
Mtunzi: Ibrahim Gama
SEHEMU YA KUMI NA HAPA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Alikuwa katika chumba kikubwa, ambacho hakikuwa na kitu chochote zaidi ya kile kiti cha chuma, alichofungwa nacho!
“Nimekuelewa bothi, thithi tunamalidha kabitha.” Yule bwana anaezungumza kwa kithethe, alihitimisha mazungumzo yake, akakata simu.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
ENDELEA...
Akapiga hatua kubwa mbele, akamnyooshea bastola aliyokuwa ameishika mkono wake wa kulia, huku akitumbukiza simu yake mfukoni kwa mkono wake wa kushoto.
Inspekta Jamila, akawa anaswali kimoyomoyo, kumuomba mungu wake, amnusuru na mkono ule wa mauti, wa madhalimu wale, akawatazama wale jamaa wengine wawili, akawaona wote kwa pamoja, wanampungia mkono wa kwaheri! Aligeuza shingo yake, upande ili asiwaone wale jamaa wanaomdhihaki, macho yake yakatazama upande wa kulia, akauona mlango.
Akiwa katika kuutizama ule mlango,mara akasikia Yule jamaa wa kithethe, akiipandisha risasi kutoka katika megazin yake, na kuipeleka chemba tayari kwa kuiruhusu itoke, ili kufanya kazi aliyoikusudia!
Inspekta Jamila, aliuona ule mlango, kitasa chake, kikiwa kinashuka chini! Akafumba macho huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.
Milio ya risasi, ilisikika ikihanikiza katika chumba kile kwa sekunde kadhaa, kisha ukimya ukatawala mle ndani, huku damu zikisambaa kwa wingi, kiasi khaswa unaweza kusema, kile kilikuwa chumba cha mauti!
Inspekta Jamila, alifumbua macho yake,akamuona mtu aliekuwa amevaa mask katika uso wake, akimfungua kamba ambazo sasa zilikuwa zinamuumiza mwilini mwake.
Akatizama pale chini, akawaona Kithethe akiwa na bastola mkononi, na wenzie wale wawili, wakiwa wamelala chini damu zikiwatoka kwa wingi mwilini mwao, wakiwa wamesambaratisha mikono na miguu, hawana dalili ya uhai!
Baada ya kufunguliwa kamba, Inspekta Jamila akasimama huku akimshukuru mungu, pia akawa anajinyoosha viungo vyake.
Hamadi?! Inspekta Jamila, alipigwa kibao cha kelbu katika shavu lake, akahisi maumivu makubwa!(KIBAO CHA KELBU, NI MKONO UNAOPIGIWA NYUMA YA KIGANJA)
Alipokuja kurudisha uso wake, akamuona yule mtu aliemfungua kamba,ambae ndiye aliyempiga, akiivua ile mask usoni mwake, huku akiwa amempa mgongo Inspekta Jamila,na yule bwana alipogeuka, Inspekta Jamila, akawa anatazamana uso kwa uso na Jeradi Mwaipopo au kifupi JM!
Inspekta Jamila, alitaharuki kupita maelezo, kasha kwa fadhaa akajikuta akitamka “JM?!”
“Yes, my name!” Jeradi Mwaipopo aliitikia kidharau, huku akimtizama usoni bila kupepesa macho! Kisha akaendelea “Bila shaka leo tumekutana, Inspeka Jamila”
-
“Naam hakika,leo tumekutana,tena tukiwa wawili,bila shaka leo,utaweza kunieleza kwa nini upo upande huu!”
Inspekta Jamila,alimwambia Jeradi Mwaipopo,huku akiwa
anachua shavu lake!
“Unajua leo ulikuwa tayari ni marehemu?Je ungewezaje
kujua kwa nini nipo upande huu?!”
JM alimwambia Inspekta Jamila,huku akiwa anamtazama
usoni moja kwa moja!
“Sina ubishi juu ya hilo,kuwa mungu angetaka,leo ningekuwa marehemu,ila naona ameniokoa na kifo kile
cha udhalili,kupitia mikononi mwako JM!”
Inspekta Jamila,alimjibu JM,katika namna ya kuvuta
muda,lakini pia kukusanya nguvu.
“Afande mimi,sijakuokoa na kifo,ila nimetaka mimi,ndiyo
nikuuwe,na siyo hao marehemu wenzako,waliyokutangulia!”
JM,alikuwa akisema maneno hayo huku,kwa mkono ule
uliokuwa umeshika silaha,akiinyooshea miili ya marehemu wale watatu,ambao sasa damu zilizokuwa zikiwamwagika,sasa zilianza kuganda!
Inspekta Jamila,alimtizama JM, usoni mwake, akagundua
kuwa hakika alikuwa hatanii hata kidogo!
“Sasa JM,hata kama utaniuwa mimi,bado na wewe
utakufa vilevile,ama utauwawa!”
Inspekta Jamila,alikuwa akimsemesha JM,ili kupoteza
muda,asaakheri huwenda akapata namna ya kujinusuru,kutoka katika mikono ya mtu mbaya kabisa alieacha zahma kubwa,katika mwenendo wa kesi ile.
“Mimi sitojali,kama nitakufa,ila nakuhakikishia umeingia
kwenye mtego wa panya,na leo umenasa kisawasawa!”
JM muda wote alikuwa akimtazama usoni,Inspekta
Jamila,kumsoma mawazo yake bila shaka.
“Sasa JM,si vibaya ukanieleza walau kwa ufupi,sababu khaswa zilizokupelekea,wewe kugeuka na kuwa upande
mwengine?!”
Inspekta Jamila alisema maneno haya,huku akionesha
utiifu,mkubwa kwa JM aliekuwa ameshikilia silaha ya moto kwa ujasiri mkubwa.
“Afande sina muda wa kupoteza hapa,naona unanikawiza kufanya azma yangu,lakini nitakwambia ili ukawaeleze huko kuzimu!”
JM alisema maneno hayo,kisha akamwemwesa kidogo,akaendelea.
“Kama nilivyokwisha kusema,katika Jeshi la Polisi,kuna baadhi ya viongozi,wameligeuza jeshi hili,kuwa kama mali yao binafsi.
Kwani wapo watu wanalitumikia jeshi,kwa miaka na miaka,lakini hawapandishwi vyeo!
Lakini pia wapo watu wanalipwa mishahara mikubwa kuliko watendaji halisi wa kazi husika!
Hao baadhi ya viongozi,wamekuwa wakijihusisha na
mambo haramu,na mimi nilipokamata,nikaambiwa
naingilia miradi ya watu!
Mwisho nikafanyiwa zengwe,nakusingiziwa kuwa
najihusisha na uhalifu,na nikafukuzwa jeshi,na leo hii,familia yangu nimeirudisha nyumbani Mbeya,ikiwa
hohehahe!”
JM aliposema maneno hayo,huzuni,hasira na dukuduku
lilimjaa moyoni mwake,akajikuta akilia kwa uchungu huku akisema.
“Nachukia kazi ya Polisi,na nawachukia Polisi,kwani hao
ndiyo walionifikisha hapa leo, wao ndiyo waliotoa picha
yangu katika magazeti,nakuniharibia,hadi nimekuwa
siwezi kupata ajira mahala popote ndani ya nchi hii,nikikomeshwa na wakubwa,wanaojali masilahi yao
binafsi,wao na familia zao,wakati wakina JM,wakitaabika kwa kuwa tu,walikuwa wakitekeleza majukumu yao sawasawa!”
Jeradi Mwaipopo alikuwa akitafuna meno yake kwa hasira,na mara akainua mkono wake uliokuwa umeshika silaha,akamuelekezea Inspekta Jamila,ili kutimiza dhamira yake ya kuua!
“No JM. Wewe mtoto wa kiume,hivyo hupaswi kumuua
mwanamke kwa risasi,tumia mikono yako bwana,unakuwa dhaifu mbona?!”
Inpekta Jamila,alikuwa akimpandisha jazba JM,lakini pia akimshusha,ili tu asiweze kuuliwa na risasi.
“Kwa hiyo wewe unataka kupigana na mimi siyo?!”
JM alimuuliza Inspekta Jamila kwa dharau ya hali ya juu!
“Bila shaka JM,kwani mimi sina silaha yoyote mwilini
mwangu,kwa nini wewe utumie silaha?! Kama kweli
unajiamini, na unajiona ni mwanaume hasa, tupa silaha
chini, tupange mtu mbili mimi na wewe!”
Inspekta Jamila,alikuwa akimtia hasira JM,ili ahamaki,na hatimae atupe silaha chini.
Naam bila wasiwasi,JM aliinama na kuiweka silaha yake chini,akawa amempa ubabu Inspekta Jamila,na
aliposimama juu huku akiwa bado yupo ubavu,JM alirusha
teke aina ya YOKO GELI,likatua ubavuni mwa Inspekta Jamila,na kumfanya apepesuke nusura adondoke chini.
(YOKO GELI.NI TEKE LAKUSITUKIZA,LINALOPIGWA UBAVU,ADUI ANAPOKUWA AMEKAA UBAVUNI MWAKO!) Inspekta
Jamila alipata maumivu kwenye mbavu zake,lau kama si kubana pumzi alipopigwa teke lile,bila shaka angevunja mbavu zake.
Baada ya kukaa sawa,akawa anatazamana uso kwa uso na JM.Ispekta Jamila akagundua kuwa mtu anaepambana nae,siyo mtu wa mchezo hata kidogo.
Hivyo alikaa katika mkao wa kupambana na mjuzi mwezie.
JM alipomuona Inspekta Jamila,amekunja ngumi huku
mguu mmoja,akiwa ameutanguliza mbele,alirusha teke lingine,safari hii,akirusha teke aina ya MAWASHI GELI.
(MAWASHI GELI,NI TEKE LINALOPIGWA KUTUMIA FUNIKA,HUKU LIKIZUNGUKA,NA LINAPIGWA USAWA WA SHINGO YA ADUI.)
Inspekta Jamila,aliliona teke lile, hivyo akachanuka
msamba,teke lile likawa linapita juu yake.
Inspekta Jamila,hakufanya ajizi,palepale alipokaa msamba,alipiga ngumi moja maridadi aina ya GEDAN
NZUKI katika korodani za JM,na akatoa mguno mkali kwa
maumivu,lakini pia akiinama na kushikilia korodani zake,huku akirukaruka mwa maumivu(GEDAN NZUKI,NI NGUMI INAYOPIGWA USAWA WA KORODANI NA KITOVU) Inspekta Jamila,alipomuona JM amepoteza kujilinda kwa maumivu aliyompa, aliinuka pale chini haraka,akapeleka ngumi nyingine aina ya SEDAN NZUKI,Jm akapiga yowe kubwa la maumivu,huku sasa mkono mmoja,ukiwa kwenye korodani,na mkono wa pili,akishika kifua chake,usawa wa chembe.(SEDAN NZUKI,NI NGUMI INAYOPIGWA USAWA
WA CHEMBE)Akawa ameuacha uso wake,alioukunja kwa maumivu ukimtazama.
Inspekta Jamila,hakuremba akapeleka ngumi ya tatu,safari hii akipiga ngumi aina ya JODAN NZUKI.
Ikawa imemlewesha JM akawa anayumbayumba.
(JODAN NZUKI, NI NGUMI INAYOPIGWA USAWA WA USO,BAINA YA PUA NA PAJI LA USO)
JM aliyumba hadi akawa karibu na ile silaha,akawa
anainama kwa tabu ili aichukue silaha ile,na Inspekta Jamila,akang’amua alichokuwa anataka kukifanya JM.
Hivyo akapiga pigo moja takatifu,akitumia teke aina ya
JAMPING MAIGELI,teke lile lilimsogeza JM hatua kadhaa
kutoka pale ilipokuwa ile silaha,na damu za pua
zikachukua nafasi yake.
(JAMPING MAIGELI,NI TEKE UNALOPIGA UKIWA UMERUKA HUKU UKIMFATA ADUI,UKIWA UNATAZAMANA NAE USO KWA USO,NA PIGO LAKE HUTUMIKA CHINI YA VIDOLE/UNYAYO.)
Inspekta Jamila alishalichungulia kaburi, hivyo akutaka kufanya maonyesho,alipigana na mtu ambae,muda wowote, anaweza kutoa roho ya mtu!
Mara kikasikika kishindo kikubwa chumbani mle,na
Inspekta Jamila alipotazama kule kilipotokea kishindo kile,alikuwa akitazamaza na Sajenti Kubuta Aliekuwa na silaha mkononi mwake.
Na kabla hajasema kitu akaingia Koplo Magane na
wakaingia askari wengine watatu,wote wakiwa
wamekamata bunduki mikononi mwao aina ya SMG.
“Sajenti KUbuta umechelewa sana bwana,ningekuwa
marehemu sasa hivi,nilikwambia tangu jana ofisini katika mikakati yetu,kuwa uwe ukinifatilia kutokana na kuwindwa kwangu,ila kwa kuwa umefika na nipo salama,basi halijaharibika neno,niambie hapa ni sehemu gani tulipo,kwani mie sijui kabisa nipo wapi!”
“Samahani Afande,kama mikakati ilivyokuwa ikisema,mimi nilikuwa pale uwanja wa ndege,nikakusindikiza hadi pale hotelini,nilipotaka kuondoka nikashuhudia jambo ambalo sikulitarajia.
Yule jamaa wa kithethe alikupiga Karate shingoni,wakakubeba haraka na kukupandisha ndani ya gari yao,mimi ningeweza kupambana nao,ila nilitaka nifike ambapo nilidhani,ndiyo yangekuwa masikani yao,ili tuwatie mbaroni wote,kwa kuwa nilikuwa peke yangu,ilibidi niongeze ngumu kutoka kituoni pale magomeni,kwani hapa tupo Maeneo ya Kawe”
Baada ya kusema maneno yale Sagenti Kubuta alitoa
pingu, ili amfunge JM,ambae sasa alikuwa amelala huku
akitweta kwa maumivu makali.
“No Sagenti Kubuta,huyo nilichukua ahadi kuwa
nitamfunga pingu kwa mikono yangu mwenyewe,hivyo inabidi nitimize ahadi yangu.”
Inspekta Jamila alimfunga pingu JM,akamuendea mzee wa Kithethe, akaichukua simu iliyokuwa mfukoni mwake,akaiangalia simu iliyokuwa ikiwasiliana na bwana Yule,namba ya simu ile iliyokuwa imewasiliana na mzee wa Kithethe, ilimtia fadhaa kubwa sana,ikamtoa machozi,akakata shauri mara moja akiwa na ile simu mkononi mwake
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Shawishi Wapenzi wa Simulizi Wapakue(Install) App ya CnZ Media