
Mtunzi: Ibrahim Gama
SEHEMU YA TISA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Alipofika Magomeni Mapipa, akaegesha gari yake katika kituo cha basi, kisha akaiangalia kwa mara nyingine ile bahasha, akaichukua na kuifungua.
Ndani ya bahasha ile kulikuwa na karatasi iliyoandikwa maneno yafuatayo;
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
ENDELEA...
HABARI INSPEKTA JAMILA. NAKUSHAURI KWAMBA, WACHA KUJIINGIZA KATIKA MATATIZO YASIYOKUWA YA LAZIMA! KWANI HUU NI MTEGO WA PANYA. BORA KWAKO KUACHANA NA KESI HII. NA KAMA UTAKAIDI UTAKIONA CHA MTEMA KUNI!
Alimaliza kuusoma waraka ule Inspekta Jamila, huku akipigwa na mshangao wa mwaka!
Kilichompa mshangao ni kwamba, huyo mtu au watu alieandika walaka huu ni nani, amejuaje kama yeye ndiyo anaefatilia kesi ile kwa sasa, kwani alipokabidhiwa kesi ile, alikuwa yeye na “IGP” tu, watatu wao ni mwenyezi mungu! Lakini pia mtu alieandika walaka ule, amejuaje kama yeye atakuwa pale kwa Dokta Zahala muda ule?!
Isitoshe walaka ule haukuandikwa kwa mkono, bali umechapishwa kwa kutumia kompyuta, kisha ukaprintiwa!
Kazi ile rasmi alipewa Jumamosi, na leo ni Jumatatu, iweje ndani ya siku mbili tu iwe imeshavuja kwamba yeye ndiye! Ukizingatia kwamba hata shoga yake Dokta Zahala, ndiyo amempa taarifa ile muda mfupi uliopita!
Alipofikia hapo ubongo wake ukawa unazidiwa kwa maswali yasiyokuwa na majibu. Pia akikubali kimoyomoyo kama kweli ule ni MTEGO WA PANYA. Mara akaona vipele vya baridi vikizizima katika mwili wake.
Akapeleka mkono mgongoni mwake usawa wa kiuno na kuigusa bastola yake ndogo ya kipolisi na faraja ikamrejea upya!
Alisonya msonyo mkubwa kiasi gari yake ingekuwa imefunguliwa vioo basi hata watu wa nje wangesikia.
Akaiweka ile karatasi ndani ya bahasha na kuitumbukiza katika mkoba wake.
Akaiweka gari barabarani na safari ya Sinza kwa Dokta Masawe ikaendelea.
Alipofika Sinza maeneo ya madukani akachepukia barabara inayoelekea katika Guest ya Namnani, na mbele kidogo akakiona kibao kinachoitambulisha Hospitali ya Dokta Masawe, kilichoandikwa “DOCTOR MASAWE DISPENSARY”, huku kikionyesha mshale kuelekeza ilipo Hospitali hiyo.
Inspekta Jamila akazidi kusisimkwa na damu isivyo kawaida.
Katika kona ya pili mbele ya barabara ile akaona maandishi mekundu na meupe pamoja na picha ya nyoka yanayosomeka “Doctor Masawe Dispensary.”
Inspekta Jamila akatambua kwamba amefika eneo alilolikusudia.
Katika eneo la maegesho ya magari la hospitali ile kulikuwa na magari kadhaa yaliyokuwa yameegeshwa katika sehemu hiyo.
Naye akawa katika harakati za kutafuta eneo la kuegesha gari lake ndipo moyo wake ulipompiga ghafla!
Gari nyekundu aina ya Toyota Caldina ilikuwa imeegeshwa mbele ya hospitali ile.
Akagundua kwamba Dokta Masawe amemkuta. Akatafuta sehemu nzuri ya kuegesha gari lake na kuiegesha gari na kushuka, akajichoma ndani ya hospitali ile.
-
“Hapana mwanamke, siwezi kuondoka hapa bila kuonana na Dokta Masawe ambaye wewe unamuita Bosi. Lakini pia sikutishii kukukamata, bali nitakukamata kweli usipokuwa makini. Kwani kwa kauli hiyo ni kupuuza agizo halali la Jeshi la Polisi na huyo bosi wako hawezi kunifundisha kazi akafanya kwa utaratibu anaoutaka yeye! Sasa mwambie hivi Inspekta Jamila anasema hataondoka hapa hadi unaongea naye. Vinginevyo anaweza kutumia PLAN, B!”
Inspekta Jamila aliongea bila kuifafanua hiyo “PLAN, B”.
Kufikia hapa yule dada akataharuki kupita maelezo, akainua tena mkono wa simu na kubonyeza namba kadhaa, akasubiri kwa muda kisha simu ile ikampa maelezo SIMU YA MTEJA UNAYEMPIGIA HAIPOKELEWI!
Akarudia tena na tena kuipiga simu ile, huku Inspekta Jamila akishuhudia lakini bado ulikuja ujumbe kama wa mara ya kwanza.
Yaani ilikuwa inaonyesha kwamba simu aliyokuwa akiipiga yule dada, mkono wake wa simu haukuwekwa katika sehemu yake.
Inspekta Jamila akamwambia yule dada, “Nipe namba ya simu yake ya mkononi.”
Yule dada akamjibu “siyo utaratibu kutoa namba ya simu ya mtu ya mkononi bila ridhaa ya mwenyewe!”
Hivyo Inspekta Jamila akawa haelewi kwa wakati ule nini amfanye dada yule kwa majibu yale.
Inspekta Jamila akatoka nje ya hospitali ile hadi katika gari yake akatoa simu yake kwenye mkoba akabonyeza nambari kadhaa na simu yake ikawa inaita.
“Dokta Zahala tafadhali naomba unipatie namba ya simu ya mkononi ya Dokta Masawe, kwani nipo kazini kwake na napata usumbufu kiasi kumuona”.
“Sawa shoga nitakutumia katika meseji sasa hivi.”
Alijibu Dokta Zahala na Inspekta Jamila akakata simu.
Kiasi cha kama sekunde ishirini simu ya Inspekta Jamila ikaingia ujumbe na kwa wahka mkubwa Inspekta Jamila akaufungua ujumbe ule uliotoka kwa Dokta Zahala, na kukuta namba zenye
tarakimu kumi, ilikuwa niyamtandao wa Voda Com.
Naye bila Ajizi akaipiga namba ile akawa anasubiri. Jibu alilolisikia kutoka katika simu ile lilimkatisha tamaa.
“Simu unayopiga kwa sasa haipatikani, tafadhali jaribu tena baadae.”
Inspekta Jamila alilewa bila ya kunywa!. Mara akakata shauri kuwa siku hizi watu huwa wana namba moja kwa mitandao tofauti.
Basi alichofanya ni kuipiga namba ile katika mitandao mingine. huku akiiseti simu yake katika mfumo wa “PRIVATE NUMBER” Alipoipiga namba ile katika mtandao wa Airtel ikawa inaita na Inspekta Jamila pumzi zikampaa.
Moyo wake ukaanza kwenda mbio kama saa mbovu kwa mchecheto mkubwa uliomjaa. Huku akiombea isiwe simu ya mtu mwingine!
“Dokta Masawe hapa nani mwenzangu?” ilisikika sauti baada ya kupokelewa ile simu.
Inspekta Jamila aliguna kwa kihoro aliposikia sauti nzito ya mtu aliyehitaji kuonana naye, hatimaye amefanikiwa kuisikia sauti yake.
“Ohoo! Dokta Shikamoo. Mimi ni Jenipha niko Mwenge nataka kukuona nina mgonjwa wangu. Je upo kazini kwako au upo nyumbani?”
Inspekta Jamila aliongopa huku akitoa heshima ya shikamoo pia akisikiliza uongo wake kama utaleta jibu gani!
“Wewe nani aliyekupa namba hii? Kwani hakuna mtu zaidi ya mke wangu na baadhi ya watu wangu muhimu ndiyo niliowapa namba hii.”
Dokta Masawe alipatwa na mshituko kwani aliyepiga namba ile lazima jina lake litokee kwenye kioo cha simu yake, Kwa sababu wote aliowapa namba ile alihifadhi namba na majina yao katika simu ile. Lakini pia namba ile ilikuwa katika simu yake inayojitegemea, hakuiweka katika mfumo wa kuidivert ingawa ilikuwa inafanana na namba yake ya voda ambayo watu wengi aliwapa namba hiyo. Na alifanya hivi kwa sababu zake maalum!
Inspekta Jamila akajibu.
“Aliyenipa namba hiyo ni katika hao watu wako muhimu na wakaribu.” Kisha akaendelea.
“Dokta sasa simu inakwisha pesa naomba unijibu basi kama leo inawezekana kukuona ili tuonane kwanza tuzungumze ili nijue gharama kabla sijamleta mgonjwa. Pia tutapoonana tutapata wasaa mzuri wa kunihoji chochote upendacho, kwani kutakuwa hakuna gharama yoyote itakayosababishwa na maongezi hayo kwangu”.
Inspekta Jamila alijibu huku akiilegeza sauti yake kidogo.
“Sawa, sasa muda huu nina kikao kidogo, wewe unaweza…”
Dokta Masawe hakumalizia kauli yake akamuuliza swali.
“Kwa nini simu yako umeiweka katika mpango wa Private Namba?”
Dokta Masawe kama aliyegutuka, alitaka kufahamu.
“Jamani Dokta simu yangu haina pesa ya kutosha bwana, inaweza kukatika muda wowote.”
Inspekta Jamila aliongea kwa sauti ya mapozi iliyotokea puani.
“Simu yangu ipo katika hali hii muda mrefu sana kiasi miezi mine, miezi miwili baadae ndiyo itakuwa katika hali ya kawaida. Kwani nimeongea na huduma kwa wateja wa kampuni yangu ya Vodacom na kuwataka waniwekee simu yangu katika hali hii, kwani mimi ni mfanyabiashara nina watu wengi niliowakopesha bidhaa zangu, nilipokuwa nawapigia katika kufuatilia madeni yangu, walipokuwa wanaona namba ya simu yangu, walikuwa hawapokei simu au uwapa watu wengine na wakanijibu majibu ya utumbo. Ndipo nilipoamua kutumia mtindo huu.”
Inspekta Jamila alitumia uongo unaofanana na ukweli na Dokta Masawe akaingia katika mtego.
“Okey sasa nimekuelewa kwani nilifikiri ni askari mmoja wa kike anayeitwa Jamila alikuwa analazimisha kuongea na mimi muda mfupi uliopita. Hivyo nilidhani labda ndiyo wewe unanichezea. Samahani sana kwa usumbufu uliojitokeza.”
Dokta Masawe alijibu kisha akatoa majibu ambayo Inspekta Jamila hadi anaondoka katika eneo lile alikuwa katika tabasamu pana, akaiwasha gari yake na kuondoka eneo lile taratibu, huku moyoni akiwa na matumaini ya kushinda kesi ile kwa kishindo baada ya mtego wake kunasa muda mfupi ujao.
Inspekta Jamila aliendesha gari yake hadi Magomeni Mwembechai, akaegesha gari yake na kushuka nje katika Mgahawa wa Mwembechai Plazza.
Akaenda katika viti vya mgahawa ule na mara baada ya kukaa tu muhudumu akamfuata na kutaka kujua mteja wao anataka kula au kunywa nini.
Inspekta Jamila akaagiza maziwa ya moto ya Ng’ombe na mayai mawili ya kuchemsha pamoja na juice ya parachichi.
Alipoletewa vitu hivyo akawa anaburudika taratibu akiwa anavuta muda wa kwenda kuonana na Dokta Masawe kama walivyopanga. Hiyo ilikuwa ni saa tano ya asubuhi.
Inspekta Jamila akawa anatafakari mambo aliyokutana nayo toka muda ule alipotoka nyumbani kwake asubuhi hadi kwenda ofisini kwake, na alipokwenda kwa Dokta Zahala namna alivyokuta waraka uliyopenyezwa ndani ya gari yake na yote yaliyotokea kwa Dokta Masawe. Alipokuja kutahamaki, Hamad! Maziwa yalikuwa yameishapoa.
Inspekta Jamila akapiga tarumbeta maziwa yale na kisha akawa anakunywa juice na mayai kwa taratibu.
Ilipotimu saa tano na dakika ishirini, Inspekta Jamila akalipa bili yake na kuiendea gari yake ili aende katika mtego wake.
Alifungua mlango wa gari na kuondoka eneo lile, akielekea kwenye mtego wake, kwani zilikuwa zimesalia kama dakika thelasini na tano, ili kuonana na Dokta Masawe ana kwa ana!
Inspekta Jamila aliwasha gari yake na kuondoka eneo lile kwa mwendo wa taratibu, akielekea maeneo ya Manzese. Dakika tano baadae, Inspekta Jamila alikuwa ameegesha gari yake katika Hoteli ya Friends Corner pale Manzese Aljentina.
Akajichoma ndani ya hoteli ile,huku wateja wachache waliokuwa pale kwa ajili ya mlo wa mchana, na wale wanywaji wa pombe wasiokuwa na muda maalumu wa kunywa, walikuwa wakimtumbulia macho Inspekta Jamila toka alipoingia hotelini pale hadi sehemu aliyokwenda kukaa!
Inspekta Jamila alikuwa amekaa katika eneo ambalo, alikuwa akimuona kila anaeingia na kutoka. Alipokuja muhudumu akamuagiza amletee kinywaji kisichokuwa na kilevi cha Malta Guness, na yule muhudumu akadai pesa yake kabisa, na Inspekta Jamila akamlipa kabisa muhudumu yule.
Kiroja kilikuja yule muhudumu alipokuja, alileta chupa tatu badala ya ile moja aliyoagizwa!
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Shawishi Wapenzi wa Simulizi Wapakue(Install) App ya CnZ Media