KUTI KAVU (15) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Ijumaa, 10 Februari 2023

KUTI KAVU (15)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
📖 KUSOMA SIMULIZI
🎬 FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
😂 VIDEO za KUCHEKESHA
📑 MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA KUMI NA TANO
ILIPOISHIA...
Inaniuma sana kukuandikia haya ila sina budi mpenzi…” hakuendelea kusoma zaidi kwa sababu ya machozi yalyoanza kumtoka. Aliikunjakunja ile barua kisha akaicoma moto ili kuifuta kumbukumbu ya barua hiyo iliyokuwa ikimwumiza.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Miezi mitatu baadaye Domi alimtembelea Doi gerezani. Uwepo wake gerezani kwa siku hiyo uliibua faraja mpya kwa Doi. Faraja ambayo aliishuhudia ikififia kwenye siku ile ambayo kesi yake ilihitimishwa kwa hakimu kumsomea hukumu yake ya kifungo cha miaka mitano jela kwa mujibu wa sheria.

Ni kipi alichohitaji tena zaidi ya faraja, hasa katika wakati mgumu kama huu, wakati ambao alikuwa anakitumikia kifungo chake! Ndiyo, alikuwa anahitaji faraja lakini si kutoka kwa Domi. Kwa Doi, Domi ndiye aliyehitaji faraja kuliko yeye.

Domi alihitaji faraja kwa sababu alisaritiwa na mpenzi katika wakati ambao alihitaji mtu wa karibu kwa ajili ya kumfariji, mtu huyo ni nani kama si yeye?

Doi alikuwa kimya baada ya kuwa wamesalimiana na Domi. Ukimya huo uliodumu kwa muda wa dakika moja ulivunjwa na Doi mwenyewe, “Hapana,” sauti ilimtoka Doi huku akijaribu kujiinua kutoka pale kwenye kiti alipokuwa. Hakuweza baada ya kuzuiliwa na mikono ya Domi sambamba na sauti yake iliyokuwa ikimsihi asiondoke.

“Niko hapa kwa ajili yako Doi,”

“Naelewa Domi , lakini…” kabla hajamalizia kauli yake, Domi alimkatisha kwa kusema, “Usiruhusu fikira zako ziwe mbali na mahali hapa, hasa katika wakati huu ambao niko hapa kwa ajili yako.”

“Siwezi Domi…. siwezi, nimesha yakosea maisha tayari,” “Hapana Doi hujakosea, maisha ndivyo yalivyo, hakuna aliyewahi kuyapatia… hakuna mkamilifu chini ya jua, kila mtu kuna mahali alipokosea. Ichukulie hali hii kama changamoto, kisha ukubaliane nayo kama changamoto unayopaswa kukabiliana nayo bila kujiuzulu…” Domi alitulia kidogo kisha akaangaza kushoto na kulia. Nadhani alitaka kuhakikisha kama kuna watu wengine tofauti na wao, walikuwepo!

Aliyarudisha tena macho yake kwa Doi, kwa sauti ya chini zaidi kuliko ilivyokuwa awali akamwambia, “Kama nilivyokwisha kusema Doi, hii ni changamoto katika mfululizo wa changamoto za kimaisha…. hali hii isikufanye ukajihangaisha kutafuta ni nini maana ya maisha, hutoipata! Na pengine utajikuta unakata tamaa ya kuishi kabisa. Kufungwa siyo mwisho wa maisha… bado nayo nafasi Doi,”

Mazungumzo baina yao yaliendelea, ni katika maongezi hayo, ndiyo Domi alimweleza Doi juu ya kifo cha mzee Masaka. Taarifa za kifo cha mzee Masaka zilimshitua sana Doi, akamhurumia Domi lakini alikuwa amekwisha chelewa, kwani Domi alishakubaliana na hali ya kuondokewa na baba yake kipenzi kwa sababu tamati ya maisha tunayoishi ni kifo.

Muda uliyoyoma wakiwa pamoja mahali pale, hatimaye ukafika wakati ambao Domi aliaga, lakini kabla hajaondoka alimkabidhi Doi bahasha akaondoka.

Doi aliifungua ile bahasha akiwa na shauku ya kutaka kujua kilchomo, hakuyaamini macho yake pale alipokishuhudia kitabu kikubwa cha hadithi aliyoipenda, kitabu kiliandikwa kwa maandishi makubwa kabisa juu ya jalada yaliyosomeka hivi, ‘KWENYE SIKU YANGU YA KUZALIWA’ aliifahamu vema hadithi hii. Moyoni alijiona msaliti asiyefaa kuigwa, chozi likamtoka.

Doi aliifungua ile bahasha akiwa na shauku ya kutaka kujua kilchomo, hakuyaamini macho yake pale alipokishuhudia kitabu kikubwa cha hadithi aliyoipenda, kitabu kiliandikwa kwa maandishi makubwa kabisa juu ya jalada yaliyosomeka hivi, ‘KWENYE SIKU YANGU YA KUZALIWA’ aliifahamu vema hadithi hii. Moyoni alijiona msaliti asiyefaa kuigwa, chozi likamtoka.
****
VITA dhidi ya madawa ya kulevya ilizidi kupamba moto kila pembe ya dunia, huku idara ya polisi katika kila nchi wakishirikiana bega kwa bega na polisi wa kimataifa ‘INTERPOL’ katika vita hiyo.

Kwa ushirikiano huu mafaniko makubwa yalipatikana ikiwemo kuwakamata wafanyabiashara wengi waliojihusisha na biashara hii wakubwa kwa wadogo. Ulinzi uliimarishwa maradufu kiasi cha kufanya mianya mingi iliyotumika kiholela hapo awali kuwa migumu katika historia ya biashara hii haramu inayopigwa vita kwa sababu ya uharibifu mkubwa inaousababisha wa kuharibu afya na akili za watumiaji.

Wale wote waliojifanya kichwa ngumu waliuawa katika makabiliano ya ana kwa na polisi katika jitihada zao za kuingiza mzigo sokoni. Wengi walikufa akiwemo Damian ambaye aliuawa sambamba na gwiji katika biashara hii haramu, aliyefahamika kama Gustavo Maritinez Sucre. Waliuawa mpakani mwa Mexico na Marekani wakiwa katika harakati zao za kuvusha mzigo wa cocain kuingiza nchini Marekani.
****
Miaka mitatu huku Domi akifurahia mapato yaliyotokana na mauzo ya vitabu vyake vya hadithi hasa kile cha ‘KUTI KAVU’ sambamba na kile cha ‘KWENYE SIKU YANGU YA KUZALIWA’ ambacho kimekwishachapishwakwenye lugha zaidi ya sita za kimataifa ikiwemo kiingereza na kifaransa.

Siku moja bwana Makeke alimtembelea Domi nyumbani kwake, ambako alimkuta yuko na mkewe.

Wakiwa sebuleni kwa Domi, makeke alikuwa amembeba mtoto mdogo ambaye umri wake ulikuwa ni kama miezi mitatu hivi.

Katika mazungumzo yaliyodhihirisha furaha iliyopo baina yao Makeke alisema, “Jamani mimi napenda kusimulia hadithi,”

“Basi leo umepata wasikilizaji wa hadithi, anza kutusimulia….” Alisema Domi huku mkewe aliyekuwa nyuma ya kochi amemuinamia akiachia tabasamu sambamba na kumminyaminya mabegani.

“Haya sasa sikilzeni hadithi yenyewe…”

“Enhe…!” sauti ya Domi na mkewe zilisikika wakijibu kwa pamoja.

Makeke alianza, “Hadithi hadithi….”

“Hadithi njoo.. uongo njoo utamu kolea…” Doi na mkewe walijibu katika namna ya mzaha iliyoongeza furaha baina yao.

“Hapo zamani za kale… si zamani sana kama zilivyo zama za mawe, hapana. Namaanisha zama hizihizi, yaani kama miaka thelasini na ushei hivi iliyopita. Palitokea kijana mmoja aliyeitwa Dominic Masaka…” alisita kidogo kisha akawatazama hadhira yake ambao bado walikuwa wakielea kwenye tabasamu halafu akaendelea, “….basi Domi huyo alianza shule ya awali, baadaye msingi, sekondari na hata chuo kikuu hatimaye akahitimu.

Baada ya kuhitimu, alitafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio, lakini hakuchoka! Ikafika siku ambayo Mungu alimuandikia, Domi akapata kazi. Aliifanya kazi kwa bidii…

Siku zikapita.. siku zikapita hatimaye Domi akamuoa Neema na sasa wana mtoto wao kipenzi anayeitwa Tumaini.Na hadithi yangu imeishia hapo.”

Hitimisho la hadithi ya makeke liliwachukua Domi na Neema ambaye ni mkewe mpaka kwenye tabasamu lililozaa kicheko kilichoungwa mkono na mtoto wao mdogo aliyekuwa amepakatwa mikononi mwa Makeke, wote wakacheka!

MWISHO

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni