SALAMU KUTOKA KUZIMU (11)

0
Mtunzi: ___

SEHEMU YA KUMI NA MOJA
TULIPOISHIA...
Pengine tatizo lingetokana na viongozi wake huko Ugaibuni. Labda ni wao wangeweza kumpinga kutokana na woga wao. Lakini mpango huo ulikuwa wake binafisi, ameubuni, ameuandaa na lazima autekeleze. Imekwisha mgharimu muda na pesa nyingi, zake binafsi wakati akiuhakiki.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Yeyote asingeweza kumshawishi abadili mpango wake, zaidi ya hayo, hakumbuki lini waliwahi kupewa changamoto nzito kama hiyo. Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Zaire (Congo), Patrice Lumbumba? Kuuawa kwa Rais Nguabi? Unyama aliofanyiwa Edward Mondolane wa Msumbiji? Hapana. Yeye Proper atafanya zaidi ya hayo. Ataifanya dunia ielekeze macho na masikio hapa.

Kengere ya mlango iliita tena. Ni nani huyo? Proper alijiuliza akificha vifaa vyake vyote. Haraka na kwa utaalamu aliuvua uso wa Proper na kujivika ule wa Profesa Chain Kimara wenye dalili zote za hekima na mshughuriko, uso uliomlaki Neema Iddy aliyekuwa amesimama mlangoni akijiandaa kubonyeza kengere kwa mara ya tatu.

“Karibu mama”, Proper alisema huku akisimama kando kumpisha mgeni wake apite. Kichwani alikuwa kajawa na mshangao mkubwa. Sura nzuri ya msichana huyu haikuwa ngeni machoni mwake ingawa hakuwahi kuiona sura hii ana kwa ana kwa leo. Ilikuwemo katika majarada yake. Ilikuwa sura ya Neema, Katibu Mahsusi wa Joram Kiango. Amewezaje kunishuku mapema kiasi hiki? Proper alikuwa akijiuliza. Si kitu, alijiambia. Nilikosea sana kumsahau. Alistahili kufa kitambo. Alistahili kwenda na Joram. Madaamu kajileta mwenyewe.
“Dada, karibu ndani”, Proper alimhimiza Neema.

“Asante, lakini sikai. Nilitaka… Ni…” Neema alikwama kidogo. Uso uliokuwa mbele yake hakuona kama ulifaa kusumbuliwa kwa maswali yaliyoeleweka. Aliuona kama uso wa msomi mwenye hekima na mengi, ingawa macho yake yalikuwa na kitu zaidi ya uso, alijiona mpumbavu kuja hapa bila subura. Huyu haelekei kuhusika katika kifo cha joram.

“Haraka ya nini?” Proper alimkatiza huku akimtengenezea tabasamu ambalo lilimtoa hofu Neema. “Utaingia ndani, utakaa, unywe walau chupa moja ya bia kisha tutaongea”.

“Hapana, hapana”, Neema alimkanusha, “Sitaki kuupoteza bure muda wako. Nilitaka ku…”

Alikatizwa tena, akashikwa mkono na kuvutwa ndani kistaarabu. Akaonyeshwa kiti ambacho aliketishwa polepole.

“Sikai sana. Samahani kwa kukupotezea muda wako, Nilitaka kujua kama unajua chochote kuhusu Joram Kiango?”, alifaulu kuuliza.

“Joram! Namjua sana. Sidhani kama yupo mtu asiyemjua, Kifo chake kimenishtua sana. Alikuwa kijana wa ajabu sana”. Kisha Proper alijitia kushituka kidogo alipouliza, “Unadhani ni kweli Joram Kiango kafa hivi hivi tu? Mimi siamini. Nadhani wamempa sumu. Wewe waonaje?” Neema alipochelewa kujibu, Proper alijitia kushituka tena, “Lakini wewe ni nani? Na ulitaka mimi niseme nini kuhusu Joram au unataka mawazo gani kutoka kwangu?”.

Neema alijiona mjinga zaidi. Huyu msomi wa watu alionekana hajui lolote. Yawezekana yule mwanamke wa ajabu, Unono, alikuwa punguani pia. Picha ya mzee huyu pengine aliiokota au kuiiba mahala na kuileta kwake. Mzee huyu hakuonekana kujua chochote cha muhimu juu ya kifo cha Joram.

Haraka Neema akainuka na kuaga.

|Haraka hii? Proper alihoji kwa mshangao. Safari hii alionyesha mshagao halisi. Alikuwa akitafuta nafasi nzuri ya kumtia Neema mikononi mwake. Japokuwa kiti alichokalia Neema kingeweza kutimiza wajibu wake lakini Proper hakukusudia kutumia njia hii. Na njia hii ilikuwa rahisi zaidi. Proper angeweza kukanyaga mahala fulani chini ya meza kisha voti kadhaa za umeme zingepita katika kiti hicho na kumwua Neema papo hapo. Hakufanya hivyo kwa sababu mbili. Mosi, alikuwa bado hajafahamu msichana huyu anajua nini na anataka nini kwake, na pia hakutaka Neema afie nyumbani kwake.

“Huwezi kuondoka bila kunywa chochote? Siwezi kuruhusu binti mzuri kama wewe atoke nyumbani kwangu pasi ya kuonja chochote, Vilevile hatujazungumza”.

“Samahani. Sijisikii kunywa chochote”.

“Na uichotaka kuuliza juu ya Joram?”.

“Nimebadili mawazo”.

“Kwanini?”.

Huku akianza kutoka ndani ya nyumba hii Neema alisema, “Nilikosea…”.

Hakujua kilichompiga. Hakusikia maumivu yoyote. Alijikuta akianguka polepole huku Profesa Chain akimtazama kwa kicheko cha kebehi. Hakuwa na uwezo wsa kupiga kelele japo alijaribu, akahisi fahamu zikimtoka taratibu.

Neema aliposhutuka kutoka katika usingizi mzito, alijikuta amelala kitandani akiwa uchi, kando Proper alikuwa amemkumbatia kwa mkono mmoja huku mkono mwingine ukizichezea chuchu zake. Lakini pia ulimi wa Proper ulikuwa katika kinywa cha Neema. Neema alishituka na kujivuta kando kwa nguvu huku akitamka maneno ambayo hayakusikika kikamilifu. Hata hivyo hakufaulu kujitoa katika mikono yenye nguvu ya Proper ambayo ilizidi kumbana.

“Bado kidogo mpenzi”, Proper alisema, “Tutafanya mara moja zaidi kisha nitakuruhusu utakwenda zako”, Sauti ilifuatiwa na kicheko ambacho katika masikio ya Neema kilijaa jeuri na kebehi.

“Nini kinatokea hapa?” Neema alifanikiwa kuuliza swali, huku mshangao ukimtoka na aibu ikianza kumwingia.

“Tunafanya mapenzi, ndio maana nikasema bado kidogo halafu nikuruhusu uondoke zako”, Proper alimjibu Neema.

“Mapenzi!” Neema alihoji huku akifoka. “Nitakushitaki”, Neema alifanikiwa kumwambia Proper.
“Kwa nani?”.

“Umeninajisi. Umenitenda pasi hiari yangu. Siwezi kuvumilia upuuzi huu, nitahakikisha unafika kwenye vyombo vya sheria”, Neema alisisitiza.

Kicheko kingine kikamtoka Proper. “Usiwe kama mtoto mdogo”, alisema Proper akiendelea kucheka, “Nani atakuelewa? Zaidi, nani atakuamini? Ulivyo mrembo kila mmoja ataamini kuwa unatosha kabisa kumfanya Profesa yeyote mwenye hisia asahau majukumu yake kwa muda ili afanye mapenzi na wewe. Nani atakanusha nikisema kuwa jana tulikutana mitaani tukaahidiana uje leo na umekuja? Au kuna yeyote aliyeniona nikikuvuta huko nje na kukuleta hapa ndani?”

Maneno hayo yalimwingia Neema. Hakuona uwezekano wowote wa kuifanya hatia ya mtu huyu idhihirike . Lakini alikuwa na hofu moyoni. Si hofu ya kufanya mapenzi bila kukusudia. Hofu yake ilitokana na kutofahamu kitu gani kilimfanya apoteze fahamu na kuvuliwa mavazi na … Pia hofu ilimzidi kwa kutokuwa na hakika na yote yaliyofanyika baada ya kupoteza fahamu. Ilikuwa kama ndoto ya kitambo anayokumbuka kwa shida. Ilikuwa kana kwamba ananusa harufu iliyomfanya apoteze fahamu. Pia, alikumbuka kuwa alimsikia mtu huyo alipokuwa akimhoji kuhusu kifo cha Joram Kiango, naye akiropoka kila kitu alichofahamu. Alimweleza juu ya yule mwanamke mwenye sura mbaya ambaye aliileta picha yake. Kisha alikumbuka kuwa alinyweshwa kitu fulani na kuambiwa, “Hiyo itakufanya usafiri leo hadi aliko mpenzi wako Joram. Usisahau kumsalimu. Baada ya hapo ndipo nguo zilipovuliwa. Akaletwa kitandani ambako…

“Pamoja na kufanya mapenzi”, Profesa Kimara, au Proper alikuwa akiendelea, “Nitakulipa vema, Sina mkono wa birika , hususan kwa mabinti awzuri kama wewe. Umenifanya nimsahau mke wangu aliyefariki miaka kumi iliyopita”. Alisema huku akiushughulisha mkono wake kutambaa kutoka katika matiti ya Neema hadi tumboni mwake, mkono huo ukateleza hadi katikati ya miguu ya Neema.

Neema akausukuma mkono huo kando na kujiinua kwa nguvu. “Sijapata kumwona mtu mshenzi kama wewe”, alifoka kwa hasira akiyaendea mavazi yake yaliyokuwa juu ya kochi.

“Kwanini mpenzi? Nipe nafasi nyingine uone jinsi nilivyo mstaarabu katika suala zima la mapenzi. Tafadhali. Mara moja tu halafu utakwenda zako…”.

Sauti ilikuwa ya mapenzi. Ni tabasamu lake ambalo lilibeba kitu kingine kabisa. Kitu kisicho karibu na mapenzi hata kidogo. Kitu ambacho kilikuwa kinyume kabisa na mapenzi na mahaba. Jambo ambalo lilimuongezea hasira Neema. Alizivaa nguo zake haraka haraka, Akautwaa mfuko wake na kuanza kutoka.

“Siku yoyote ukijisikia tena kufanya mapenzi unakaribishwa”. Proper alisema huku akifungua pochi lake na kutoa kiasi cha pesa.

“Sihitaji chochote kutoka kwako”, Neema alifoka huku akitoka.

Alipofika kituo cha basi alifungua mkoba wake kuangalia. Kila kitu kilikuwa sawa isipokuwa bastola yake! Hakujua cha kufanya.

Alipofika nyumbani, Neema aliketi juu ya sofa akajaribu kufikiri, mara akahisi hana nguvu za kufikiri lolote. Alichokitaraji ni pumziko tu. Mara akausikia usingizi mzito ukimnyemelea. Kitanda alikiona mbali. Akajinyoosha juu ya kochi usingizi mzito ukamchukua.

Ulikuwa usingizi wa aina yake. Ulimchukua moja kwa moja na kumtoa katika dunia hii na kumpeleka katika dunia nyingine. Dunia yenye kiza kizito. Dunia isiyo na hisia.

Unono alipoingia alimkuta Neema katika usingizi huo. Awali hakufahamu kinachotokea. Akapoteza dakika kadhaa akilihusudu kwa wivu umbo zuri la Neema ambalo lililala kifudifudi juu ya kochi. Kisha akapoteza dakika zingine kadhaa akijaribu kumwamusha kwa kumsukuma. Mara akaiona damu nzito iliyokuwa ikimtoka Neema midomoni na puani, Ulimi ulivyoponyoka kutoka kinywani na kuduwaa nje, upande mmoja. Akayaona macho yalivyotoka nje. Kila kitu kilitangaza mauti ya Neema.

“Amekufa”, Unono alifoka huku akiruka kurudi nyuma.

Kifo. Unono alikifahamu sana. Alikifahamu sana toka wazazi wake wote wawili walipokufa kwa ajali ya gari wakati huo akiwa na umri wa miaka mitano tu. Alikifahamu kifo miaka minne baadaye wakati shangazi yake aliyekuwa mlezi wake wa pekee, alipofariki kwa kipindupindu. Naam, alikifahamu kifo na madhara yake. Lakini hakupata kuwa karibu na kifo kiasi hiki. Hakuwahi kumugusa mtu aliyekata roho na kumsukasuka. Hivyo, alipouondoa mkono wake juu ya mwili wa Neema, aligeuka na kuanza kutoka nje mbio, huku akipiga kelele.

Hakwenda mbali kabla ya kutokea gari yenye dereva mwenye haraka zake, ambayo ilimgonga Unono na kumwua pale pale.

Watu walioshuhudia ajali hiyo, hasa baada ya kumuona alivyokuwa akikimbia hovyo barabarani, na kumuona alivyokuwa, waliamini mara moja kuwa alikuwa ‘Mwendawazimu mmoja’ amegongwa na gari na kufa.

                        ******************************

Miongoni mwa watu walioshuhudia ajali hii ni Proper. Kama watu wengine yeye pia ajali hii ilimsikitisha. Tofauti ni kwamba yeye hakusikitika kwa kuona maisha ya binadamu yakiteketea ghafla katika hali ya kutisha kama hiyo, la. Kwanza hakuna jambo lolote lililomsisimua katika maisha yake zaidi ya kumuona mtu akikata roho. Hakuna mchezo alioupenda au kuujua zaidi ya kuua ama kushuhudia kifo.

Proper alisikitika kukosa fursa na kuzungumza na Unono ili kujua yote anayofahamu juu yake na wapi alikopata picha ambayo Neema aliizungumzia wakati alipomhoji baada ya kumlewesha kwa dawa zake.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)