivyo ukweli ulivyo. Ila hali ya maisha imenilazimu kufanya hivi, naomba usinielewe vibaya tafadhali.

Nafanya hivi kwa ajili yetu sote yaani mimi na wewe na wote wanaotuzunguka, kwa maana ya familia. Si kama sikupendi, ila siyapendi maisha duni, maisha ambayo tumekuwa wafungwa wake kwa muda mrefu sasa.

Inaniuma sana kukuandikia haya ila sina budi mpenzi…” hakuendelea kusoma zaidi kwa sababu ya machozi yalyoanza kumtoka. Aliikunjakunja ile barua kisha akaicoma moto ili kuifuta kumbukumbu ya barua hiyo iliyokuwa ikimwumiza.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni