
Mtunzi: Ibrahim Gama
SEHEMU YA SITA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Yaani jamaa anaweza kumchukua yule Demu Mikocheni nyumbani kwake, na kumpeleka labda bwalo la polisi ostabey akalipwa shilingi elfu ishirini! Au siku nyingine humpeleka Bagamoyo na kumuacha kwenye hoteli za kitalii siku za mwisho wa wiki, akalipwa laki moja!
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
ENDELEA...
Sasa aliposikia mshikaji wetu Mwaduga yuko ndani tena kwa kesi ya mauaji ya yule Demu, mshikaji aliniambia haya ninayokwambia, na akasema Bel white mshikaji wangu jamaa yenu keshapotea, kwani ile ni mali ya wazee Yaani tumsahau! Sasa wewe sister unadhani hiyo ni kesi ya kitoto hiyo?”
Yule abiria alisogea katikati ya kiti cha dereva na abiria, huku akiwa na simu yake mkononi muda wote tangu amepanda gari ile, akasema kwa shauku kubwa.
“Duh ebwana we! Hiyo kweli ni kasheshe, Yaani ndiyo ilivyokuwa hivyo? Na mbona kule mwanzo ulisema wauaji na majambazi wanaachiwa tu wanatembea na jamaa yenu anaozea jela, kwa nini msiisaidie polisi kuwakamata na jamaa yenu akaachiwa?”
Yule abiria akazidi kuchimba. Na hadi walipofika Kimara Suka hotel akawa ameshapata hadi jina la yule Dereva Taxi wa mjini na namba yake ya simu, pamoja na namba yake Dereva Taxi huyu aliempeleka Kimara aliemtambua kwa jina la Bel white.
******
Ilikuwa siku ya Ijumaa Dokta Zahala akiwa nyumbani kwake maeneo ya Keko bora, alikuwa anaonekana kuwa ni mtu wa mawazo mengi, kisha kama aliyekumbuka jambo akatoa simu yake kwenye “Hand Begi” na kubonyeza tarakimu kadhaa na simu ya upande wa pili ikatoa maelezo badala ya kuita!
“IMU UNAYOPIGA IMEZIMWA AU IPO NJE YA ENEO, TAFADHALI JARIBU TENA BAADAE.”
Dokta Zahala akakata na kubonyeza namba zingine na simu ya upande wa pili ikaanza kuita.
“Shoga vipi mbona kimya au ndiyo nimekupa kazi kubwa kiasi hata simu yako ya kawaida umeizima?”
Aliongea Dokta Zahala mara tu simu ya upande wa pili ilipopokelewa, na kuongeza kuwa.
“Duh pole sana, sasa leo nipo mapumziko, kama unayo nafasi njoo nyumbani nitakuwepo. Kwani nina neno lililonifanya nikupigie simu!”
Aliongeza Dokta Zahala na kisha akakata simu.
Dakika Arubaini baadae kengele ya geti la mlango iliita, na mfanyakazi wa Dokta Zahala akakimbilia kwenda kufungua mlango. Dokta Zahala akamkaribisha shoga yake, na wakakumbatiana kama kawaida yao wanapokutana!
Dokta Zahala na Inspekta Jamila walikuwa marafiki tokea chuoni pale Mlimani, walipomaliza masomo, Jamila akaenda kujiunga na Jeshi la Polisi na kutokana na Elimu yake haikumchukua muda mrefu kupata nafasi aliyonayo, baada ya kuongezeka utendaji kazi wake katika Jeshi la Polisi.
Na Dokta Zahala alikuwa anachukua masomo ya udakitari, Baada ya mama yake mdogo aliekuwa nesi katika hospitali ya Kcmc Moshi, kumshawishi asomee mambo ya utabibu akimwambia unalipa sana, na kweli leo hii yupo katika nyumba yake mwenyewe pale Keko Bora!
“Leo soda yako ya lemon unayoipenda sina kwenye jokofu langu, je ukatafutiwe huko nje madukani au utakunywa hizi zilizopo?”
Dokta Zahala alimwambia shoga yake huku akiangua kicheko.
“Akili yangu ilivyovurugwa, sina chaguo lolote lililo bora, wewe nipe kinywaji chochote mimi nitakunywa, ilimradi kisiwe na kilevi!”
Alijibu Inspekta Jamila na akamalizia kwa kicheko. Baada ya wote kupata vinywaji cha juice, hatimae Dokta Zahala akavunja ukimya.
“Haya shoga yangu ukamwona yule Dada siku ile na mwanae sijui umefikia wapi, kwani alinitia huruma sana yule Dada.”
Inspekta Jamila akamuhadithia shoga yake kila kitu bila ya kumficha chochote huku akimwambia kuwa, ameamua kumueleza yote kwa ukamilifu! kwani kazi na maisha yake yapo hatiani toka yeye kujihusisha na kesi ile bila maelekezo kutoka kwa wakubwa zake, na ikija kubainika kwamba anajua hadi uhusiano uliokuwepo wa “IGP” na Marehemu Hamida, basi atakuwa katika mashaka mazito!
“Lakini pia nataka wewe shoga yangu uwe unalifahamu kwa undani jambo hili, ili ikitokea lolote kuhusu maisha yangu uwe na pakuanzia!”
Alisema kwa masikitiko Inspekta Jamila.
“Duh pole na hongera shoga!” Alisema Dokta Zahala.
“Sasa mimi nilikutafuta ili nijue kama ulimsaidia yule Dada, lakini pia kuna kitu kipya nataka kukueleza!”
Alisema Dokta Zahala na kuinua glasi ya Juice nakupiga funda moja, huku akimuangalia shoga yake alivyokaa kwa umakini mkubwa.
-
“Dokta yale uliyonipa yananinyima Raha hadi sasa, Leo unataka kunipa mzigo mwingine?!” Alilalamika Inspekta Jamila.
“Hili ni jambo nyeti sana ndio maana nikaona nikwambie wewe shoga yangu, lakini pia kama Raia Mwema nina haki kwa nchi yangu kuisaidia kwa kutoa mchango wangu!”
Alikazia Dokta Zahala.
“Mmmh” alishusha pumzi ndefu Inspekta Jamila na kukohoa kidogo kisha akasema.
“Haya Raia Mwema lete taarifa!”
Dokta Zahala akaangua kicheko, kisha akaanza kwa kusema.
“Jana imeletwa maiti pale kazini ikielezwa ni ya Ajali, kiasi kila mtu anaamini hivyo! Ila baada ya saa kadhaa nilipokwenda kuifanyia uchunguzi, maiti ile ilinishangaza! Kwani “Rigor Mortis”, Yaani zile athali za kifo kwa maiti zilijitokeza mapema sana, ukizingatia maiti ile haikutokwa na damu nyingi,wala haikuwa na majeraha makubwa!”
“Basi nikiwa ni Daktari, jambo lile lilinifanya nifanye uchunguzi wa kina. Nakweli niligundua mtu yule hakufa kutokana na ajali, bali alikufa kabla ya ajali!”
Dokta Zahala alipeleka funda lingine la juice kinywani mwake, kisha akaendelea.
“kwani vipimo vimenijulisha kwamba, mwili ule ulitokwa na uhai mapema sana asubuhi, na amekunywa au amenyweshwa sumu! kwani mabaki ya sumu ile imeonekana katika mwili wake! Sasa swali linakuja. Askari wa Doria wakati wanaelekea sehemu ya Bagamoyo kiasi cha saa moja nyuma hawakukuta ajali ile, wakati wanarudi ndiyo wakaiona gari iliyopata ajali. Marehemu alikutwa amebanwa kwenye usukani wa ile gari akiwa ameshafariki. Mnamo saa tano za asubuhi. Je aliendeshaje gari ikiwa mtu amekufa asubuhi mishale ya saa moja, kisha saa tano ndiyo apate ajali tena akiwa anaendesha gari?!”
Dokta Zahala alisimama kidogo kisha akaendelea.
“Ndipo nikaona nikwambie wewe, kwani askari walioandika maelezo hayo ninayokwabia, wanaamini yule Bwana waliemtambua kwa jina la Kiyarwenda Mwemezi Mkazi wa Mikocheni B, kutokana na kitambulisho cha kupigia kura alichokutwa nacho katika eneo la tukio, amefariki kwa ajali ya gari.”
Inspekta Jamila alitoa macho pima baada ya kusikia habari ile hasa jina la marehemu Kiyarwenda Mwemezi. Kwani ni yule jirani yake Hamida kule Mikocheni, aliyekuwa akimuhoji kuhusu kifo cha marehemu Hamida. Hata naye aliposikia ajali ile, alikuwa anahisi kuna kitu kilichojificha katika ajali ile kumbe alikuwa sahihi na mawazo yake!
“Sawa Dokta, sasa ugumu wa swala hilo nikumpata au kuwapata watu waliofanya hivyo, Yaani waliohusika katika mauaji yale. Na kwa nini walifanya mauaji yale. Kwani nahisi bado yapo katika mlolongo wa kesi hii niliyojipachika, na sasa naona mambo mengi sana kiasi yanazidi kuniweka katika wakati mgumu. Kwani kama kuuwawa kwake jirani yule kunatokana na kujua mambo mengi ya marehemu Hamida na mumewe, au imeshabainika kama niliongea nae, sasa wahusika wa kadhia hii wanajaribu kuharibu ushahidi!”
Inspekta Jamila, alisema maneno hayo huku, akionekana kuwa ni mwenye chembechembe za woga, hasa akizingatia kuwa kesi ile, yeye hakukabidhiwa jalada lake.
Watu gani hao wanaofatilia nyendo zake katika muda mfupi namna ile.
Akaiweka wazi hisia yake kwa Dokta Zahala wote wakaingia katika lindi la mawazo mazito!
“Kitu cha hatari nilichokifanya shoga ni kwamba, nilichukua vipimo vile kitaalam zaidi, kwani niliweka kile kifaa maalum cha kisasa kilicholetwa hivi karibuni kutoka China, ambacho kina uwezo wa kung’amua tukio la mwisho kabla mtu hajafa aliloliona!”
Dokta Zahala huku akimkazia macho Inspekta Jamila, alichukua gilasi iliyokuwa na juisi akainywa yote, kisha akaendelea kusema.
“Ukitaka kupata picha ya aliyoyaona mtu kabla hajafa, itakubidi ufumbue macho ya marehemu, kisha uweke kifaa kile kama miwani ,na kifaaa kile kita scan picha ya mtu au kitu cha mwisho macho yale kuona! Hivyo nimefanikiwa kupata picha za watu wawili ambao marehemu kabla ya kukata roho, alikuwa anatazamana nao ana kwa ana!”
Dokta Zahala akakandamiza jambo lingine lililomfanya Inspekta Jamila kuinuka katika kiti alichokalia na kwenda kumkumbatia shoga yake yule huku akitamka maneno mfululizo.
“mungu wangu, mungu wangu!”
Sasa wakiwa bado wamekumbatiana, Dokta Zahala akaendelea kusema ile azma yake iliyomfanya amwite shoga yake nyumbani kwake muda ule.
“Hivyo lililonifanya nikuite wewe, ni pamoja na kukupa habari hii kwa kina, na nikukabidhi picha zenyewe, ili uanze kazi yako!”
“Sio nianze kazi yangu, niendeleze kazi yangu, kwani kazi nilishaianza tokea Jumapili, alipofika ofisini kwangu, yule Dada anayeitwa Eshe Muhidini, ambaye wewe ndiyo uliemuelekeza aje kwangu.”
Alijibu Inspekta Jamila na kuendelea.
“Sasa huyo maiti uliyemfanyia uchunguzi ndiyo yule jirani yake Hamida aliyenipa Mwanga katika upelelezi wangu, kwani ukimtoa yule mahabusu Mwaduga, mtu wa kwanza kumuhoji alikuwa ni Ndugu Kiyarwenda Mwemezi ambaye sasa ni marehemu! Yeye ndiyo aliyenifungua ya kwamba, kabla sijapeleleza kifo cha Hamida, napaswa kwanza kufahamu kifo au kilichopelekea kifo cha mume wake Hamida, Bwana Bartazal Halimu!”
Alisema kwa msisitizo Inspekta Jamila huku akiwa amesimama wima na akiachiana na shoga yake kutoka katika kukumbatiana.
Dokta Zahala akainuka nakuenda chumbani kwake, alipotoka alikuwa ameshika bahasha mkononi ikiwa imefungwa, na juu ya bahasha ile kuliandikwa maneno Dear Jamila! Akamkabidhi Inspekta Jamila bahasha ile na kumwambia.
“Mambo yote yapo humo ndani ya bahasha hii!”
Inspekta Jamila akaipokea ile bahasha na saa hiyo hiyo akaaga na kuondoka!
*******
Ilikuwa ni saa kumi na mbili za jioni, kikao kilikuwa kinafanyika katika ofisi ya “IGP” kilichokuwa na watu wasiozidi sita.
“IGP” mwenyewe na mlinzi wake, Afande Kubuta, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, Kamanda wa Kanda Maalum na Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, watu wote hawa wakiwa wametoa kofia zao katika vichwa vyao, kasoro “IGP” walikuwa katika mjadala mzito wa namna matukio ya uhalifu Mkoa wa kipolisi wa Kinondoni yanavyoendelea, pia kushughulikiwa kwa kesi ya marehemu Hamida Baltazal.
Baada ya “IGP” mwenyewe kutaka faili la kesi hiyo ili kutazama mwenendo mzima wa kesi hiyo, na baada ya kusoma kwa makini taarifa zilizoandikwa katika faili lile ndipo alipoitisha kikao hicho cha dharula.
“Sasa nimewaita hapa, baada yakuona maelezo yaliyopo katika faili hili hayatoshelezi, na hayaridhishi katika kuiendesha kesi hii, lakini pia kuna jambo lisilo la kawaida limejitokeza!”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Shawishi Wapenzi wa Simulizi Wapakue(Install) App ya CnZ Media