KUTI KAVU (3) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumatatu, 6 Februari 2023

KUTI KAVU (3)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA TATU
ILIPOISHIA...
Njiani Dominic aliendesha gari kwa kasi, kwa nia na madhumuni ya kuwahi nyumbani na kumpasha mapenzi wake kuwa; matatizo yote yaliyokuwa yakisababishwa na ukosefu wa pesa sasa yametamatishwa, baada ya yeye, yaani Dominic kupata kazi katika kampuni ya mawakili ya KWITALE ADVOCATES & COMPANY.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Punde si punde Dominic alikuwa nyumbani, Domi alishuka kwenye gari kwa haraka akaanza kukimbia kuueleka mlango wa nyumba, huku moyoni akiwaza namna Doi atakavyofurahi baada ya kuwa amempasha juu ya habari hizi njema.

Kinyume na matajio yake Domi alikutana na kufuli kubwa lililokuwa likining’inia mlangoni. Mapigo ya moyo wake yakabadirika ghafla na furaha yake ikatumbukiwa nyongo. Mambo yamekwenda kinyume kabisa na jinsi alivyotarajia!

Dominic alitarajia kumkuta Doi nyumbani kama ilivyo kawaida yake, lakini hakumkuta! “Doi huwa haondoki bila kuaga leo imekuwaje?” Dominic alijiuliza bila kupata majibu. Kwa upole na unyonge wa hali ya juu, aliingiza mkono mfukoni na kutoa funguo, akafungua mlango na kuingia ndani ili kumsubiri mpenzi wake. Alipoingia ndani akaitupia kitandani ile bahasha aliyokuwa nayo mkononi mwake, kisha akaingiza mkono mfukoni na kutoa lile burungutu la noti na kuzitandaza kitandani ili Doi akija, aje azione.

Dominic akakaa kitandani, akaishika ile bahasha aliyoitupia kitanadani na kuitoa ile hundi aliyopewa kazini na baada kufanya hivyo akaitoa nakala ya mkataba wa ajira ambayo alipaswa kubaki nayo kama kumbukumbu yake na yenyewe pia akaiweka kitandani sambamba na ile hundi na pesa taslimu alizo nazo ili mpenzi wake akija avione vizuri.

Domi alijiaminisha kuwa, yawezekana Doi akawa amemsindikiza mgeni, na kama ni hivyo basi atakuwa maeneo ya jirani na asingekawia kurudi.

Wakati huo saa ya ukutani ilionesha kuwa ni saa 11:06 jioni, muda mfupi baada ya saa 10:40 muda ambao aliwasili nyumbani hapo, ambapo wanaishi yeye na Doi.

Muda uliyoyoma Domi akimsubiri Doi bila mafanikio. Aliendelea kusubiri huku akipanga kutekeleza mipango yake mingi iliyokwama kwa ukosefu wa pesa ambayo sasa imepatikana. Domi aliwaza kuwatumia pesa wazazi wake ambao wako kijijini Nyamuswa. Aliwaza pia namna ya kutekeleza mipango ya ndoa yake na Doi ili waishi kihalali kama mke na mume. Domi aliyawaza yote haya wakati akimsubiri mpenzi wake ambaye mpaka muda huo alikuwa bado hajarudi.

Licha ya kutokula tangu asubuhi, Domi hakuwa anahisi njaa hata kidogo, na hakuna alichohitaji kwa wakati huo zaidi ya mpenzi wake ambaye alimwacha nyumbani asubuhi.

Muda ulizidi kuyoyoma bila Doi kuonekana! Wasiwasi ukaanza kumwingia Domi, “Amekwenda wapi huyu?” Domi alizidi kujiuliza maswali bila kupata majibu. Domi akasimama kutoka pale kitandani alipokuwa amekaa na kuanza kutembeatembea mule chumbani kama mwehu, mara aende, mara arudi, hatimaye akachoka na kurudi tena pale kitandani alipokuwa amekaa awali akakaa tena, mpaka wakati huu ilikuwa imeshatimu saa 12:37 jioni.

Domi alijiegesha pale kitandani akapitiwa na usingizi bila kujijua. Giza likaenea mule chumbani, na baadaye mbu wakaanza kusikika kwa milio iliyojiunda kwa kuzigonganisha mbawa zao. Mbu wale wenye kiu ya damu walimtafuna Domi akiwa usingizini, na walipozidi kujibidiisha walimwamsha Domi kutoka usingizini. Alipoamka alikuta giza limeenea chumba kizima. Mpaka wakati huo Doi alikuwa hajarejea!

Domi aliwasha taa ya kandiri na mwanga ukashika hatamu mule chumbani.

Wasiwasi ukazidi kumwingia Domi, “Au ameenda nyumbani kwao?” maswali juu ya maswali yalizidi kumpa wakati mgumu.

“Doi ni mtu mzima. Kwa nini afanye jambo la kitoto kama hili?” alikusanya noti zake akaziweka kwenye bahasha ile kubwa pamoja na ile hundi na nakala yake ya mkataba wa ajira.

Wakati huo ilikuwa imeshatimu saa 3:30 usiku kwa mujibu wa saa ya ukutani ambayo iliendelea kuzunguka.

Domi alipoona mbu wanazidisha kero akaamua kushusha chandarua ili kujisitiri dhidi ya mbu wale ambao walikua kero kwake. Kabla hajafanya hivyo alianza kwa kuhamisha vitu vilivyokuwa kitandani ili akung’ute pale juu ya kitanda kwa minajili ya kupunguza vumbi na kuondoa mchanga.

Alianza kwa kutoa shuka iliyokuwa imekunjwa akaiweka juu ya kiti kilichokuwa mule chumbani. Baadaye akaushika mto ili kuutoa auweke pale kwenye kochi alipoiweka shuka. Alipounyanyua mto macho yake yalikutana uso kwa uso na kitu kilichomshitua. Macho ya Domi yalikuwa yakikabiliana na bulungutu la noti za kimarekani, sanjari na kipande cha karatasi kilichokua pembeni ya zile noti. Domi alipigwa na butwaa baada ya kuviona vitu hivyo, akahisi yuko ndotoni lakini akaibishia nafsi yake kwa kujiaminisha kuwa yuko timamu. Moyo wa Domi ukakosa utulivu kifuani mwake kwa kudundadunda kama spika!

Akili ya Domi ilikuwa ikiwaza na kuwazua juu ya kile anachokiona pale kitandani. Wasiwasi ukamzidia tena, akaanza kuhisi anapagawa huku anajiona. Alivitumbulia macho vitu vilivyokuwa pale kitandani kwa muda wa dakika zipatazo kama tano hivi, uvumilivu ukamshinda, akanyoosha mkono wake wa kuume na kulishika lile bulungutu la dola za kimarekani, akalisaili kwa muda halafu akakili kuwa yuko sahihi, kuwa; anachokiona ni bulungutu la dola za kimarekani. Akalihamishia lile bulungutu mkono wake wa kushoto ili ule wa kuume autumie kuchukua ile karatasi ambayo imekunjwa na kuonekana kama kipande. Domi akaichukua ile karatasi kisha polepole akaikunjua na kuanza kuisoma.

Wakati anaisoma ile barua, Domi alihisi kurukwa na akili. Mapigo ya moyo wake yaliongezeka zaidi na miguu ikaanza kumtetemeka, alikosa kabisa uvumilivu akakaa kitandani huku mtiririko wa machozi ukiyapamba mashavu yake. Ilisikitisha sana!

Domi mtoto wa kiume alikua analia! Maumivu aliyoyapata moyoni yalitosha kumfanya atokwe na machozi kwa kile kilichoandikwa kwenye ile barua ambayo ilikuwa mikononi mwake akiisoma.

MZEE wa makamo, mzee ambaye umri wake unaweza kufikia miaka 60 alikuwa akikokota baiskeli yake aina ya ‘Avon.’ Mzee yule aliendelea kuikokota baiskeli yake mpaka kwenye mti uliokuwa mbele ya nyumba yenye ukubwa wa wastani, nyumba ambayo ilikuwa imeezekwa kwa bati ambazo zimetawaliwa na mabaka yaliyosababishwa na kutu.

Mzee yule aliegesha baiskeli yake kwenye ule mti wenye kivuli, ambao ulikuwa kwenye eneo la mbele la nyumba ile.

Alipojiridhisha kuwa baiskeli yake iko salama alishusha pumzi ndefu kama ishara ya kutua mzigo wa safari ndefu. Akanyoosha kidole chake ambacho kinafuatana na kidole gumba, akakikunja kile kidole kikawa kama ndoano kisha akakomba jasho usoni pake na kulikung’utia pembeni. Yule mzee alirudia lile zoezi mpaka alipoona kuwa inatosha akakoma.

“Mama Domii” yule mzee aliita na sauti kutoka ndani ikasikika, “Abee,”

“Dume la mbegu nimesharudi, niletee maji ya kunywa tafadhali” alisema yule mzee huku karuhusu macho yake yaendelee kutalii mazingira ya nyumbani kwake. Nyumba ambayo ilitazamana na barabara iendayo Bunda. Kwa uapande wa kushoto ukiwa kama unatazama barabarani, nyumba yake ilipakana na nyumba nyingine yenye miti mingi ya miembe na kwa upande wa kulia , ilipakana na nyumba nyingine kubwa iliyokuwa na mti wa ukwaju pembeni yake. Hapo ndiyo kwa mzee Masaka, baba yake na Dominic Masaka. Mahali ambapo ni urefu wa viwanja vitatu vya mpira kutoka kwenye mti mkubwa wa Mong’we ukiwa kama unaelekea Bunda.

“kililililiiiii…..” sauti ya mama Domi ilisikika akipiga vigelegele huku mkononi akiwa ameshika kombe kubwa la bati lenye maji ndani yake.

“Pole na safari baba Domi” alisema kwa rafudhi ya kiikizu huku akipiga magoti kumpatia mumewe maji.

“Uanamme mapambano, nashukuru nimeenda na kurudi salama” kwa mbwembwe kama ilivyo kawaida yake Mzee Masaka alisema wakati akiyapokea maji aliyoletewa na mkewe.

Alikunywa fundo moja kubwa la maji bila kuyameza, akayatembeza mdomoni kwa mtindo wa kusukutua kisha akayatema pembeni. Akalinyanyua tena lile kombe kubwa na kuliweka mdomoni, aliposhusha lilikuwa tupu!

“Nikuongeze?” mama Domi aliuliza.

“Yanatosha mke wangu, tukae unipe habari za hapa.”

“Hapa ni kama ulivyotuacha, tuko salama salmin. Kama wasemavyo waswahili, ila Tina ndiye hayupo, amekwenda kufanya usafi kanisani, wiki hii ni zamu ya jumuia yetu”

“Aliondoka hapa nyumbani saa ngapi?” Mzee Masaka aliuliza.

Mama Doi akajibu “Aliondoka hapa tangu saa tatu asubuhi.”

“Tangu saa tatu mpaka sasa hivi? Usafi huo usafi gani, au ndiyo tuseme ameachiwa kanisa zima asafishe peke yake?” aling’aka mzee Masaka, mzee asiye na masikhara hata kidogo katika suala la malezi na makuzi ya watoto.

“Siyo hivyo baba Domi” Mama Domi alijibu kwa sauti iliyojawa na wasiwasi.

“Kumbe je?” Mzee Masaka alizidi kuuliza.

Safari hii mama Domi hakujibu kitu na badala yake alibaki akimtazama mumewe kwa woga.

“Mama Domi…Mama Domi.. angalia usiniharibie mtoto” Mzee Masaka alisema huku akiingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake na kutoa kijimfuko cha nailoni ambamo ndani yake mlikuwa na tumbaku. Mzee Masaka akachukua tumbaku kiasi na kuiweka mkononi halafu akakifunga kile kijimfuko cha nailoni, akakirudisha tena kwenye mfuko wa koti lake kilimokuwa awali.

Aliifikicha ile tumbaku kiasi iliyokuwa mkononi mwake, kisha akachukua kipande cha karatasi, akakinyoosha vema akaiweka tumbaku yake kwenye kipande hicho cha karatasi alichokiandaa, kisha akaisokota katika umbo la sigara. Alipomaliza akamgeukia mkewe ambaye muda wote alikuwa kimya akimtazama. “Naomba unilee moto mke wangu.”

“Jamani baba Domi, si ungekula kwanza halafu ndiyo uvute hayo masigara yako?”

“Hii ndiyo inanipa hamu ya chakula mke wangu, we niletee moto kwanza halafu nikishavuta utaleta chakula” Mzee Masaka alisema kwa sauti ya kubembeleza.

Mama domi aliinuka huku maneno yakimtoka, “Hayo masigara yako unayong’ang’ania ndiyo maana huponi kifua. Kila siku kukohoa tu, kwa sababu ya hayo masigara yako.”

Mzee Masaka aliyasikia maneno yote yaliyokuwa yakisemwa na mkewe. Yalikuwa ni maneno yaliyosemwa kila siku na mama Domi, lakini katika hali ya kutojali, mzee Masaka aliendela kuvuta tumbaku siku hadi siku, “Ntaaccha tu mke wangu, mbona ugimbi niliacha.” Alisema mzee Masaka kwa lengo la kujitetea baada ya kubaini ukweli wa wazi uliofumbatwa kwenye kauli ya Mama Domi.

Haukupita muda mrefu mama Domi alirejea akiwa na kijinga cha moto mkononi, akamkabidhi mumewe ambaye moja kwa moja aliiwasha tumbaku yake akaanza kuvuta. Alivuta mikupuo ya haraka haraka halafu akaruhusu moshi mwingi utoke nje kupitia tundu za pua yake.

Kwa jinsi moshi ulivyokua ukitokea puani kwa mzee Masaka, nilizifananisha pua zake na bomba la kutolea moshi kwenye pikipiki au trekta.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni