KUTI KAVU (7) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumatano, 8 Februari 2023

KUTI KAVU (7)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA SABA
ILIPOISHIA...
Dominic alirudi kutoka kazini akiwa amechoka. Baada ya kuegesha kwenye maegesho yake, akaanza kupanda ngazi kuelekea kwenye Apartment yake ambayo ilikuwa ghorofa ya kwanza. Apartment ambayo amepangishiwa na kampuni anayoifanyia kazi kama mkataba wa ajira unavyoeleza.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...


Kwenye makazi hayo mapya, yaliyokuwa maeneo ya ilala, Domi aliona angalau sasa ameanza kuishi kama ambavyo siku zote alitarajia kuishi; kazi nzuri, nyumba nzuri na kadhalika.



Kutokana na uchovu uliosababishwa na kazi nyingi za kutwa nzima, Domi alipitiwa na usingizi muda mfupi baada ya kuwa amejiegesha kwenye kochi!



***

Mnamo majira ya saa 9 alasiri, Doi alikuwa ndani ya Tax akielekea uwanja wa ndege tayari kwa safari ya Parris. Njiani aliwaza mambo mengi sana. Aliwaza jinsi atakavyokuwa akishafika Ufaransa. Alipoyafikira maisha ndani ya Parris, aliiona saa yake kama vile haisogei!



Doi alitamani kufumba na kufumbua awe tayari ameshafika ndani ya jiji la Parris, nchini Ufaransa. Aliwaza pia jinsi atakavyowamiss ndugu zake hasa baba yake na mama yake. Moyoni aliwaza kuwa, atakaporudi awanunulie angalau gari, ili na wao wafaidi matunda ya kuzaa.



Katika kuwaza kwake, Doi hakumsahau Dominic, mwanaume aliyempenda Doi kuliko kitu chochote. Aliwaza jinsi Domi anavyopata tabu kwa kumkosa. Doi aliumia sana na kumuonea Domi huruma, katika lindi hilo la mawazo machozi yakaanza kumtoka. Akajipangusa kwa kutumia leso yake, alipotupa macho nje ya gari alibaini kuwa yuko maeneo ya JET CORNER, eneo lililo mita chache kabla ya kufika uwanjani, eneo ambalo kuna njia inayochepuka kwenda Yombo Buza, eneo ambalo yeye na Domi walikuwa wanaishi.



Kona hiyo ilimkumbusha mengi ya nyuma, alikumbuka kuwa; kwa mara ya kwanza aliipita njia hiyo kuelekea Buza kwa ajili ya Dominic. Na inawezekana asingeipita kama asingekua kwenye uhusianao na Dominic.



Akiwa kwenye lindi hilo la mawazo, hatimaye sauti ikamtoka, “Kwa heri Domi wangu” alisema Doi huku machozi yakimtoka. Akachukua leso yake akajipangusa tena.



“Dada tayari tumefika,” sauti ya dereva ilisikika na kumgutua Doi kutoka mawazoni.

Akashuka, wakasidiana na dereva kubeba mizigo mpaka eneo ambalo abiria hukaaa kusubiri ukaguzi. Baada ya kumfikisha pale, dereva alirudi garini na kuondoka. Doi alibeba mizigo yake kuelekea chumba cha ukaguzi kilichopo pale uwanjani.



Kama ilivyo kawaida ya viwanja vingine, uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK NYERERE pia kuna utaratibu wa kukagua mizigo ya wasafiri kwa sababu za kiusalama. Askari waliokuwa pale uwanjani kwa ajili ya ukaguzi walikuwa makini sana, hii ni baada ya uwanja huo kukumbwa na kashfa ya kupitisha kilo 150 za madawa ya kulevya aina ya ‘CRYSTAL METHAMPHETAMINE.’ Hivyo ili kulinda kazi yao na heshima ya nchi, iliwabidi wafanye kazi yao kwa umakini mkubwa sana.



Abiria aliyekuwa mbele ya Doi alikaguliwa, na alipomaliza kukaguliwa ikafuata zamu ya Doi kwa ajili ya kukaguliwa.



Walianza na mkoba na baadaye begi. Mizigo ya Doi ikawekwa pembeni na Doi akaamuliwa kukaa pembeni sanjari na mizigo yake.



Kitendo cha kuambiwa kae pembeni yeye pamoja na mizigo yake kilimshtua sana, kilimshtua kwa sababu abiria aliyekaguliwa kabla yake alipita moja kwa moja baada ya ukaguzi, hivyo ikambidi Doi aulize, “Vipi jamani mbona mimi nawekwa pembeni?” kabla hajajibiwa alishtushwa na kundi la askari walioingia mule ndani.

“Uko chini ya ulinzi, wewe pamoja na mizigo yako,”

Doi alipigwa na butwaa, askari wale walimchukua msobemsobe na kumpeleka ndani zaidi, “Nimefanya nini jamani, mbona sielewi?”



Huko ndani mizigo yake ilitawanywatawanywa kwa ajili ya kunya kufanya uchunguzi wa kina. Doi alichanganyikiwa hakujua ni kwa nini anafanyiwa vile!

Mara unga mweupe ukawa unatolewa kwenye mishikio ya mkoba wake na kwenye mishikio ya begi lake na wale askari waliokuwa wakifanya upekuzi.

“Leo umepatikana,” sauti ya askari ilisikika ikisema na kuzidi kumchanganya zaidi Doi, “Jamani mimi sijui lolote,” alilalama Doi lakini hakuna aliyemjali.

“Mmezoea hapa madawa yenu, mnatuharibia kazi na kulitia doa taifa. Sasa kimefika kiama chenu” Alisema akari ambaye alikua anamalizi kuyakusanya yale madawa na kuyaweka pamoja.

Doi alilia sana!



Dakika chache baadaye alichukuliwa maelezo na kufungulikiwa jalada, halafu akatolewa na kupakizwa kwenye gari la polisi chini ya ulinzi mkali wa askari wenye bunduki huku waandishi wa habari wakipiga picha.



Mpaka wakati huo, Doi alikuwa amechanganyikiwa kabisa, safari yake ya Ufaransa ikawa imeota mbawa na uelekeo ukawa ni kituo cha polisi cha kati





KAMA Kuna kitu Mudi alikiamini maishani, basi ni kujitambua. Aliamini ili uweze kufanikiwa ni lazima ujitambue kwanza; wewe ni nani, unatoka wapi, uko wapi, unaelekea wapi na mtu sahihi kwako ni nani, ili uweze kufanikisha yote unayoyahitaji.



Siku hiyo ya jumamosi, Mudi aliaga na kuelekea zake kibaruani kama ilivyo ada. Huku akiendelea kuwasiliana na bi Udaku kwa siri kubwa. Kwa pamoja walipanga kufanya mawasilano ili Udaku afuatilie nyendo za Zai kwa siku hiyo. “Ukimuona anatoka tu, we mfuatilie kimya kimya ikibidi kodi hata pikipiki mimi nikija nitalipa” ilikuwa ni sehemu ya maelekezo aliyoyatoa Mudi kwa Udaku.



Huku nyuma Zai alijipamba isivyo kawaida! Alikuwa amependeza ndani ya vazi lake la baibui, kilemba aghali kichwani, na mwili wake ukiwa umepulizwa uturi wenye kunukia haswa!



Baada ya kujitazama kwenye kioo kwa mara kadhaa, Zai arliridhika na muonekano wake, akautwaa mkoba wake akautupia begani tayari kwa kuondoka. Akafunga mlango wa chumba chake kisha taratibu akawa anaiacha nyumba.



***

Wakati Zai anajiandaa, Bi Udaku naye alikuwa akijiweka tayari kuanza kufuatilia nyendo zake. Hivyo wakati anaondoka, bi Udaku alimtanguliza kwa hatua kadhaa mbele huku akichukua tahadhali kubwa ili asiweze kuonekana na macho ya Zai.

“Hallow… kaka Mudi,” Bi Udaku aliongea kupitia simu yake, na sauti ya upande wa pili ikajibu, “Hallow.. jirani nakupata..”

“Aisee.. huku mkeo amejipamba haielezeki! Yaani amejipamba ile balaa…” Alisema Bi Udaku kwa mbwembwe nyingi na kumuweka Mudi kwenye wakati mgumu.

“Enhe, amevaaje?”

“Amevaa baibui moja matata sana na kichwani ametupia kilemba cha hatari chenye rangi ya dhambarau…. Hayo marashi sasa… yaani mkeo ananukia njia nzima.” Alizidi kuongea bi Udaku kwa kumpamba na kumnanga Zai kwenye simu.



Huku Mudi alipagawa… alipagawa kiasi cha kuhisi kuchanganyikiwa. “Sasa naomba ule naye sahani moja… hakikisha hakupotei machoni, mfuate hatua kwa hatua na uwe unanijulisha kupitia simu.” Mudi alitoa maelekezo kwa bi Udaku, maelekezo yaliyoonekana kumfurahisha sana bi Udaku.



***

Zai alivuka barabara na kusimama upande wa kushoto, akaipiga bajaji mkono, ikasimama akajitoma ndani, ikaondoka!



Baada ya Bajaji kuanza mwendo, Bi Udaku naye kwa haraka alivuka barabara, akaiendea pikipiki iliyokuwa upande wa pili, “Ifuate ile Bajaji nyekundu, ifuate kwa umakini ili asiweze kujua kama wanafuatwa”



“Wameshakuliza au? maana watoto wa mjini hawakawiagi” alisema yule dereva wa pikipiki wakati anaiondoa pikpiki yake tayari kwa kuifuata ile Bajaji.

“Haya hayakuhusu, jali biashara yako” alisema bi Udaku na yule dereva wa pikpiki akasema, “Utalipa zaidi ya kawaida, hapa ni sawa na kuiweka roho yangu mkononi kwa kutibua michongo ya watu,”

“kaza mikono motto wa kiume, pesa ndiyo imekuleta kazini,” alizema Udaku na Yule dereva akakaa kimya. Wakawa wanaifuatilia ile Bajaji ambayo ilikuwa mita chache mbele yao.

“Hallow..”

“Yeah.. nambie..”

“Ameshuka hapa Mwisho wa Lami”

“Kama nilivyosema… hakikisha hakupotei machoni.” Mudi alizidi kusisitiza na bi Udaku akaongeza umakini zaidi kwa Zai ambaye baada ya kushuka alienda moja kwa moja akapanda daladala inayoishia JET CORNER.

Isingekuwa rahisi kwa Zai kumtambua Bi udaku kwa sababu alikuwa amevaa ‘helmet’ iliyomfanya asitambulike na yeyote ambaye angemwona.



“Ngriii… ngriiii” Simu ya bi Udaku iliita, “Hallow Mudi” bi Udaku aliongea na sauti ya upande wa pili ikajibu, “Kuna mpya..?”

“Hapana.. gari bado halijaondoka” Bi Udaku alisema.

“Ok, usiruhusu akupotee machoni” Mudi alisisitiza na Bi Udaku akajibu, “Sawa”



****

Mudi alikabidhi gari kwa rafiki yake ambaye alifahamika kama Deiwaka. Akachukua pikipiki ambayo alikuja nayo Deiwaka, akaipiga moto na kwa kasi ya ajabu akaendesha mpaka JET CORNER, ambapo alifika na kusimama kando ya barabara mbele kidogo ya geti la CTM-TILES

“Gari limeanza kuondoka,” bi Udaku aliongea kupitia simu yake ya mkononi.

“Tayari nimeshafika JET CORNER, we lifuatilie hilo gari kwa nyuma na kama atashuka kabla ya JET nifahamishe..”

“Powa..” Alijibu bi Udaku.

Gari lilitembea mpaka LUMO, bi Udaku akiwa analifuatilia kwa nyuma, pale LUMO lilisimama lakini hakuna abiria aliyeshuka, ila kuna abiria wawili waliingia kwenye gari hilo, likaondoka huku bi Udaku akilifuatilia kwa nyuma kwa pikipiki aliyokodi. Baada ya LUMO lile gari halikusimam tena mpaka lilipofika JET CORNER, abiria wote wakashuka akiwemo Zai.



***

Akiwa pale pale pembeni ya barabara mbele kidogo na lilipo geti la CTM-TILES, Mudi alimshuhudia Zai akishuka kutoka kwenye gari aina ya TOYOTA HIACE iliyotoka Machimbo. Alikuwa amependeza ndani ya mavazi yake nadhifu aliyovalia. Kwa madaha kabisa Zai alitembea kuelekea kule zinakopaki gari ziendazo, Banana, Gongo la mboto, Chanika na Pugu.



Wakati bado Mudi amemkodolea macho Zai wake, simu yake iliita. “Hallow Jirani, bibie ameshuka hapa JET CORNER, na hivi tunavyoongea yupo kwenye kituo cha magari yaendayo Gongo la mboto. Nafikiri safari yake iko uelekeo huo.” Alisema bi Udaku.

“Nimeshamuona, sasa unawezza kurudi nyumbani niachie sehemu iliyobaki… nitaimaliza mwenyewe.” Alisema Mudi kwa sauti iliyojaa gadhabu, licha ya kujitahidi kuificha hali hiyo lakini iliweza kutambulika sawia masikioni mwa bi Udaku..



Gari la kwanza liliondoka Zai akiwa bado yupo kituoni, likaja pili likaondoka zai akiwa bado yuko palepale kituoni. Gari la Gongo la mboto likaja pale kituoni, Zai akajitoma ndani kwa madaha na kwa kujiamini, gari likaondoka.



Mudi kwenye pikipiki yake akaanza kulifuata kwa nyuma lile gari alilopanda Zai, huku akiwa ameacha umbali wa mita kadhaa zilizowatenganisha baina yao.



Gari lilisaga Lami mpaka Uwanja wa ndege bila Zai kushuka, likatembea mpaka Posta.. hapo pia lilisimama lakini Zai hakuonekana kushuka . Lilipita Njia panda segerea, Banana, Mombasa bila Zai kushuka huku Mudi akilifuata kwa nyuma gari hilo aina ya TOYOTA –DCM.

Gari alilopanda zai lilipofika Gongo la Mboto lilisimama na Zai akashuka huku Mudi akimshuhudia kwa uangalifu ndani ya helmet iliyomfanya asiweze kutambulika na yeyote.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni