Mtunzi: ___
SEHEMU YA KUMI NA TATU
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Kulingana na nafasi zenu najua kazi hiyo ni ndogo mno. Kitakachofauata niachieni mimi.
“Nini kitafuata?”, mjumbe mmoja aliropoka kwa shauku.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
TUENDELEE...
“Mara ngapi nimewaambia kuwa bendera kadhaa zitapepea nusu mlingoti kwa siku kadhaa katika nchi kadhaa wa kadha?. Nataka kufanya jambo fulani ambalo halijawahi kutokea sasa kifanyike. Kitu ambacho bado hakijafikirika. Kitu ambacho historia haitakisahau. Kwa muda mrefu amekufa kiogozi mmoja. Safari hii nataka kuona viogozi wengi wamekufa wote kwa wakati mmoja. Tena nitafarijika kama watakufa pamoja katika viti na meza zao. Huenda wataanguka mmoja baada ya mwingine, wakati wakiagana. Ama kweli litakuwa jambo la kusisimua sana…”
“Kusisimua!” Mmoja wa wajumbe aliropoka na kufoka baada ya kupatwa na mshangao. “”Kusisimua!”, alirudia tena, “Sikuwa na hakika. Sasa nimeamini kuwa una wazimu. Hata hivyo, wazimu wako unakudanyanya sana kukutuma udhani kuwa mimi naweza kushiriki kuinua mikono yangu katika kuwaangamiza watu ambao licha ya kwamba, hawana hatia, wanajitesa kutwa kucha kuwasaidia wanyonge wanaonyimwa haki zao?”.
Mjumbe huyo ambaye sasa alikuwa amesimama wima, akitetemeka kwa hasira huku akitokwa na jasho aliwatazama wajumbe wenzake. Alipoona wote wana dalili ya kumuunga mkono aliongeza. “Huna budi kulionea aibu wazo lako la kipumbavu…”
“Keti”, Proper alimwamru. “Hujui unalosema. Maneno yako yamejaa ndoto au nyimbo ambazo hao unaowaita viongozi, sijui watetezi wa wanyonge gani, wamekuwa wakizijaza katika vichwa vyenu. Nani anayemtetea nani katika dunia hii? Mnyonge hujitetea mwenyewe. wale wanachofanya ni kutetea matumbo yao. maisha na vyeo vyao tu kwa visingizio vingi. Wamehitimu katika taaluma ya kusema maneno mazuri na kutoa ahadi tamu katika masikio ya wanyonge kiasi cha kuwafanya waonekane kama miungu ambayo wanadamu wanaitegemea!”,
“Hata hivyo”, mjumbe huyo alidakia, “Siwezi kushiriki upumbavu kuangamiza damu za watu wasiokuwa na hatia”.
“Bado hujajua usemalo”, Proper alimjibu kwa mara nyingine. “Naweza kuwa mwema kukukaribisha katika mpango huu ambao utasaidia kuyabadili maisha yenu kuwa ya heti na utajiri mkubwa. Lakini siwezi kuwa mpole kiasi hicho kiasi cha kuacha mpango huu ambao nimeuandaa kwa miaka mingi uharibike kwa ajili ya woga na ujinga wa yeyote kati yenu. Nadhani sasa nimeeleweka?”.
Proper akanyamaza kidogo ili kutoa nafasi kwa wajumbe waweze kuyatafakari maneno yake.
Ulikuwa ujumbe wa kutisha kwa wajumbe walioshiriki mkutano huo, Kilichofuata yalikuwa maafa na ukatili mkubwa kwao au yeyote ambaye angethubutu kukanusha au kutoa siri hii. Ukweli huo uliwatia hofu wajumbe hata wakatazamana kwa dalili ya kukata tamaa ya maisha.
Kama anayesoma mawazo yao. Proper akarudia kuongea kwa sauti ile ile ambayo japokuwa haikuwa kali, wala yenye hasira, lakini sauti hiyo iliubeba ujumbe kamili, alieleza jinsi alivyodhamilia kutenda yote aliyosema. “Najua kwamba majalada yenu kazini hayaonyeshi doa lolote, Na raia wengi nchini wanayo picha nzuri juu yenu. Picha iliyowawezesha mkachaguliwa kushika nyadhifa katika sehemu mbali mvali muhimu za uongozi. Lakini kuna upande wa pili wa picha hizo. Upande wenye kila aina ya uovu, ukatili, na kukiuka taratibu za nchi. Nyie mnadhani upande huo wa pili ni siri zenu binafsi ambazo hakuna anayefahamu. Kwa bahati mbaya au nzuri, mimi nafahamu kila jambo. Namfahamu kila mmoja wenu vilivyo. Pia ninao ushahidi mzuri ambao ukiwekwa hadharani utayafanya majina yenu yanuke kama takataka”.
Wajumbe walianza kuchanganyikiwa. Ndio kwanza wakaifahamu ‘bahati’ iliyowafanya wateuliwe kushiriki katika kundi hili. Proper alikuwa amewateua baada ya kuwapeleleza kwa muda mrefu na kuwaweka katika kona moja ambayo ilikuwa vigumu kujitoa. Wakaanza kutapatapa, kila akijiuliza ni vitendo vingapi alivyofanya kwa siri na vimefahamika.
Kuna yule ambaye kabla hajateuliwa kuwa mbunge alikuwa mfanya biashara mkubwa wa magendo ya madini na bangi alivyosafirisha kwenda nje ya nchi. Hadi sasa biashara hiyo hajaiacha kwani uchumi wake unategemea biashara hii. Biashara hii imemfanya ajenge jumba la kifahari huko Ughaibuni na kufungua kiwanda hapa nchini akitumia majina ya mtu mwingine. Haya kumbe yanafahamika.
Mwingine ni yule ambaye huuza siri za nchi kwa mashirika ya kijasusi huko nje ya nchi. Wao humlipa pesa nyingi sana pia wamemwahidi hifadhi ya kisiasa endapo lolote lingemtokea. Mambo haya yakifanyika kwa siri sana, hakujua kabisa kama yangeweza kufahamika. Kumbe…
Na kuna huyu ambaye aliyeshiriki katika kuandaa kifo cha mgombea mwenza katika uchaguzi wao. Kadhalika alikuwa, kiungo muhimu katika kufanikisha kifo cha kiongozi shupavu ambaye alionekana kuwa kauawa na majahili wa nje. Kitendo ambacho kilimpatia pesa za kutosha. Kama yote hayo yanajulikana!… Kama kuna ushahidi!…
Kila mjumbe alijikuta katika nafasi ngumu mno kwa maisha yake ya baadaye. Baada ya kutazamana tena, na kila mmoja kuona hofu katika macho ya mwenzake, waliyarejesha macho yao kwa Proper kwa namna iliyosihi. Kukiwa hakuna jambo ambalo alihitaji zaidi ya hilo, Proper aliongeza.
“Labda yupo ambaye haogopi aibu. Ambaye yuko tayari nitoe ushahidi huo, Au kama kuna mwingine anabuni mbinu ya kutoroka akajifiche mbali. Ndoto za aina hiyo ningeshauri, mziondoe akilini. Ingawa sioni fahari kusema haya lakini sina budi kukufahamisheni kuwa hatua tuliyofikia katika suala hili ni ndefu mno. Hivyo yeyote atakayekiuka kwa njia yoyote afahamu kuwa hatafika mbali. Kifo kitakuwa kando kikimsubiri. Wala hatajua kapigwa na kitu gani?. Atakayenusurika ni yule mwenye uwezo wa kutoroka bila roho yake tu”.
Hofu ilizidi kutawala mioyo ya wajumbe hao. Tamaa na matumaini yao yote ya utajiri zaidi na vyeo ikaanza kudidimia. Walio waoga walijiona kama ambao tayari wako safarini kuelekea kuzimu. Mashujaa kiasi waliduaa tu. Wale ambao wana mioyo migumu zaidi walimtazama. “Kwame”, kwa namna ya kupima uwezo wa kifo chake yeye kabla na baada yao.
Kama anaesoma mawazo yao Proper alisema. “Naona wapo wanaodhani kuwa nastahili kufa”, akacheka kidogo, “Hilo ni wazo la kipuuzi kuliko yote. Mimi ni mtu ambaye hafi kwa urahisi. Na kabla hujaniua utakuwa umefufa wewe, bila kujua kitu gani kimekupiga”. Akacheka tena kabla ya kuongeza, “Pamoja na hayo ndugu zangu mawazo yote ya nini? Maelezo yangu niliyokupeni hayakuwa ya kuwatisha isipokuwa kuwaonyesha hali halisi ilivyo. Nina hakika hakuna baya lolote litakalotokea kusababisha hali hiyo. Bado nawaomba tusiogopane. Tuwe marafiki na tutimize wajibu wetu vyema. Tusisahau kuwa mpango huu una utajiri ambao wengi wenu hamjawahi kuugusa na vyeo ambavyo msingeweza kuvikalia”.
“Wala msihofu kuwa utawala wenu utakuwa wa kidikteta hata muwe kama maadui wa wananchi wenyewe. Mbinu zitafanyika mara tu baada ya vifo vya wakubwa wachache, ili majina yenu yazibe mapengo hayo. Sifa zenu zitaimbwa redioni na kutangazwa magazetini, vikao vyote vya chama havitauona ubovu wenu, hata raia watawapenda na kuwategemea. Mmoja wenu atakuwa Rais. Ni kazi ndogo sana, mradi kila mmoja atimize jukumu lake dogo lililoko mbele yake”.
Ingawa sauti ya Proper ilikuwa inasema ukweli, wajumbe waliona kama anawadhihaki.
Kutoka hapo Proper aliharakisha kukiendea chumba ambacho kilikuwa na mtambo wake wa kupeperushia habari. Alipofika, alitazama saa yake na kusubiri dakika kadhaa, kisha alibonyeza hapa na pale. Mara ikatoka karatasi iliokuwa na maandishi yaliyosema:
Ua limechanua bustanini lafaa kuchumwa.
Proper alielewa maana ya ujumbe huo. Ilikuwa lugha ya siri ambayo ilikuwa ikimfahamisha kuwa kulikuwa na mzigo wake mahali pao pa siri.
Mahali hapo ni katika chumba chake cha pili katika nyumba yake nyingine, mtaa fulani. Katika kona moja ya chumba hicho, lipo kasha la takataka ambalo haliwezi kuvutia macho. Humo huwekwa ujumbe wa hatari zaidi ama silaha, madawa ya kulevya na kadhalika. Yote yake ambayo viongozi wake wa nje huofia kupeperushwa katika mtambo wao kwa hofu ya kunaswa katika mitambo ya adui, huletwa hapa, nae kuarifiwa.
Lililomtoa jasho Proper ni kutokumjua mtu huyo ambaye makao makuu walikuwa wakimtumia kuleta habari hizo. Kwa mjibu wa madaraka yake, ni yeye aliyekuwa mkuu wa mambo yote ya kijasusi katika kanda hii. Watu wote walikuwa chini yake. Wala hakufahamu wakati gani anafanya shughuli zake. Proper alikuwa na shauku kubwa ya kufahamu. Aliwahi kukiuka utaratibu na kuanza kuendesha upelelezi ili amfahamu. Lakini alishangaa alipopewa onyo kali kutoka makao makuu kwa kitendo hicho ikamlazimu kutii, ingawa kwa shingo upande.
Kwa hivyo, alipokuwa akiendea ujumbe huo, alikuwa mtu mwenye mashaka hasa alipozigatia kuwa ujumbe alituma haukuhitaji jibu refu zaidi ya ‘Ndiyo’ alipofika chumbani humo katika sura ya jina tofauti alijifungia na kuliendea kasha hilo. Alipekuwa taka chache za karatasi kabla hajaifikia bahasha pana ambayo iliandikwa herufi moja tu juu ‘P’ akaitatua kwa uangalifu akashangazwa na harufu tamu ya poda au manukato ambayo iltoka katika bahasha hiyo. Kwa jinsi alivyokuwa na haraka ya kufahamu jibu la pendekezo lake, hakusita kujiuliza maana na dhamila ya harufu hiyo tamu, Alichofanya ni kuanza kuisoma.
Agenti 034/X/P
Tumepokea taarifa yako na kuipitia kwa makini. Tumeshangazwa sana na wazo lako la kinyama. Inaonyesha hujui kwanini uko hapo. Tumekuweka hapo si kwa ajili ya kutenda ukatili wa kujifurahisha bali katika kulinda maslahi yetu kiuchumi na kisiasa.
Wazo lako ni hatari sana kwani linakusudia kumwaga damu nyingi kuliko inavyostahili, jambo ambalo litafanya, kati ya unaokusudia kuwateketeza hujui kama tunao watu wetu tunaowategemea ingawa hadharani tunawaruhusu wajifanye kama wanatulaumu, kutulaani. Kuondoka kwao madarakani kuna hatari ya kuja watu ambao pengine tutashindwa kuwamiliki. Kwa muda mrefu tumevumilia vitendo vyako ambavyo haviambatani na wajibu wako. Umekuwa ukiutumia wadhifa tuliokupa kuufariji moyo wako wenye kiu ya kumwaga damu. Safari hii umevuka kiwango. Ofisi hii imeshindwa kustahamili zaidi. Pamoja na kukuonya uondoe ndoto za kipuuzi kama hizo, tunakutaka uichukulie barua hii kama taarifa ya kukupokonya madaraka yote uliyokuwa nayo. Kuanzaia sasa. Uko huru…”
Proper alipofikia hapo, aliruka kando ghafla akageuka nyuma yake akitazama kila upande, bastola yake ikiwa mkononi tayari kwa lolote. Hakuona chochote alikuwa peke yake chumbani hakuamini.
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)