Notifications
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…
  • MY DIARY (22)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILITULIPOISHIA...Alitumia vizuri umbo lake la kimiss kutembea kimiss na kuweka mapozi ya maana. Na baada hapo alilala kwenye kile kigodoro na akachojoa vyote isipokuwa kufuli jeupe ambalo nalo alipewa hapo hapo kwa ajili ya kazi hiyo. IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi sikumpa nafasi Joyce niliingilia nafasi yake na kuchukua ule uume wa bandia nikamfuta yule dada.…
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…

MUUZA CHIPS (83)

Mwandishi: MoonBoy

SEHEMU YA THEMANINI NA TATU
ILIPOISHIA...
Simu ilikata, lakini chidi haamini maneno ya Sabra…

"ana maana gani huyu mtu"

Aliongea chidi huku akitaka kupiga simu lakini roho haitaki…

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
"we mama, nipe dakika tano narudi sasa hivi"

Aliongea chidi na kuyafuata maneno ya sabra..

"chidi jamani, unaniacha kisa nimekataa ulichokitaka kwangu"

"ebu tuyaache ayo"

"chidi jamani, basi nimekubali njoo basi"

Eeehhh chidi kuskia mama sarah kakubali kurukwa ukuta, mana anampenda sana chidi na hatamani kumpoteza… Chidi alishaanza kuondoka lakini kuskia kakubaliwa tu, alijikuta anasita kutoka, mana anaitamani sana hio sehemu….

Chidi alirudi mpaka kitandani na kuanza kumshika shika mama sarah, wakati huo mama sarah tayari keshakubali na tena kakaa mkao ule ule unaorakiwa, mana kakubali kwa hali yake, na chidi alivyo mwehu wala hakutaka kumkopesha,…

Lakini kadri anavyozidi kumshika shika mama sarah, akili yake haikuwa sawa, yaani alikuwa anawaza maneno ya sabra kuwa akamchukue mdogo wake kule alipokuwa,….

Chidi hakuwa mjinga kiasi hicho

"kama ni huyu mwanamke yupo, nitamshuhulikia nikirudi"

Chidi alijisemea kimoyo moyo kisha akamuacha mama sarah bila hata kumgusa kitu,..

"we chidi una nini lakini"

"narudi muda sio mrefu"

"lakini mbona sikuelewi"

"narudi, tena nipe gari yako mara moja niwahi"

Chidi aliomba gari kwa mama sarah na kuondoka kwenda kule kwa akina sabra,..

Tukija huku kwa akina miriam tunamuona miriam anatoka na kupanda gari yake,… Alikuwa akimfuata sarah kule hotelini kwao, mana alimpigia simu ili aje lakini sarah alisema mama yake hayupo

Hivyo miriam akachukuwa jukumu la kumfuata sarah kule hotelini kwao…

Robo saa mbele miriam alishafika kwa akina sarah

"heeeee Miri umemuacha nani huko hotelini kwenu"

Aliuliza sarah baada ya kumuona miriam kafika hotelini kwao, mana kwa sasa hoteli ilishanunuliwa na akina sarah, hivyo sio ya akina miriam tena

"mama yupo na nimemuaga"

"Enhee sema shost, uliniambia kuna kitu unataka kusema"

"ndio shost,… Mama si alinifuma naongea na omary,.. Mwenzangu ila safari ya kwenda Uingereza imeanza tena"

"heeeeeeeeee mama yako nae, sasa anataka upate mwanaume wa aina gani, au anataka mzungu"

"mi ata sijui, yaani natamani hata kujiua sarah"

"apana miri, huko mbali sasa unapofika, usiseme hivyo"

"sasa nifanyeje sarah,.. Mana nikiumwa tena ataona ni kamchezo kangu"

"mmmhhh kiukweli leo sina hata cha kukushauri miri wangu"

Miri alikuwa anatamani kulia bila kujua atafanya nini mana anampenda sana omary wake,.. Na hatamani kumuacha

"Sarah, mi nachukuwa uamuzi mgumu, liwalo na liwe, ila naomba uniseidie kitu sarah please"

"kitu gani tena miri"

Walichokiongea walituficha mana waliongea kwa siri sana lakini tutajua huko mbele,..

Baada ya kufanya maongezi yao miriam aliondoka kurudi hotelini kwao… Alipofika tu alikutana na mama yake

"haya, umeshajiandaa… Mana kama ni tiketi nimeshakata mchana hivyo keaho nakutakia safari njema"

Miriam hakuwa na la kusema lakini moyoni mwake kuna jambo kalipanga baina yake na sarah, sasa sijui itakuwaje

Sasa tukija huku kwa chidi, akiwa ndani ya nyumba ya shemeji yake anamtafuta halima ambaye ni mdogo wake,.. Lakini hakumuona nyumba nzima,.. Aliingia mpaka chumbani kwa shemeji yake ambaye ni jasmini,

Aliangalia lakini hakumuona, sasa ile anaondoka, alishangaa kuona masanamu yakiwa ndani ya kabati la vioo, afu masanamu yenyewe, yameashiria alama za kishetani mambo ya freemason,.. Chidi aliduaa na kushindwa kuelewa, lakini mara simu yake inaingia sms, kucheki alikuwa ni sabra

"we chidi, sisi tupo karibu sa kama upo ndani toka haraka, mana dada kabadirika sana yaani sio yule unaemjua"

Chidi alipomaliza kusoma sms hio alitoka lakini hajamuona halima, alipofika kwa mlinzi akamuuliza

"oya eti kale katoto kametoka nje"

Chidi alimuuliza mlinzi wa geti hilo

"ndio ameenda twisheni"

"unapajua hapo twisheni"

"hapana sipajui"

Chidi alikasirika sana,.. Lakini hakutaka kupoteza muda alitoa gari mpaka nje ya nyumba na kuondoka mbali kidogo kule alipoelekezwa na mlinzi kuwa ni njia hio ndio ya kuendea tuisheni lakini hapajui twisheni penyewe..

Haikupita hata dakika tano jasmini na mdogo wake sabra ndio wanaingi, yaani angechelewa tu kidogo angelikutwa,… Lakini jasmini aliona kuna tairi za gari jingine…

"we kapwiku, ni gari gani imeingia huku"

Aliuliza jasmini

"ni yule kijana mdogo wake boss"

Mlinzi alijibu kuwa ni yule kijana mdogo wake boss,.. Jasmini alijua tu atakuwa ni chidi… Hakutaka kuuliza tena lakini moyoni mwake alikuwa akijiuliza kuwa

"huyu chidi kafata nini huku"

Alijiuliza mwenyewe kimoyomoyo huku akiingiza gari lake kwenye paking,… Lakini kabra hajaliweka sawa aliina ngoja aulize tena

"we kapwiku… Huyo kijana alifuata nini"

"alikuwa anamuuliza mtoto boss"

"mtoto gani"

"yule mschana"

Jasmini kuskia ni yule mschana aliwasha gari haraka ili awahi kumchukuwa halima mana yeye ndio anajua hio twisheni ilipo, ila wakati huo chidi kapaki pembeni kama atamuona mdogo wake, lakini huku kwa jasmini nae anakuja kuelekea twisheni,.. Mana keshajua kuwa chidi anataka kumchukuwa mdogo wake, hivyo amuawahi kabla hajakutana nae..

Sasa na wakati huo twisheni ndio wanatoka, sasa chidi akawa katulia tu hapo barabarani ili kuona kama atapiata hapa, lakini mara akaona katoto kamoja kamebeba daftari…

"mtotooo ujambo"

"sijambo shkamoo"

"marahabaaa… Unatoka wapi"

"natoka twisheni"

"twisheni yenu ipo wapi"

"pale mbele, unaingi hivi afu utaona kibao cha twisheni yetu"

Chidi kuambiwa hivyo aliondoa gari fasta bila kuchelewa, lakini kwa ile spidi anayokuja nayo jasmini sijui kama chidi atawahi,.. Mana mpaka aangaze macho afuate kibao mpaka lini,..

Sasa kama bahati tu, Halima katokea barabarani,

"dadaaa we dadaa"

Chidi alimuita mdogo wake kwa heshima

"abeee kaka"

"njoo haraka,… Ingia kwenye gari"

Alimfungulia mlango kisha akaingia… Yaani ile anaingia tu na jasmini ndio anafika hapo na kushuka kwa haraka kuelekea huko ndani ili akamchukue, lakini halima alishaingia kwenye gari saa mingi sana, na kwakuwa jasmini hajui gari ilioingia kule kwake, alishindwa kujua kama ndio gari hii alioipita hapa,… Chidi hakuchelewa, aliondoa gari ili kurudi nyumbani,…

Sasa jasmini kutoka alishangaa kuona gari alioipita hapa sasa hivi tu haipo,.. Ndio akajua basi keshachukuliwa… Lakini akilini mwake alikuwa akijiuliza, hii taarifa kapewa na nani.. Mana alikuwa hajui,..

Sasa chidi akiwa njiani mara simu iliita, kucheki alikuwa ni miriam.

"haloo boss"

"acha zako chidi, boss niwe mie"

"ok sema"

"naomba unipitie hapa mnarani"

"kuna nini"

"we njoo tu utajua baadae"

Simu ilikata lakini chidi hakuelewa kwanini aliambiwa ampitie hapo mnarani,

Sasa huku hotelini kwa akina miriam, mama alikuwa akimtafuta miriam ampe tiketi yake akae nayo hamuoni, lakini gari ya miriam ilikuwepo maeneo ya paking hivyo ilionyesha kuwa miriam yupo na hakwenda mbali,…

Chidi alifika mnarani na kumkuta kaketi chini ya mti, yaani alivyokaa utafikiri sio matajiri yaani alikuwa tofauti sana…

Miriam aliingia ndani ya gari lakini hio gari alioingia anaijua mwanzo mwisho..

"omary, hii gari umeipata wapi"

"ni ya mama mmoja hivi"

"mama sarah si ndio eee"

Sasa chidi yeye hajui kama anaitwa mama sarah, hivyo alikataa

"hapana anaitwa grace"

"sa ndio mama sarah huyo"

Sasa chidi kuona mbona kama kinasanuka kitu ikabidi akubali huku akisema

"ni yule mama alienileta kule hotelini kwenu"

"ndio huyo huyo, ana mtoto anaitwa sarah"

"ok sasa wewe vipi… Unaenda wapi"

"kwako"

Chidi alitoa macho kuskia miriam anakwenda kwake

"mamuu, unakwenda kwangu kufanya nini"

"ina maana ni vibaya kuja kwako"

"aaahhh mamuuu"

"nini babuu we twende… Afu huyu ni mtoto wako nini"

Aliuliza miriam huku akimuangalia kwa umakini ili kumfananisha na chidi na ni kweli walikuwa wanafanana kwa mbalii sema halima alikuwa ana uweusi kidogo na chidi yeye ni maji ya kunde yaliong'aaa,

"hapana ni mdogo wangu"

"muongooo"

"kweli"

"waooooo basi ni kawifi kangu… Njoo mwaya wifi yangu"

Miriam alimchukuwa halima na kumpakata,.. Halima alikuwa na umri wa miaka kama saba au nane, ni mkubwa kidogo alikuwa ana kaumbo kazuri hivyo kila mwanamke anaemuona basi anampenda tu,..

"mamuu mi sijakuelewa unajua"

"chidiiiii, mi nataka leo nikalale kwako"

"mi nadhani unataka kuniletea kesi mamuu"

"nimeaga nimesafiri hivyo nitakuwa kwako kama siku mbili hivi"

"mamuuuuuuu… Siku mbili?… Hapana aisee utaniletea shida… Sasa huko uliposema umesafiri wakiulizwa afu wakisema haupo"

"usijali"

"mamuuuu"

"please baby… Naomba uniamini"

Chidi alichoka hata kuongea hivyo aliwasha gari na kuelekea nyumbani kwa chidi mahari alipopangisha kijana huyo,..

Lakini chidi roho inamdunda kwasababu mama sarah yupo kule, afu mbaya zaidi alimuacha yupo uchi, afu ana miriam je itakuwaje, yaani ni bonge la msala,..

Chidi alimtumia mama sarah sms kuwa

"mamy vaa nguo zako nakuja na mdogo wangu"

"ujinga gani huo chidi jamani, mbona unanikata mudi"

"kweli kuna shida imetokea hivyo nakuomba mamy"

Chidi aliweka simu pembeni wakati huo miriam na halima walikuwa wanacheka mno, yaani miriam tayari keshazoeana na halima ndani ya dakika chache tu..

Punde sii punde gari inaingia nyumbani kwa chidi,.. Miriam anashuka kwenye gari huku akiwa kampakata halima,..

Na chidi nae kashuka na kuzima gari

Lakini miriam alishtuka kwa kuona viatu vya kike, tena haviukuwa vya kitoto,… Unajua miriam yeye anajua chidi kaachiwa gari na mama sarah lakini hajui kama mama sarah yupo ndani,.. Yaani anajua kaachiwa tu gari,..

"omary.. We omary"

"nini tena si uingie"

"hebu njoo babuu"

"nini…"

Chidi alitoka nje tena mana alikuwa keshaingia

"hivi viatu ni vya nani"

Sasa mama sarah nae kasikia sauti ya kischana schana, ikamshawishi atoke ili amuangalie huyo mschana anaeongea na chidi, mana chidi alimtumia mama sms na kumwambia kuwa anakuja na mdogo wake,.. Sasa mdogo gani mkubwa hivyo, sasa mama sarah ile anapanua pazia aone huyo mdogo wake chidi,..

Alishangaa kumuona ni mtoto wa rafiki yake, tena anaheshimiana nae kupita maelezo,.. Sasa miriam nae kupiga jicho kamuona mama sarah,… Na alikuwa hajui kama atakuwepo huku ndani japo kajua kuwa gari ni yake, lakini hajui kama atamkuta humu ndani..

"we miriam umekuja kufanya nini huku"

Aliuliza mama sarah huku akitoka nje ili aulize vizuri… Wakati huo miriam kimyaa

"si nakuuliza we mtoto, umefuata nini huku"

Mama sarah alikuwa anachimba mkwara lakini hata yeye alikuwa anaona aibu kukutwa ndani tena peke yake kwenye chumba cha kijana ambae hajaoa..

INAENDELEA...

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
51 Muuza Chips Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni