KUTI KAVU (4) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumanne, 7 Februari 2023

KUTI KAVU (4)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA NNE
ILIPOISHIA...
Alivuta mikupuo ya haraka haraka halafu akaruhusu moshi mwingi utoke nje kupitia tundu za pua yake.

Kwa jinsi moshi ulivyokua ukitokea puani kwa mzee Masaka, nilizifananisha pua zake na bomba la kutolea moshi kwenye pikipiki au trekta

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Baada ya kuwa amepiga mikupuo kadhaa, mzee Masaka alimgeukia tena mkewe, “Mbona hujaniuliza yaliyojiri huko nilikokuwa nimeenda?”

“Nilikuwa nasubiri upumzike kwanza baba Domi, enhe mmefikia wapi?”

“Huyu Mzee Tungu anazidi kunichokoza, si unakumbuka sehemu ya shamba letu aliyokkuwa ameimega?”

“Ndiyo nakumbuka.” Mama Domi alijibu huku akijiweka tayari kusikiliza mumewe anachomwambia.

“Basi amemega tena, na safari hii ameingia kwa hatua mbili zaidi. Nimejaribu kumuelewesha lakini anajifanya mgumu kuelewa.” Mzee Masaka alisema huku akiweka msokoto wake wa tumbaku mdomoni tayari kwa kuvuta tena.

“kwa hiyo umeamuaje?” mama Domi aliuliza.

“Mimi ni kama unavyonijua, sitaki matatizo na mtu, nimeamua hili suala nilipeleke mbele ya sheria. Likiwa huko, sheria itachukuwa mkondo wake.”

“Kweli baba Domi, ni bora haya mambo yakazungumziwe mahakamani. Isije ikawa kama ya Mzee Keelo na watoto wa mama Sabela, si unakumbuka walivyokatana mapanga ?”

“Nakumbuka sana, huyu mzee Tungu anafikiri anaweza kunidhulumu mimi shamba langu kama alivyomdhulumu mzee Kisilo! Hapa ameula wa chuya, mimi ndiye mzee Masaka, nitaisaka haki yangu kwa udi na uvumba mpaka nihakikishe inapatikana” mzee Masaka alisema huku akijipigapiga kifuani.

Mama Domi alimtazama mumewe kwa jicho la umakini halafu akatikisa kichwa chake juu chini, chini juu kama ishara ya kukubaliana na mumewe halafu akaondoka, na mara baada ya muda mfupi alirudi akiwa na sinia kubwa lililojaa maboga, karanga za kuchemsha, mahindi ya kuchemsha, maharage na njugu za kuchemsha. Vyote vikiwa vimechemshwa kabla ya kukauka. Mchanganyiko huu wa chakula huitwa ‘Imisumo’ katika jamii ya waikizu, chakula ambacho hupendelewa sana hasa wakati wa mavuno.

“Hewaaa..” mzee Masaka alisema wakati ananawa kwa lengo la kula, “Hapa ndipo nipokupendea mke wangu, hii ‘imisumo’ ndiyo mahala pake hapa. Watu wananiita Mzee kijana, yote hii ni kwa sababu unanijali mke wangu.” mzee Masaka aliyasema haya akiwa ameshamiri tabasamu usoni pake. Wakatazamana na mkewe, kisha kwa pamoja wakaangua kicheko cha furaha.
*****
KUPITIA dirishani, dirisha la kioo, juu kabisa kwenye ghorofa ya 18, Doi alikuwa akilisawiri vema jiji la Dar es salaam. Aliliona jinsi jiji hili linavyopendeza hasa nyakati za usiku.

Akiwa pale dirishani, Doi alikuwa akiwaza mambo mengi sana. Aliwaza jinsi Domi atakavyokuwa anapata tabu baada ya kuondoka kwake, aliwaza pia jinsi Domi atakavyoumizwa na barua aliyomwandikia na kumwachia pale chini ya mto muda mfupi kabla hajaondoka. Hata ilifika wakati akajuta ni kwa nini aliiandika ile barua.

Doi aliumia sana, alijua fika kuwa; kwa jinsi Domi anavyompenda, na kwa jinsi maneno ya kwenye barua yatakavyomwumiza, Domi hatokuwa na nguvu ya kujishughulisha na zile dola alizomwachia!

Mawazo yalizidi kumtafuna Doi, akawa kama vile anamuona jinsi anavyopata tabu. Moyoni Doi akajiona ni mwenye hatia, kwa unyama alioutenda. Akatamani aondoke pale hotelini ili aende nyumbani akamwone Domi na kumwomba msamaha. Lakini angewezaje kufanya hivyo baada ya yote aliyoyaandika kwenye barua?

Doi alijua fika kuwa Domi anapata tabu, na anapata tabu kwa sababu ya kumpenda yeye. Doi akajiona msaliti asiyestahili kuigwa, “Nisamehe Domi” Doi alijisemea moyoni huku machozi yakimtoka.

Akiwa katika lindi hilo la mawazo, Doi alihisi kuguswa na kitu maungoni mwake, akashtuka!
***
Wakati Doi akiwa dirishani, juu kabisa kwenye ghorofa ya 18 ndani ya chumba cha hotel ya ‘JB BELMONT HOTEL. Ni katika wakati huohuo, Domi alikuwa nyumbani kwake amekaa kwa kujikunyata huku akiwa amejiegemeza mlangaoni, mlango wa chumba chake ambao ulikuwa haujafunguliwa kwa siku ya pili mfululizo.

Akiwa pale mlangoni, Domi aliweza kuyatalii barabara mandhari ya humo chumbani kwake.

Ni kweli Domi alikubali yeye ni masikini wa kipato, kwa kuangalia hadhi ya nyumba anayoishi, na thamani ya samani zilizomo. Domi aliumia sana!

Haikuwa mara ya kwanza kwa Domi kuumizwa na hali ya maisha yake, ameumizwa mara nyingi, lakini hii ya kukimbiwa na mpenzi wake, mwanamke ambaye alimwona ndiye kila kitu kwake ilimuumiza sana.

Domi aliyazungusha macho yake chumba kizima, yalipotua kwenye picha aliyopiga wakiwa pamoja na Doi, Domi alijikuta akiita, “Doi.. Doi...” Kwa sauti hafifu yenye kukwamakwama. Alipoona hajibiwi Domi alisimama na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye ile picha akaishika, akainyanyua kutoka pale ilipokuwa kwa mkono mmoja, akaisogeza karibu kisha kwa kutumia kidole gumba, na kwa taratibu sana Domi aliigusa ile picha upande aliokuwa Doi, machozi yakamtoka sambamba na maneno aliyoyatamka kwa uchungu, “Umasikini ndiyo umekufanya unikimbie? Ina maana hukuamini kuwa ni kweli nilikuwa nazitafuta pesa kwa ajili yetu? Au ulidhani nimeridhika na hali hii ya maisha? Tumepitia shida ngapi Doi? Nilikwambia mama…nilikwambia haya yote yana mwisho na mwisho wake ndiyo huu umefika. Kama pesa tayari imeanza kuja, rudi mpenzi wangu Doi.. ruuudi” maneno haya yalikuwa yakimtoka Doi sambamba na machozi.

Akiwa bado ameshikilia ile picha, Domi alipepesa macho na kuziona zile dola za kimarekani zikiwa pale kitandani. Alipoziona zile pesa hasira zikamvamia ghafla, hapohapo nguvu ya ajabu ikamjia, akaivugumisha ile picha akaitupa ukutani, kioo kikavunjika vipandevipande na kuzagaa mule ndani. Domi akajihisi hali isiyo ya kawaida tumboni mwake, hapo ndiyo akakumbuka kuwa hajala kwa siku ya pili mfululizo. Njaa iliyokuwa imetulia sasa ikaanza kuchachamaa tumboni mwake, hitaji la kupata chakula likamjia!

Domi alichukua funguo za gari akatoka nje na kwenda mpaka alipoiegesha gari yake aliyopewa kazini, alipofika aliufungua mlango akaingia garini, akaiondoa gari kwenda kutafuta chakula.
***
Doi alishtuka baada ya kuwa ameguswa maungoni mwake, alipogeuka alikutana na busu zito kutoka kwa Damian, “Hi baby” Damian alisalimia.

“Hi” Doi aliitikia lakini kwa sauti ya unyonge.

Miongoni mwa watu ambao wako makini na wayafanyayo, Damian ni mmoja wao. Damian alikuwa ameshaigundua hali aliyo nayo Doi, kwa utundu wa hali ya juu Damian alianza kujariu kuirejesha furaha ya Doi, “Relax baby” Damian alisema huku akiwa amemkumbatia Doi.

“Halafu kabla sijasahau mpenzi, nina bonge la zawadi. Na hii ni kukuonesha kuwa mimi siyo mtu wa ahadi hewa” Damian alisema kabla hajamshushia tena Doi mvua ya mabusu ambayo yalizidi kumchanganya kabisa.

“Fumba macho mpenzi” Damian alisema tena kwa sauti iliyojaa mahaba.

“Nhu! Jamani Damian, kwani vipi?” hatimaye Doi alifungua kinywa na kuzungumza.

“Fumba macho, kuna kitu nataka nikuoneshe mpenzi”

“We nawe una mambo” Doi alisema huku akiruhusu macho yake yafumbe kama alivyoraiwa na Damian.

Baada ya Doi kufumba macho Damian aliisogelea ile bahasha aliyokuwa ameiweka kitandani wakati anaingia mule chumbani, akaifungua na kutoa kilichomo kisha akamkamshikisha Doi ambaye bado alikuwa ameyafumba macho yake. Kwa mikono miwili Doi akashikilia alichoshikishwa na Damian.

“Haya sasa fumbua macho yako mpenzi” Damian alisema.

Doi alifumbua macho yake na kujikuta ameshikilia sanamu ya plastiki, aliitazama ile sanamu bila kujua ni sanamu ya nini na ina maana gani. Alijiuliza maswali mengi bila kupata majibu, Uzalendo ukamshinda, ikabidi aulize, “Hiki ni nini Damian?”

Damian akamtazama Doi kwa jicho la kisanii halafu akacheka kidogo kabla ya kusema, “That is Parris….hiyo ndiyo Parris mpenzi” Damian alisema.

Kinyume na matarajio yake Damiana alimshuhudia Doi akiwa katika hali ya mashangao.

Damian akajua bado hajaeleweka na kabla hajajua cha kusema alimsikia Doi akisema, “Parris… una maana gani kusema hii ndiyo Parris?”

Kwa umakini wa hali ya juu ikabidi Damian afungue Darasa kwa Doi ambaye alionekana kutoielewa suprise ya Damian, “Sikiliza baby, hiyo sanamu ni sanamu ambayo husimama kama ishara ya jiji la Parris, yaani kama vile hapa Dar es salaam, kuna mnara wa askari na huo mnara wa askari ndiyo kama nembo ya utambulisho wa jiji hili la Dar, hivyo basi nimekuletea hiyo sanamu ya mnara wa ‘EIFEL’ ambao uko jijini Parris, kukujulisha kuwa nitakupeleka Parris, Ufaransa ukapumzike kama ishara ya mapenzi yangu kwako.” Damian alijitahidi kueleza kadiri alivyoweza kumwelewesha Doi.

Angalau sasa Doi alianza kuelewa Damian anamaanisha nini kwa kumletea sanamu ile.

Doi alibaki mdomo wazi baada ya kusikia maelezo ya Damian. Hakuyaamini masikio yake ikabidi aulize tena, “Damian, tafadhali…naomba unifafanulie vizuri.” Damiana bila hiyana wala kuuma uma maneno akamwambia, “Nitakupeleka Parris ukatembee, ukatembee ili uione dunia. Uone jinsi watu wanavyoponda raha ndani ya jiji la maraha duniani, Parris!”

Masikio ya Doi sasa yalisikia sawia kile alichokuwa akikisema Damian.

Ujumbe huo ulizibadiri kabisa fikira za Doi, Doi akaanza kuwaza jinsi atakavyokuwa mara atakapokuwa jijini Parris, Ufaransa.

Mara nyingi amewasikia watu mabalinbali wakiongea na kusimuliana juu ya maisha ya Parris, jiji ambalo huaminika kuwa ni kivutio cha wapenda starehe duniani, jiji la waponda raha! Amekuwa akisoma na kusikia kuwa mtu fulani maarufu yuko kwenye fukwe za Parris akiponda raha.

Kwa shauku ya kutaka kujua mengi Doi alishindwa kuvumilia ikabidi aulize tena, “Tunaenda lini Damian?”

Swali hilo ndilo alilolitarajia Damian, “Muda wowote kuanzia sasa” Damian alijibu.

Doi alikuwa bado hajayaamini masikio yake, mawazo juu ya Parris yakakipamba kichwa chake.
***
Majira kama ya saa 3:30 usiku Domi alikuwa katikati kabisa ya jiji la Dar es salaam. Ikiwa ni siku ya pili tangu Doi atoweke nyumbani, aliamua kutoka kwa ajili ya kutafuta chakula baada ya kutokula kwa siku mbili mfululizo.

Domi alikuwa akilipandisha gari lake ghorofa ya pili, mahali yalipo maegesho ya magari ndani ya jengo la ‘MAFUTA HOUSE’

Haikuwa kawaida yake kuonekana maeneo hayo, iwe mchana au usiku kwa sababu ya kutokuwa na pesa. Kwa mara ya kwanza alifika hapo miaka mitatu nyuma akiwa mwaka wa tatu wa masomo yake. Alifika hapo kwa kupelekwana rafiki yake ambaye ndiye alikuwa mwenyeji wake ambaye kwake yeyeilikuwa ni kawaida yake kuhudhuria kwa lengo la kucheza muziki hasa nyakati za mwisho wa juma.

Siku hiyo alikuwa na pesa kiasi mfukoni mwake, akaamua kuja kupata chakula katika mgahawa wa SAVANA LOUNGE. Ni katika jengo hilohilo ndiyo Damian na Doi walichukua chumba tangu siku iliyopita.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni