Notifications
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…
  • MY DIARY (20)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINITULIPOISHIA...Nikamwambia kuhusu namba zangu za simu amuombe aliyemtuma anisaidie na kuhusu hilo la pili je hatuwezi kufanya kesho kwa sababu kuna mahali nilikuwa nikienda? Alifikiria kwa sekunde kadhaa na kuniambia kuwa hapana anaomba nimsaidie leo kama yeye alivyonisaidia mimi kwa sababu ningekuwa kwenye foleni nisingeweza kuondoka kirahisi hivyo kama ninavyofikiria.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (19)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TISATULIPOISHIA...Baada ya hapo niliendelea kumdadisi juu ya tukio lile lakini hakuwa tayari kufunguka zaidi ya kusema aliumia sana. Hapo nikaamua kuutafuta ukweli kwa kutumia mbinu za kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilimwekaa mikono begani na kumwambia pleaee dear naomba uniambie ukweli ili nijue nakusaidiaje? Basi Ramadhani akaanza kulalamika kuwa baba yake amekuwa akimwingilia…
  • MY DIARY (18)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA NANETULIPOISHIA...Halafu eti akawasha simu na kuonesha zile picha alizotupiga kweli huyu rafiki yangu alikuwa hamnazo sio picha tu alituchukua video kabisa na sauti. Akanambia ngoja ampigie paparazi mmoja hivi aje ili atengeneze habari tupate hela. Kauli hiyo ilinikosesha amani na kunikera sana akanmabia eti kuna namna ya kufanya ili sura yangu isitokee.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (17)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SABATULIPOISHIA...Nilijifikiria mara mbili nikajikuta namkubalia kwani alionekana ni mpole na mstaarabu sana.Basi tukaenda hadi kwake ambapo haikuwa mbali na hapo tulipokuwa na kweli alikuwa na chumba na sebule na sebuleni kwake niliona picha ya ukutani akiwe yeye na mke wake nahisi ilikuwa siku ya harusi yao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikasema huyu kijana atakuwa amefunga ndoa…
  • MY DIARY (16)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SITATULIPOISHIA...Mwanamke akaamua kuingia jikoni na kukarangiza viazi na nyama rosti na kilipoiva kililetwa mezani tukaendelea kujenga afya. Sikuaamini kama Joyce alikuwa anakumbuka hata kupika kwa sababu alibadilka sana na alikuwa akiishi maisha ya starehe.. Lakini aliniprovu wrong kwa kutoa rost ya hatari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baada ya kula alinambia kuwa alikuwa amechoka…
  • MY DIARY (15)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TANOTULIPOISHIA...Hapo mzungu wa watu hakuweza kuvumilia tena aliichomeka yote.Mmmmmh mmmmmh ishiiiiiiiiiiii yeaaaaaahhhhhhhh yeaaaaaaah ni miguno niliyoitoa mara baada ya kusikia joto tamu la kiungo hicho.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Ikabid nijivute kwa nyuma ili lengo likiwa ni kukaa vizuri ili kichwa cha nyoka kiwe juu juu ya pango langu ili niweze kukisugua sawa sawa na pia…
  • MY DIARY (14)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA NNETULIPOISHIA...Nikamuuuuliza hivi wewe haugopi maradhi? Akanijibu kuwa angekuwa haogopi basi angeshakufa. Sikiliza Leah hapa nipo na vile vipimo vya ukimwi hivyo usiwe na wasiwasi tutapima wote wanne kama wapo fresh tutaingia kazini wewe si unatafuta hela ya kujiunga na chuo au?IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kabla sijajibu akanambia nitakupa na dawa ya kumeza ya kuzuia mimba na pia…
  • MY DIARY (13)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TATUTULIPOISHIA...Joyce akaanza kujimiminia mwenyewe, kweli dunia ina mambo wakati wenzake wakichanganya nay ale maji makubwa yeye alikuwa akinywa kavu kavu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi mimi sikuwa na jinsi zaidi ya kuaagiza ile bia yangu ambayo alinifundisha yaani savanna. Safari hii hakusubiri ili ifike mwisho ili anitambulishe bali tulivyoanza tu kunywa akawaambia wale…
  • MY DIARY (12)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MBILITULIPOISHIA...Niliamua kufanya ziara ili nijue pakoje na mwisho wa siku niliamini kuwa kutokana na umaarufu wa marehemu baba yangu isingekuwa kazi sana kulipata shamba lake..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilitembea kijiji hadi kijiji huku nikijaribu kuuliza kwa wenye viti wa mtaa kama walikuwa wakimjua marehemu Bura. Kwa kweli kazi ilikuwa ngumu sikuweza kuvimaliza vijiji…

JULIANA (5)

Jina: JULIANA

SEHEMU YA TANO
ILIPOISHIA...
Alikuwa na kila kitu, utajiri, alikwenda alipotaka kwenda lakini suala la kutokuwa na mtoto ndilo lililokuwa likimtesa usiku na mchana, kitendo cha mkewe kusema kwamba alihisi alikuwa na mimba, kikampa furaha tele.

Baada ya wiki mbili, akaenda kupima, akaambiwa kwamba alikuwa mjauzito kitu kilichompa furaha.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
Mapenzi yakaongezeka, kila wakati Gideon alikuwa akimpigia simu mkewe kumjulia hali. Alimuomba Mungu kila siku kwamba siku ya kujifungua mkewe ajifungue salama kabisa.

“Hamjambo!” alisalimia Gideon huku akimwangalia mkewe.

“Hatujambo?”

“Ndiyo! Si mpo wawili! Wewe na huyo hapo,” alisema Gideon huku akicheka.

“Hahah! Hatujambo! Tumekumisi tu!”

“Kweli?”

“Yeah! Hasahasa huyu hapa,” alisema Juliana huku akimuonyeshea mumewe tumbo lake.

Gideon akamsogelea, akalishika na kisha kuweka sikio lake katika tumbo lile. Lilikuwa dogo, halikuanza kuonekana lakini kwake hakutaka kushindwa, alihitaji kuonyesha mbwembwe zote hata kabla mtoto hajazaliwa.

Kutokana na furaha kubwa aliyokuwa nayo, Gideon akaanza kuwaambia marafiki zake wengi kuhusu ujauzito ule, kila alipotembea alijiona kuwa kidume kwani kulikuwa na wanaume wengi ambao hawakuwa na watoto, kwake, alijiona kuwa na nguvu kuliko wote.

Malenzi mema kwa mkewe yakaongezeka, akazidi kumjali, mapenzi yakanoga sana mpaka alipotimiza miezi tisa na hatimaye kwenda kujifungua, akafanikiwa kupata mtoto wa kike waliyempa jina la Jesca.

“Ni mtoto mzuri sana,” alisema rafiki yake huku akimwangalia mtoto huyo.

“Kweli?”

“Yeah! Kachukua kila kitu kutoka kwa mama! Ila hivi vikono hivi ni vya baba pyua,” alisema rafiki huyo na kuanza kucheka.

Hiyo ndiyo ikawa furaha yao, ndiyo ikawa mwanzo wa kupendana zaidi na zaidi. Gideon hakuwa akitulia kazini, kila siku alikuwa akirudi nyumbani mapema kabisa, alipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumbeba mtoto wake, kwake alikuwa kila kitu, alikuwa tayari kupoteza kila alichokuwa nacho lakini si mtoto huyo.

Wakawa karibu zaidi na mtoto wao, walimpenda na kumpa kila kitu alichotakiwa kupewa. Miezi ikakatika, siku zikaenda mbele, waliendelea kumpenda kila siku huku wakiahidi kumfanyia mambo mengi katika maisha yake.

Alipofikisha umri wa miaka miwili, akaanza chekechea katika Shule ya Watoto ya Livingstone Day Care ambayo ilikuwa ikisomwa na watoto wa matajiri tu. Walitaka kumpa elimu bora, hawakupenda kumuona akipokea elimu ya kawaida kwa kuamini kwamba hakukuwa na kitu ambacho kingemkomboa zaidi ya kuwa na elimu tu.

Mtoto alipofikisha miaka minne, wakapanga kupata mtoto mwingine kwa kuwa tayari Jesca alikuwa mkubwa. Wakajadiliana na kukubaliana kwamba kusingekuwa na tatizo lolote lile kama tu wangepata mtoto wa pili.

Zoezi lao lilichukua miezi mitatu lakini hakukuwa na majibu yoyote yale. Kila mmoja alishangaa, walijitahidi sana, walikuwa vyakula vingi vya kuirutubisha afya zao na vizazi vyao lakini Juliana hakufanikiwa kushika ujauzito.

Walipoona kila kitu kimeshindikana ndipo wakaamua kwenda hospitalini kuona kama kulikuwa na tatizo lolote lile.

Walipofika huko, daktari akawapima na baadaye kuwapa matokeo ambayo yaliwashtua wote wawili.

“Hamtoweza kupata mtoto,” alisema daktari huku akiwaangalia wote wawili.

“Kwa nini?”

“Mkeo ana kansa ya kizazi,” alijibu daktari huyo huku uso wake ukionyesha huzuni kubwa.

Hawakuamini kile walichokisikia, walimwangalia daktari yule, mioyo yao ilichoma kupita kawaida. Juliana akahisi moyo wake ukichoma kuliko kawaida, akayafumba machoo yake na kuanza kulia.

Hakuamini kwamba alikuwa na kansa ya kizazi, daktari akawaambia kwamba haikuwa imekomaa hivyo kulikuwa na nafasi ya kuiwahi kitu kilichowafanya kuanza kuhangaikia tiba.

Walikwenda kila kona, Juliana alitumia dawa za kila aina lakini kitu cha ajabu ni kwamba hakufanikiwa kupona kansa ile ambayo ilikuwa ikiendelea kumtafuna kila siku.

Ugonjwa ukampa mawazo, kila alipokuwa akikaa, mawazo yake yalikuwa katika ugonjwa huo uliokuwa ukimtesa kila siku. Moyo wake ulimuuma mno, hakukuwa na mtu wa kumfariji zaidi ya mume wake mpendwa.

Gideon alihuzunika, kila alipomwangalia mke wake, moyo wake ulimuuma mno. Juliana alimsikitisha, alikuwa akikonda, mawazo yalimtesa na kila wakati aliona kabisa kwamba angekufariki dunia.

Alimuonea huruma mume wake, alikuwa akihangaika mno, kila kulipokuwa na tetesi kwamba dawa ilikuwa ikipatikana, alikwenda huko. Alinunua dawa za kila aina, kwa Wachina, Wakolea na nyingine za asili ilimradi mke wake apone kansa ile lakini haikusaidia kitu.

Alihuzunika, wakati mwingine alipokuwa ofisini, aliufunga mlango na kuanza kulia. Moyo wake ulichoma mno, wakati mwingine alimwambia Mungu kwamba lile jaribu alilompa lilikuwa kubwa mno na asingeweza kulibeba peke yake.

“Mungu! Hili ni jaribu kubwa sana! Nitawezaje kulibeba?” alimuuliza Mungu huku akiwa ofisini kwake.

Kila alipokuwa alimfikiria mke wake, Juliana. Aliona kabisa hizo ndizo zilikuwa dakika za mwisho kumuona mke wake huyo akiendelea kupumua. Hakuacha kuomba, alisali kwa nguvu zote, aliamini kwamba kuna siku Mungu angetenda muujiza na mke wake kurudi kwenye hali ya kawaida.

“Mke wangu! Una imani kwamba utapona?” aliuliza Gideon huku akimwangalia mke wake.

“Nina imani nitapona, ila….” Alisema Juliana.

“Unaposema ila inaonyesha huna imani! Naomba uwe na imani mke wangu!

Mungu wetu ni mponyaji, kama alimponya mwanamke mwenye baada ya kushika vazi la Yesu Kristo, kama aliwaponya vipovu, kansa ni nini mbele yake? Amini kwamba Mungu ni mponyaji, unachotakiwa ni kuamini kwani mungu hufanya kazi na wanaoamini,” alisema Gideon huku akimwangalia mke wake huyo.

Japokuwa aliambiwa maneno mengi na mume wake kwamba alitakiwa kuamini lakini moyoni mwa Juliana hali ilikuwa tofauti kabisa. Kichwani mwake zikaja picha za watu mbalimbali waliokuwa wakiugua kansa na mwisho wa siku kufariki dunia, hakuona kama angepona, aliamini kwamba mumewe alikuwa akimwambia maneno mengi kama kumtia moyo lakini ukweli ni kwamba asingeweza kupna.

Alilia mchana kutwa, moyo wake uliendelea kulia. Kila alipomwangalia mtoto wake, Jesca moyo wake ulimuuma, alikuwa mtoto mdogo ambaye bado alihitaji malezi kutoka kwake, hakujua angefanyaje kama angekufa, hakujua ni kwa jinsi gani mtoto wake huyo angeumia usiku na mchana.

Miaka ikakatika, hali yake ikazidi kuwa mbaya, ugonjwa ule ulimtesa na mwisho wa siku kuanza kutafuna nywele zake. Zinaanza kunyonyoka, akaanza kubaki na upara kichwani. Alitia huruma, aliumia mno kwani hizo zote zilikuwa ni dalili kwamba asingeweza kupona tena.

“Mke wangu! Amini kwamba Mungu anaweza kukuponya,” aliisikia sauti ya mumewe moyoni mwake.

Akahisi akipata nguvu kubwa, akaanza kuingiwa na kumbukumbu za watu waliokuwa wakiumwa sana na mwisho wa siku kuponywa. Kama Mungu aliiumba dunia, kama Mungu aliumba binadamu wote duniani, ilikuwaje kuhusu ugonjwa wa kansa, angeshindwa vipi kumponya mtu aliyekuwa na ugonjwa huo?

“Mungu naomba uniponye,” alisema Juliana huku akiwa amepiga magoti.

Alimuomba Mungu kila siku, alimuamini kwamba kuna siku angemponya tena lakini hilo lilionekana kuwa gumu kutokea. Mwili wake ulizidi kudhoofika, kansa iliendelea kusambaa na mbaya zaidi wakati mwingine alikuwa akitoka damu nyingi sehemu za siri kama mwanamke aliyeingia kwenye simu zake.

Hilo ndilo lililomtesa zaidi, likamfanya kukaa ndani, akajifungia, hakutaka kutoka kwani muda wowote ule damu zilikuwa zikimtoka sehemu za siri. Huo ndiyo ulikuwa msiba mkubwa, aliomboleza kila siku, wakati hali ikiwa imekuwa hivyo, wakati ambao alikuwa akihitaji sana msaada na faraja kutoka kwa mume wake, hapo ndipo Gideon akaanza kubadilika.

Hakuwa karibu naye kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, alichelewa kurudi nyumbani kitu kilichomfanya kuwa na maswali mengi juu ya kitu kilichokuwa kikiendelea kwa mumewe.

Alitamani sana kuzungumza naye lakini mwanaume huyo hakuwa na muda. Moyo wa Juliana ulimchoma, japokuwa alikuwa na maumivu makali katika mwili wake lakini kufanyiwa vitu kama hivyo na mwanaume aliyempenda kwa moyo wa dhati kwake ilikuwa ni zaidi ya maumivu.

Alilia, hakuna aliyemfuta machozi, alihuzunika, hakukuwa na wa kumfariji. Wakati mwingine aliisikia sauti moyoni mwake ikimwambia kwamba aachane na mumewe kwa kuwa alikuwa amepata mwanamke mwingine lakini Juliana hakutaka kukubaliana na hilo.

“Gideon! Hapana! Hawezi kuwa na mwanamke mwingine,” aliibishia sauti aliyokuwa akiisikia moyoni mwake.

“Aya! Utakapoletewa mwanamke ndani ya nyumba ndipo utakapoamini kwamba amepata mwanamke mwingine, tena mzuri zaidi yako, na ana afya nzuri sio kama wewe goigoi ambaye muda wowote ule unakufa,” aliisikia sauti hiyo maneno ambayo yaliuchoma moyo wake vilivyo.

Kansa iliendelea kumtesa Juliana, hakuwa na furaha, muda wote alikuwa akilia, alimuomba Mungu kumponya kansa ile au kubadilisha kila kitu na mwisho wa siku kugundua kwamba kila kilichoendelea kilikuwa ndoto.

Alimpenda sana mume wake, Gideon lakini kwa kipindi hicho mwanaume huyo alikuwa bize na mambo yake, upendo uliondoka, akawa anachelewa kurudi nyumbani, hakutaka kabisa kuona akiendelea kuwa na mwanamke mgonjwa kama alivyokuwa Juliana.

Moyo wa mwanamke huyo ulimuuma kupita kawaida. Bado aliendelea kutoka damu sehemu za siri, aliumia, alihitaji msaada kutoka kwa mume wake lakini mwanaume huyo hakuwa na muda naye.

Wakati mwingine akawa anampigia simu, hakuwa akipokea na hata alipomtumia ujumbe kwenye simu yake mwanaume huyo hakuwa anajibu kitu kilichomfanya kujisikia vibaya mno.

Wakati Juliana akiteseka kitandani, Gideon alikuwa kwenye penzi la mwanamke mwingine aliyeitwa Juliet. Lilikuwa penzi jipya, penzi lililochipukia kwa kasi kubwa, penzi ambalo lilimfanya kuanza kumsahau mke wake.

Alihitaji faraja, alihitaji kulala na mwanamke, mkewe hakuwa akiweza kufanya kitu chochote kile, alionekana kama sanamu hivyo kwa hali aliyokuwa akipitia ilikuwa ni lazima kutafuta mwanamke mpya ambaye angeufanya moyo wake kuwa na furaha muda wote.

Akawa akitoka na Juliet kwenda sehemu mbalimbali, alikuwa na pesa, alitumia pesa zake kumfurahisha msichana huyo pasipo kumkumbuka mwanamke ambaye alichuma naye.

Kila alipokuwa na Juliet, Juliana alikuwa akipiga simu, aliichukua simu yake na kuangalia, alipoona jina la mke wake, alicheka sana na kumuonyeshea Juliet ambaye alimwambia amsahau mwanamke huyo kwani hakuwa chochote kile.

“Achana naye!” alisema Juliet.

“Ndiyo ninachofanya. Unajua namchukia sana yule mwanamke,” alisema Gideon huku akionekana kuwa na hasira.

“Jamani! Basi tukampoteze,” alishauri Juliet.

“Tumpotezaje?”

“Tumuue!”

“Sawa. Ngoja nikafanye mipango, mwanamke yule hatakiwi kuishi. Kwanza pale alipokuwa tayari maiti,” alisema Gideon.

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
53 Juliana Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni