BARUA KUTOKA JELA (24)

Zephiline F Ezekiel
0
Mtunzi: Ibrahim Gama

SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE
ILIPOISHIA...
Inspekta Jamila alimfunga pingu JM,akamuendea mzee wa Kithethe, akaichukua simu iliyokuwa mfukoni mwake,akaiangalia simu iliyokuwa ikiwasiliana na bwana Yule,namba ya simu ile iliyokuwa imewasiliana na mzee wa Kithethe, ilimtia fadhaa kubwa sana,ikamtoa machozi,akakata shauri mara moja akiwa na ile simu mkononi mwake

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

ENDELEA...
*****Inspekta Jamila,aliingia hotelini kwa nguvu, akakutana uso kwa uso na Mpenzi wake,akiwa amekaa akiegemea mto,huku akiwa amepatwa na mshituko mkubwa!

“Karibu sweety,vipi mbona hivyo?”

Hatimae Shany alifunguka kwa kutoa kauli.

Inspekta Jamila,alimtazama mpenzi wake,kwa jicho la

husda!

“Mimi siyo sweety wako tena kuanzia sasa,wewe ni

mshenzi,na muuaji mkubwa!”

Inspekta Jamila baada ya kusema maneno hayo alikwenda kwa kasi ili amvamie Shany,lakini alipiga hatua mbili tu,hakuweza kuipata hatua ya tatu,Shany aliinua mkono wake na Bastola ikawa inaonekana waziwazi ikimlenga

Inspekta Jamila!

“Hatua moja mbele,nikusaini kifo! Mimi ninakujua kuliko

unavyojijua wewe!”

Shany alisema maneno hayo huku akisimama kutoka

kitandani,na kumkabili Inspekta Jamila.

Huku akiwa amesimama, kwa taharuki,Inspekta Jamila,alisema kwa fadhaa.

“Hata nawe pia?! Mtu niliekuthamini,kukupenda,kukuheshimu na kukupa mapenzi ya dhati,leo umekuwa nyoka wanigeukia?!Kwa lipi lakini baya,nililokutendea?!”

-

“Siku mbili zijazo,nitakuwa katika orodha ya matajiri

wanaotajika duniani,kwani mpango wangu ukishafanikiwa,nitapata pesa nyingi sana,Jamila wewe ni kikwazo kikubwa,katika kufikia malengo yangu,samahani sana,kwani bila ya hivi,siwezi kutimiza malengo yangu!”

Shany alimwambia Inspekta Jamila, akiwa amemuoneshea mtutu wa bunduki,usoni mwake.

Mara baada ya kusema hayo,Inspekta Jamila alilia kwa

huzuni kubwa,na mara Shani akakipeleka kidole husika,katika kiwambo cha kufyatulia risasi,ili amalize kazi yake!

Mara risasi ikalia na Inspekta Jamila,akalala chini!

Alipokuja kuinua uso wake,alimuona Shany anavuja Damu mkononi,huku silaha yake,ikiwa ipo chini!

Kabla hajatahamaki,alimuona mtu akitokea chini ya kitanda na Inspekta Jamila alipomuona mtu Yule,macho yalimtoka pima fadhaa ikamjaa,taharuki na Wahka ukachukua nafasi!

“Naitwa Jongo Janga,ukipenda niite JJ, natoka makao makuu ya usalama wa taifa,kitengo kisichokuwa na mipaka!”

Ilikuwa ni sauti ya ukakamavu,kutoka kwa Yule mtu alietoka uvunguni mwa kitanda kile,ambae Inspekta

Jamila,alimtambua kama muokota chupa za plastiki, na vyuma chakavu!

Alisema maneno yale,na kuonesha kitambulisho chake

juu,katika namna ya kutoa nafasi ya kusomwa!

“Lakini,usalama wa taifa unahusika vipi na kesi hii,lakini pia umeingiaje humu chumbani bila kuonekanwa?!”

Inspekta Jamila,alimuuliza Jongo Janga,huku akiwa

amepatwa na mshangao mkuu!!!

“Bastola ile ya kimada,wa bosi Serikalini,anaeitwa

Hamida,kauwawa Mikocheni!”

Jongo Janga,alikuwa anasoma moja kati ya beti za

BARUA KUTOKA JELA.Kisha akaendelea kusema huku

akimuelekezea mtutu wa Bunduki Shany,aliekuwa

amesimama akishikilia mkono wake uliokuwa unavuja damu!

Shany Karama Rashidi a.k.a SHANKARA nyoosha mikono

yako juu!”

Inspekta Jamila moyo wake ulipiga sarakasi,kwa mshituko alipolisikia jina lile lililokuwa katika waraka,likihusishwa na aliekuwa mpenzi wake,ama kweli usilolijua,litakusumbua!

Shany alitii amri na kunyoosha mikono juu,Jongo Janga,akapiga hatua kubwa na kuisogeza ile silaha ya Shany,kwa mguu.

“Lakini nataka kujua,wewe umeingiaje humu ndani?!”

Inspekta Jamila,alikuwa na dukuduku la kutaka kujua

namna Jongo Janga,alivyoingia mle ndani.

“Mara baada ya wewe kutekwa,nilikuwa nashuhudia! Na baada ya dakika zisizozidi tatu,Huyu bwana alikwenda nje,ili kumalizia mzigo wake uliokuwa ndani ya gari,kwani

alikuwa akifahamu mtego aliouandaa!nami kwa mwanya huo nikaingia chumbani humu,ingawa alikuwa amefunga na funguo,kwani sisi tunapotaka kuingia mahala popote,huwa tuna uwezo wa kufanya hivyo kwa funguo zetu zenye uwezo wa kufungua mlango na kufuli lolote!”

Jongo Janga,aliondosha shaka ya Inspekta Jamila,na

akatoa pingu,mfukoni mwake,akamrushia Inspekta

Jamila,ili amfunge Shany Karama Rashidi au kwa kifupi Shankara!

Inspekta Jamila,huku akimfunga pingu aliekuwa mpenzi wake,akajisemea moyoni mwake,

“Ama kwa hakika,huu ni mtego wa panya!”

Shany muda wote alikuwa ameinamisha uso wake chini,kwa jinsi alivyoaibika na kufadhaika.

“Shankara,huwezi tena kwa sasa,kulipua chochote ndani

ya nchi hii,waambie hao waliokutuma,serikali ya

Tanzania,ipo makini na ina usalama wa kutosha! Tunazo

taarifa kuwa kesho ilikuwa ulipue bomu,katika benki kuu

ya Tanzania na mitambo yako ambayo ingeingia kesho

hapa nchini kwa njia ya Bahari,hivi ninavyoongea na

wewe,tayari tupo nayo katika himaya yetu!”

Jonga Janga,alizizima ndoto za Shany katika moyo wake.

“Yaani wewe Shany,umekuwa na roho ya tamaa namna

hiyo? Unadiriki hata kuuw......!!!

“...Kuuwa huyo ndiyo kazi yake inayompa pesa!Huyu,ndiyo kiongozi wa genge la uhalifu nchini.Amekuwa

akifadhili sana vitendo hivyo,na huyu Shany,ndiye

aliekuwa akifatwa na kina Jeradi Mwaipopo,pale kwa

macheni!”

JJ alimkatisha na kuingilia mazungumzo yale.

Inspekta Jamila,alimchukia Shany,kama mtu ambae,hakuwahi kuwa mpenzi wake!

Kwa mikono yake alimfunga pingu mikononi,akazikaza

pingu zile hadi namba ya mwisho,zikambana Shankara,akalalamika zilegezwe,lakini hakuna mtu,aliemsikiliza!

Shany akiwa mbele ya Inspekta Jamila,huku Jongo Janga,akiwa anapekua mizigo yake,akawashangaza askari wale.

Alizunguka na pigo moja aina ya ORAKEN,likatua katika

shingo ya Inspekta Jamila likampeleka chini kama mzigo, akadondokea kichwa, akanyooka pale chini,akiwa

hatikisiki,yaani alikuwa kama gogo!

Shany haraka akatimua mbio,kuuwahi mlango,lakini

hakufika, Jongo Janga alifyatua risasi mbili,kila moja ikawa imepigwa mguu wake na Shankara akadondoka,huku akipigiza uso wake katika sakafu akatoa yowe kubwa na kutupatupa miguu yake!

(ORAKEN,NI PIGO LINALOPIGWA NA MPIGAJI,AKIWA AMEMPA ADUI MGONGO,HUZUNGUKA NA KUPIGIA NYUMA YA KIGANJA NA LIPIGE SHINGONI KWA ADUI)

Mara Sagenti Kubuta,aliwasili mahala pale, na timu yake,baada ya kumuhifadhi Jambazi,mkorofi Jeradi Mwaipopo katika kituo cha Polisi cha kati.

Na gari nyingine ikiwapeleka wale maiti,katika hospitali

ya taifa ya Muhimbili.

*******

Inspekta Jamila,alipokuja kupata fahamu,alijikuta katika chumba kimoja tulivu,kikiwa na watu watano wakiwa wanamtazama.

Alipotazama vizuri,akaiona sura moja ngeni machoni

mwake, Dokta Zahara akasogea karibu yake, na

kumwambia.

”Pole sana shoga yangu,lakini unaendelea vizuri”

Inspekta Jamila,alitaka kusema jambo,lakini alishindwa,machozi yakawa yanamtiririka,kisha akageuza sura yake,akakutana na Jongo Janga akiwa anamtazama kwa upole.

Inspekta Jamila,alimkazia macho na hatimae

akazungumza katika sauti ya kwikwi.

“Yupo wapi Shankara?!”

Yule mtu aliekuwa mgeni katika macho ya Inspekta Jamila,akasogea karibu na kusema.

“Pumzika Kwanza,ili upate nguvu sawasawa,kwani

ubongo wako,umepata maumivu makubwa,ingeweza

kukulelea Busting chuma ingepasua mishipa ya fahamu.

Hivyo unatakiwa upumzike,ili urudi katika hali yako ya

kawaida!”

Alikuwa ni Dokta Rehema Kanyela,aliekuwa akimtibia kwa karibu,yeye pamoja na Dokta Zahara.

“Inspekta,pumzika umefanya kazi kubwa sana,unahitaji

pongezi kwa kweli.Nimekuja kukuona mara baada ya

kuruhusiwa kutoka kwa madaktari wanaokutibu,ambao tumeona awepo shoga yako,lakini pia yupo mtu wetu hapo ambae ni Dokta na ni Inspekta mwenzio kwa ajili ya

usalama ambae ni Inspekta Rehema Kanyela.Shankara na Jeradi Mwaipopo,wapo chini ya ulinzi mkali,tunaendelea kuwahoji,hivyo tulia,kila kitu kipo sawa umenisoma Inspekta?!”

Ilikuwa ni sauti ya IGP aliemwambia kijana wake

kinachoendelea na kumaliza kwa swali.

“Nimekuelewa Afande,ila kuna kitu kinanichanganya

kidogo ile BARUA KUTOKA JELA, imewapataje watu wa

usalama wa Taifa?”

“Unatakiwa kutii Inspekta,siyo kuuliza tena kumbuka

barua zote zinazotolewa nje kutoka gerezani huwa

zinapitiwa na afisa usalama nae ndiyo anatoa idhini kama

zichapishwe pale gerezani na kutolewa nje au

zikachapishwe nje na kutumwa sehemu husika. Hata Mwaduga Dingo,alipopeleka barua yake ikachapishwe na

kuruhusiwa kutolewa nje,amini ilishapita kwa watu wa

usalama!Hivyo kwa nukta hiyo,sidhani kama utakuwa na mashaka yoyote katika nafsi yako!” IGP alihitimisha

maneno yake,kwa kijana wake,na Inspekta jamila,hakuinua tena mdomo wake,kuuliza au kusema chochote

kile.

Siku tatu baadae Inspekta Jamila,alikuwa katika kikao na IGP,yeye na Sagenti Kubuta, na IGP alikuwa akiongoza kikao kile kama kawaida,akawa anawaeleza vijana wake.

“Inspekta Jamila,kupitia watu wa usalama,tumepata

uthibitisho mkubwa kuwa kwenye gari yako,kulifungwa

kifaa maalum na Shankara,ambacho kila ulipokuwa na

gari ile,ulikuwa unaonekana katika GPS.Na gari hiyo

uliyonunuliwa na Shankara, ilikuwa imewekwa mitambo ile toka Japan,ilipotoka gari ile.”

IGP alikuwa akizungumza huku akiwatazama vijana wake,walivyokuwa wamepigwa na butwaa,kisha akaendelea kutoa habari.

“Hivyo kila ulipokuwa ukizungumza,iwe kwa simu,au na yeyote,kulikuwa na chombo maalum,kilichokuwa kinatoa

taarifa,kila kilipotakiwa kufanya hivyo,kwa mantiki hiyo,mambo yako mengi, yalikuwa yanajulikana na watu wale,katika namna ambayo,ingesumbua kufahamu katika hali

ya kawaida!”

Inspekta Jamila,alikuwa akitingisha kichwa kwa kuelewa taarifa ile nyeti sana.

“Shankara ni wakala wa ugaidi,alipokuwa huko ng’ambo, alipewa mafunzo ya ulipuaji mabomu,na kupitia Interpol,tumeweza kupata taarifa,na usalama wa Taifa, wameshadhibiti kila jambo,vinginevyo Taifa lingepata zahma kubwa sana!”

IGP alihitimisha taarifa yake,na kuwataka vijana wake

kama wana maswali.

“Nimekuelewa Afande,vipi kuhusu Jeradi Mwaipopo,alipohojiwa alikuwa na lipi jipya?!”

Inspekta Jamila,alitaka kufahamu.

“Jeradi Mwaipopo,hakufata taratibu za kazi tangu wakati

yupo kazini,anaposema chochote wakati huu,kinakuwa hakina maana sana!Yeye anazifahamu ngazi husika,kama

alionewa,alipaswa kupanda ngazi za juu ili kutoa taarifa

ifanyiwe kazi,kama alikaa nayo taarifa yake,kwa muda

huu,ninaipokea kama changamoto!”

IGP baada ya kusema hayo, akachukua gilasi ya maji

akanywa,kisha akaendelea.

“JM na Shankara,na mke wa marehemu Dokta Masawe,siyo muda mrefu,watafikishwa mahakamani,mara baada ya Shankara kupata nafuu majeraha ya risasi na Jm kifua

chake kimepata matatizo,nae yupo hospitali,wote wakipata nafuu,watafikishwa katika vyombo vya sheria,ili wakajibu mashitaka yao!”

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

 Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Shawishi Wapenzi wa Simulizi Wapakue(Install) App ya CnZ Media

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)