BARUA KUTOKA JELA (11)

Zephiline F Ezekiel
0
Mtunzi: Ibrahim Gama

SEHEMU YA KUMI NA MOJA
ILIPOISHIA...
Kwani aliikumbuka kauli ya Bwana Masudi, yule jirani yake Mwaduga, alipomwambia kuwa.

“Nilimsikia akiongea kwa kithethe, tunatho Elfu tatu tupeleke kwa macheni”

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

ENDELEA...
Leo akiwa na Dokta Masawe anamsikia jamaa akiongea kwa kithethe, na hata wasifu wake alioambiwa na Masudi, hakika unashabihiana nae.

Huyu bwana ni katika wale watu wawili, ambao Inspekta Jamila, hakuweza kuwatambua awali.

Inspekta Jamila Pia akafikiri kuwa, wale jamaa huenda ikawa ndiyo waliopanda Taxi ya Mwaduga pale katika barabara ya Namnani! Hapo mapigo ya moyo yakazidi kumuenda mbio, huku damu ikimchemka!.

Inspekta Jamila aliinua simu yake juu kuelekea kwa yule Jamaa wa Kithethe huku akiwa anacheka hadi jino la mwisho linaonekana,huku akiendelea kuchezea simu akamwambia yule bwana kithethe.

“Huo wivu sasa unaouleta, kama unaona Dokta anafaidi basi njoo na wewe ukae!”

Hatimae kwa jibu lile wote watatu wakaangua kicheko.

Dokta Masawe alimjibu yule bwana; “Nakuja sasa hivi kwani namalizia malizia maongezi ya mwishomwisho!”

Na yule jamaa akamwambia, “Mimi thikuonei wivu, ila ulithema kuna thehemu unatakiwa thaa nane, na hivi thatha ni thaa thaba na nuthu”

Baada ya kusema hayo mzee wa kithethe akarudi kwa wenzie kwenda kuendelea na makulaji!

Dokta Masawe na Inspekta Jamila wakakubaliana kesho jumanne baada yakutoka Muhimbili katika “Clinic” yake wakutane maeneo ya Ilala Amana, ili waongozane hadi nyumbani kwake Inspekta Jamila, ambaye Dokta Masawe alimtambua kwa jina la Jenipha, ili akatoe huduma kwa mgonjwa.

Baada ya kuafikiana, Dokta Masawe, aliondoka katika meza ile, na kurudi katika meza ya maswahiba zake.

Inspekta Jamila akifurahia kuwa mtego wake umenasa vizuri na hasa umekuwa ni MTEGO WA PANYA kwani huingia aliyekuwepo na asiyekuwepo! Au labda niseme ilikuwa jiwe moja kwa ndege watatu!

Inspekta Jamila akaendelea kunywa kinywaji chake cha ofa baada ya kile alichoagiza kwa pesa yake kukimaliza.

Huku macho yake yakiwaangalia wale jamaa waliokuja na Dokta Masawe, mara akamuona Dokta Masawe ameinuka na kuagana na jamaa zake kisha akatoka nje ya hoteli na kutokomea kusikojulikana.

Inspekta Jamila alingoja kama kiasi cha dakika tatu toka kuondoka kwa Dokta Masawe, aliinuka katika kiti alichokalia na kwenda chooni huku akipita Karibu kabisa na meza ya wale jamaa, kisha ule mkono uliokuwa umeshika simu yake, akawanyooshea mkono na kuwapungia akiwapa salamu, huku nao wote wakiwa wanamtazama na walimuitikia salamu yake huku wakiwa wamepigwa na ganzi kwa mshangao! Wakistaajabia urembo wake.

Geradi Mwaipopo alikuwa yupo tofauti na wenzake, kwani yeye aliitazama ile simu ya Inspekta Jamila, kisha akamkazia macho ya udadisi mkuu!

Inspekta jamila, yeye akapitiliza moja kwa moja hadi katika vyoo vya wanawake na kuingia chooni.

Ilimchukua kama dakika tatu hivi akiwa kule chooni, alipotoka nusura aanguke kwa mshangao, kwani sehemu waliokuwa wamekaa kina Jeradi Mwaipopo, sasa ilikuwa na viti vitupu!

wale jamaa walishatoka eneo lile.

Inspekta Jamila alimuona yule muhudumu wa kike akiondosha chupa zilizokuwa zimezagaa kwenye meza ile!

Inspekta Jamila kwa mwendo wa haraka alitoka nje ili awawahi watu wale, na hatimae awafatilie kusudi iwe rahisi kuwatia mkononi mwa Sheria.

Alipotoka nje akaiona gari moja aina ya Toyota Mark II nyeupe ikiingia barabarani kuelekea maeneo ya Kagera ikiwa inatoka katika sehemu ile ya hotel!

Kitendo bila kuchelewa, Inspekta Jamila aliwahi kwenye gari yake ili awafatilie wale wahalifu, lakini alipofika usawa wa gari yake, ilibidi akae chini kwa jinsi alivyochoshwa!

Tairi la mbele upande wa dereva wa gari yake lilikuwa limelala chini lina pancha!

“Nooo! Haiwezekani.”

Hatimaye Inspekta Jamila, alipata nguvu na kutoa kauli.

Inspekta Jamila, alikuwa hakubaliani na hali aliyoiona katika gari yake.

Tairi za gari yake, zilikuwa mpya kabisa, tena ni TUBE LESS hivyo hata kama angekuwa amekanyaga msumari tairi lisingelala mapema kiasi kile!

Akiwa pale chini kwenye kikuta akiwa amekaa, aliishuhudia ile gari ikipotea machoni mwake,huku naye akiwa amekata tamaa!

Mara walitokea jamaa wawili waliokuwa wanaosha magari katika eneo lile, wakamwambia Inspekta Jamila.

“Vipi sister unayo jeki na spana tuchakarike chap chap?”

Inspekta Jamila akawaangalia wale jamaa na kuridhika kwamba siyo watu wabaya, akapatana nao bei ili wambadilishie tairi wamuwekee tairi la akiba.

Inspekta Jamila akainuka pale alipokuwa na kuuendea mlango wa gari yake, ili afungue apate kutoa jeki na spana yakufungulia tairi, akasikia sauti kutoka kwa wale jamaa ikimwambia.

“Tulia hivyo hivyo Inspekta Jamila! Kwani kujaribu kubisha ni sawa kabisa na kusaini kifo!”

-

Mmoja kati ya wale jamaa wawili alimwambia Inspekta

Jamila huku mkononi akiwa ameshikilia Bastola aina ya

Chinise.

Inspekta Jamila alisikia maneno yale yakimuingia hadi kwenye damu,huku akiwa amemuelekezea mgongo yule jamaa anaemuamrisha maneno yale.

Inspekta Jamila alitaka kugeuka,lakini jamaa aliikoki ile bastola huku akimwambia.

“Stop!Mkononi kwangu nina silaha ya moto,na ndani yake

kuna risasi nane hivyo sitosita kuitumia kama tu utaleta ukaidi.sikiliza ujumbe wangu kwa makini,na nitakuacha huru uendelee kupumua!Kwani maisha yako nimeyashika

yapo mkononi mwangu!”

Wakati jamaa mmoja amemtuliza Inspekta Jamila,yule mwengine alitoka mbio akaingia katika gari iliyokuwa

imeegeshwa jirani kabisa na gari ya Inspekta Jamila

akaiwasha na kuiweka mkao wa kutoka!

“Elekea kwenye hiyo gari na upande,kisha nikupe ujumbe

wangu huku gari ikiwa inatembea,nikishamaliza kukupa ujumbe wangu na ukaukubali nitakuacha huru na hai,ila kama utaendelea kukaidi kama tulivyokuagiza katika waraka mfupi kule Muhimbili,nitayakatiza maisha yako Inspekta!”

Moyo wa Inspekta Jamila ukapiga Pah huku ukimuenda

mbio!

Alichofanya nikuelekea katika ile gari huku damu ikimchemka,na jamaa akimfatilia kwa Karibu nyuma yake.

Alipofika katika mlango wa ile gari,aliangalia mle ndani ya gari nakumuona mtu mmoja tu aliekaa nyuma ya usukani ambae ni yule jamaa aliejifanya muosha magari,gari waliyokuwa wanaiosha ndiyo iliyofunguliwa mlango ili aingie!

Hapo kulitokea kitu mbacho hakuna aliekitegemea katika

wale jamaa.Inspekta Jamila aliinama kama anaetaka

kupanda ile gari,na yule jamaa aliemshikia bastola nyuma yake, akasogea Karibu zaidi ili aingie pamoja nae.

Inspekta Jamila kwa wepesi wa ajabu alirusha teke aina ya OSHIRO na kuipangusa ile bastola mikononi mwa yule

jamaa,na ile bastola iliruka juu!{OSHIRO,ni teke la kisigino linalopigwa kwa kuzunguka ukiwa umempa adui mgongo.}

Yule jamaa akiwa amefadhaishwa kwa kitendo kile,akaruka juu ili aidake ile bastola.

Na hilo lilikuwa ni kosa la mwaka kwake,Inspekta Jamila alirusha teke lingine,safari hii akipiga teke aina ya

MAIGERI na kumpata yuje jamaa katika kifua usawa wa

chembe,na yule jamaa akatupwa nyuma kama gunia

nakuanguka kwa kishindo akidondokea kisogo!

{MAIGERI,ni teke linalopigwa kwa unyayo wa chini ya

vidole vya mguu ukiwa unatazamana na adui}

Inspekta jamila kwa kasi ya ajabu, aliitoa bastola yake

mgongoni kwa mkono wake wa kushoto,na kuikoki wakati

huohuo akiidaka ile bastola ya yule baradhuli kwa mkono

wake wa kulia, akawa na bastola mbili mikononi mwake!

Inspekta Jamila aliichanua mikono yake ikawa kila mtu

katika wale jamaa wawili anatazamana na mdomo wa

bastola.

Moja akiielekeza magharibi, na nyingine upande wa

mashariki kwa namna walivyokaa wale watekaji wake!

Yule jamaa aliekuwa ndani ya gari, alipoona mambo

yamegeuka akakanyaga mafuta kwa nguvu, na gari ile aina ya Toyota Chesser Automatic yenye Silinda sita, iliondoka kasi huku ikichimba eneo lile ikiwacha vumbi la hali ya juu!

Inspekta Jamila sasa kwa mikono miwili ambayo

imekamata bastola mbili,alijitupa chini kama Mkizi akilala kifudifudi huku akizielekeza zile bastola kule kwenye ile gari na kufyatua risasi mfululizo zilizopiga kwenye tairi za gari ile, na akaishuhudia gari ile ikiruka juu na kupinduka juu chini! Huku ikiwa imeshaingia katika barabara ya morogoro ikawa Boneti la gari ile ikipanda kikuta kinachotenganisha barabara,na Buti lake likiwa barabarani

huku Magurudumu yake yakizunguka hali ya kuwa yapo juu!

Kilichofatia ni mtafaruku na fadhaa ya hali ya juu kwa

wakazi wa maeneo yale,kwani watu walikuwa wanakimbia hovyo huku wakipiga kelele,pia wapo waliokuwa wanakimbilia ili waone kilichotokea.

Inspekta Jamila akamgeukia yule jamaa pale chini,akapiga

goti na kumuelekezea zile bastola mbili zilizokuwa

mikononi mwake, akamuona yule jamaa anakohoa damu

tena mfululizo.

Inspekta Jamila akaingiza mkono katika mkoba wake

uliokuwa unaning’inia begani muda ule,akatoa simu yake

na kubonyeza tarakimu kadhaa kisha baada ya kupokelewa simu ile alisema.

“Specil order nipo manzese Aljentina hapa,Friends corner

hotel ongeza nguvu tafadhali,kuna wahalifu nimepambana

nao.”

Baada yakusema yale akakata simu na kumsogelea yule jamaa pale chini, huku watu wakiwa wamejaa eneo lile,akairudisha simu yake katika mkoba wake kisha akaitoa risasi iliyokuwa Chemba tayari kwa kufyatuka kutoka katika bastola ya yule jambazi pale chini pamoja na magazine yake,akaitumbukiza katika mkoba wake.

Akabakiwa na bastola moja tu sasa akamnyooshea yule

mtekaji wake na kumwambia.

“Safari yetu ya pamoja bado ipo! Ila itabidi tusubiri gari

nyingine,kwani yangu ina pancha na ile yenu imepinduka!”

Kiasi cha dakika tano baadae Gari aina ya Land Rover 110

Difender mbili za polisi,huku mitutu ikiwa mikononi

ziliwasili eneo lile,na tafrani ikaanza upya kwani watu

walikuwa wanakimbia hovyo eneo lote likajaa hekaheka

tupu.

Inspekta Jamila akatoa maelekezo kwa wale askari wa Doria Kenda,na mara moja yule jambazi alisombwa msobemsobe akarushwa ndani ya ile gari ya polisi huku afande mwingine akishughulikia kubadilisha tairi katika

gari ya Inspekta Jamila.

Kule katika Barabara ya Morogoro,askari wa usalama

barabarani walikuwa wanayaongoza magari kupita,huku simu za upepo zao zikiwa zinawasaidia kuwasiliana na watu wa ‘Break Down’ ili kuja kuiondosha ile gari iliyopata

ajali.

Yule jambazi alietaka kutoroka na gari,baada yakuona wamedhibitiwa, alikuwa anatolewa chini ya uangalizi wa askari polisi, kwani alikuwa amenaswa na usukani wa gari ile.

Inspekta Jamila akamuendea yule Jambazi aliepambana nae pale alipolala ndani ya gari ya polisi na kumwambia.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

 Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Shawishi Wapenzi wa Simulizi Wapakue(Install) App ya CnZ Media

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)