KUTI KAVU (6) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumanne, 7 Februari 2023

KUTI KAVU (6)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA SITA
ILIPOISHIA...
Wakati huo mzee Vioja alikuwa ametumbukwa na jicho la mshangao na fadhaa.

“Ni kweli, mimi sijatuma pesa” alisema Domi kwa sauti iliyojaa masikitiko makubwa.

Mzee Vioja alimtazama Dominic kwa umakini halafu akamuita, “Dominic,”

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...
“Naam baba,”

“Hebu nieleze kila kitu bila kuficha mwanangu…” Mzee Vioja alisita kidogo na kuruhusu fundo kubwa la mate lipite kooni mwake kuelekea tumboni, halafu akaendelea. “Kulikuwa na mgogoro wowote baina yako na na Doi?”

“Hapana, hatukuwa na mgogoro wowote,”

Mzee Vioja alitulia kidogo akawaangazia macho kwa zamu, wote Dominic na mama Doi aliyekuwa ubavuni kwake upande wa kushoto, halafu akamalizia kwa Dominic aliyekuwa amekaa kinyonge mbele yao, akaendelea, “Labda…kuna tofauti yoyote uliyokuwa umeibaini kwa mwenzako kwa siku za hivi karibuni, nikiwa na maana kabla hajaondoka?”

“Hapana baba, sikuwa nimeibaini tofauti yoyote mpaka siku niliyofika na kutomkuta kabisa Doi” alipokuwa anayasema haya, Domi alipatwa na uchungu usioelezeka, lakini alijikaza kiume.

“Mama Doi, hebu tupe nafasi kidogo,” Alisema mzee Vioja na Mkewe akaondoka pale sebuleni na kuwaacha Dominic na mzee Vioja ambaye ni baba yake na Doi.

Baada ya mama Doi kuondoka Mzee Vioja alimgeukia Dominic na kusema, “Mwanangu, hebu nieleze vizuri kwa sababu hapa tumebaki wanaume tu”

Domi alimueleza kila mzee Vioja, alimueleza juu ya barua na pesa amabazo alizikuta chini ya mto.

Baada ya kuelezwa Mzee Vioja alisikitika sana kwa jinsi binti yake alivyomtia aibu.hata hivyo baada ya maongezi hayo Dominic aliaga na kuondoka.
***
Doi alikuwa akiustaajabia mkoba ambao Damian amemnunulia, pamoja na begi kwa ajili ya safari yake ya Parris nchini Ufaransa. Ulikuwa ni mkoba safi wa ngozi uliovutia kutazamwa na kila jicho lenye uono! Mkoba wa rangi nyeusi, wenye mishikio ya iliyotengenezwa kwa bati la shaba nyeupe na kurembwa kwa rangi ya dhahabu. Hakika mkoba huu mzito uliipendeza nafsi ya Doi.

Ukiachilia mbali mkoba, begi ambalo Damian alimnunulia kwa ajili ya safari hiyohiyo ni begi la bei mbaya, lilikuwa ni begi zito la ngozi lililotengenezwa nchini italia. Doi alivitazama vitu hivyo kwa macho ya kustaajabia. Akiwa bado anashangaa begi la safari na mkoba wake, Damian akamkabidhi tikiti ya ndege, “Hii ni tikiti yako kwa ajili ya safari” Alisema Damian wakati akimkabidhi tikiti ya ndege ya shirika la ndege la Emirates.

Doi aliipokea ile tikiti akiwa anatetemeka, hakuamini kama kweli safari yake ya Parris ilikuwa imeiva!

Aliisoma ile tikiti ili kujiridhisha zaidi. Ni katika kusoma huko ndiyo akagundua kuwa ile tikiti ilikuwa yake peke yake.

“Vipi, mbona tiketi ipo yangu tu, kwani wewe husafiri?” Doi aliuliza.

“Kwa nini nisisafiri? Mimi pia nitasafiri ila hatutaongozana. Mimi nitasafiri kesho kuelekea Michigan, Marekani. Kuna mambo naenda kuyaweka sawa halafu ndiyo niende parris next week kwa ajili ya kukupokea wewe jumamosi kama tiketi yako inavyoonesha.” Maelezo ya Damian yalimshtua kidogo Doi, kwani alitarajia kuona wanasafiri pamoja, kinyume na fikra zake, kila mtu atasafiri kwa wakati wake kama alivyofafanua Damian.

“Lakini mbona hukuwa umesema mapema?” Doi alimtupia Damian swali.

Damian alifikiri kidogo halafu akauliza swali badala ya kujibu swali aliloulizwa na Doi, “Kwani kuna tatizo?”

“Hapana, ila…” kabla hajamalizia kauli yake Damian alimuwahi, “Ni kweli nimefanya kosa kwa kutokueleza mapema juu ya jambo hili. Ila naomba unilewe kuwa sina nia mbaya, nataka niwahi mapema nikafanye kazi zilizo mbele yangu ili tuwe na muda mwingi wa kuyafurahia maisha tukiwa Parris, au waonaje?”

“Kama ni hivyo basi sawa, ila utaniacha mpweke sana”

“Najua ila usijali, nitakuachia pesa ya kutosha ili ikupunguzie upweke kwa kufanya ulipendalo”

Mazungumzo yao yaliisha kwa kuwatupa kwenye dimbwi la kicheko!

Siku iliyofuata Damian, alipanda ndege na kumuacha Doi akiwa na ukwasi wa pesa kwa ajili ya kufanya lolote la kumuondolea upweke kama alivyoraiwa na Damian.

Ndege ilipoiacha ardhi, Doi alirudi hotelini ambako aliendelea kukaa mpaka siku ya siku ilipofika. Siku hiyo Doi aliandaa kila kitu chake cha safari ikiwemo pasi ya kusafiria, kibali cha kukaa Ufaransa pamoja na mizigo yake yote aliyokuwa ameiandaa kwa ajili ya safari.

Jambo lililomtesa Doi ni kusafiri bila ndugu yake yeyote kujua juu ya safari yake. Doi alishindwa kujua ataagaje nyumbani kwao. Pia alijua kuwa; Domi asingeweza kuvumilia kukaa muda wote huo bila kwenda kwao, yaani kwa mzee Vioja. Alijua kama Domi alienda kwao na yeye akaenda ataivuruga safari yake, kwa kuhofia kuhojiwa juuu ya anakokwenda na ilikuwaje akaondoka kwa Domi.
***
Baada ya kuwa amepigiwa simu na Udaku jirani yake, kuhusiana na simu zinazopigwa na mkewe hasa nyakati za jioni, Mudi alipuuza kwa kuamini kuwa ni umbea na hakujishughulisha na suala hilo kabisa.

Siku moja akiwa kibaruani kwake, Mudi aliwaza juu ya taarifa ile ya Udaku. Aliona si vema kupuuzia kabisa ujumbe ule na pia si vema kuchukua maamuzi ya haraka. “Inabidi kufanya uchunguzi kwanza, isije ikawa ni mbinu ya kutugombanisha na Zai” Mudi aliwaza yote haya wakati yuko barabarni anaendesha.

Ikatokea siku akiwa kituoni anasubiri abiri abiria, majira kama ya saa 10:15 jioni, Mudi alichukua simu na kumpigia Zai, simu iliita mara moja na mara sauti ya Zai ikasikika kutokea upande wa pili, “Hallow,”

“Halioo bibie” Mudi alijibu baada ya kusikia sauti ya Zai upande wa pili.

“Nakusikia mme wngu, habari za kazi?”

“Za kazi njema tu, nimekukumbuka sana mke wangu”Mudi alisema

“Usijali mme wangu, mi nipo kwa ajili yako”

“Ok basi hakuna shida tutaonana baadaye nikirudi” Alisema Mudi na kukata simu.

Saa moja baadaye Mudi alipiga tena simu kwa Zai ili kuona kama ataweza kugundua lolote lenye kuhusiana na kile alichokisema bi Udaku, kama ilivyokuwa awali, Zai hakuchelewa kupokea simu aliipokea mara tu ilipoanza kuita wakongea.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bi Udaku, Mudi alitarajia kukuta simu ya Zai inatumika kwa muda huo, lakini kinyume na matarajio yake simu haikuwa inatumika kama alivyotarajia. Siku hiyo ikapita Mdi akiwa kwenye mninginio wa taharuki!

Siku iliyofuta ilikuwa ni siku ya alhamis, siku hiyo Mudi aliamua kukabidhi gari kwa mtu mwingine kwa muda. Mtindo huo ulikuwa ni kawaida kwa madereva wengi wanapokuwa wamechoka au kupatwa na dharula, mtindo huo ulikuwa maarufu kama deiwaka. Mudi alikabidhi gari kwa dereva mwingine ‘Deiwaka’ ili aendeshe mpaka yeye atakaporudi.

Majira ya kama saa 10:30, Mudi alifika nyumbani kwake alikopanga maeneo ya Yombo Buza. Kwa kunyata alizunguka nyuma ya nyumba na kwenda mpaka lilipo dirisha la chumba chake ambacho wanaishi yeye na mpenzi wake, Zainabu Mpotoshi.

Alipofika pale dirishani Mudi alitulia tuli ili aweze kusikia yanayojiri ndani. Mudi alitega sikio na kusikiliza kama kuna atakaloweza kulisikia kutoka ndani.

Kama ilivyoeleza taarifa ya Bi Udaku ni kweli Zai alikuwa bize akionega na simu!

Mudi alikuwa akiyasikia barabara maneno yote aliyokuwa akiongea Zai na simu ya upande wa pili. Mudi alihisi kuchanganyikiwa kwa maneno aliyokuwa akiyasikia, “Usijali, hiyo jumamosi nikija utafurahi….mimi ndiye Zai binti Mpotoshi” Zai aliendelea kujinadi kwenye simu.

Mudi alishindwa kabisa kuvumilia akatoa simu yake mfukoni akampigia Zai, akasikia simu inaita ikifuatiwa na suti ya Zai, “Subiri kidogo mpenzi wangu, n’takutafuta baada ya muda ya mfupi,” Mudi alizidi kuchanganyikiwa alipoyasikia maneno hayo.

Mara akagutushwa na sauti ya mkewe, “Hallow,” sauti ambayo ilisikikia mara baada ya mlio wa muito wa simu kukoma. “Hallow.., niambie mpenzi?” alisemaMudi huku donge la uchungu likiwa limemkaba kooni.

“Ninalo basi..” Sauti ya Zai ikasikika kupitia spika ya simu ya Mudi na kwenye matundu ya nyavu za dirishani alipokuwa amejibanza.

Mudi alijitahidi ili aendelee kuongea na simu licha ya uchungu aliokuwa nao, “Nimekukumbuka mke wangu…”

“Usijali mme wangu nipo kwa ajili yako” hiyo ilikuwa ni sauti ya Zai, sauti iliyojaa unafiki ambao Mudi ameshaubaini.

“Powa basi, baadaye” Alijibu Mudi na kukata simu.

Baada ya kukata simu Mudi aliendelea kukaa dirishani, haikupita muda akamsikia tena Zai anaongea na simu, “Enhe nambie mpenzi wangu”

Hasira zikampanda Mudi, lakini akamuomba Mungu aendelee kumpa ujasiri na subira ili aendelee kuusikiliza upuuzi wa Zai, mwanamke aliye mwamini na kumuweka ndani kama mke. Akamthamini kwa kila kitu, mahaba motomoto, fedha na mavazi! Zai atake nini kwa Mudi asipewe?

Mudi akazunguka kutoka kule nyuma ya nyumba alipokuwa, akaenda mpaka mlangoni kwake, akausukuma mlango akakuta umefungwa kwa ndani! Akaamua kubisha hodi na mara baada ya muda mfupi Zai akafungua.

“Vipi, mbona umejifungia saizi?” Mudi alimtupia swali la kizushi. Bila aibu wala woga Zai akajibu, “Nilikuwa nimelala mme wangu,” Alijibu Zai huku akiachia mwayo wa kinafiki.

Hapo akili ya Mudi ikazidi kupambanua mambo, akajikaza kiume bila kuonesha tofauti yoyote kwa Zai, akaingia ndani. Alipoingia ndani Mudi alivua fulana aliyokuwa amevaa akaitupa kwenye kochi lililokuwa mule chumbani, kisha yeye mwnyewe akajitupa kitandani kama mzigo!

“Pole mme wngu, umechokaje,” alisema Zai huku akikaa kitandani na kuruhusu mkono wake uchezee manywele yaliyotapakaa kifuani kwa Mudi.

“Nimechoka sana Zai wangu, na hizi kazi zetu za kuamka usiku usiku hizi we acha tu,”

“Ngoja nikuwekeee maji ya kuoga” alisema Zai na kunyanyuka kutoka pale kitandani alipokuwa amekaa na na kuelekea nje.

Hiyo ilikuwa ni bahati kubwa sana kwa Mudi, moyoni alikuwa akiomba itokee nafasi kama hiyo ya kuachwa chumbani peke yake, nafasi amabyo kweli imetokea.

Zai alipotoka tu nje Mudi aliamka pale kitandani kama ninja, kwa kasi ya ajabu alikisaili chumba kizima na mara macho yake yakatua kwenye kabati la vyombo. Moja kwa moja akaielekea hotpot iliyokua kabatini akaifunua. Mudi hakuamini macho yake baada ya kuishuhudia simu aina ya Nokia ya tochi ikiwa imezimwa na kufunikwa ndani ya ile hotpot!

Mudi alifunika lile hotpot na kurudi kitandani, akilini alipiga mahesabu makali ya kutega mtego siku ya jumamosi.

Punde si punde Zai alirejea, akafungua kabati la nguo na kumtolea Mudi taulo. Mudi alivua nguo, akajifunga lile taulo, akaelekea bafuni huku akiongozwa na Zai aliyem’bebea sabuni na mswaki.

***
Dominic alirudi kutoka kazini akiwa amechoka. Baada ya kuegesha kwenye maegesho yake, akaanza kupanda ngazi kuelekea kwenye Apartment yake ambayo ilikuwa ghorofa ya kwanza. Apartment ambayo amepangishiwa na kampuni anayoifanyia kazi kama mkataba wa ajira unavyoeleza.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni