
Mtunzi: Enea Faidy
SEHEMU YA NNE
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Eddy usifanye ivo bhana utamuumiza mwenzio" alisema rafiki mmoja wa Eddy kwani alimuonea huruma sana Dorice.
"Achana nae mpumbavu huyo"
"Lakini kumbuka mlikotoka"
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
TUENDELEE...
"Achana na mimi kama unampenda si umchukue!"
Maneno Yale yaliziidi kumuumiza Dorice, aliinuka pale chini akajifuta vumbi maana bweni lilikuwa na vumbi kupita kiasi.
"Sawa Eddy! Daima kumbuka sio kila king'aacho ni dhahabu... Utanikumbuka!" Alisema Dorice kwa huzuni na kutoka.
"Akukumbuke nani wewe? We boya tu huna lolote" Eddy aliropoka maneno hayo huku akiwashangaza rafiki zake kwani daima hawakujua kama Eddy angemchukia Dorice kiasi kile kutokana na mapenzi yao yalivokuwa.
"Ama kweli watu wanabadilika..!" Alisema rafiki take Eddy na kuondoka zake.
Dorice aliondoka zake mpaka bwenini kwao, akachukua begi lake dogo na kuweka vitu vyake muhimu. Isipokuwa nguo za shule na madaftari, baada ya kupaki vizuri akachukua kanga akaivaa baada ya kutoa nguo kisha akaenda bafuni kuoga.
Alipooga na kujiandaa vizuri alikaa kitandani kwake huku kila Mara akitazama SAA yake ya mkononi ambayo alipewa na Eddy enzi za mapenzi yao. Ilikuwa SAA nzuri ya Dhahabu."Ikifika SAA kumi na mbili jioni lazima nitoroke ... Siwezi kubaki hapa!" Aliwaza Dorice akiwa kitandani kwake.
Muda huchelewa sana pale unapousubiri ndivyo ilivokuwa kwa Dorice. Muda ulichelewa lakini ukafika, kigiza kilipoanza tu akachukua begi lake na kutoka bwenini. Hakuvaa nguo za shule hivyo haikuwa rahisi kugundua kama ni mwanafunzi wa pale. Taratibu akazipiga hatua ili atoroke shuleni pale.
Licha ya kwamba alisumbuliwa na maswali ya wanafunzi wenzake ila hakujali ingawa aliwapa majibu ya uongo yanayoridhisha.
Shule ya mabango ilikuwa imezingirwa na miti mingi hivyo akapita katikati ya miti hiyo ili asioneakane kirahisi. Alipokuwa anaendelea kutembea ghafla akaona kitu mbele yake akashtuka.
********
Jioni ile tulivu Eddy na Doreen walikutana kwenye mti mmoja mzuri na tulivu. Walikuwa wamekumbatiana kimahaba huku wakipeana denda za kutosha.
"Baby nakupenda sana" alisema Eddy
"Nakupenda pia ila..."
"Ila nini mpenzi?"
"Sharti la kuwa na mimi ni kwamba hutuwezi kufanya mapenzi..." Alisema Doreen.
" eh! Kwanini?"
"Tukifanya hivyo kuna kitu kitatokea kwako?"
"Mh Doreen! Mbona sikuelewi, tutaishije kama wapenzi?"
"Nivumilie tu... Ila bado nina bikra"
"Nataka niitoe bikra yako Doreen please!"
" huwezi kufanya mapenzi na mimi, pia kuna sharti lingine mbali na hilo..."
"Bby hapa siwezi kuwa na wewe bila kufanya mapenzi, siwezi! Halafu pia siwezi kukuacha au huniamini?"
Alisema Eddy akiwa amezidiwa na hamu ya mapenzi na ilikuwa kazi ngumu sana kwake kujizuia....
MIPANGO YA MAZISHI kumzika mwalimu John ilikuwa tayari imekamilika, ndugu walikuwa tayari wamewasili kwa majonzi. Huzuni iliwatawala sana kwani mwalimu John alikuwa ndiye tegemezi la familia yote kwa ujumla. Kelele za vilio zilitawala mtaa mzima aliokuwa akiishi mwalimu John, kila MTU alisema lake juu ya msiba ule lakini ukweli haukujulikana.
Make wa mwalimu John alipoteza fahamu kila Mara huku akijutia tendon alilomfanyia mumewe kwa kumpiga na upawa kichwani .Lakini alijiahidi kutomwambia mtu yoyote akihofia kukamatwa kwa kosa la mauaji. Nyuso za watu wote zilitia huruma sana kwa kuondokewa na mwalimu John kipenzi cha watu wengi.
Walimu kutoka shule ya sekondari Mabango walikuwepo pale msibani wakimuaga mwalimu mwenzao.
Jeneza la gharama lilitengenezwa, mwili wa mwalimu John ukawekwa ndani ya jeneza. Make wa mwalimu John alikuwa haamini kama mume wake ndo anapelekwa kuzikwa.. Aliachia yowe Kali lililowashtua wote pale msibani "Rudi mume wangu.. Rudi mpenzi wangu usife..." Alilia mke wa John.
Wazazi wake walikuwa wakigalagala chini kama wehu,hawakujali vumbi lililokuwa limetapakaa ardhini kutokana jua Kali la kiangazi.
Hatimaye Jeneza lililokuwa limebeba mwili wa marehemu John likaingizwa kwenye gari kwaajili ya kupelekwa makaburini huku likisindikizwa na nyimbo za huzuni zinazopigwa misibani. Watu wote wakaelekea makaburini kwani magari ya kutosha yalikuwa yamekodiwa.
Mwalimu John alikuwa ndani ya Jeneza akilia kwa sauti ili Atolewe kwani alikuwa hajafa. Lakini hakuna MTU yeyote aliyesikia kilio cha Mwalimu John wala kuhisi, " Inamaana wananizika mzimamzima?" Alijiuliza mwalimu John huku moyo wake ukiwa umezimia kwa mile akionacho.
"Haiwezekani nizikwe mzima mzima! Hapana" alisema Mwalimu John huku akijaribu kujiinua lakini mwili wake ulikuwa bado mzito kama vile umegandishwa na barafu. Akiwa ndani ya jeneza hilo akasikia kicheko kikali sana kutoka kwa Doreen.
"Doreen nisamehe tafadhali" alijitetea Mwalimu John.
Machozi yalizidi kumtoka kwa kasi sana , ndipo alipokumbuka kosa lake kwa Doreen.
Zilikuwa ni wiki mbili tangu Doreen ahamie shule ya Mabango, kutokana na uzuri na utanashati wa mwalimu John. doreen alivutiwa nae sana hivyo akaamua kumwambia ukweli mwalimu wake kuwa anampenda na anahitaji kuwa naye kimapenzi. Mwalimu John alimtazama binti yule kwa jeuri na dharau kisha akamjibu " We mtoto ni mpumbavu sana! Umezunguka kote huko ukaona uniletee umalaya wako hapa? Mbwa koko wewe hebu niondokee hapa!"
"Mwalimu John hunitaki? Unanitusi? Sasa nitakuonyesha kazi!" Alisema Doreen kwa kujiamini sana kisha akaondoka zake
.
Wakati Mwalimu John akiendelea na kumbukumbu hizo ghafla akahisi jeneza lake linanyanyuliwa Tayari kwa kumuweka kaburini...
*********
Dorice alipokuwa akitembea ghafla akazungukwa na chatu mkubwa sana kila upande. Dorice alishtuka sana, mapigo yake ya moyo yakamwenda kasi sana akiwa haelewi la kufanya.
Kutokana na woga Dorice aliangusha chini mkoba aliokuwa ameubeba lakini ghafla akakumbuka kitu. Akaokota mkoba wake kwa ujasiri sana kama vile hakumjali chatu yule kisha akatamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe. Ghafla bin vuu chatu yule akatoweka kimuujiza, Dorice akaendelea na safari yake.
Alitembea mwendo wa kama dakika tano hatimaye akafanikiwa kuiacha mipaka ya shule, akaingia barabara kuu ya kokoto ambayo ilizingirwa na miti kila upande. Akaendelea kupiga hatua moja baada ya nyingine kuelekea alikokusudia.
Safari ilikuwa ndefu sana na Giza likazidi kuiteka dunia ingawa mbalamwezi ikawa taa kwa msichana yule mwenye kujiamini.
Dorice alitembea taratibu baada ya kuchoka kutokana na mwendo mrefu hatimaye akafika kwenye kijito kidogo kilichotawaliwa na ukimya wa ajabu. Hakukiwa na sauti ya vyura wala wadudu palikuwa kimya mno. Dorice akavuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu sana kisha akaketi pembeni ya kijito kile kimya.
Alikaa karibia robo SAA nzima akiwa ameinamisha kichwa chake ghafla akasikia kishindo kizito ambacho kilimshtua mawazoni.
*********
Eddy aliendelea kumng'ang'aniza Doreen wafanye mapenzi lakini Doreen aliendelea na msimamo wake ule ule kuwa hawezi kufanya mapenzi.
"Doreen tafadhali mpenzi...!"
"Siwezi Eddy!"
"Hapana Doreen, kama ni hivyo niruhusu niwe na msichana mwingine!"
"Kwa hilo usije kuthubutu maana utahatarisha uhai wako?"
" kivipi?"
"Elewa hivo"
Eddy alishtuka kidogo lakini akaachana na mawazo hayo akaendelea kumbembeleza Doreen. Doreen aliendelea kukataa Katakata ingawa nayeye pia alitamani kufanya mapenzi na Eddy ila kuna kitu alikumbuka kikamtia hofu, akazidi kumkatalia.
Uvumilivu ulimshinda kabisa Eddy akajikuta anamtoa Sketi Doreen huku nae akishusha suruali yake. Akambwaga chini Doreen na kutaka kufanya nae mapenzi, kabla hajafanya chochote Eddy aliachia yowe Kali sana....
..VIJANA wanne wenye nguvu walinyanyua jeneza alililokuwamo Mwalimu John kisha taratibu walipiga hatua kuelekea kwenye nyumba yenye pembe NNE na kina kirefu kiasi aliyotengenezewa mwalimu John.
Sauti za vilio zilizidi kutia simanzi katika eneo lile LA makaburini. Nyimbo za huzuni zilitawala eneo hill huku kila mmoja akisikitika moyoni mwake.
Ndani ya jeneza hilo mwalimu John alikuwa akihangaika sana kuwaita vijana wale ili wasimzike lakini katu hakusikika. Alizidi kupiga kelele za kuomba msaada lakini ikabaki kuwa kazi bure. Sauti iliyojaa huzuni kuu ya mkewe Monalisa ilizidi kupenya vyema masikioni mwake, hali hii ilzidi kumtia simanzi mwalimu huyo ambaye sasa alikuwa amekata tamaa ya kuishi tena.
"Daah Doreen hafai" alijisemea mwalimu John huku machozi yakimtiririka kwa kasi kwani bado alikuwa haamini kama kweli anazikwa akiwa mzima.Vijana wale walilishusha jeneza like lenye mapambo ya kupendeza ndani ya kaburi kisha wakatulia kidogo ili mchungaji atupie neno LA mwisho.
Mchungaji alichukua udongo kidogo na kusogelea vyema kwenye shimo alilowekwa mwalimu John."Uliumbwa kwa mavumbi hakika utarudi mavumbini, Bwana alitoa Bwana ametwaa jina LA Bwana lihimidiwe... " Mchungaji aliyasema maneno hayo kwa huzuni kisha akaumwaga kaburini udongo ule aliokuwa ameushika mkononi.
Mwalimu John aliyasikia vyema maneno hayo yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wenye sumu. Hakika mwalimu John alikiri kuwa kweli duniani kuna watu na viatu, Doreen alikuwa kiatu chakavu kisichofaa kuvaliwa hata na kichaa.
Vijana walishika vyema sepetu zao ili waanze kutupa udongo kaburini na kumzika mwalimu John lakini kabla hawajaanza kutupa udongo, kilizuka kimbunga kikali cha ghafla kilichofanya watu wapoteane. Jeneza likafunuka ghafla mwalimu John akainuka kutoka kwenye jeneza.
********
Eddy aliachia yowe Kali sana ambalo lilijirudia Mara kadhaa. Yowe hill lilitokana na maumivu makali sana aliyoyapata kwenye sehemu zake za siri. Maumivu yalikuwa makali sana hivyo alianguka chini na kupoteza fahamu.
Wakati wote huo Doreen alikuwa amebadilika sura na kuwa sura kama sura ya paka. Kucha zilimtoka kama za chui anayekabiliana na hatari. Kichwa chake kilikuwa na mapembe marefu. Hivyo akawa na umbile la kutisha sana ambalo hakuna kiumbe wa kawaida angeweza kustahimili kumtazama hata kwa nusu sekunde.
Licha ya kwamba Doreen alikuwa kwenye umbile lile la kutisha lakini alionekana mnyonge sana. Machozi ya damu yalikuwa yakimshuka taratibu kwenye macho yake. Alimsogelea Eddy na kukaa karibu yake huku akimgusa taratibu mwilini mwake.
"Eddy mpenzi wangu nakupenda sana.. Nisamehe kwa kilichotokea.. Halikuwa kusudio langu hata kidogo, ila umelazimisha... Nakupenda sana na ninakuahidi kukupenda maisha yangu yote...!" Alisikika Doreen akiongea kwa huzuni ila sauti yake ilikuwa ilikuwa nzito ya kutisha iliyoambatana na mwangwi mkali.
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)