MUUZA CHIPS (65)
Sehemu ya Sitini na Tano, na hii kazi, na mama saida, sarah na mama, mama sarah na, akianza kukasirika kana, ana nia ya, anapkonywa tonge mdomonimama
Zephiline F Ezekiel
6 min read
Mwandishi: MoonBoy
SEHEMU YA SITINI NA HAPA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Na yule mmoja alienda kwenye gari na kupuliza sumu ya umbea… Yaani waanze kuonge umbea umbea ili vicheko viwe vingi mpaka yule dereva ageuke nyuma… Hivyo kinachotafutwa ni dereva ageuke nyuma kwa utamu wa vicheko vya mama zake…. Baina ya mama sarah na mama saida…..
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Sasa huku ndani ya gari, yule mmoja akafanikiwa kumwaga sumu ya umbea mule ndani ya gari na ni kweli, umbea ulianza hivi…..
"sasa tulieni nimuage kamwisho mana ndio mwisho wa kuwa nae tena"
"we muage tu baby wako wala hatuna shida nae"
"Chidi mpenzi wangu, naomba unisamehe sana, ni pesa ndio imenipelekea kufanya hivyo,… Ugua pole chidi wangu"
Mama sarah alipomaliza kumuaga chidi kwa kutumia picha,… Walianza kucheka wote wawili kwa kicheko cha kejeli huku gari ikiwa spidi kali kana kwamba hapo wamebakiza dakika 15 tu kufika kwa mganga kwa hio spidi wanayoitembelea wao ili kuwahi masaa saba yasiishe
"He heeeeeeeeee HaaaaaLooooooooo…. Mwenetu umeponaaaaa"
Sasa kumbe Dereva wa gari hio, ndio huyo huyo kijana mwenyewe anaekwenda kushughulikiwa nguvu za kiume,….
Sasa yeye nae alikuwa ana shauku sana ya kuongea na wamama hao waliokuwa wakicheka na kumtaja kuwa keshapona,… Sasa kile kicheko cha mama sarah na mama saida kilimfurahisha ridhiwani na kumfanya ageuka na wakati gari ilikuwa na spidi kubwa mno,…
"mama nashuku…… "
Sasa kabla ridhiwani hajamaliza kuongea neno kwa mama yake, ghafla mama kuna kitu kaona katikati ya barabara…
"wewe ridhi angalia mbele"
Maskini ya mungu ridhiwani alikuwa ni kijana mwenye huruma na binaadamu wenzie, kwani mbele ya gari hio palikuwa na mwanamke mzee aliokuwa akivuka katika barabara hio,.. Ridhiwani kwa umahiri wake alikata kona kubwa ili kumkwepa yule bibi kizee asimgonge,.. Kwa kufanya hivyo imekuwa ni kosa katika familia hio,.. Kwakuwa gari ilikuwa kwenye spidi kubwa ambayo ridhiwani alishindwa kuidhibiti,… Huezi amini gari ilibingilika mara tatu mpaka kichakani, sasa wakati huo pale kwenye gari ikiwa imetulia haijulikani kama watu wamekufa au wapo hai,
Lakini kulionekana wasamaria wema waliowahi kuwaseidi,…
Walikuwa ni watu wachache sana lakini huezi amini Eti walilileta gari mpaka pembezoni mwa barabara, kazi ambayo ilitakiwa ifanywe na katapila lakini wao wameweza,.. Lakini pia katika hao hao wasamalia wema kuna mmoja alionekana kuwa mwizi, kwani alikuwa akitafuta pesa katika mikoba ya akina mama hao na wakati huo mama sarah na mama saida pamoja na ridhiwani woote walizimia lakini hatujui kama wamezimia ama wamekufa, mana hawajatolewa katika gari,..
"kama huoni beba mkoba wote"
Aliongea mmoja kati ya wasamalia hao
"oohhh hiii hapa"
Waliona walichokuwa wakikitafuta, Lakini ghafla walitoweka katika mazingira ya kutatanisha,…
Sasa baada ya watu hao kuondoka ndio tunaona gari inatikisika kana kwamba kuna mmoja wao yupo hai,.. Alioanza kuamka alikuwa ni Ridhiwani,
"mama…. Mama… We mama amka"
Ridhiwani aliwaamsha wamama hao wote wakaamka na hakuna alieumia wala aliekufa, woote walikuwa wazima kabisaaaa
HIVYO NDIVYO ILIVYOKUWA, KABLA YA AJALI KUTOKEA, ILISABABISHWA NA NINI…. SASA TUENDELEE NA STORY YETU, IKIWA KUMBUKUMBU IMEISHIA HAPO… NADHANI KUANZIA HAPO ANAPOMUAMSHA MAMA YAKE, MNAJUA KILICHOENDELEA HAPO… SASA TUENDELEE NA STORY MBELE KWA MBELE
Tukija huku mjini kwa akina mama sarah na mama saida, wakiwa wapo hotelini wakijipongeza kwa kunusurika katika ajali iliokusudiwa, walikuwa hawaamini kama kweli wamepona,..
"mama saida,… Wewe usijali kushindwa kwa njia ya kwanza haimaanishi kuwa tutashindwa na njia ya pili"
Aliongea mama sarah huku akimfariji mwanamke mwenzie, kana kwamba wapo pamoja kwa kila jambo…
"usijali mama sarah, mimi mbona sina presha, ila tatizo ni mwanangu, anaumia sana pale anapoona wenzake wana wasichana"
"sawa….. Ila mama saida… Kule njiani uliniambia una wazo, je? Ni wazo gani hilo"
Aliongea mama sarah ili ajue kama ni njia mpya wajue waanze vipi,..
"kweli nina wazo juu ya kazi yako… Ila sijui kama utanielewa vizuri"
Mama sarah alishtuka baada ya kusikia hivyo mana anajua hapa kibarua kitakuwa kimeota nyasi…
"huyu mama saida anataka kuninyima hili dili nini…. Ina maana Bilioni moja nitaikosa hivi hivi… Haiwezekani aniachishe kirahisi kama ndio wazo lake"
Aliongea kimoyomoyo huyu mama saraha kana kwamba labda mama saida ana nia ya kuikatisha hii kazi ya kupata mbegu za kiume,.. Mama sarah hataki kuiacha Bilioni moja hata kidogo…
"mama sarah,… Najua kwa upande wako umri umesonga sana kama mimi mwenzio… Na hii kazi kwako nahisi kama nakuonea mama sarah"
Aliongea hivyo mama saida huku mama sarah akianza kukasirika kana kwamba anapkonywa tonge mdomoni…
"mama saida… Ina maana unataka kuniambia niachane na hii kazi jamani??"
Kweli mama sarah alikuwa ana nia ya kumuumiza kijana chidi, tena alikuwa hata hajali tena kama chidi ni kipenzi chake tena, kwa sasa alikuwa akiangalia pesa kwanza kisha ubinaadamu pembeni, sasa leo mama saida kachafukwa, anataka kumnyang'anya kazi mama sarah mana inachukuwa muda mrefu sana pasina kufanikisha lengo, Roho ilikuwa ikimuuma sama mama wa sarah huku akiwa kama haamini kama mama saida ataweza kumnyima hio dili ya bilioni moja, tena aliambiwa ataongezwa milioni 500 kwa hio pesa anayotumia kununulia hizo mbengu, mana chidi kakataa kuvaa kondomu mpaka apewe pesa
"mama sarah,… Najua kwa upande wako umri umesonga sana kama mimi mwenzio… Na hii kazi kwako nahisi kama nakuonea mama sarah"
Aliongea hivyo mama saida huku mama sarah akianza kukasirika kana kwamba anapkonywa tonge mdomoni…
"mama saida… Ina maana unataka kuniambia niachane na hii kazi jamani??"
Aliongea mama sarah huku akiwa kama kakasirika, mama sarah alikuwa hataki kabisa kuacha kuifanya kazi hio
"mama sarah, mimi simaanishi uiache kazi, ila kuna njia nataka kuitumia hapo"
"njia gani mama saida"
Aliongea kwa mshangao mama sarah kana kwamba ana shauku ya kujua njia inayotakiwa kutumiwa na mama saida…
"mwanangu saida, nataka nimshirikishe… Nama naona wewe unatumia pesa nyingi sana alafu hukamilishi mama sarah"
"mmmhhhh mama saida, katoto chako kalivyo kazuri vile unataka ukaingize kwenye haya mambo"
Mama sarah alianza kuwa na pingamizi kwasababu, saida ni mschana mzuri sana ambae hakuna hata mwanaume mmoja aneweza kuoisha na saida asimuangalie… Yaani mtoto mwenyewe kakaa kama muarabu sio muarabu.. Yaani ni Afrikast, (mtu aliochanganywa mbegu) saida ni mzuri haswa yaani ni kazuri vibaya mno, sasa mama saida yeye anataka kumtumia mtoto wake saida ili matumizi ya pesa kama alioitoa mama sarah yasiwepo tena,…
Sasa mama sarah hataki kitendo kama hicho mana hataki kijana chidi awe na mpenzi mwingine zaidi yake, haya leo aende akanogewe na kitoto kama hicho huoni hata mapenzi kwa mama sarah yatapungua…
"Kwahio kama mimi sitoki kwenye kazi, je kazi yangu mimi ni ipi"
Mama sarah aliuliza swali zuri sana kwa mama saida,
"mimi nataka wewe umuonyeshe saida huyo kijana"
"sasa kama ni hivyo, huoni malipo yangu yatapungua"
Mama sarah yeye alihofia malipo yatapungua
"wala hata hqyawezi pungua,.. Ila kazi yako ni kumuonyesha huyo huyo kijana na ikiwa tofauti, hapo sintotoa pesa"
"ok… Kwahio unaamini mtoto wako ataliweza"
"bila shaka, ataliweza. We unamwonaje saida"
"kweli saida ni mzuri, tena ni zaidi ya mzuri"
"najua hizo pesa hawezi kutumia kqma wewe ulivyotumia"
Mama sarah na mama saida walimaliza kikao chao hapo hotelini huku wakipata moja moto moja baridi,….
Tukija huku hitelini kwa akina miriam,… Maskini ya mungu miriam kama ni kupenda basi kazidisha upendo mara kadhaa, mana alikuwa hatulii katika kiti chake cha kibosi kila mara anakwenda jikoni kumwangalia chidi kama karudi,… Kila akitaka kumwandikia meseji anakumbuka vile alivyojibiwa kunya, afu akamwambia asubiri kwanza, hana hata hamu ya kutuma sms,… Kila mara miriam anakuja jikoni kuangalia kama mpishi huyo kesharudi ama vipi,.
"oya washkaji eee, mbona omari anauliziwa sana na huyu boss"
Aliuliza mpishi mmoja wa chipsi, na alimuuliza mpishi mwenzie
"aahhh si unajua omari ni mgeni hapa, afu isitoshe omari si ndio mpishi mkuu kwa sasa"
"Aaahaaaaaaaa sawa nimeelewa… Lakini kama ni chipsi mbona zipo bado au kuna kitu anataka apikiwe nini"
"wala tu, sema omari ni mgeni hivyo anachungwa sana mana anaonekana ni mtoro sana wa kazi"
"aahhh afukuzwe tu"
Kuna baadhi ya vijana hapo hitelini walikuwa hawampendi kijana chidi,… Walikuwa wakitamani afukuzwe ili hio nafasi aliopewa chidi apewe mmoja wapo,…
Tukija huku nyumbani kwa Ibrahim,… Mke wa Ibrahim akiwa anaongea na simu wakati huo wa jioni kama saa 11 hivi,
"wewe sabra umepanda gari gani mbona hufiki"
Mke wa Ibrahim alikuwa akiongea na simu, lakini alionekana ni yule mdogo wake aliomwambia kuwa aje huku Arusha amtafutie chuo, mana kafeli form four,..
"heeee dada mimi nimeshafika kitambo tu, sema nimepitia kwa mashost zangu"
"we mtoto mjinga kweli wewe, yaani mimi naumiza kiiiiichwa kumbe upo huko kwa felia wenzio… Ndio mana umefeli we mjinga sana"
"dada nakuja"
"fanya haraka giza linaingia hili"
"sawa nakuja"
Simu ilikata huku mke wa Ibrahim akiwa na hasira sana na mdogo wake,… Yaani kafika mapema lakini kapitia kwa mashostito zake,…
"huyu chidi mbona nae harudi jamani"
Mama king alijiuliza huku akiendelea kufanya kazi zake,… Wakati huo halima alikuwa akijisomea huko chumbani kwake…
Tukija huku kwa chidi, aliokuwa kashiba pesa, yaani hata kutoka hatamani kabisa, anahisi akitoka tu zile pesa zitaibwa,.. Kaganda huko ndani hataki hata kutoka, macho yake yoote yapo kwenye lile begi tu, na hapo alipo hata njaa hasikii ng'ooo mana pesa imejaa kwenye kibegi, milioni miamoja ulizani mchezo nini wewe, ukiipata hata wewe unaweza kupagawa, Sasa chidi akiwa hapo mara simu yake inaita, kucheki jina alikuwa ni shem lake,
"haloo shem"
"eee chidi jamani mbona hurudi"
"aaahhh leo nipo nyumbani bwana nyumba yangu imefubaa"
"kwaio leo huji"
"aahhh kwa leo siji wacha nilale huku huku"
"chidi jamani, au mtoto wa kike nini hapo"
"wala tu nipo peke yangu"
"njooo bwana nikupe"
"No, hata hivyo kama ningekuja nisingetaka"
"basi leo ulikuwa na demu wewe"
"ndio"
"haaaaaaaaaaaaaaa… Chidiiiiiiiiiiiiii, ina maana mimi sijakuridhisha ile jana"
"uliniridhisha sana ila sema nilikutana na kitoto kisu kweli nilishindwa kuvumilia"
"chisi we malaya eeee"
"heee shem unanitukana ivyo"
"no ni utani tu bwana usichukie"
"ok poa, but leo siji napumzika kwangu"
"mmmhhh sawa"
Simu ilikatwa huku chidi akiendelea kulala zake,… Na hapo hajala chakula cha mchana afu jioni ndio hio inakuja
INAENDELEA...
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni