Notifications
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…
  • MY DIARY (22)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILITULIPOISHIA...Alitumia vizuri umbo lake la kimiss kutembea kimiss na kuweka mapozi ya maana. Na baada hapo alilala kwenye kile kigodoro na akachojoa vyote isipokuwa kufuli jeupe ambalo nalo alipewa hapo hapo kwa ajili ya kazi hiyo. IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi sikumpa nafasi Joyce niliingilia nafasi yake na kuchukua ule uume wa bandia nikamfuta yule dada.…
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…

MTU WA UFUKWENI (2)

Mwandishi: Andrew Mhina

SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA...
Hilo halikumtisha na alimtahadharisha mkewe kutofuatilia chochote juu ya maneno ya majirani zao kusudi wasijenge uhasama zaidi. Busara ya kunyamaza ilimfanya ashinde na kurudisha hali ya urafiki kwa wale waliojaribu kujitenga nao kutokana na wivu.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
Kila wakati Dr.Kimbe alikuja nyumbani kwao na kuwasalimia wazazi wake huku akiwaachia kiasi kizuri cha fedha kwa ajili ya kulimia mashamba yao. Furaha yao ilizidi baada ya mtoto wao wa pekee kutaka kuoa. Walimsimamia kwa mambo yote na kumwozesha kwa furaha. Hatua hii ilifurahiwa sana na wazazi wake na baadhi ya wanakijiji.

Sherehe yake iliweka historia nyingine kwa kuwa ya fahari. Mbuge wa jimbo lao alihudhuria sherehe hiyo akiongozana na mkuu wa wilaya na marafiki zao. Msururu wa magari uliokuwepo wakati wa kuja na kuondoka baada ya harusi ni alama nyingine kubwa iliyowekwa katika historia ya wanakijini hao. Vyote hivi vilimfanya Dr. Kimbe kugoma kurudi kijijini kwao mara baada ya kufukuzwa kazina kutangazwa katika Hospitali zote.

Kosa hilo ambalo kiukweli halikuwa la kwake lilimtia fedheha kubwa na kumfanya akose amani katika maisha yake. Baada ya kutoka Dar-es Salaam aliazimia kushukia Korogwe katika kijiji cha Makuyuni alikokuwa amepewa shamba na babu yake mzaa mama yake. Alipangisha nyumba kijijini hapo wakati akishughulikia Ujenzi wa nyumba yake ndogo. Baada ya miezi sita alihamia kwenye nyumba yake ya vyumba viwili na sebule. wakati huo akiwa analima shamba alilopewa urithi na babu yake.

Taarifa za kufukuzwa kazi wazazi wake walizipata baada ya miezi miwili. Aliwaambia kwa njia ya barua na kuwataarifu kuwa yeye yuko makuyuni na kamwe asingekuja kijijini hapo kwa hali yake aliyonayo. aliogopa fedheha kwake na kwa wazazi wake waliojinyima kumsomesha. Taarifa hiyo iliwafadhaisha lakini wangefanyaje? waliendelea kumwombea mtoto wao ili apate kazi nyingine ya maana kuliko kutegemea kilimo cha mkono. Kiwango cha Elimu alichokuwa nacho hakikustahili kumfanya arudi kijijini kutegemea jembe la mkono. Mwaka wa pili baada ya kuwepo kijijini makuyuni, Mjomba wake aliyezaliwa na mama yake alikuja juu na kudai apewe shamba la baba yake. Maneno makali na kutishia kumpeleka mahakamani, vilimfanya Dr. Kimbe akubali kuachia shamba hilo. Hali hiyo ilisababishwa pia na kukosa japo maandishi kidogo kutoka kwa babu yake kuwa alimrithisha yeye. Kwa ujumla ni kwamba alipewa shamba hilo kwa kauli tupu isiyo na ushahidi wa maandishi.

Baada ya kunyang’anywa shamba lake alibadilika na kuwa zaidi ya maskini, kwani hakuwa na maarifa mengine zaidi. Hali yake ilikuwa mbaya sana, hadi kumpelekea mtoto wake Ramson kuzaliwa katika mazingira magumu kiasi hicho. Hali ya madeni ilizidi kuwa mbaya kiasi kutokana na vibarua alivyofanya vya shamba kutokukithi mahitaji yao. Hali hii ilisababisha mtoto wao kupata ugonjwa wa Utapiamlo. Mzee Kihedu alilia machozi siku aliyowatembelea kijijini hapo, hakuamini kumwona mwanaye katika hali hiyo. Mwisho wa yote aliamua kumshauri arudi kijijini Taabu ya nini.

“Baba kwakweli ningetamani nirudi, lakini nakwepa macho ya watu. Nitawaangalia vipi wanakijiji walioniona niko juu kimaisha na sasa narudi nikiwa na hali hii? Rafiki zangu niliowazidi elimu baada ya wao kufeli mitihani ya kujiunga na Elimu ya Sekondari, nitawaambia nini wakati nikijiunga nao tena kijijini kulima na kuchunga mbuzi? Na wewe baba yangu utajisikiaje baada ya kuhangaika kwa ajili yangu, mpaka kuuza baadhi ya mashamba yako kwa ajili ya kunisomesha?

Utasema nini tena wakati ukidhihakiwa na rafiki zako kwenye vijiwe vya kahawa jioni? Hapana baba Mimi sirudi huko.” Alisema Dr.Kimbe. Maneno haya yalikuwa na ukweli wote lakini Mzee Kihedu hakuyajali yote hayo. “Kimbe wewe ni mwanangu, hapa yuko mkaza mwanangu na mjukuu wangu. Uthamani wa maisha yenu umezidi hayo maneno, ambayo yatachukua muda mfupi tu na watu watayaona ya kawaida. Isitoshe wewe una marafiki wengi nje ya nchi, unaweza kuwaandikia na baadaye ukapata kazi nzuri zaidi ya hiyo uliyoachishwa.

Kumbuka mimi ni Mzee sasa na mama yako. Ninani atakayeangalia mashamba yako na mifugo iliyopo? Twende na ujifanye huyaoni wala kuyasikia maneno ya wanakijiji, kwa faida yako mwenyewe. Unadhani mjukuu wangu atakuwa katika hali gani baadaye ukiendelea hivi? Hebu tafuta mteja wa nyumba yako umuuzie na uondoke hapa urudi nyumbani sawa!” Alisema mzee Kihedu. Mwisho wa Yote Dr. Kimbe alikubali kuondoka kijijini Makuyuni na kuuza nyumba yake na mwishowe akarudi Kijijini Taabu yanini.

Maisha yalikuwa sio mabaya katika familia hii, mwaka umepita sasa tangu Bwana Kimbe afike kijijini hapa. Mashamba yalisimamiwa vema na mifugo ilistawi sana na kuongezeka. Bidii yake katika kazi viliwafumba midomo wambea wote waliokuwa wakijaribu kufuatilia maisha yake. Hakuwa akionekana kwenye vilabu vya pombe wala kwenye kijiwe kama wengine wanavyofanya kila siku. Yeye na mke wake na wazazi wake ndio marafiki wakubwa. Mfumo wake wa maisha ya ukimya na uchapakazi vilimletea furaha na heshima kwa watu wengi.

Mafanikio yalikuja kwa kasi sana na kubadilisha afya zao zilizokuwa dhaifu kwa ugumu wa maisha walipokuwa Makuyuni. Kila wiki walikuwa wakikutanika pamoja na wazazi wao kwa ajili ya kikao cha familia kujadili mambo ya maendeleo yao. Ramsoni alishakuwa na kufikia umri wa kupelekwa kwenye shule ya Chekechea. Miaka minne ilitosha kumfanya ajiunge na shule hiyo. Kwa ujumla ni kwamba maisha yalirudi kuwa mazuri kwa Dr. Kimbe na familia yake.

Kwa Upande wa Mzee Kihedu alijawa na furaha kwa kuungana na mwanae kijijini hapo kuliko hata alipokuwa kazini. Mazao yaliongezeka mara nyingi zaidi ya alipokuwa peke yake. Bidii na utaalamu wa kilimo pamoja na ubunifu wa mambo aliokuwa nao Dr. Kimbe, vilimfanya awe mbali sana kimaendeleo kuliko wanakijiji wote. Wengi wa wanakijiji walikuwa wakitegemea minazi yao tu. Lakini yeye alilima mazao mbalimbali na kufuga mifugo mingi mbalimbali.

Ni kweli kilikuwa ni kilimo cha mkono lakini alikifanya kwa ubunifu mkubwa. Wafanyakazi wa shambani walirahisisha kazi na kusababisha maendeleo kwa familia hizo mbili. “Kwakweli baba ninafuraha sana katika maisha yangu mpaka hapa.” Dr.Kimbe alimwambia baba yake jioni moja wakati walipokuwa kwenye kikao cha familia. “Ndio Mwanangu! Hata mimi ninakuona umebadilika sana na unatufurahisha mimi na mama yako.” Alisema Mzee Kihedu huku akionyesha tabasamu la ushindi.

“Kwa kweli mwanangu furaha yangu na baba yako ni kubwa sana, kwani hata upweke hatuna tena. Pia ninafurahi niko na mkaza mwanangu hapa na tunashirikiana vizuri. Mjukuu wetu Ramson naye anatufanya tufurahie maisha kwa uchangamfu wake.”Wote walitabasamu na kutoa miguno kuashiria kumkubalia mama kwa maneno yake. “Labda ungetueleza juu ya furaha yako maana ni wewe uliyeanzisha mazungumzo haya.”

Alisema Mzee Kihedu akimgeukia mwanae ili asikie kutoka kwake zaidi. “Unajua Baba niliathirika sana kifikra baada ya kuachishwa kazi? Kwa mawazo yangu nilijua kuwa sasa nimekwisha!Mbaya sana ni taarifa zangu za kufukuzwa kazi zilivyosambazwa katika Hospitali zote nchini. Hii ilinifanya nikose ujanja hata wa kuomba kazi mahali popote. Kuchanganyikiwa kwangu kukanifanya niamue kujiweka mbali sana na watu wanaonijua. Niliona aibu sana kurudi tena hapa kijijini.

Akili zangu kidogo zilizobaki nikachanganya na za mke wangu, zikatuelekeza kwenda kujificha Makuyuni. Shamba alilonipa babu Sengasu, likawa sababu ya mimi kwenda kujihifadhi kijijini pale, ili nilime na kuendesha maisha yangu na familia. Balaa jingine ni pale mjomba chambo alipokuja na kuninyang’anya shamba lile. Kwakweli nilijiona kama ambaye ulimwengu wote umeniinamia na kunidhihaki!

Sikuona kwamba maisha yangu yalikuwa na mwelekeo tena, kwani huku kijijini sikuwa ninafikiri habari yake. Sikutaka fedheha ya kudhihakiwa na watu walionijua hali yangu hapo mwanzo.”Alisema Dr. Kimbe kwa hisia kali.“Nilikuona siku nilipokuja kukutaka urudi nyumbani.” Alisema mzee Kihedu kisha akakohoa na kuendelea tena.. “Hofu yako kwa wanakijiji kuwa watakuonaje ilikuwa na ukweli wa asilimia ishirini tu. Asilimia nyingi zilikuwa zikisimamia haki ya wewe kurudi nyumbani kwenu.” Waswahili wana msemo usemao: “Ng’ombe akivunjika mguu, hujikokota na kurudi kwao.”

Hapa ni kwako! Mkataa kwao ni mtumwa! Angalia ulivyotaka kujifanya mtumwa, kwa kwenda kuishi mahali pengine na kutegemea shamba ambalo ulipewa bila hata kipande cha karatasi, kukudhibitisha kuwa ni lako. Hebu tuachane na hayo ilimradi uko nyumbani sasa. Vipi kisima watu wako wameshamaliza kukichimba?” Alihitimisha kwa swali mzee Kihedu na kuingiza mada nyingine.

Kwakweli kisima bado hakijakamilika inavyoonekana maji yako chini sana, inabidi waendelee kuchimba kusudi tupate unafuu kwa ajili ya umwagiliaji wa mazao.” Alisema Dr.Kimbe. “Ramson mmemwacha amelala au anachora mapicha yake?” Aliuliza Mzee Kihedu baada ya ukimya mfupi. Alikuwa akipenda sana kuwa na mjukuu wake karibu mara zote lakini Ramson alipenda kujitenga mwenyewe muda mwingi huku akijisomea na kuchora mapicha mbalimbali.

Japo alikuwa ni mdogo lakini alikuwa anaonyesha kuwa na kipaji hasa cha uchoraji na akili nyingi darasani kwao. “Nilimwacha amelala alisema kuwa alikuwa anasikia usingizi.” Alijibu mke wa Kimbe kwa mara ya kwanza katika kikao chao hicho. “Vizuri mwache alale amefanya kazi kubwa sana leo. Unajua alipotoka tu shuleni tuliungana kwenda shamba la minazi, aliwasimamia mbuzi wakati mimi nikisimamia watu wa kuangua nazi.

Mpaka tunarudi jioni hii yuko hoi kwa kukimbizana na mbuzi.” Aliongea hayo kwa sifa kidogo Mzee Kihedu na wote walicheka. Mwisho wa yote waliagana kwa sala kusudi wakalale. “Kwa hiyo kesho utakuwa kule kwenye kisima au fundi atasimamia hiyo kazi?” Aliuliza mzee kihedu akitaka kujua ratiba ya kesho yake.

“Baba unajua kazi usipoisimamia mwenyewe haiendi? Inabidi niwepo pale, vibarua wanaendelea na kazi yao kwenye shamba la Mtimbwani. Labda wakija na kusema wamemaliza kazi nitaenda haraka na pikipiki ili nikakague kazi yao kabla sijawalipa.” Alisema Kimbe huku akiusogelea mlango.

“Kesho nitakwenda na Ramson akaone kisima kinavyochimbwa.” Alimalizia. Sawa tu ila keshokutwa tutakwenda naye mjini Tanga, nataka kumtembeza maeneo mbalimbali, maana naenda kununua baadhi ya mahitaji ya nyumbani.” Alisema Mzee kihedu.

“Sawa baba nawatakia usiku mwema baba na mama.” aliaga. “Asante na nyinyi pia.” Walijibu Mzee Kihedu na mkewe kwa pamoja. Walitoka Kimbe na mkewe na kuelekea kwenye nyumba yao iliyoko kama mita mia mbili kutoka Nyumbani kwa Mzee Kihedu.

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
53 Mtu wa Ufukweni Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni