
Mtunzi: Ibrahim Gama
SEHEMU YA KUMI NA NNE
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Wakati Afande Kubuta alikuwa anaendesha gari, Inpekta Jamila alikuwa anamchunga Dokta Masawe aliyekaa naye katika kiti cha nyuma ya gari ile, huku akiiperuzi simu ya Dokta Masawe.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
ENDELEA...
Katika kupekua pekua kwake, akakutana na ujumbe uliomsisimua.
Ujumbe huo ulikuwa unasomeka hivi;
“Dokta kuwa makini na yule dada uliyekuwa unaongea naye pale friends corner Hotel, kaa naye mbali kwani yule dada ni shushushu. Hivyo kwa taarifa kamili tutaongea hiyo kesho saa tisa kama tulivyopanga tukikutana pale Baracuda, nikuandikiapo ujumbe huu tayari ameshawamaliza Juja na mwenzake Mwaky, hivyo kuwa makini sana hakikisha leo hulali nyumbani kwako”!
Inspekta Jamila alipoangalia namba iliyotuma ujumbe ule na muda, aliona jina lililotuma ujumbe ule limeandikwa MWAIPOPO.
Na ametuma ujumbe ule jana saa moja usiku.
Inspekta Jamila akamuuliza, Dokta Masawe, wakati huo gari yao ikiwa katika eneo la Sanene kule Tabata Segera wakirudi mjini.
“Huyu Mwaipopo ni yule Geradi Mwaipopo uliyekuwa naye jana mchana pale Friends Corner Hotel?”
Dokta Masawe hakujibu kitu alikaa kimya. Inspekta Jamila akamwambia.
“Bado muda wako Dokta Masawe, bali muda ukifika utatueleza kila kitu na wewe mwenyewe utatupeleka kwa hao jamaa zako.”
Inspekta Jamila alizungumza kwa hasira, huku aiuma meno yake, na uendelea kumsimanga Dokta Masawe.
“Daktari kama wewe serikali inakuamini, lakini wewe umeshindwa kuibeba amana, yani wala huelekei kwani unalipwa pesa nyingi sana kwa kwenda kwako kazini siku ya Jumanne na Alhamisi, Yaani siku saba za wiki wewe unakwenda kazini siku mbili na bado una Zahanati yako bila shaka hata wale wagonjwa unawahamisha kutoka katika hospitali ya serikali na kuwapeleka katika Zahanati yako, kwa tamaa iliyokujaa ya pesa. Ukisikia Wachaga kwa kutafuta pesa wanaongoza, basi ndio utafute hata pesa za roho za watu?!”
Afande Kubuta aliendesha gari,na sasa alikuwa yupo katika maeneo ya Tabata Sigara wakienda ofisini kwao. Nusu saa baadae wakawa wanaingia katika jengo la Wizara ya mambo ya ndani ya nchi.
Dokta Masawe akatelemshwa ndani ya gari ile, wakaingia nae ofisini wao.
Walipofika ndani ya ofisi, Inspekta Jamila aliangalia saa ya ukutani iliyokuwa ofisini mle, nakuona ilishatimu saa saba na nusu za mchana, alitoa simu yake katika mfuko wa suruali aliyovaa ya kitambaa cha suti iliyomkaa vyema, ikimbana sehemu ya mapajani na kuonyesha hipsi zilivyotokeza, na makalio yalivyotuna kwa nyuma, na chini suruali ile ilimwaga katika mtindo wa Bwanga huku miguuni akiwa amevaa viatu vya ngozi vya kutumbukiza.
Alibonyeza namba kadhaa na baada ya muda simu ya upande wa pili ikawa hewani,na Inspekta Jamila akatoa maelekezo.
“Nendeni mkatege katika eneo la Baracuda Baa, pale katika kona yakwendea Tabata Chang’ombe na Vingunguti machinjion. Kwani mnamo majira ya saa tisa, yule mualifu tunaemtafuta, Jeradi Mwaipopo atakuwa maeneo yale.”
Baada yakuongea maneno yale akakata simu.
“Hivi mnanikamata kwa kosa gani, mpaka mnanidhalilisha kiasi hiki?!”
“Dokta Masawe unajuwa tulilokukamatia, na kitu tunachotaka kutoka kwako”
Inspekta Jamila alimjibu Dokta Masawe alieanza kupata sauti baada ya kusikia na mwenzake akiwindwa!
“Sawa lakini huna ushahidi wowote kama mimi na wewe tuliwahi kupanga mpango wowote, lakini pia sijashiriki jambo lolote baya na wewe ukalishuhudia, basi kama hivyo ndivyo kosa langu lipo wapi?”
Dokta Masawe alijaribu kujitetea, na Inspekta Jamila hakumjibu kwa mdomo, alichofanya aliivua Flash Disc yake kutoka shingoni alipokuwa ameivaa, nakuipachika katika sehemu yake katika Computer iliyokuwa mle ndani ya ofisi,na kuifungua.
Baada ya sekunde zisizozidi ishirini, Computer ile ikaifungua ile Flash Disc na kuisoma.
picha za Video zenye sauti zikawa zinaonekana!
Dokta Masawe akajishuhudia toka alipokuwa anainuka katika meza aliyokuwa amekaa na wenzake hadi alipofika katika meza ya Inspekta Jamila.
Ngoma haikuishia hapo! Alionekana mzee wa kithethe alipoyaingilia maongezi yao, picha zikamalizia kwa wale jamaa zake waliokuwa wamekaa nae awali akiwemo Geradi Mwaipopo!
Ama kwa picha zile Dokta Masawe alifadhaika sana, kiasi alipoteza matumaini kabisa yakunusurika na kifungo pindi ushahidi ule ukifikishwa mahakamani, kwani atakuwa hana la maana atakalojitetea kwalo!
“Ndugu zangu naomba tuyamalize maswala haya hapahapa yasifike mbele!”
Dokta Masawe alianzisha mazungumzo yakupelekea kutoa hongo.
Afande Kubuta alitaka kusema neno, Inspekta Jamila alimzuia kwa ishara ya mkono kisha akamuuliza Dokta Masawe.
“Unataka tuyamalizeje sema tunakusikiliza”
“Mimi nipo tayari kutoa kiasi chochote cha pesa ili mambo haya yaishie hapahapa”
Dokta Masawe alikuwa anatafuta MLISI! Inspekta Jamila akamwambia.
“Sisi tupo tayari kukuachia bila ya kuchukua hata senti tano yako, lakini tunataka utupe ushirikiano ututajie wale wahusika wenzio majina yao na wanapokaa, lakini pia unafahamu nini kuhusu kifo cha Marehemu Bartazal na mkewe Hamida.ukitwambia hayo kwa ufasaha tutakuachia, kinyume na hivyo wewe utaozea jela uwaache wenzio walioshirikiana na wewe wawe wanapeta mitaani kwa kunywa Lager!”
Maneno yale yalimchoma sana Dokta Masawe na kwa kweli hakuwa tayari kwenda jela, hivyo akajikuta katika wakati mgumu, hatimae akaanza kutapika mambo ambayo Inspekta Jamila na Afande Kubuta yaliwaacha midomo wazi!
Dokta Masawe alianza kwa kusema.
“Mimi na Bwana Bartazal tulifahamiana kiasi miaka mitatu iliyopita, mara ya kwanza kuonana na Bwana Bartazal, ilikuwa pale kazini kwangu Muhimbili alipokuja kutibiwa mguu baada ya kuvunjika katika ajali ya gari. Nilipomfanyia upasuaji na kumuunga mguu wake alianza kuwa Karibu na mimi, kiasi yeye na mkewe walikuwa wakija katika Zahanati yangu mara kwa mara, Bwana Bartazal akiwa na hamu sana ya mtoto na mkewe alikuwa haonyeshi dalili ya ujauzito!
Bwana Bartazal siku moja akasema nikiwa mimi na yeye na mkewe. Dokta Masawe kama mke wangu akijaaliwa kupata ujauzito, mali zangu zote nitamuandikisha yeye! Kwani yeye ndiyo mimi na mimi ndiyo yeye pamoja na mtoto wetu mtarajiwa, kwani mimi binaadamu sina uhakika na mwisho wa maisha yangu, hivyo nachelea nisije kufa kisha mtoto na mke wangu wakaja kunyang’anywa mali na ndugu zangu, kama baadhi ya Jamii nyingine za Watanzania zinavyofanya!”
Dokta Masawe alisimama kidogo, kisha akaendelea.
“Baada ya kuniambia maneno yale, miezi miwili baadae Hamida alinijia peke yake akaniambia kwamba, nina mpango wangu nakuomba sana utilie baraka zako, kwani mume wangu wewe anakuamini sana, hivyo chochote utakacho mwambia wewe atakikubali! Mimi kuanzia sasa naweza kuachika katika ndoa, kwa sababu mume wangu anataka mtoto, na mimi sina uwezo wa kuzaa’ kwani nilipokuwa shuleni nilipewa mimba na mwalimu wangu wa darasa, kisha akanipeleka kwa Daktari mmoja rafiki yake akanitoa mimba ile! Kumbe alinitoa vibaya akasababisha mfuko wa uzazi kuuharibu! Hivyo hata ningekutana na wanaume wa dunia nzima, Hamida mimi siwezi kupata ujauzito! Chondechonde nakuomba nistili na ndoa yangu.”
Kama kulikuwa kuna mtu katika wakati ule alikuwa na huzuni na uchungu, basi alikuwa ni Inspekta Jamila.
Kwani alikamatika kusikiliza mkasa ule kwa shauku kubwa. Na Dokta Masawe akaendelea kusimulia mkasa ule mzito.
“Mimi nikamuuliza nawezaje kukusaia na kuiokoa ndoa yako?! Yeye akanambia, mimi nataka kujidanganya kuwa ninahisi mimba, hivyo kwa vyovyote vile mume wangu atanileta kwako ili uje kunithibitisha kama kweli nimenasa! Sasa ikitokezea tukaja kwako, usifanye makosa, nithibitishe kuwa ninayo mimba tena ya mtoto wa kiume!
Aliponiambia maneno hayo, nikamwambia itakuwa ngumu sana kufanya hivyo, kwanza itaniharibia CV yangu, lakini pia mumeo akishajua kwamba huna mimba bali ulikuwa ukimuongopea si ndipo utakapoachika? Akasema laa, yeye hatofika huko mpaka kujua kuwa anamuongopea, kwani atakapo mwambia kuwa ana mimba na mimi nikaithibitisha, Mumewe atamuandikisha mali zake zote!
Nae baada yakuandikishwa mali hizo, haitochukua muda mrefu atamuua mumewe, ili Dili lake lisibumbuluke!”
Alipofika hapa Inspekta Jamila alianza kumchukia Marehemu Hamida, nakumuona kuwa yeye ndiyo chanzo cha mambo yote haya kwa tamaa zake!
“Ehee baada ya hapo nini kikaendelea?”
Inspekta Jamila akamuimiza Dokta Masawe ili aendelee kwani alitaka kujua hatima ya jambo lile lilivyokuwa.
“Mimi nilikataa katakata, kwani sikuiona faida nitakayoipata katika jambo lile zaidi ya dhambi. Lakini Hamida alinihakikishia kuwa, kama nitakubali kushirikiana nae katika mpango wake huo, atanigawia Robo ya mali yake yote atakayoandikishiwa na mumewe! Nami Shetani akanitawala, nikashawishika nikajikuta nashiriki katika mpango huo!”
Dokta Masawe alizungumza huku machozi yakimtoka, akionyesha kujutia kitendo kile, lakini wapi Maji yakisha mwagika hayazoleki.
Dokta Masawe alifuta machozi kisha akaendelea.
“Nilipomkubalia alinipiga busu zito, akaniachia na pesa shilingi Elfu hamsini tasilimu, akaniaga nakutoka. Baada ya kama wiki tatu baadae Hamida alikuja na mumewe ili kuja kupima ujauzito, nami nikajua mchezo umeshaanza! Nilimchukua vipimo vya damu ya mshipa pamoja na mkojo wake nikajifungia navyo maabara, nilipotoka nilimpa Hongera Bwana Bartazal na atarajie mtoto wa kiume!
Kwa kweli Bwana Bartazal alionyesha furaha isiyo kifani, kwani alimkumbatia mkewe na kumbusu mbele yangu, huku akiniambia, Dokta niliwahi kuahidi mbele yako kuwa mke wangu akipata ujauzito, nitamuandikisha mali zangu zote, kwa kuwa hili limetimia, basi na mimi sina budi ila kutimiza ahadi yangu kwani Ahadi ni deni!”
“Bwana Bartazal alimuandikisha mali zake zote mkewe.
Ilipofika miezi mitatu Hamida akanijia nakuniambia, sasa umefika wakati wakupata Robo ya mali yangu, kama tulivyokubaliana, na ili jambo hilo litimie, bado juhudi zangu zinahitajika!
Nazo nikumpa mbinu ya kumuuwa mume wake mpendwa Bwana Bartazal Halim.
Nikifanikisha hilo, muda si mrefu nitafungua Hospitali kabisa, badala ya Zahanati! Nami kwa kuwa Shetani alikuwa anatawala mbele yangu, nikampa vidonge vya SALBUTAMOL kumi ili amtilie kwenye Juice. Nakweli Hamida alivichukua vidonge vile nakumtilia mumewe vyote kwenye Juice kama nilivyomuagiza, na mara yule bwana alipokunywa Juice ile, saa moja baadae akawa marehemu Baltazar!”
Inspekta Jamila na Afande Kubuta walikuwa wanatingisha vichwa kwa huzuni ,wakimsikitikia marehemu Bartazal kwani niya yake njema, imemtoa roho yake
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Shawishi Wapenzi wa Simulizi Wapakue(Install) App ya CnZ Media