Mtunzi: ___
SEHEMU YA PILI
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Meli hiyo iliyokuwa na mabaharia katili kupita kiasi. Walimpokea Prosper kwa ukatili usiosemekana. walimtendea mengi maovu, akitukanwa na kusimangwa.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
TUENDELEE...
Aliishi kwa taabu mno, akiyastahamili yote hayo, mwishowe, akawa mnyama kama mabaharia wale.
Alisuguliwa akasugulika, akageuka kuwa Baharia binadamu mwenye moyo wa mnyama. Akamchukia kila mtu na hata kuichukia nafsi yake mwenyewe. Wakati wote Prosper alitawaliwa na fikra potofu. Alitamani kutenda jambo ambalo lingeiumiza jamii. Kwa bahati mbaya, hakuwa mwana sayansi mwenye vipaji vya ugunduzi, ugunduzi ambao ungemwezesha kuiteketeza jamii. Angekuwa na uwezo wa kujitengenezea bomu la nuklia angeifanya dunia itoweke katika uso wa ulimwengu.
Kwa kuwa, hayo yalikuwa mbali na uwezo wake, lakini alifanya ukatili mdogo tu. Hakuona shida kumtosa baharini mtu yeyote aliyebainika kudandia meli kama alivyofanya yeye alipokuwa mtoto. Wala, kwake haikuwa dhambi kufanya mapenzi na mwanamke na kisha kukata koo la mwanamke huyo asubuhi.
Pamoja na ukatili huu kuufanya kwa siri, lakini sifa zake ziliyafikia masikio mbalimbali. Mmoja kati ya watu waliovutiwa na unyama wa Prosper aliona fahari kukutana nae katika meli hiyo kwa siri. Wakaiacha meli hiyo. Safari yao ikaishia katika chuo kimoja kilichofichika kikiwa na watu wachache wenye moyo kwama wa Prosper. Kilikuwa chuo cha ujasusi kilichokuwa chini ya nchi kadhaa kubwa na tajiri. Kilifundisha mbinu kadha wa kadha kuhujumu siasa, uchumi na msimamo wa nchi kongwe na changa ambazo hazikuwa tayari kulegeza misimamo yao na zile zenye msimamo mkali.
Prosper alipohitimu tayari alikuwa hodari wa yote, kuandaa mauaji, kusababisha mapinduzi, kudhorotesha uchumi. Alikuwa mtu aliyeipenda sana kazi yake, na alifanya mengi yaliyowafurahisha na kuwatisha viongozi wake. Aliweza kusafiri hadi Afrika Kusini ambako alijitangaza kama mpigania uhuru na aliaminika na kushirikishwa katika harakati za ukombozi. Lakini aliweza kutoroka na siri zote huku akiwa tayari ameua na kuwaacha wapigania uhuru wakiuana wenyewe kwa wenyewe. Mtindo huo ameutumia sehemu mbalimbali duniani. Ingawa waliohujumiwa walimhisi baada ya kuondoka, lakini kwa jinsi alivyokuwa akiwaendea katika sura tofauti, na majina bandia, hakuna aliyeweza kumweka katika kumbukumbu.
Mfano ni leo alipokuwa akitoka na msichana huyu aliyechanganyikiwa; Waridi. Wajumbe wote wa mkutano ule ambao walibahatisha kuuona uso wake wasingeweza kumfikiria kuwa ndiye mtu yule yule waliyekuwa naye mkutanoni kwa jinsi alivyobadilika. Hata mwendo wake ulikuwa tofauti. Leo alitembea huku akichechemea kidogo.
Gari dogo aina ya Toyota lilikuwa likiwasubiri mara tu walipoifikia barabara.
“Ingia ndani ya gari”, Prosper aliamuru.
“Samahani…, samahani kaka, tu… tunaelekea wapi?”, Waridi alifanikiwa kuupata ulimi wake ambao alihisi ulikuwa mzito kutokana na hofu.
Prosper akaukunja uso wake huku akisema, “Sitaki maswali”, akapita upande wa dereva na kumfungulia mlango Waridi. Alipoingia ndani ya gari na kuketi, gari likatiwa moto na kuteleza juu ya barabara, likijitahidi kukwepa mashimo. Walipoifikia barabara ya Morogoro, gari hilo liliekezwa katikati ya jiji. Wakaiacha Magomeni, wakaingia Upanga, wakipita hapa na pele hata waridi asijue kama walikuwa wapi,
Gari lilisimama mbele ya jumba moja kubwa sehemu ambayo hisia zilimwambia Waridi kuwa ni katikati ya Jiji. Prosper alitelemka na kumwagiza Waridi amfuate. Walipokaribia mlango mmoja kati ya milango kadhaa ya jumba hilo, Prosper alimnong’oneza Waridi akisema; “Unasikia? sitiki vurugu la aina yoyote hapa ndani. Uwe binti mtulivu kama ulivyo sasa. Utafaidika na kutoka salama. Vinginevyo…” akaiacha sentesi hiyo ikielea na kuanza kushugulikia funguo.
Walipoanza kuingia, mlango wa pili ulifunguka na uso wa mzee wa Kihindi kujitokeza ukichungulia. “Aha… ni bwana Chain siyo? Karibu sana”.
“Shukrani”, Prosper alijibu.
“Naona leo uko na mama, au siyo?, Mhindi huyo aliendelea akitabasamu. “Shauri kazi ya vitabu iko chosa kidogo. Lazima starehe na dada kidogo”.
Prosper naye akajitia kucheka, “Eh, ndiyo. Lakini huyu ni sekretary wa kampuni yetu. Yeye amekuja kuchukua maandishi fulani kwa ajili ya kuchapishwa kwenye mashine wakati nitakapokuwa safarini”.
“Ah”, Mhindi alijibu huku akimtazama Waridi kwa tamaa ya wazi. Hili lilikuwa moja kati ya majumba ambayo Prosper alikuwa amepangisha vyumba ambavyo aliviyumia kwa shughuli zake. Hapa, mbali na kufahamika kwa jina la Chain Kimara, pia walimtambua kama msomi ambaye alikuwa akiutumia muda wake mwingi kufanya utafiti wa mambo kadha wa kadha ambayo alikuwa akiyaandikia kitabu. Hivyo, muda wote ambao Prosper alijificha chumbani akifanya shughuli zake za siri, wao waliamini kuwa alikuwa akiendelea na mipango ya kuhakikisha kitabu chake kinatoka. Akiwa hapa, hata sura yake ilionekana kama ya Profesa asiyependa kuuchezea muda wake kama ilivyokuwa tabia yake ya kisomi na kistaarabu.
Huko ndani picha ilikuwa hiyo hiyo, Waridi alilakiwa na chumba kikubwa kilichojaa vitabu vya kila aina , vilivyopangwa kistaarabu katika dawati maalumu. Katikati ya chumba hiki kulikuwa na meza kubwa yenye dalili zote za mashughuliko. Chumba cha pili kilikuwa na kitanda kipana, friji, radio na mahitaji yote ya chumba cha malazi. Ni katika chumba hicho alikokaribishwa Waridi.
Akajibwatika juu ya kochi lililomwelekea Prosper, aliyeketi juu ya kitanda.
“Nimekuita hapa ili nikutume kuua mtu”, Prosper alimweleza Waridi. Dakika ishirini zijazo nataka mtu huyo awe safarini akielekea kuzimu. Sasa hivi yuko katika baa moja hapa mjini akinywa pombe. Hiyo iwe pombe yake ya mwisho”, Prosper alisita akamtazama Waridi. “Utanisaidia kuifanya kazi hiyo bi mdogo”, akaongeza kwa sauti ya unyenyekevu.
“Siwezi kuua…” Waridi aligugumia.
Prosper alikunja uso akamwangalia Waridi kwa hasira huku akisema. “Sina haja ya kukukumbusha mara kwa mara kuwa najua yote yaliyompata marehemu Bomba. Naweza kutoa siri hiyo wakati wowote nawe ukajikuta ukining’inia juu ya kitanzi. Nitakufanyia hisani ya kuficha habari hiyo iwapo tu nawe utanisaidia kumtoa duniani mtu huyu. Tumeelewana?”,
Waridi hakujua ajibu nini. Kwa kila hali. alimwona mzee huyu kampatia na kamweka mahali panapomstahili. Hofu yake kubwa haikuwa kitanzu tu bali ilimuumiza kutajiwa mara kwa mara jina hilo la Bomba. Ilimuumiza sana kukumbuka kifo cha mtu huyo kilivyotokea na jinsi alivyotoa macho wajati anakata roho. Ilimuumiza zaidi Waridi kukumbuka kuwa dhambi hiyo ya kuua alikuwa ameifanya bure kabisa.
Ni miezi kadhaa tu iliyopita. Wakati huo Waridi alikuwa Waridi wa ukweli. Ua la uhakika ambalo kila nyuki alilitamani, kila kipepeo alilimezea mate. Lakini si wote waliolifikia. Na wachache waliofaulu kuligusa, hawakuwa vipepeo wala nyuki wa kawaida. Walikuwa zaidi.
Uzuri wa msichana huyu ulianza kujitokeza tangu alipokuwa kinda. Alipofikia umri wa miaka mwili tu, kila mtu alibaini kuwa mtoto huyu alikuwa hazina ya uzuri. Alipofika miaka sita watu walianza kunong’ona. Alipohitimu miaka kumi, wanaume wasiokuwa na staha, walianza kumnyatia. Miaka kumi na miwili Waridi alikuwa tayari akiwa kama malkia wa nyuki na kama nilivyosema awali; kwa vipepeo.
Pengine uzuri wake huo ulitokana na ule mchanganyiko maalumu katika umbo lake. Mchanganyiko wa damu za watu weusi, Wahindi, waarabu na Wazungu ambao walishiriki kumtengeneza. Kwani mama yake pia alikuwa mtu wa nipe nikupe. Alifanya biashara yake katika mji wa Mwanza, katika mojawapo ya vibana vibovu, akimkaribisha yeyote mwenye ‘chochote’. Mama huyu hakumfahamu kabisa mtu maalumu aliyeshirikiana naye kumpata Waridi binti yake wa pekee. Alichofahamu ni kuwa, kumpata binti mzuri ambaye watu walianza kumwita Waridi, hata jina lake la awali likasahaulika.
Kwa Waridi hakujua kama alikuwa mzuri kupidukia, lakini alishangaa kuwaona watu wazima kwa vijana wakimfuata na kumtaka kitu ambacho hakukifahamu maana ama umuhimu wake. Kitu kile ambacho alimwona mama yake akikifanya mara kwa mara kitandani.
Kisha akafahamu. Ilikuwa baada ya kukamatwa kwa nguvu na mzee mmoja aliyemtupa sakafuni, akamvua nguo na kumwingilia miguuni kwa namna ambayo ilimtia Waridi maumivu makali yaliyoambatana na faraja.
Waridi akayafahamu hayo, akaifahamu thamani ya uzuri wake, akaanza kuingiwa na kiburi. Akajidekeza na kutupilia mbali masomo. Huyo akamtoroka mama yake na kuingia mjini Tabora,ambapo aliishi kwa faraja kubwa. Daima wanaume walikuwa tayari kumhudumia kwa maneno matamu, malezi, mavazi huku akipewa fedha za kutosha.
Lakini Waridi hakutosheka. Daima alidai hiki na kile kwa wanaome ambao kila mmoja alijitahidi kutoa alichonacho. Lakini baada ya kupata walichohitaji wakamwepuka. Hivyo akauona mji wa Tabora haufai. Akasogea hadi Dodoma ambapo pia hakukaa sana, akapanda hadi Arusha. Mji huo ulipomchoka, akapaa na kushuka Jijini Dar es Salaam.
Ni hapo alipokutana na Bomba Kimara. Kijana huyu mwenye asili ya Kiarabu mtu ambaye Maua alimhitaji. Siku zote alionekana ‘kajaa’, Fedha kwa Bomba hazikuwa na tatizo. Wala hakuna uchungu kuzitumia. Kadhalika, fedha zake hazikuwa mfukoni kama wanaume wengine. Zake zilitoka katika soksi. Kitita cha elfu kumi kumi kikiwa kimefungwa kwa mpira kingewezaje kukaa mfukoni? Walizitumia fedha hizo na Waridi wakishirikiana kuhama baa moja kwenda nyingine, madansa, sinema, mahoteli na kila aina ya starehe.
Walikuwa wakiishi Magomeni Mikumi katika nyumba za msajili wa majumba ambayo Bomba alikuwa amekodi. Ni mara chache sana nyumba hii ilipowaona wapangaji wake, kwani mara nyingi walikuwa kama si Kunduchi Beach, basi wako Kilimanjaro Hoteli au Mbowe Hoteli na sehemu nyingine za starehe wakitumia.
Halafu ikafika ile siku ambayo Bomba alirudi nyumbani mapema kutoka kule alikokuwa akienda mara kwa mara na kurudi na pesa. Safari hii alirudi na mfuko wa ngozi ambao aliutua juu ya kitanda. Alionekana mtu mwenye wasiwasi mwingi kinyume na tabia yake. Hakujua kwa Waridi alikuwa chumbani humo akimtazama.
“Vipi mwenzangu?” Sauti ya Waridi ilimzindua. Akamgeukia akijaribu kutabasamu lakini tabasamu lilikataa.
“Waridi, kwenu ni wapi?” Bomba alihoji ghafla.
Swali hili lilimshangaza sana Waridi. Muda wote walioishi pamoja hawakuwahi kuulizana maswali ya aina hiyo.
‘Kwanini?” Bomba akaendelea. “Nataka urudi kwenu. Mimi naona maisha hayaniendei vizuri”, Bomba akaeleza.
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)