KUTI KAVU (5) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumanne, 7 Februari 2023

KUTI KAVU (5)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA TANO
ILIPOISHIA...
Siku hiyo alikuwa na pesa kiasi mfukoni mwake, akaamua kuja kupata chakula katika mgahawa wa SAVANA LOUNGE. Ni katika jengo hilohilo ndiyo Damian na Doi walichukua chumba tangu siku iliyopita.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
Domi aliingia katika mgahwa huo wa SAVANAH ambao uko ghorofa ya tatu, na Damian na Doi walichukua chumba ghorofa 18 katika jengo hilohilo.

Baada ya kuegesha gari lake Domi aliingia mgahawani na kukaa kwenye meza ya pembeni, meza ambayo ilimpa uhuru wa kuona karibu kila pembe ya ukumbi wa mgahawa ule wa SAVANAH, meza ambayo Domi aliiona kuwa inamfaa zaidi.

Domi aliagiza chakula na kutulia kwenye meza hiyo huku akila polepole.
***
“Damian..” Sauti ya Doi ilisikika ikiita.

Damian aliyekuwa anatazamana uso kwa uso na Doi aliitika, “Naam mpenzi...”

“Ni kweli tunaenda Ufaransa?” Doi aliuliza.

“Ndiyo mpenzi…inabidi twende Ufaransa kwa mapumziko ya mwezi mmoja kabla hatujarudi na kufunga ndoa yetu” Alisema Damian kwa ushawishi wa hali ya juu.

Doi alimtazama tena Damian kwa macho ya kutoamini, Damian akawa ameligundua hilo. Ili kuumaliza utata akauliza, “Kwani we hutaki kwenda ufaransa?”

“Hapana, siyo kama sitaki…”

“Kumbe je?” Damian alimtupia Doi swali la udadisi.

Doi alifikiri kidogo, halafu akajibu, “Unajua nyumbani wanaelewa kuwa mimi niko kwa Domi…na mpaka sasa sijui kama Domi ameshakwenda nyumbani kuniulizia au bado, na pia….”

Kabla hajaendelea Damian alimkatisha, “Usiwe na wasiwasi na hilo hata kidogo, ngoja kwanza niandae utaratibu wa safari, mipango ya safari ikikamilika wewe utapeleka zawadi kidogo nyumbani, na ukiwa huko nyumbani ndiyo utajua kama wazazi wanajua lolote kuhusu wewe kutokuwepo kwa Domi au la, baada ya hapo ndiyo tutajua cha kufanya au wewe unaonaje mpenzi?” Damian alimlainisha Doi kwa maneno, na ili kumfunga kabisa Damian alihitimisha maelezo yake kwa swali la mtego kwa Doi.

Bila hiyana Doi alijibu, “Sawa” Baada ya kusema hayo, Damian alimuomba Doi waelekee ghorofa ya tatu kwa lengo la kupata chakula cha usiku kwenye mgahawa wa SAVANAH LOUNGE. Saa 4:15 Damian na Doi waliingia kwenye lifti kwa ajili ya kwenda kupata chakula kwenye mgahawa uliokuwa ghorofa ya tatu.
***
Chakula kilipita kwa tabu sana kwenye koo la Domi. Alijilazimisha kula lakini alishindwa kabisa. Mawazo juu ya Doi yalizidi kumtesa. Alishindwa kuelewa kama aliyefanya hivi ni Doi yule anayemjua au ni Doi gani? Dominic alizidi kujiuliza ni lini Doi alianza kumsaliti? Alitamani amuone ili amuangalie vizuri na kumfananisha ili aone kama anafanana na kile alichokifanya.

Katika watu ambao Domi aliwaamini, Doi ni mtu pekee. Domi hakumwamini mtu yeyote isipokuwa Doi, na ndiyo maana mpaka muda huo Domi hajataka kuamini kama Doi ndiye aliyemfanyia hivi.

Mawazo yalipozidi kumtinga Domi, alishindwa kabisa kula. Aliisogeza sahani ya chakula pembeni kisha akatoa noti mbili za elfu kumikumi akaziweka mezani kwa malipo ya chakula alichokula akaondoka. Wakati huo ikiwa ni saa 4:12 usiku.
******
USIKU wa manane bwana alishtuka usingizini akamwamsha bibi kwa kumpapasa. Bibi alipoamka alimkumbatia bwana ambaye pia alimkumbatia bibi, kwa pamoja wakakumbushana dhamira ya wao kuwa pamoja usiku ule.

Baada ya kufanya tendo hilo takatifu bila Baraka za watakatifu, wote wakapitiwa na usingizi. Masaa machache baadaye, “Ngriii..ngriii..ngriii….” Sauti ya kengele ya kutegeshwa kwenye simu ilisikika, wote wakaisikia wakanyanyua vichwa vyao juu.

Zai aliwasha taa halafu akamsalimu bwana wake, “Wajisikiaje mpenzi?”

“Mi niko salama, hofu ni kwako mahabuba”

“Nami pia niko salama” Zai alijibu kisha akashuka kitandani, akajifunga khanga iliyofunika mwili wake kuanzia kifuani mpaka magotini, akaenda kumwandalia mume wake maji ya kuoga ili aoge kabla hajaenda kazini.

Baada ya Mudi kutoka kuoga, alikuta Zai amekwishamuandalia nguo za kuvaa. Mudi alipomaliza kujiandaa alimuaga mpenzi wake kama ilivyo kawaida yao. Akaondoka huku nyuma akimuacha mkewe ambaye aliendelea na usafi wa nyumba.

Uwepo wa Zai nyumbani kwa Mudi ulimfanya Mudi ayafurahie maisha tofauti na hapo mwanzo kabla hajaanza kuishi na Zai. Kwa kazi yake ya udereva wa daladala, Mudi alijitahidi kuhakikisha mahitaji yote ya muhimu hayakosekani nyumbani. Kila aliporudi usiku kutoka kazini alimpatia Zai kiasi cha pesa ili akitunze kama akiba yao ya baadaye. Akamjali kama mpenzi wa roho yake, kwa mavazi na kila kilicho cha muhimu kwa mwanamke.

Mara kwa mara gari lake linapokwenda mpaka ‘Yombo Machimbo’ Mudi alimpigia Zai simu ili akachukue mboga, matunda na bidhaa kadha wa kadha kwa mahitaji ya nyumbani. Licha ya kumpatia kila siku kiasi cha pesa kwa ajili ya matumizi hayo ya nyumbani.

Akiwa amepaki gari lake kituoni maeneo ya Buguruni kwa lengo la kusubiri abiria, mara ghafla simu yake ya mkononi iliita, “Hallow Mudi hapa. Nani mwenzangu?”

Sauti kutoka upande wa pili ikamjibu, “Ni mimi Udaku, jirani yako, chumba cha pili hapa nyumbani tunapoishi”

“Ahaa , jirani habari yako?” Mudi alisema kuashiria kuwa ameshamtambua.

“Safi jirani, hapo ulipo tunaweza kuongea?” Sauti ya Udaku jirani yake na Mudi ilisikika.

“Ongea tu jirani, nakupata”

“Samahani jirani, unaweza kuniona mmbeya lakini hili inabidi ulifanyie kazi”

“Lipi hilo jirani?” Mudi aliuliza ili kupata ufafanuzi zaidi.

“Mida kama hii, yaani kuanzia saa 10 mpaka sa 12 jioni kila siku, mkeo huwa anaongea sana na simu mpaka ananitia mashaka juu usalama wa hizo simu anazopiga. Sikiliza kaka Mudi, naomba usinielewe vibaya,” alisema Udaku.

Mudi alishangazwa sana na ile taarifa aliyopewa na jirani yake. Akilini mwake aliona kuwa ni taarifa ya kipuuzi na isiyo na mantiki yoyote. Na kwa Mudi, Udaku hakuwa na jina jipya zaidi ya mmbeya.

Mudi alijibu, “Ahsante” halafu akakata simu.

Baada ya kukata simu, Mudi aliingia kwenye tafakuri nzito, “Yaani huyu Udaku anaacha kufanya mambo yake anaanza kuchunguza mambo ya watu, hizi ndiyo tabu za uswahilini”

Akiwa kwenye lindi hilo la mawazo, Mudi alishtuliwa na sauti ya kondakta wake, “wawahishe baba… wawahishe, gari limeshapendeza,”

Mudi akondoa gari, baada ya kuamriwa na kondakta wake.

***
Dominic alikuwa amejinyoosha kwenye kiti cha mbele cha gari lake alilopewa na kampuni, alikilaza kile kiti ili ajinyooshe kwa kujinafasi zaidi. Akiwa kwenye kiti hicho, Domini alikuwa anawaza mambo mengi juu ya Doi. Ni wazi kabisa kuwa Domi hakutaka kukubaliana na kile alichokifanya Doi, “Au ametekwa?” Domi aliwaza.

“Isije ikawa ametekwa halafu akalazimishwa kuandika ile barua. Oooh no… hapana hajatekwa huyu. Kama ametekwa, watekaji wake wanataka nini? Ningeweza kusema wanataka pesa… lakini siyo rahisi kwa sababu nimekuta pesa ndani,” mawazo juu ya mawzo yalimzonga Dominic.

Jambo moja lilimuia gumu Domi, nalo ni kupiga simu nyumbani kwa kina Doi ili kuuliza kama anaweza kupata taarifa yoyote yenye kuhusiana na Doi. Jambo hili lilikuwa gumu kwa sababu, ndugu wote wa Doi hawakuwa wameridhia Doi kuishi na Dominic kwa sababu ya umasikini aliokuwa nao. Walijitahidi sana kumzuia Doi lakini pingamizi zao hazikufua dafu, Doi akaenda kuishi kwa Dominic bila kujali umasikini wake.

Pamoja kuyatambua yote hayo Dominic alipiga moyo konde, akawasha gari na kuondoka kuelekea Mbagala Kibonde Maji ambako ndiyo nyumbani kwao na Doi.

Mita chache kabla hajafika nyumbani kwa kina Doi, Domi aliegesha gari lake na kuanza kutembea kwa miguu kuelekea nyumbani kwa kina Doi. Alipofika alibisha hodi akaitikiwa. Kinyume na matarajio yake, Domi alipewa mapokezi ambayo hata yeye yalimshangaza.

“Karibu…karibu baba ukae…” ilikuwa ni sauti ya mzee Vioja baba yake na Doi, mzee ambaye alikuwa mwiba kwenye uhusianao wa Doi na Dominic.

Mapokezi aliyopewa Domi yalimtia wasiwasi, kwani hata mama na baadhi ya ndugu wa Doi walionekana kumchangamkia sana.

“Karibu baba,” Sauti ya mama Doi ilisikika akikmkaribisha.

“Ahsante, Shikamoo baba… shikamoo mama” Domi aliwasilimia wote kwa heshima na taadhima.

“Habari za siku mwanetu?” Sauti ziliwatoka wote kwa pamoja, baba na mama na Doi. Hali hii ya kutoa sauti kwa pamoja iliwafanya watazamane usoni kabala ya kugutushwa na suti ya Domi, “Nzuri tu, za hapa?”

“Za hapa pia ni nzuri, karibu sana baba..”

Bada ya salamu na maongezi ya hapa na plale, baadhi ya ndugu wa Doi waliokuja kumsalimia Domi waliondoka na kuwaacha baba na mama Doi wakiwa na Domi sebuleni. Ukimya ukatawala baina yao!

Wakati Domi akiwa anayatafakari yale mapokezi. Baba na mama Doi nao walikuwa wakiwaza yao. Ukimya ukaendelea kushika hatamu kwa muda kidogo.

“Mwanangu Domi…” hatimaye mzee Vioja aliuvunja ukimya ule. “Mwanetu Dominic,” Mzee Vioja aliita tena kwa sauti ambayo ilikuwa imebeba mamlaka ya baba mwenye hekima.

“Naam baba,” Dominic aliitikia kwa heshima ya hali ya juu.

“Kwanza kabisa tunashukuru kwa pesa ulizotutumia, mimi na mama yako tunassema ahsante sana mwanetu” Dominic aliyasikia barabara maneno ya mzee Vioja, lakini hakujua aseme nini kwa wakati huo. Akilini mwake alikuwa akiwaza bila mafanikio. “Pesa…Pesa nilizotuma?” Dominic alijua wazi kuwa yeye hakuwa amewatumia pesa wazazi wa Doi. Na hapo ndiyo akagundua kuwa ; yawezekana Doi alikuja kwao kuleta pesa, na katika ujio wake huo hakuwa ameweka wazi kuwa alishaondoka nyumbani kwake, yaani kwa Domi. Akiwa kwenye lindi hilo la mawazo, Domi alishtuliwa na sauti ya Mzee Vioja, “Dominic” mzee Vioja aliita

“Naam baba” Domi aliitika

“Unaonekana mwenye mawazo sana, vipi Doi yuko salama, au kuna tatizo gani huko nyumbani?” Mzee Vioja aliuliza na kumfanya Domi atambue kuwa fikra zake ziko sahihi kuwa, wazazi wa Doi hawajui kama binti yao hayuko nyumbani kwake. Ikambidi ajiweke sawa kabla hajaanza kuongea.

“Baba na mama,” Domi aliita kwa heshima kama ishara ya kutaka kuwaweka sawa ili wasikie kwa makini kile anachotaka kuwaambia, “Ukweli ni kwamba, mimi sijatuma pesa, na mpaka sasa tunavyoongea leo ni siku ya tano tangu Doi atoweke nyumbani”

“Unasemaje?” sauti ziliwatoka baba na mama Doi kwa pamoja hali iliyomfanya Domi ashtuke.

“Ina maana hizi dola hujatuma wewe?” Mzee Vioja aliuliza.

“Mimi sijatuma dola zozote wazazi wangu”

“Na mbona Doi amesema ni zawadi kutoka kwa mkwe wetu, ina maana kuna mkwe zaidi yako?” Mama doi alimtupia swali Dominic, swali ambalo lilizidi kumchanganya kabisa Domi.

Wakati huo mzee Vioja alikuwa ametumbukwa na jicho la mshangao na fadhaa.

“Ni kweli, mimi sijatuma pesa” alisema Domi kwa sauti iliyojaa masikitiko makubwa.

Mzee Vioja alimtazama Dominic kwa umakini halafu akamuita, “Dominic,”

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni