KUTI KAVU (8) - CnZ Media

CnZ Media

Jisomee Simulizi Mpya Kila Siku

Jumatano, 8 Februari 2023

KUTI KAVU (8)

Je unajua kwamba Simulizi zote unazozipata hapa zipo kwenye app ya CnZ Media?

Humo Pia Utakuta:
๐Ÿ“– KUSOMA SIMULIZI
๐ŸŽฌ FILAMU na TAMTHILIA za KITANZANIA
๐Ÿ˜‚ VIDEO za KUCHEKESHA
๐Ÿ“‘ MAKALA za AFYA na MAPENZI

Install app hii GUSA HAPA utavipata vyote hivyo bure kabisa

Jina: KUTI KAVU

SEHEMU YA NANE
ILIPOISHIA...
Lilipita Njia panda segerea, Banana, Mombasa bila Zai kushuka huku Mudi akilifuata kwa nyuma gari hilo aina ya TOYOTA –DCM.

Gari alilopanda zai lilipofika Gongo la Mboto lilisimama na Zai akashuka huku Mudi akimshuhudia kwa uangalifu ndani ya helmet iliyomfanya asiweze kutambulika na yeyote.

WAKATI UNAFUNGUA KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE WALAU KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UPO NJE YA APP INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KWA WAKATI

SASA ENDELEA...




Aliposhuka tu kwenye gari lile la Gongo la mboto ambalo lilikuwa limefika ukomo wa safari yake, zai alishuka akajisogeza kwenye gari zinazoenda Chanika akajitoma ndani.



“Anaenda wapi huyu? Hajawahi kuniambia kama ana ndugu maeneo haya, sasa huku anaenda kwa nani?” Wakati Mudi anaendelea kujiuliza maswali hayo, gari alilopanda Zai likaanza kuchapa mwendo huku Mudi akilifuatilia kwa nyuma kwa umakini wa hali ya juu.



***

Huku Nyamuswa, mama na baba Domi walikuwa wamekaa na binti yao anayeitwa Tina. Walikaa kwa mazungumzo ya kifamilia mara tu baada ya chakula cha mchana. Hii haikuwa mara yao ya kwanza, walizoea kukaa pamoja na kuzungumza kuhusiana na familia yao, juu ya nini kifanywe au kipi kisifanywe kwa manufaa ya familia yao na jamii kwa ujumla.

Hiki kilikuwa ni kikao cha sita kufanyika bila uwepo wa Domi, kwa sababu tu hakuwepo nyumbani. Tofauti na vikao vingine vyote, kikao cha siku hii kilimuhusu zaidi Domi.



“Kama nilivyosema jamani, Domi amefanikiwa kupata ajira, na amesema twende wote Dar es salaam tukajue anapoishi, pamoja na kusalimiana kwa sababu hatujaonana naye siku nyingi” Hiyo ilikuwa ni sauti ya kavu ya mzee Masaka, ambaye baada ya kuongea aliweka pumziko na kisha kumuangalia mama Domi na baadaye binti yao Tina kwa zamu kama vile kuna kitu anataka kusikia kutoka kwao kabla hajaendelea.

Ikawa hivyo, mama Domi alijiweka sawa pale kitini alipokaa kisha akasema, “Kama amebahtaisha kamfupa hilo ni jambo la kheri sana, na nimefurahi sana kusikia hivyo. Lakini hili la kwenda sisi wote mpaka Dar es salaam limekuwa la ghafla mno!”

“Kwa nini unasema ni ghafla mama?” Tina mdogo wake na Domi alirukia.

“Hah… hapo unakosea Tina, mwache mama yako azungumze kisha nawe utazungumza. Yawezekana majibu ya swali lako yalikuwa kwenye maelezo yanayofuata,” Alisema mzee Masaka na kuungwa mkono na mkewe, “Ni kweli Tina mwanangu, una haraka gani?” Alisema mama Domi halafu akaendelea, “…nasema ni ghfla kwa sababu, hiyo ajira aliyoipata Domi… ameipata hivi karibuni. Si ndiyo? Mama Domi aliwatupia swali na kisha kuwaangalia usoni pao kwa zamu. Wote kwa pamoja, yaani Mzee Masaka na bintiye wakajibu, “Ndiyo”

“Basi kama ndivyo, ni wazi kuwa bado anahitaji muda zaidi wa kujipanga”

“Kweli kabisa” Mzee Masaka aliunga mkono maelezo ya mkewe huku Tina akiwa ametulia kimya akifuatilia kwa makini.

“Mi naona ni bora mmoja wetu akatuwakilisha huko mjini ili tumpe muda zaidi wa kujipanga… ili siku moja atupokee wote huko mjini”Alimaliza mama Domi.



Maelezo ya mama Domi yalionekana kuwaingia wote na wakakubaliana na mawazo yake .

Walijadiliana ni nani aende, mwisho wote wakakubaliana aende mzee Masaka.



***

Mudi aliendelea kulifuatilia lile gari alilopanda Zai mpaka ameneo ya kona ya Kigogo Fresh ambapo mara baada ya gari kufika Zai alishuka.

Baada ya Zai kuwa ameshuka, gari lile likaendelea na safari.



Mudi alikuwa amesimama mita kadhaa nyuma kabla ya ya eneo kilipo kituo. Hivyo kutokea pale alipo aliweza kumuona Zai wakati anashuka kutoka kwenye lile gari na kuvuka barabara.



Mudi naye alivuka, kwa umakini wa hali ya juu kabisa akaendelea kumfuatilia Zai bila yeye kujua.



Mara baada ya kuvuka barabar Zai alishika njia ndogo iliyokuwa ikiongoza kuelekea yalipo makazi ya watu. Alivuka mtaa wa kwanza, wa pili kisha akapinda kushoto ambako aliongoza moja kwa moja kwenye nyumba ndogo ambayo ilikuwa haijaisha sawasawa.



****

Mapunda kijana mwenye urefu wa wastani, alikuwa akitoka bafuni. Mkononi alikuwa ameshikilia ndoo ambayo bila shaka ilikuwa ni ya kuogea. Mwilini mwake alikuwa amejisitiri kipande cha suruali ambacho kiliishia magotini.



Mapunda alijongea taratibu mpaka kwenye msingi wa nyumba katika upande ambao haukuwa na tofali hata moja, isipokuwa msingi ambao Mapunda aliiweka ndoo yake ya kuogea.



Mapunda alikuwa akiishi kwenye nyumba hiyo, nyumba ambayo alikuwa akiishi kama mlinzi kwa sababu mwenyewe alikuwa mbali na alitaka ahamie hapo baada ya nyumba yake hiyo kuwa imekamilika, hivyo alimuweka Mapunda kwa shughuli mahsusi ya kusimamia mafundi na pia kulinda vifaa vingine vya ujenzi ambavyo vilikuwa hapo hapo kwenye chumba cha pembeni.



Akiwa anaweka ndoo yake pale kwenye msingi, Mapunda alimuona mgeni wake akija kwa madaha huku akisukumwa na upepo mwanana wa kadiri, upepo ambao uliiwahisha harufu nzuri ya uturi aliojipulizia Zai mpaka kwenye pua zake.



Baada ya kumuona mgeni wake, Mapunda alitabasamu na Zai naye akajibu mapigo.

Zai alipiga hatua na hatimaye akawa amefika mpaka alipokuwa Mapunda, wakakumbatiana na kubusiana huku nyuso zao zikiwa zimeshamiri furaha isiyo kifani.

“Vipi mpenzi,?” Mapunda alisalimia huku akizungusha mkono wake kwenye kiuno cha Zai na kumkokota kuelekea ndani.

“Safi tu, za hapa?” Zai alijibu wakati anapiga hatua sambamba na Mapunda kuelekea ndani.



****

Baada ya kupinda mtaa wa kwanza , njia ikaanza kuwa finyu na mbovu kiasi cha kutoruhusu pikipiki kupita. Kwa tabu Mudi aliikokota pikpiki yake lakini hakufanikiwa, pikipiki ikagoma kabisa kupita kwenye njia ile finyu na mbovu.



Mudi alipoona njia inaleta usumbufu, aliizima pikipiki akaiegesha pembeni kwenye upenu wa nyumba. Akaanza kumfuatilia Zai kwa miguu huku kichwa chake kikiendelea kukingwa na ile helmet ili asiweze ktambulika.



Mudi alijibanza nyuma ya mnazi na kumshuhudia Zai akikumbatiwa, na baadaye kukokotwa kwa kushikwa kiuno kuelekea ndani.

‘Ahaa…. Kumbe, hivi kuna kitu gani huyu zai amekikosa kutoka kwangu? Simridhishi kwa lipi, Fedha, mapenzi au kitu gani? Huyu mwana izaya huyu…. Dah.. ngoja,” Alijisemea Mudi wakati akiwashuhudia wezi wake wakiingia ndani.



Mudi alitembea kwa kunyata mpaka kwenye ile nyumba, akazunguka kwa nyuma mpaka lilipo dirisha akatega sikio.

Kabla hajasikia lolote Mudi aliamua kujivuta nyuma kwa umakini zaidi ili asiweze kusikika na walio ndani, “Kwani nahitaji kusikia nini tena?” Mudi aliwaza.

“Haya niliyoyaona yanatosha kunithibitishia kuwa ninasalitiwa. Huyu mpuuzi huyu…. Leo ndiyo amelikalia kuti kavu” Mudi alijisemea wakati anaondoka kutoka pale alipokuwa kwa mtindo wa kunyata, kuelekea kule ulipo mlango wa ile nyumba ambayo wamo wezi wake.

Mudi alifika mpaka mlangoni pale akiwa mwenye hasira na mawazo tele. “Nifanye fujo?.... aah hapana haina haja” Mudi aliuegemea ukuta wa ile nyumba kimgongomgongo huku akiomba busara itawale maamuzi yake. Aliugeukia tena ule mlango akaugonga, “Ngo…ngo ngoo…”

“Nani?” Sauti ya kiume kutoka ndani ilisikika ikihoji.

“Mimi Jafari fungua,” Mudi aliamua kubuni jina akiamini kuwa; ni kawaida, kuwa unapobisha hodi popote pale, na ukaulizwa wewe ni nani, unataja tu jina lolote na mlango utafunguliwa.





Ikawa ni kama vile alijua. Mlango ulifunguliwa na Mapunda akatoka nje akiwa amelowa jasho. Mapunda alimtazama Mudi huku akijaribu kuvuta kumbukumbu ni wapi amewahi kumuona, lakini hakufanikiwa kukumbuka ni wapi aliwahi kumuona.

“Oya vipi?” Mapunda aliuliza.

Mudi alikaa kimya kidogo halafu akanyanyua midomo yake, “Oya mshikaji sikiliza,”

Mapunda akajiweka vizuri huku akiitazama sura ya Mudi kwa umakini, sura iliyojaa ujasiri na jazba. Wasiwasi ukamwingia Mapunda na mapigo ya moyo yakambadilika ghafla!

“Sisi wote hapa ni wanaume unasikia man…. Huyo uliye nae ndani ni mke wangu. Hatujafunga nae ndoa lakini nimeishi nae kwa muda mrefu sana. Kwao wananijua na kwetu wanamjua” Mudi alisema na kumsababisha Mapunda aingiwe na hofu kwa kukutwa na mke wa mtu. Kwa woga akauliza, “Huyu Asha ni mkeo?” Mapunda aliuliza kwa mshangao.

“Haitwi Asha, jina lake ni Zai… Zainabu Mpotoshi. Hapa sikuja kufanya fujo, nakuachia huyo mke simtaki tena…. Ila nakuomba umuite aje … aje ahakikishe kuwa ni mimi na nimezijua nyendo zake” Alimaliza Mudi kisha akajivuta hatua moja nyuma kama vile anajiandaa kufanya chochote.

Maneno ya Mudi yalimchanganya Mapunda kiasi cha kuifanya akili yake ichoke ghafla, bila kutarajia chuki ikamjia Mapunda dhidi ya Zai aliyekuwa ndani akitetemeka kwa woga.

Akauachia mlango aliokuwa ameushikilia kuuzuia ili usifunguke wote kwa lengo la kusitiri yaliyomo ndani, alipouachia mlango ulifunguka wote ukawa wazi kama goli na kuacha pazia lililokuwa likining’inia kuyasitiri ya ndani.

“Karibu ndani kaka… ingia uje tuzungumze” Maneno yalimtoka Mpunda.

“Hapana kaka… hapa panatosha, muite tu huyo Malaya aje anione niondoke.

Mapunda aligeuzia shingo yake kule ndani akamuita Zai, “Oya.. hebu simama ue hapa”



****

Wakati Mudi anaanza kuongea Zai, aliitambua fika sauti yake, na maneno yote aliyoyaongea Mudi aliyasikia barabara. Hofu ikamwingia, ubaridi ukamwingia na malaika yakamsimama mwilini na kufanya vipele vidogovidogo vya baridi vionekane juu ya ngozi yake.

Zai akajiona amelikalia kuti kavu, akajiona hana jinsi katika maisha, Zai hakujua nini kitafuata baaada ya hapo.

Zai alimdanganya Mapunda kuwa hajolewa na anaishi kwao na wazazi wake, hiyo bado haitoshi.. alimdanganya kuwa anaitwa Asha kumbe jina lake ni Zai.

Akiwa kwenye lindi la mawazo, Zai aligutuliwa na sauti ya Mapunda ikimuita, “Oyaa… hebu simama uje hapa”

Zai alipoinyanyua shingo yake aliyokuwa ameiinamisha chini kwa aibu, alimuona Mudi akiwa nje amesimama huku mikono yake akiwa ameifumbata kifuani.

Zai alihisi kama mkojo unamtoka, akiwa bado anajishauri cha kufanya, Mapunda alimfuata pale kitandani na kumvutia mlangoni!

Pale mlangoni Zai alisimama akiwa na khanga yake moja tu, iliyokuwa imemfunika kuanzia kifuani mpaka magotini. Zai alihisi kupatwa na aibu.. aibu ya karne, machozi yakamtoka na kuyaharibu mashavu yake mazuri ambayo kwa wakati huo yalikuwa yamepoteza mvuto kwa sababu ya michilizi machozi.

Zai alitamani akimbie lakini hakuweza, mkono wake mmoja ulikuwa umeshikiliwa na Mapunda, hivyo asingeweza kuchoropoka… na mbele yake alikuwepo Mudi hivyo asingeweza kufika mbali kabla hajakamatwa endapo angejaribu kufanya upuuzi wa kutaka kukimbia.

Akabaki ameganda kama nyamafu asijue la kufanya!

“Oya braza demu mwenyewe si ndiye huyu?”

“Ndiye huyo huyo, Zai…. Zainabu Mpotoshi, mwanamke niliyempenda nikampa kila kitu” Mudi alisema huku akiwa amesonta kidole kuelekea pale mlangoni waliposimama Zai na Mapunda.

“Yaani hawa wanawake bwana…. mi angeniambia kuwa ni mke wa mtu wala nisingehangaika naye… ona sasa! Powa kaka, yaani akitoka hapa ndiyo mwisho wa mimi na yeye sitaki tena kumuona” Mapunda alisema na maneno yake yalisikika sawia masikioni mwa Zai aliyekuwa pembeni yake. Maneno yale yalimchoma moyo kiasi cha kumfanya aangue kilio cha sauti. Akajiona kama mjinga na mpumbavu wa mwisho chini ya jua, akaliona kuti kavu alilolikalia likidondoka na yeye akiwa juu yake. Alilia sana.

USIIKOSE SIMULIZI INAYOFUATA

Kama Una Channel Youtube Haupati Watazamaji Karibu Tuzisambaze Video Zako, Utagharamia Tsh 10 kwa Kila View(Mtazamaji) 1
Wasiliana Nami Kwa WhatsApp +255718274413

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni