KITABU CHA SHETANI (2)

0
Mtunzi: Aziz Hashim

SEHEMU YA PILI
TULIPOISHIA...
Kwa kuwa alikuwa na uelewa mkubwa wa namna ya kuchezea simu na kompyuta, muda mfupi baadaye alifanikiwa kuifungua simu hiyo, juu kabisa akakutana na picha ya msichana yule aliyemtoa nishai, jambo lililomfanya awe na uhakika kwamba ni kweli ile simu ni yake na aliiangusha pale alipoikuwa anaangalia jinsi gari lake la kifahari lilivyogongwa na bodaboda.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Katika hali ambayo hakuitegemea, Edmund alijikuta macho yake yakiganda juu ya picha ya yule msichana, akawa anamtazama huku akiwa ni kama haamini alichokuwa anakiona. Mwisho alishusha pumzi ndefu na kuendelea kuishangaa simu hiyo.

Kitu kingine kilichozidi kumshangaza, licha ya kufanikiwa kuifungua simu hiyo sehemu ya kwanza, kila kitu ndani ya simu kilikuwa kimefungwa kwa namba maalum za usalama, kuanzia kwenye meseji, kwenye picha, kwenye majina na kila kitu.

***

Gari la kifahari, Jeep Grand Cherokee (New Model), lilikuwa likipasua lami kwa mwendo wa kasi, wakati mwingine dereva akilazimika kuyapita magari mengine yaliyokuwa yanasuasua mbele yake kuelekea Mikocheni. Dakika kadhaa baadaye, tayari lilikuwa limewasili Mikocheni, dereva akapiga honi, walinzi wawili wenye bunduki wakafungua geti kisha likaingizwa mpaka sehemu ya maegesho, nje ya ghorofa refu la kisasa lililokuwa na mandhari ya kuvutia mno.

“Mungu wangu, simu yangu nimeiweka wapi tena?”

“Simu gani bosi? Mbona hapo umeshika simu mbili mkononi?”

“Ile simu yangu ninayoitumia siku zote, siyo hizi,” alisema msichana mrembo wakati akiteremka kwenye gari, na kusababisha walinzi waache kila walichokuwa wanakifanya kwa ajili ya kumsaidia bosi wao huyo.

Licha ya kusaidiana kupekua kwenye gari karibu kila sehemu, hawakufanikiwa kuiona simu hiyo, jambo lililosababisha msichana huyo aanze kutokwa na machozi.

“Ina vitu vyangu vingi sana vya siri, siwezi kuruhusu ipotee, haiwezekani,” alisema msichana huyo akionesha kuchanganyikiwa mno.

“Hebu jaribu kuipiga,” alishauri mlinzi mmoja, wazo ambalo msichana huyo aliona linafaa, kwa kutumia simu yake nyingine, aliipiga simu hiyo. Kwa bahati nzuri, bado ilikuwa hewani, ikawa inaita.

“Inaita! Inaita,” alisema msichana huyo akionesha kuwa na shauku kubwa ya kusikia nani atapokea.

***

Edmund aliendelea kufanya kazi zake lakini bado akili yake ilikuwa haitulii. Alitamani kufahamu vitu vingi zaidi kuhusu yule msichana mrembo aliyemtoa nishai asubuhi hiyo na njia pekee aliona ni kupitia simu ya msichana huyo.

Akaamua kuanza kuishughulikia, kabla hajafungua sehemu nyingine, alikopi mafaili yote yaliyokuwa kwenye simu hiyo (back up) na kuhamishia kwenye kompyuta yake.

Akiwa Anahangaika kuifungua kwa kutumia mbinu alizokuwa anazijua mwenyewe, simu hiyo ilianza kuita. Akashtuka na kuanza kila alichokuwa anakifanya, akawa anaitazama inavyoita huku akijishauri kama apokee au la. Mwisho aliamua kuipokea.

“Haloo!”

“Haloo, samahani sana kakaangu naomba msaada wako. Mimi ni mwenye hiyo simu nimeipoteza hata sijui niliiangushia wapi. Nakuomba unielekeze popote ulipo nakuja na nakuahidi kuwa nitakupa shilingi milioni moja ‘cash’ ukinisaidia kuipata simu yangu,” ilisikika sauti upande wa pili ambapo bila hata kuuliza Edmund alijua ni ya yule msichana aliyemtoa nishai asubuhi. Kwa kuwa lengo lake halikuwa kuichukua simu hiyo, aliamua kumuelekeza ofisini kwao, Hashcom Mobile, Bamaga-Mwenge jijini Dar es Salaam. Baada ya kukata simu, msichana yule aliingia kwenye gari lake na kuondoka kwa kasi kubwa, akiwaacha wale walinzi wakitazamana.

Dakika chache baadaye, tayari alikuwa amewasili Bamaga, akafuata ramani aliyoelekezwa na kutokezea kwenye ofisi aliyokuwa akifanyia kazi Edmund. Akapaki gari lake na kwenda kujitambulisha kwa walinzi kisha akaruhusiwa kuingia ndani. Alipoingia tu getini, alitoa simu yake na kuipiga tena ile namba, ikawa inaita.

“Edmund kuna mgeni wako mapokezi,” sauti ya mfanyakazi mwenzake ilisikika, alipotazama simu iliyokuwa inaita, Edmund akajua lazima ni yule msichana amewasili. Harakaharaka akainuka na kujiweka vizuri nguo zake ambazo bado hazikuwa zimekauka vizuri, akatoka kuelekea mapokezi.

“Mambo!” Edmund alimsalimia yule msichana baada ya kumkuta mapokezi, akiwa amejiinamia akiiwaza simu yake. Salamu hiyo ilimfanya ainue uso wake, macho yake na ya Edmund yakagongana.

Mshtuko alioupata ulionekana waziwazi kwani ni kama hakutegemea kwamba mtu aliyemuokotea simu yake ni Edmund, kijana ambaye muda mfupi uliopita alimuonesha dharau ya kupindukia.

“Po..a,” alijibu msichana huyo kwa kubabaika, Edmund akamuonesha ishara kwamba amfuate kwani mapokezi palikuwa na wageni wengine wengi, wakaongozana mpaka kwenye chumba maalum cha mazungumzo, yule msichana akiwa bado haamini macho yake.

“Wewe ndiye uliyeniokotea simu?” alisema msichana huyo kwa upole mno, tofauti kabisa na alivyokuwa mwanzo.

“Yaah! Naitwa Edmund, bila shaka unanikumbuka,” alisema Edmund, kauli iliyozidi kumuweka yule msichana kwenye wakati mgumu.

“Naomba unisamehe sana kakaangu kwa kilichotokea asubuhi. Nilitoka nyumbani nikiwa nimevurugwa ndiyo maana nikawa mkali sana kwenu. Tafadhali nakuomba unisamehe,” alisema yule msichana kwa upole huku mara kwa mara akikwepesha macho yake yasigongane na ya Edmund aliyekuwa ametulia anamtazama kwa makini.

Edmund alishusha pumzi na kumwambia asiwe na wasiwasi ameshamsamehe ndiyo maana ameamua kumpa ushirikiano ili aipate simu yake.

“Ooh! Ahsante sana kakaangu, yaani hata sijui namna ya kukushukuru, simu yangu ina vitu vingi sana vya muhimu, yaani umenikoa kweli,” alisema msichana huyo huku akimpa mkono Edmund, tabasamu hafifu likiwa limechanua kwenye uso wake.

Kitendo cha kupeana mkono na msichana huyo, kilimfanya Edmund ahisi kama amepigwa na shoti ya umeme, akabaki amezubaa mpaka msichana huyo alipoamua kutoa mkono wake mwenyewe.

“Una akaunti benki?”

“Yaah ninayo, vipi kwani.”

“Nataka nikuhamishie fedha zako kama nilivyokuahidi. Shilingi milioni moja ‘cash’ kwa msaada ulionipa.

“Hapana, sihitaji malipo kutoka kwako dadaangu, nimekusaidia tu.”

“Hapana Edmund, chukua tu kwa sababu mimi ndiyo niliyeahidi kukupa, nitajie namba yako ya akaunti tafadhali,” alisema msichana huyo lakini Edmund akaendelea kushikilia msimamo wake.

Ni kweli Edmund alikuwa na shida ya fedha na kupewa shilingi milioni moja katika siku kama hiyo, tarehe za mshahara zikiwa mbali kabisa kungemsaidia sana lakini hakutaka kuonesha udhaifu, akashikilia msimamo wake.

“Ngoja nikakuchukulie simu yako,” alisema Edmund na kuinuka, akawa anatoka kwenye chumba hicho cha mazungumzo na kumuacha yule msichana amekaa palepale alipokuwa amekaa awali.

Alipofika mlangoni, aliufungua na kugeuka nyuma, akashangaa kumuona yule msichana akimtazama kwa macho ya wizi, macho yao yakagongana kisha harakaharaka yule msichana akakwepesha macho yake. Edmund akatoka, muda mfupi baadaye akarejea akiwa na simu hiyo.

“Hii hapa,” alisema huku akimkabidhi, msichana huyo akaipokea huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.”

“Siamini! Jamani ahsante we kaka,” alisema msichana huyo huku akinyoosha tena mkono wa shukrani kumpa Edmund, wakashikana tena. Hali kama iliyomtokea awali alipopeana mkono na msichana huyo ikajirudia tena, akabaki kujishangaa kwani haikuwa kawaida yake.

“Basi chukua hii utakunywa hata soda naona zawadi yangu umeikataa,” alisema msichana huyo huku akiingiza mkono mwingine kwenye pochi yake ya kisasa, Edmund akataka kukataa tena lakini alikuwa amechelewa kwani msichana huyo alimuwekea noti kadhaa za shilingi elfu kumikumi kwenye mfuko wa shati lake.

“Mbona hujaniuliza jina langu? Au bado una hasira na mimi?” msichana huyo aliuliza huku tabasamu lake likizidi kuchanua na kuupamba uso wake, akazidi kuonekana mrembo. Edmund alishindwa cha kujibu zaidi ya kutabasamu, ni kweli tangu msichana huyo afike, hakuwa amemuuliza jina lake na huenda kama mwenyewe asingeanza, angeondoka bila kumuuliza.

“Hii ni ‘business card’ yangu na hilo hapo ndiyo jina langu,” alisema huku akimkabidhi Edmund kadi ya kisasa ya mawasiliano. Akaipokea na kuitazama vizuri.

“Samantha!”

“Yes! That’s my name.” (Ndiyo! Hilo ndiyo jina langu) alisema msichana huyo kwa lafudhi laini, Edmund akazidi kujikuta katika wakati mgumu.

“Nisikupotezee muda wako najua upo kazini, narudia tena kukuomba radhi kwa yote yaliyotokea asubuhi na nakushukuru sana kwa wema wako,” alisema msichana huyo huku akiinuka, akachukua kila kitu chake na kuagana na Edmund.

“Ngoja nikutoe mpaka nje,” alisema Edmund huku naye akisimama, wakatoka kwenye chumba cha maongezi, wakaelekea mapokezi kisha Edmund akamsaidia kufungua mlango wa nje, wakatoka na kuelekea kwenye gari la kifahari alilokuja nalo msichana yule.

“Hebu jaribu kuibipu simu yangu,” alisema msichana huyo na kumtajia Edmund namba, bila kuelewa lengo la msichana huyo, Edmund alifanya kama alivyoambiwa, simu ikaita.

“Haya kazi njema kaka, nakushukuru sana,” alisema Samantha na kubonyeza rimoti aliyokuwa ameishika, gari likawaka taa za pembeni na kutoa mlio wa kuashiria kwamba milango imejifungua.

Msichana huyo akatembea kwa maringo hadi kwenye gari, akaingia na kukaa nyuma ya usukani, akawasha gari na kutetemsha kioo, akawa anampungia mkono Edmund ambaye bado alikuwa amezubaa, akiwa ni kama haamini alichokuwa anakiona mbele ya macho yake.

Akaondoka eneo hilo akiwa ndani ya gari lake la kifahari, Jeep Grand Cherokee (New Model) na kumuacha Edmund amesimama palepale.

“Mundi vipi mshkaji wangu, mbona umepigwa na butwaa kiasi hicho? Naona ulikuwa na chombo cha ukweli kinoma,” Sam, mlinzi wa kampuni aliyokuwa akifanyia kazi Edmund alimtania baada ya kumuona bado amezubaa palepale nje, Edmund akatabasamu na kurudi ofisini kuendelea na kazi zake.

“Ebwana eeh! Yule malaika uliyekuwa naye ni nani arifu? Nipigie pande na mimi nijiweke,” Clarence, rafiki yake Edmund alimtania baada ya kurejea, wote wakaishia kucheka tu. Edmund akakaa kwenye kompyuta yake na kushusha pumzi ndefu, akakumbuka kwamba msichana yule mrembo alimuwekea fedha kwenye mfuko wake wa shati.

“Shilingi laki moja? Mungu wangu, huyu dada anafanya kazi gani kwani?” alisema Edmund baada ya kuhesabu fedha hizo. Akajikuta akishindwa kuzuia tabasamu lisiupambe uso wake. Muda mfupi baadaye, simu yake ilianza kuita, harakaharaka akapokea.

“Nashukuru sana kakaangu nimefika ofisini, kama utapata muda baadaye naomba nije kukuchukua tukapate lanchi pamoja kama shukrani yangu kwako,” alisema Samantha.

“Ok hakuna shida dada’angu,” alijibu Edmund kisha simu ikakatwa, tabasamu pana likachanua kwenye uso wake kwani licha ya ukweli kwamba msichana huyo alikuwa amemfanyia kitendo cha kumdhalilisha sana asubuhi ya siku hiyo,

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)