Notifications
  • MWALIMU MKUU (6)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA SITAILIPOISHIA...Hatimae rameki alipata nafuu alizinduka Mama ake alifurahi kumuona mwanae akiwa amepata fahamu“””Eeeee mungu kweli umesikia kilio changu asante sana(uku alifurahi)pole mwanangu””IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“”Asante mama”alijibu ramekiMama rameki na mama loly walirudi nyumbani kumchukulia rameki chakula kwani tangu asubui akupata mlo.*********Upande wa bi sani alifurahi…
  • MWALIMU MKUU (5)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA TANOILIPOISHIA...Mama roly alivyosikia rameki anataka kumwaga alimtema yule nyoka na kumficha pangoni mwake, rameki alimpambu mama roli kwa kasi ya ajabu kama ndege ya vita ikimbiavyo angani“Ramekiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!! tombaaaa”rameki na mama roli walipiga madafu kama manne “heeee rameki siamini???!!”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwannn??”rameki aliuliza“DUDU LOTE HILI…
  • MWALIMU MKUU (4)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA NNEILIPOISHIA...Mwalimu mkuu alistuka kuguswa na kitu kwenye makalio yake alijua rameki atakuwa kaweka mzigo nyuma yake rameki alivyoona ajakaa vizuri alisogea ili akae vizuri mwalimu mkuu alistuka kitu kama tango kikimgusa tena alipitisha mkono ili aone nn alistuka “MUNGU WANGUU”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Rameki alistuka mwalimu mkuu alivyoshika tango lake akapaza sauti“AAAAAA MWALIMU…
  • MWALIMU MKUU (3)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA TATUILIPOISHIA...chausiku alishangaa kuziona zile sale “JAMANI NANI KAKUPA MWANANGUU??!!”aliuliza chausiku kwa mshangao“Kaka juma”alijibu ramekiIKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“Oooh juma jamani mungu akubariki ooooh asante mungu”alitamka mama rameck uku akinua mikono juuRameck alizijalibu zile nguo hakika alipendeza sana adi mama ake alimfagilia kwa vigeregere “jamani juma mungu akuwekee…
  • MWALIMU MKUU (2)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA MBILIILIPOISHIA...“MUNGU WANGU YULE SI MZEE ALINANI???!!!”aliuliza chausiku kwa mshangao chausiku alimuangaria mzee alinani ambae amepoteza furaha yake ya kusomaMzee alinani alikuwa anakuja kuangaria bishala zake pale sokoni kwa kina chausiku.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Mzee alinani alistuka kumuona chausiku alikwepesha macho yake kwa aibu alitoka kwenye soko lile, chausiku alimpitia…
  • MWALIMU MKUU (1)
    Jina: MWALIMU MKUUMtunzi: __SEHEMU YA KWANZA“MAMA USIFE MAMA NITAISHI VP NA HII MIMBA MAMA”ilikuwa ni sauti ya mdada aitwae chausiku akimwambia mama ake asifee bado anamtegemea mama ake na mimba yakee“CHAUSIKU MWANANGU NAJUA MIMI NDIYO TEGEMEZI LAKOO NILIPAMBANA NA KILIMO ILI USOMEE LAKINI UMECHEZEA SHIRINGI CHOONI MWANANGU UMESHIKA MIMBA BADO MWAKA MMOJA TUU UMALIZE LAKINI NDO IVYO MWANANGU MIMBA NDO ISHAINGIA SINA BUDI KUKUFUKUZA INGALI UKO MOYONI MWANGU NAKUPENDA MWANANGU CHAUSIKUU ILA…
  • THE NIGHTMARE (9)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TISAILIPOISHIA...“mmenifananisha, mimi ndio kwanza naigia ofisini mida hii.” Aliongea yule afande na kuigia kituoni.“sasa aliyekuwa anatuhoji ni nani kama sio huyo?”Alijikuta anajiuliza mwenyewe swali lililompa utata mkubwa kichwani mwake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wakati wakiwa hawajui hili wala lile, walishangaa kuona maaskari wakijazana pale na ambulance ikafika…
  • THE NIGHTMARE (8)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NANEILIPOISHIA...Walipofika feri, walipewa nahodha mwingine tofauti na yule aliyemuota na boti ilikuwa ndogo tu ya kawaida tofauti na ile aliyoiota.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Sharji alijikuta anapiga makelele baada ya kumuona Balqis akiwa amejaa damu mdomoni huku ametoa makucha yake akimfata kwa nia ya kumdhuru.“AAAAAAAAAAAGH”Sharji alipiga kelele na kukurupuka.…
  • THE NIGHTMARE (7)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SABAILIPOISHIA...“kha!!!!”Ulikua mshangao mkubwa kwa watu karibu wote baada ya kumuona Sharji akiwa na taulo akitoka chumbani kwa Balqis.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wengine walicheka na kaka yake alionekana kutoifurahia hali ile.“sasa wewe unatutia wasi wasi bure, si ungesema tu kama unaenda kulala kwa huyu dada?” aliongea kaka yake na kukirudia kile chumba alichompangia…
  • THE NIGHTMARE (6)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SITAILIPOISHIA...“toa loud speaker bwana.”Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya…

KIJIJINI KWA BIBI (25)

Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO
TULIPOISHIA...
"we happy vipi, una nini leo?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti

yake kwa sauti yenye mshangao huku akiusukuma mlango kwa utaratibu

mzuri ili asimdhuru binti yake aliyekuwa amelala,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"baba sijisikii vizuri, naona kizunguzungu", Happy aliongea huku

akiwa bado amelala chini.

Baba yake akamnyanyua, kisha akamrudisha chumbani kwake,

"nikupelekee hospital mwanangu?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti

yake kwa sauti ya huruma,

"hapana baba, nafikiri ni tatizo la muda", Happy alijibu huku

akijifunika shuka,

"Hapana, lazima uende hospitali, ngoja nimalize kuoga nikupeleke"

Mchungaji Wingo alimwambia mwanae,

"Baba hii hali ya kawaida tu, itaisha" Happy alijibu baba yake,

"Usichukulie vitu kirahisi rahisi, we jiandae tu nikupeleke"

Mchungaji Wingo aliongea huku akitoka nje.

"hii ya leo balaa, sijui baba angenichukuliaje?", Happy alijiuliza

mwenyewe huku akiwa na tabasamu la mshangao na pia akimshukuru

Mungu kwa kumuepusha na dhahama hii.

Omari alipotoka kwa mchungaji mbio mbio mpaka alipofika nyumbani,

akasukuma mlango akaingia kwa fujo hadi ndani,

"ehe, vipi mwenzetu?", Omari alipokewa na sauti ya Sajenti Minja

aliyekuwa anamshangaa,

"nilikuwa nakimbia kimbia, kuweka mwili fiti", Omari alijibu akiwa

katika tabasamu la uongo huku akipumua bila mpangilio,

"haya bwana, mi nilifikiri umefumaniwa na mke wa mtu uko, maana

mbio ulizokuja nazo si mchezo", Sajenti Minja aliongea na kufanya

vicheko vilipuke sebule yote.

"Hanna mjomba, huku ugenini siwezi kufanya hivyo" Omary alijibu

huku akijilazimisha kutabasamu,

"Sisi tutajuaje bwana, nyie vijana mna mambo mengi" Mama Kayoza

aliongea,

"Hakuna mama" Omari aliongea huku akiingia ndani, akamwita Kayoza,

wakaingia ndani,

"duh, jomba uko noma", Omari alianza kwa mtindo huo,

"vipi tena baab?", Kayoza akauliza kwa mshtuko,

"mchungaji kanikuta juu ya mwili wa mwanae kaka", Omari akapasua

lililomkuta,

"naisi kama sijakusikia vizuri vile, ebu rudia", Kayoza akauliza

kwa stahajabu,

"nimesema kuwa, mchungaji kanikuta ndani kwake", Omari akaongea

tena alichomaanisha,

"ikawaje kaka?", Kayoza akauliza huku akiwa bado haamini

anachoambiwa.

Omari akamsimulia yote, mpaka alipofanikiwa kukimbia.

"duh, pole mwanangu", Kayoza akampa pole Omari,

"Cha kushukuru ni kuwa nimetoka salama" Omary aliongea huku akivua

fulana yake,

"Sasa huyo Happy kwa hali uliyomuacha nayo si itakuwa baba yake

amejua?" Kayoza aliuliza,

"Sijui bwana, kama baba yake atahisi labda inaweza kuwa tatizo, ila

kuniona hajaniona" Omary alimjibu mwenzake,

"Ila usirudie kufanya ujinga kama huo tena, yule mwanamke ni

shetani angalia usiwe unamsikiliza kila anachokushawishi" Kayoza

alimshauri Omary,

"haina noma, kuna mpya gani hapa?", Omari akauliza,

"kesho saa nne tutaenda kwa mganga", Kayoza akamtaharifu Omari.

"maeneo gani",Omari akauliza,

"mi mwenyewe sijajua bado", kayoza akajibu,

"Dah, Mimi nina wasiwasi yasije yakatokea kama ya kwa yule mganga"

Omary aliongea,

"Sasa usiseme hivyo, cha muhimu ni kumuomba Mungu tu atusaidie"

Kayoza alimwambia Omary,

"Mungu tunamuomba ila pia tahadhari lazima" Omary alimwambia

Kayoza,

"Basis usiende, nitaenda Mimi na mjomba" Kayoza aliongea huku

akionekana hajafurahishwa na maneno ya Omary,

"Nitaenda tu" Omary aliongea kwa upole baada ya kugundua Kayoza

amepaniki,

"Sasa kama utaenda kwanini unaleta maneno ya kutishana?" Kayoza

aliuliza,

"Basi yaishe kaka, nisamehe kwa maana sikudhani kama utamaindi"

Omary aliamua kujishusha ili mambo yaishe,

"Hatugombani hapa, tunaeleweshana tu" Kayoza alimwambia Omary,

"Sawa nimekuelewa ndugu yangu" Omary alijibu,

"Kama umenielewa sawa, Mimi nipo sebuleni" Kayoza aliongea huku

akielekea nje na kumuacha Omary akiwa amejimwaga kitandani.

.*

Kesho yake asubuhi Sajenti Minja aliwapitia wakina Kayoza, na

safari ya kwenda kwa mganga ikaanza.

Njia nzima hakuna alieongea, ndani ya gari kulikuwa na mziki laini

wa unbreak my heart ulioimbwa na mwanamama wa kimarekani

anayejulikana kama Tony braxton.

Sajenti Minja alikuwa akiufatilia ule wimbo kwa sauti ya chini,

Omari yeye alikuwa na mawazo yake, Kayoza pia alikuwa anafikiria

anachokijua.

"Huo wimbo vipi?" Kayoza aliuliza baada ya Sajenti Minja kurudia

zaidi ya mara tatu kuupiga ule wimbo,

"Si naupenda tu" Sajenti Minja alijibu kwa kifupi,

"Mimi najua mtu akiupenda wimbo lazima kuna tukio linahusihana na

huo wimbo" Omary alichangia,

"Ebu acheni ujuaji, sasa mnataka niweke nyimbo gani? au niweke hayo

manyimbo yenu yenye yo yo nyingi?" Sajenti Minja aliuliza,

"Wewe tuambie tu kuhusu huo wimbo, acha kujikanyaga" Kayoza

alimwambia mjomba ake huku akicheka,

"Au shangazi hasomeki?" Omary akaongeza na swali,

"Ebu niacheni bwana" Sajenti Minja aliongea huku akizima redio ya

gari.

Kwa mganga waliingia mishale ya saa sita kasoro robo, wakapokelewa

na msaidizi wa mganga, ila kwa bahati nzuri hawakukuta foleni

ndefu, watu walikuwa wachache tu.

Baada ya nusu saa, zamu yao ikafika wakaingia ndani, kile kitendo

cha kayoza kuingiza mguu katika mlango wa nyumba ya mganga, pale

pale akabadilika na akawa katika taswira ya kutisha sana, ila

alikuwa hawezi kutembea, aliganda pale pale, Sajenti Minja alipata

uoga huku akidhani kuwa zile bakora za kipindi kile zinarudi tena

kwa hiyo akakaa mbali kabisa na Kayoza hata alipogundua kuwa Kayoza

ameganda pale, bado alikuwa anaogopa kumsogelea. Unacheza na viboko

nini.

Mganga akapelekewa taharifa kuhusu lile tukio, Mganga ikambidi

atoke katika chumba chake cha kazi na kwenda mahali alipo Kayoza,

alipofika akamuangalia zaidi ya dakika kumi, kisha mganga akafunga

macho yake, alafu akatoa pumzi kumuelekea kayoza kwa njia ya mdomo,

pale pale Kayoza akadondoka chini huku akiwa katika ile ile taswira

ya kutisha.

"Mtoeni nje" Mganga akawaamuru wamtoe nje, wakambeba wakampeleka

nje, wateja waliokuwa nje wanasubiria tiba wote walikimbia

walipomuona Kayoza katika hali ile ya kutisha.

"Aliyekuja na huyu kijana yupo Wapi?" Mganga aliuliza huku

akimuangalia msaidizi wake,

"Yule kule" Msaidizi wake aliongea huku akinyoosha kidole kuelekea

alipo Sajenti Minja,

"Mbona amekaa mbali sana?" Mganga aliuliza huku akishangaa,

"Hata sisi hatujui, labda anamuogopa" Msaidizi wake alijibu,

"Kamuite" Mganga alimtuma msaidizi wake na yule bwana akaenda

kumuita.

Sajenti Minja alipofika alimsalimia mganga kisha mganga akawaambia

aliefuatana na Kayoza amfuate ndani, Sajenti Minja na Omari

wakamfuata mganga.

Mganga alikuwa ni mwanamke wa makamo, alikuwa na macho mekundu

sana, akamkazia macho Sajenti Minja, kisha mganga akasema,

"Minja mna tatizo kubwa sana" Mganga aliongea na Sajenti Minja

alishtuka kusikia mganga kamtaja jina lake, ila akapata matumaini

ya kumaliza tatizo,

"ila kwako naamini litaisha", Sajenti Minja alijitutumua na kumjibu

mganga,

"bibi yake mzaa baba yupo hai", Mganga akamtupia swali Sajenti

Minja,

"ndio mama", Sajenti Minja akajibu,

"anaishi wapi?", Mganga akauliza tena huku akiwa amemkazia macho

Sajenti Minja,

"anaishi Bukoba vijijini", Sajenti Minja akajibu,

"Sasa itabidi huyo kijana apelekwe uko", Mganga akawaambia Sajenti

Minja,

"tumpeleke wapi?", Sajenti Minja akauliza ili apate ufafanuzi

zaidi,

"mpelekeni kijijini, kijijini kwa bibi yake" Mganga aliongea akiwa

amefunga macho………

"Ebu mtaje, ni upuuzi huu" Mkuu wa Polisi aliongea na kumfanya Babu wa monchwari atulie kidogo kwa maana alikuwa amelisahau jina la Sajenti Minja,

"Mbona humtaji?" Mkuu wa Polisi aliuliza kwa hasira na kumgutusha Babu wa monchwari aliyekuwa bado analitafuta jina la Sajenti Minja,

Baada ya muda akalikumbuka jina, na akaona haina haja ya kuuficha uovu, akaamua kulitaja jina sasa. Kabla hajalitaja kwanza akaamua atabasamu, akatoa tabasamu la ushindi kwa maana alijua akimtaja Sajenti Minja ndio utakuwa mwisho wa mchezo na yeye ndio utakuwa mwanzo wa utajiri wake,

…Babu wa mochwari akaendelea kutabasamu,

"Mzee acha mzaa, nimekwambia umtaje huyo askari" Mkuu wa polisi aliuliza kwa ukali na kumfanya Babu wa monchwari ashtuke,

"askari mwenyewe si yule mwenye nanii, nini ile, ha, nimemsahau, ila nikimuona nitamjua", Babu wa mochwari aliendelea kuongea kwa kujiamini, ila hakutaka kumtaja moja kwa moja Sajenti Minja kwa kuwa alitaka kumfanyia jambo la kushtukiza Mkuu wa Polisi,

"mzee usinichanganye, maana sikuelewi", Mkuu wa polisi aliongea kwa ukali,

"niamini mwanangu, huyo muuaji napajua hadi anapokaa", Babu wa monchwar aliendelea kumwaga sera zake za kumshawishi Mkuu wa Polisi amuamini,

"Anakaa maeneo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Anakaa maeneo ya kota, karibu na kanisani" Babu wa monchwari alijibu huku akitabasamu,

"Mzee unachoongea ni kweli au leo umeamua kunichezea akili tu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimuangalia kwa jicho kali Babu wa monchwari,

"Kama itabainika nakudanganya, niweke ndani hata miaka mitatu" Babu wa monchwari alijibu kwa kujiamini,

"Na wewe ulimjuaje huyo mtuhumiwa, au mna mahusiano naye ya kindugu, ujirani au urafiki?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Babu wa monchwari,

"Mi naona kama maswali yako yanapoteza muda vile, cha msingi ulichotakiwa kufanya ni kutuma vijana wako wakamkakate alafu ndio mahojiano yaanze" Babu wa monchwari alimshauri Mkuu wa polisi,

"Usinifundishe kazi mzee, ninachokifanya hapa ninakijua" Mkuu wa Polisi aliongea kwa hasira,

"Sawa mkuu, aya endelea na maswali" Babu wa Monchwari alijikuta ananywea na kuwa mtumwa kwa muda ule mfupi,

"Je kwa ujuzi wako, mtuhumiwa anaweza kuwa na silaha ya moto kama bastola au bunduki?" Mkuu wa polisi aliendelea kuhoji,

"Mimi ninapajua anapokaa tu, hayo mengine siyajui" Babu wa monchwari alijibu lakini sura yake ilionesha hakuyapenda kabisa hayo maswali, kwa maana aliona kama yanamchelewesha tu,

"Nimekuuliza hivyo ili nijue tumuingiliaje tutakapoenda kumkamate" Mkuu wa polisi alimuelesha Babu wa monchwari baada ya kugundua hapendi kuulizwa,

"Ana mwili wa kawaida tu, ni kakijana tu kachekibobu ambacho hakawezi kushika hata jembe" Babu wa monchwari alijibu,

Mkuu wa polisi akalainika, akatoka nje, kisha akawatafuta askari watatu aliowaamini, akawapa bunduki, kila mmoja risasi thelathini, kisha akawapa yule Babu kama dira ya safari yao,

"Mwanangu unanipa askari watatu!? hivi unamchukuliaje yule kijana?" Babu wa monchwari aliongea huku anasikitika,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
59 Kijijini kwa Bibi Simulizi Z59
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni