KIJIJINI KWA BIBI (25)
Zephiline F Ezekiel
5 min read
Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"we happy vipi, una nini leo?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti
yake kwa sauti yenye mshangao huku akiusukuma mlango kwa utaratibu
mzuri ili asimdhuru binti yake aliyekuwa amelala,
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
"baba sijisikii vizuri, naona kizunguzungu", Happy aliongea huku
akiwa bado amelala chini.
Baba yake akamnyanyua, kisha akamrudisha chumbani kwake,
"nikupelekee hospital mwanangu?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti
yake kwa sauti ya huruma,
"hapana baba, nafikiri ni tatizo la muda", Happy alijibu huku
akijifunika shuka,
"Hapana, lazima uende hospitali, ngoja nimalize kuoga nikupeleke"
Mchungaji Wingo alimwambia mwanae,
"Baba hii hali ya kawaida tu, itaisha" Happy alijibu baba yake,
"Usichukulie vitu kirahisi rahisi, we jiandae tu nikupeleke"
Mchungaji Wingo aliongea huku akitoka nje.
"hii ya leo balaa, sijui baba angenichukuliaje?", Happy alijiuliza
mwenyewe huku akiwa na tabasamu la mshangao na pia akimshukuru
Mungu kwa kumuepusha na dhahama hii.
Omari alipotoka kwa mchungaji mbio mbio mpaka alipofika nyumbani,
akasukuma mlango akaingia kwa fujo hadi ndani,
"ehe, vipi mwenzetu?", Omari alipokewa na sauti ya Sajenti Minja
aliyekuwa anamshangaa,
"nilikuwa nakimbia kimbia, kuweka mwili fiti", Omari alijibu akiwa
katika tabasamu la uongo huku akipumua bila mpangilio,
"haya bwana, mi nilifikiri umefumaniwa na mke wa mtu uko, maana
mbio ulizokuja nazo si mchezo", Sajenti Minja aliongea na kufanya
vicheko vilipuke sebule yote.
"Hanna mjomba, huku ugenini siwezi kufanya hivyo" Omary alijibu
huku akijilazimisha kutabasamu,
"Sisi tutajuaje bwana, nyie vijana mna mambo mengi" Mama Kayoza
aliongea,
"Hakuna mama" Omari aliongea huku akiingia ndani, akamwita Kayoza,
wakaingia ndani,
"duh, jomba uko noma", Omari alianza kwa mtindo huo,
"vipi tena baab?", Kayoza akauliza kwa mshtuko,
"mchungaji kanikuta juu ya mwili wa mwanae kaka", Omari akapasua
lililomkuta,
"naisi kama sijakusikia vizuri vile, ebu rudia", Kayoza akauliza
kwa stahajabu,
"nimesema kuwa, mchungaji kanikuta ndani kwake", Omari akaongea
tena alichomaanisha,
"ikawaje kaka?", Kayoza akauliza huku akiwa bado haamini
anachoambiwa.
Omari akamsimulia yote, mpaka alipofanikiwa kukimbia.
"duh, pole mwanangu", Kayoza akampa pole Omari,
"Cha kushukuru ni kuwa nimetoka salama" Omary aliongea huku akivua
fulana yake,
"Sasa huyo Happy kwa hali uliyomuacha nayo si itakuwa baba yake
amejua?" Kayoza aliuliza,
"Sijui bwana, kama baba yake atahisi labda inaweza kuwa tatizo, ila
kuniona hajaniona" Omary alimjibu mwenzake,
"Ila usirudie kufanya ujinga kama huo tena, yule mwanamke ni
shetani angalia usiwe unamsikiliza kila anachokushawishi" Kayoza
alimshauri Omary,
"haina noma, kuna mpya gani hapa?", Omari akauliza,
"kesho saa nne tutaenda kwa mganga", Kayoza akamtaharifu Omari.
"maeneo gani",Omari akauliza,
"mi mwenyewe sijajua bado", kayoza akajibu,
"Dah, Mimi nina wasiwasi yasije yakatokea kama ya kwa yule mganga"
Omary aliongea,
"Sasa usiseme hivyo, cha muhimu ni kumuomba Mungu tu atusaidie"
Kayoza alimwambia Omary,
"Mungu tunamuomba ila pia tahadhari lazima" Omary alimwambia
Kayoza,
"Basis usiende, nitaenda Mimi na mjomba" Kayoza aliongea huku
akionekana hajafurahishwa na maneno ya Omary,
"Nitaenda tu" Omary aliongea kwa upole baada ya kugundua Kayoza
amepaniki,
"Sasa kama utaenda kwanini unaleta maneno ya kutishana?" Kayoza
aliuliza,
"Basi yaishe kaka, nisamehe kwa maana sikudhani kama utamaindi"
Omary aliamua kujishusha ili mambo yaishe,
"Hatugombani hapa, tunaeleweshana tu" Kayoza alimwambia Omary,
"Sawa nimekuelewa ndugu yangu" Omary alijibu,
"Kama umenielewa sawa, Mimi nipo sebuleni" Kayoza aliongea huku
akielekea nje na kumuacha Omary akiwa amejimwaga kitandani.
.*
Kesho yake asubuhi Sajenti Minja aliwapitia wakina Kayoza, na
safari ya kwenda kwa mganga ikaanza.
Njia nzima hakuna alieongea, ndani ya gari kulikuwa na mziki laini
wa unbreak my heart ulioimbwa na mwanamama wa kimarekani
anayejulikana kama Tony braxton.
Sajenti Minja alikuwa akiufatilia ule wimbo kwa sauti ya chini,
Omari yeye alikuwa na mawazo yake, Kayoza pia alikuwa anafikiria
anachokijua.
"Huo wimbo vipi?" Kayoza aliuliza baada ya Sajenti Minja kurudia
zaidi ya mara tatu kuupiga ule wimbo,
"Si naupenda tu" Sajenti Minja alijibu kwa kifupi,
"Mimi najua mtu akiupenda wimbo lazima kuna tukio linahusihana na
huo wimbo" Omary alichangia,
"Ebu acheni ujuaji, sasa mnataka niweke nyimbo gani? au niweke hayo
manyimbo yenu yenye yo yo nyingi?" Sajenti Minja aliuliza,
"Wewe tuambie tu kuhusu huo wimbo, acha kujikanyaga" Kayoza
alimwambia mjomba ake huku akicheka,
"Au shangazi hasomeki?" Omary akaongeza na swali,
"Ebu niacheni bwana" Sajenti Minja aliongea huku akizima redio ya
gari.
Kwa mganga waliingia mishale ya saa sita kasoro robo, wakapokelewa
na msaidizi wa mganga, ila kwa bahati nzuri hawakukuta foleni
ndefu, watu walikuwa wachache tu.
Baada ya nusu saa, zamu yao ikafika wakaingia ndani, kile kitendo
cha kayoza kuingiza mguu katika mlango wa nyumba ya mganga, pale
pale akabadilika na akawa katika taswira ya kutisha sana, ila
alikuwa hawezi kutembea, aliganda pale pale, Sajenti Minja alipata
uoga huku akidhani kuwa zile bakora za kipindi kile zinarudi tena
kwa hiyo akakaa mbali kabisa na Kayoza hata alipogundua kuwa Kayoza
ameganda pale, bado alikuwa anaogopa kumsogelea. Unacheza na viboko
nini.
Mganga akapelekewa taharifa kuhusu lile tukio, Mganga ikambidi
atoke katika chumba chake cha kazi na kwenda mahali alipo Kayoza,
alipofika akamuangalia zaidi ya dakika kumi, kisha mganga akafunga
macho yake, alafu akatoa pumzi kumuelekea kayoza kwa njia ya mdomo,
pale pale Kayoza akadondoka chini huku akiwa katika ile ile taswira
ya kutisha.
"Mtoeni nje" Mganga akawaamuru wamtoe nje, wakambeba wakampeleka
nje, wateja waliokuwa nje wanasubiria tiba wote walikimbia
walipomuona Kayoza katika hali ile ya kutisha.
"Aliyekuja na huyu kijana yupo Wapi?" Mganga aliuliza huku
akimuangalia msaidizi wake,
"Yule kule" Msaidizi wake aliongea huku akinyoosha kidole kuelekea
alipo Sajenti Minja,
"Mbona amekaa mbali sana?" Mganga aliuliza huku akishangaa,
"Hata sisi hatujui, labda anamuogopa" Msaidizi wake alijibu,
"Kamuite" Mganga alimtuma msaidizi wake na yule bwana akaenda
kumuita.
Sajenti Minja alipofika alimsalimia mganga kisha mganga akawaambia
aliefuatana na Kayoza amfuate ndani, Sajenti Minja na Omari
wakamfuata mganga.
Mganga alikuwa ni mwanamke wa makamo, alikuwa na macho mekundu
sana, akamkazia macho Sajenti Minja, kisha mganga akasema,
"Minja mna tatizo kubwa sana" Mganga aliongea na Sajenti Minja
alishtuka kusikia mganga kamtaja jina lake, ila akapata matumaini
ya kumaliza tatizo,
"ila kwako naamini litaisha", Sajenti Minja alijitutumua na kumjibu
mganga,
"bibi yake mzaa baba yupo hai", Mganga akamtupia swali Sajenti
Minja,
"ndio mama", Sajenti Minja akajibu,
"anaishi wapi?", Mganga akauliza tena huku akiwa amemkazia macho
Sajenti Minja,
"anaishi Bukoba vijijini", Sajenti Minja akajibu,
"Sasa itabidi huyo kijana apelekwe uko", Mganga akawaambia Sajenti
Minja,
"tumpeleke wapi?", Sajenti Minja akauliza ili apate ufafanuzi
zaidi,
"mpelekeni kijijini, kijijini kwa bibi yake" Mganga aliongea akiwa
amefunga macho………
"Ebu mtaje, ni upuuzi huu" Mkuu wa Polisi aliongea na kumfanya Babu wa monchwari atulie kidogo kwa maana alikuwa amelisahau jina la Sajenti Minja,
"Mbona humtaji?" Mkuu wa Polisi aliuliza kwa hasira na kumgutusha Babu wa monchwari aliyekuwa bado analitafuta jina la Sajenti Minja,
Baada ya muda akalikumbuka jina, na akaona haina haja ya kuuficha uovu, akaamua kulitaja jina sasa. Kabla hajalitaja kwanza akaamua atabasamu, akatoa tabasamu la ushindi kwa maana alijua akimtaja Sajenti Minja ndio utakuwa mwisho wa mchezo na yeye ndio utakuwa mwanzo wa utajiri wake,
…Babu wa mochwari akaendelea kutabasamu,
"Mzee acha mzaa, nimekwambia umtaje huyo askari" Mkuu wa polisi aliuliza kwa ukali na kumfanya Babu wa monchwari ashtuke,
"askari mwenyewe si yule mwenye nanii, nini ile, ha, nimemsahau, ila nikimuona nitamjua", Babu wa mochwari aliendelea kuongea kwa kujiamini, ila hakutaka kumtaja moja kwa moja Sajenti Minja kwa kuwa alitaka kumfanyia jambo la kushtukiza Mkuu wa Polisi,
"mzee usinichanganye, maana sikuelewi", Mkuu wa polisi aliongea kwa ukali,
"niamini mwanangu, huyo muuaji napajua hadi anapokaa", Babu wa monchwar aliendelea kumwaga sera zake za kumshawishi Mkuu wa Polisi amuamini,
"Anakaa maeneo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza,
"Anakaa maeneo ya kota, karibu na kanisani" Babu wa monchwari alijibu huku akitabasamu,
"Mzee unachoongea ni kweli au leo umeamua kunichezea akili tu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimuangalia kwa jicho kali Babu wa monchwari,
"Kama itabainika nakudanganya, niweke ndani hata miaka mitatu" Babu wa monchwari alijibu kwa kujiamini,
"Na wewe ulimjuaje huyo mtuhumiwa, au mna mahusiano naye ya kindugu, ujirani au urafiki?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Babu wa monchwari,
"Mi naona kama maswali yako yanapoteza muda vile, cha msingi ulichotakiwa kufanya ni kutuma vijana wako wakamkakate alafu ndio mahojiano yaanze" Babu wa monchwari alimshauri Mkuu wa polisi,
"Usinifundishe kazi mzee, ninachokifanya hapa ninakijua" Mkuu wa Polisi aliongea kwa hasira,
"Sawa mkuu, aya endelea na maswali" Babu wa Monchwari alijikuta ananywea na kuwa mtumwa kwa muda ule mfupi,
"Je kwa ujuzi wako, mtuhumiwa anaweza kuwa na silaha ya moto kama bastola au bunduki?" Mkuu wa polisi aliendelea kuhoji,
"Mimi ninapajua anapokaa tu, hayo mengine siyajui" Babu wa monchwari alijibu lakini sura yake ilionesha hakuyapenda kabisa hayo maswali, kwa maana aliona kama yanamchelewesha tu,
"Nimekuuliza hivyo ili nijue tumuingiliaje tutakapoenda kumkamate" Mkuu wa polisi alimuelesha Babu wa monchwari baada ya kugundua hapendi kuulizwa,
"Ana mwili wa kawaida tu, ni kakijana tu kachekibobu ambacho hakawezi kushika hata jembe" Babu wa monchwari alijibu,
Mkuu wa polisi akalainika, akatoka nje, kisha akawatafuta askari watatu aliowaamini, akawapa bunduki, kila mmoja risasi thelathini, kisha akawapa yule Babu kama dira ya safari yao,
"Mwanangu unanipa askari watatu!? hivi unamchukuliaje yule kijana?" Babu wa monchwari aliongea huku anasikitika,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni