Notifications
  • MY DIARY (50)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA HAMSINITULIPOISHIA...Nilimnongo’oneza kuwa atumie kinga ili nisimwambukize ukimwi akanijibu kwa sauti ya mahaba nisiwe na hofu yeye yupo tayari kufa kwa ajili ya penzi langu hivyo hawezi kutumia kinga kwa mke wake aliyemoa tena siku muhimu kama hiyo.Sikutaka kumbishia yeye ndo muaamuzi wa mwisho kuhusu afya yake hivyo nilimuacha aendelee kufanya yake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kumbe na…
  • MY DIARY (49)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TISATULIPOISHIA...Baada ya maneno ya kusilimu ambayo waliambiwa wayatamke kiongozi huyo alisema neno ya mwisho kabla hajashuka.” Kila alie na akili timamu, mwenye busara naa anaetaka haki, na kusimama pamoja na haki, basi akiangalia dunia ilivyo na jinsi inavyokwenda basi lazima kutakuwa na nguvu kuuu nayo ni mwenyezi mungu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuna vitu vingi sana…
  • MY DIARY (48)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA NANETULIPOISHIA...Familia yangu haikukubali kabisa mimi kuolewa na rangi nyeusi hivyo walinitenga na kusema hawanitambui kuwa mimi ni ndugu yao.Lakini kutokana na mapenzi mazito niliyokuwa nayo kwa baba yake na Leah nilijikuta nipo tayari kwa lolote hivyo nikahama na kwenda kuishi Tanzania.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Katika miaka hiyo tuliyokaa nilibahatika kupata mtoto huyu…
  • MY DIARY (47)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA SABATULIPOISHIA...Lakini ilifikia mahali ndoto hiyo inanijia hata mchana nikiwa nimekaa mahali tulivu.Ilikuwa inanipa taswira nzuri ya sehemu ambayo madini yalikuwepo.Basi nilianza mikakati ya kulitafuta eneo hilo na hiyo ni mara baada ya ushauri wa mpenzi wangu Candy hapo akimaaanisha yule dada aliyekuwa naye pale jukwaaani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Candy alinisihii sana…
  • MY DIARY (46)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA SITATULIPOISHIA...Nilikuwa kama niliyepigwa butwaa nisiamini nilichokuwa nakiona mbele yangu. Oooooh my God hold me on yalikuwa ni maneno yaliyonitoka kutoka kwenye uvungu wa moyo wangu mara baada ya kumuona James kwa uzuri zaidi na kuamini kuwa yule kweli alikuwa ni kaka yangu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilishindwa kuelewa nini kimetokea mpaka yeye kurudi katika hali yake ya…
  • MY DIARY (45)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TANOTULIPOISHIA...Ndio niliona hipo haja ya kuokoka na kuishi maisha ya utakatifu kwa maana nishaishi maisha yote ya kuwa mbali na mungu. Nakumbuka nilipokuwa mdogo kipindi hicho naujua mlango wa kanisani tuisahawahi kufundishwa kuwa mtetezi wa kweli wa maisha ya mwanadamu ni Mungu.Na siku zote alaaniwe mtu yule amtegemeaye mwanadamu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Sio kazi ya…
  • MY DIARY (44)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA NNETULIPOISHIA...Yani alianza kutaka uhusiano na mimi tena uhusinao wa mapenzi.Mda wote alikuwa akiniganda kama luba.Na mimi nilikuwa mjanja sana maana nilijifanya sinywi pombe wala kuvuta sigara.Pia baada ya kugundua kuwa wahusika wengine walikuwa wanajiachia niliamua kujifanya mshauri wa mapenzi na mahusiano.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilikuwa nawasshauri sana mshiriki wa…
  • MY DIARY (43)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TATUTULIPOISHIA...Wakati nabadilisha staili kwa kukichua kile kifaa na kukiweka vizuri huku nikibinya ile switch hili iongeze spidi Mark aliingia. Ni kweli nilimuona ila sasa sikuwa na jinsi ilibidi nimalizie furaha hiyo ya uwongo uwongo. Yaani wazungu jamani sijui walifikiria nini maana kile kifaa ukikiminya kwa juu kinakuwa kinajizungusha chenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (42)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA MBILITULIPOISHIA...Uzalendo ulinishinda ikabidi nimuulize ni kwanini bado wanatumia njia hiyo ya kizamani kutunza kumbukumbu wakati siku hizi kuna kitu kinachoitwa Human Resource Informaion system ambapo kumbukumbu zote za wafanyakazi kama waliochishwa kazi, wagonjwa, walioenda likizo ,waliopandishwa vyeo na taarifa nyingine muhimu uhifadhiwa kwa kutumia komputa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (41)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA MOJATULIPOISHIA...Mark anashangaazwa sana na mwanamke huyo lakini kwa kuwa shida yake ilikuwa ni hela anaamua kuachana nae na kuanza maisha mapya hapo jijiini Dar es salaamMaisha yanaendela lakini Mark amekuwa tajiri na mtu mwenye mafanikio sana kiuchumi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Pamoja na mafanikio hayo ni mtu ambaye mapenzi bado yalikuwa yakimuumiza siku hadi siku.Filamu…

KIJIJINI KWA BIBI (22)

Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
TULIPOISHIA...
"jamani mbona unanifanyia hivyo, au kwa kuwa nimekwambia

nakupenda?" Binti Mchungaji alilalamika kwa huruma.

"sikia binti, hapa unapoteza muda wako bure, kiukweli kabisa mi

siwezi kukubalia ombi lako" Kayoza aliongea kwa ujasili kwa maana

aliona bora amueleze ukweli tu kuliko kumpotezea muda,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Binti

Mchungaji alijishusha sana, alafu akajenga chuki kali sana kwa

Kayoza.

"Kwanini umeamua kufanya hivyo? au kwa kuwa nimeamua kukueleza

hisia zangu?" Binti Mchungaji aliongea huku machozi yanamtoka,

"Nimefanya hivi kwa sababu nakupenda na najipenda pia" Kayoza

aliongea kwa sauti ya chini kisha akaondoka kumfuata Omary,

"anajiona mzuri kumbe hana lolote, ni shetani tu ananyonya damu za

watu, na kesho nitaitoa taharifa polisi ili nipate yale mapesa

waliyotangaza" Binti Mchungaji aliongea kimoyo moyo huku akiwa

anarudi kanisani na hasira kibao zikiwa zimemtawala.

"kaka umeniangusha" Omari aliongea huku akitabasamu

"achana nae, mtoto wa mchungaji alafu anaendekeza ukicheche" Kayoza

alijibu.

"Ila mpaka mwanamke akuambie maneno nayo, ujue anakupenda kweli"

Omary alimwambia Kayoza,

"Akampende baba yake na mama yake, mimi sina taimu nae" Kayoza

alijibu kijeuri,

"Sawa bwana, kufanya hivyo umemuepusha na kifo",Omary aliongea,

"Sijamuepusha, sema nimemsogezea mbele kifo kwa maana kifo

hakiepukiki" Kayoza aliongea wakati wanafika eneo la nyumbani kwao.

*""""

Ilipofika alfajili, Sajenti Minja aliondoka kanisani na kuelekea

moja kwa moja nyumbani kwake kupumzika, kwa kuwa alichelewa sana

kulala alijikuta anautandika usingizi mzito.

Mida ya saa nne akakurupuka kitandani kwake, ni kawaida yake

kujisachi anapoamka, hasa pale anapolala na nguo alizotoka kutembea

nazo,

alipojisachi, akakuta hana kitambulisho cha ofisini,

"mh, kitakuwa wapi, ila ngoja nikakicheki kwa dada kule na nidoee

chai kabisa" sajenti Minja alijiongelesha peke yake.

Akaenda kuoga na kujisafisha kinywa kisha akajiandaa ili aende kwa

Dada yake.

Akatoka nje akawasha gari, akaondoka

Binti wa mchungaji aliamka ana hasira sana siku hiyo, aliamka saa

tatu, ila mpaka saa nne alikuwa ameshawapiga makofi wadogo zake

wawili kutokana na hasira alizonazo. Tena aliwapiga kwa makosa

madogo madogo tu yasiyo na msingi.

Binti Mchungaji alipomaliza kazi zake, akaenda kuoga, kisha akanywa

chai, akavaa viwalo vyake vilivyompendeza, akamuaga mama yake kuwa

anaenda kununua nguo.

"leo ndio mwisho wake, anaringa kama hana dhambi!" Binti Mchungaji

aliongea kimoyo moyo wakati akitoka ndani ya geti la nyumba yao na

kuishika barabara iendayo sehemu kilipo kituo kikubwa cha polisi

cha mkoa,

"nikifika pale polisi namueleza askari yeyote, hata wasiponipa hela

sawa, nataka tu nimkomeshe" Binti Mchungaji aliendelea

kujiongelesha Mwenyewe, mara akasikia gari inapiga breki miguuni

kwake, alishtuka na kuruka pembeni mpwa barabara, maana alikuwa na

mawazo kiasi kwamba hakujua kama anatembea katikati ya barabara,

"punguza mawazo dada, mbona we bado mdogo tu" yule dereva wa ile

gari alimwambia binti wa mchungaji.

"samahani kaka yangu" binti wa mchungaji alijitetea.

Kisha yule dereva wa gari akashuka ili kuiangalia gari yake iko

salama, maana breki aliyoipiga ilikuwa Kali sana.

"aha! Kumbe polisi!" Binti Mchungaji alijikuta anahamaki baada ya

kumuona yule dereva wa ile gari amevaa gwanda za polisi.

"ee, kwani vipi?" yule polisi aliuliza huku akimuangalia Binti wa

Mchungaji,

"kuna habari njema nataka kukwambia" Binti Mchungaji alisema huku

furaha yake ikionekana dhahiri machoni pake,

"habari gani hiyo?" yule polisi akamuuliza huku akiwa na shauku ya

kutaka kujua,

Yule binti akageuka nyuma kuangalia kama kuna mtu anakuja,

aliporidhka kuwa hakuna mtu, akasema,

"yule kijana anayenyonya damu za watu anakaa palee" Binti Mchungaji

akasema huku akiionyeshea nyumba ya Mama kayoza ambayo ilikuwa

inaonekana kwa mbali kidogo.

"Una uhakika binti?" Askari aliuliza huku akiwa ahamini

anachoambiwa,

"Twende unipeleke" askari aliongea huku akimfungulia Mlango binti

Mchungaji ambayo aliingia kwenye gari kwa madaha kwa maana

alishaimaliza kazi aliyokusudia kuifanya….

Binti Mchungaji akaingia ndani ya gari na kukaa siti ya mbele,

"Wewe umejuaje kuwa huyo kijana ndiye mnyonya damu?" Askari

aliuliza huku akimuangalia Binti Mchungaji machoni,

"We hutakiwi kuniuliza, unachotakiwa ni kwenda kumkamata" Binti

Mchungaji aliongea,

"Akikataa kuwa sio yeye unafikiri tutafanyaje, inatakiwa uniambie

umejuaje kuwa ndiye yeye ili ninapoenda kumkamata niwe na ushahidi"

Askari aliuliza,

"Ameshawahi kuja kanisani kwetu ili tumuombee ili apone na ahachane

na hayo mambo ya kuua kwa kunyonya damu" Binti Mchungaji alijibu,

"Kumbe hata yeye hapendi we kunyonya damu na kuua?" Askari aliuliza

huku akimtazama,

"Itakuwa hapendi, na ndio maana alikuja kanisani kuombewa" Binti

Mchungaji alijibu,

"Sasa kama hata yeye hapendi kuua kuna haja gani ya kumkamata na

wakati anaonekana ni mtu mwema?" Askari aliuliza,

"Wewe kaka ni hakimu au askari? Maana unauliza tu badala ya kwenda

kumkamata mtuhumiwa, au unaogopa kunyonywa damu?" Binti Mchungaji

aliuliza kwa hasira,

"Samahani, naomba nikuulize swali la mwisho kabla sijaenda

kumkamata" Askari alitoa ombi,

"Sitaki swali, kama hauendi niambie nishuke, mbona askari mpo wengi

tu, nitaenda kuwaambia Askari wengine" Binti Mchungaji aliongea kwa

jeuri huku akiangalia pembeni,

"Naomba uniruhusu tu nikuulize hill swali, baada ya hapo

sitokuuliza tena" Askari aliongea kwa upole,

"Na liwe la mwisho kweli, haya uliza" Binti Mchungaji aliongea kwa

mbwembwe,

"Je huyo mnyonya damu angekua ndugu yako ungetoa taharifa polisi?"

Askari aliuliza huku akiwasha gari,

"Inategemea na undugu wenyewe, kama ni wa mbali namchomea tu" Binti

Mchungaji aliongea huku akifurahi gari kuwashwa kwa maana alipata

uhakika wa kutimiza malengo yake,

"Angekuwa mtoto wa Dada yako au wa kaka yako je?" Askari aliuliza

huku akiliondoa gari,

"Huo ni undugu wa karibu kabisa, siwezi kwenda kumsemea polisi

kamwe" Binti Mchungaji aliongea huku akijitengeneza nywele vizuri,

akiwa bado anajiweka vzuri alishangaa yule askari akisimamisha gari

na kumpiga Kofi zito la usoni,

"Unanipigia nini sasa?" Binti Mchungaji aliuliza huku akiwa

amejishika uso, ila yule Askari hakumjibu, akamuongeza jingine la

uso tena pale pale alipopapiga mwanzo,

"Unanipigia nini sasa?" Binti Mchungaji aliuliza huku akisikilizia

maumivu,

"Hiyo tabia yako ndio imekuponza" Askari aliongea huku akitabasamu,

"Tabia gani jamani" Binti Mchungaji alilamika huku akiwa amejishika

shavu,

"Umbea, sio kila kitu kinatolewa taharifa" Askari aliongea huku

akimuongezea kofi na kisha akafungua mlango wa gari ili yule

msichana ashuke.

Binti akatelemka haraka haraka na yule Askari akaiondoa gari kwa

spidi ya juu.

Gari la yule askari lilipopotea, yule binti mchungaji nae

akahairisha safari yake,

"akha mwenzangu, huyu mmoja tu nimekutana nae njiani kanipiga vibao

namna hii, je nikienda huko polisi si wataniua kabisa?" yule binti

wa mchungaji aliongea huku akiwa ameshika njia ya kwenda kwao.

Sajenti Minja aliingia kwa Dada yake asubuhi na kuwakuta wakiwa

wamekaa,

"Hivi huyu Mchungaji wenu ana binti mkubwa?" Sajenti Minja aliuliza

baada ya salamu,

"Anae binti mkubwa kabisa, kwani vipi?" Mama Kayoza aliuliza,

"Aisee yule sio mtu mzuri kwetu, so nimekutana nae hapo njiani

akanisimamisha na kuanza kunipa habari za Kayoza" Sajenti Minja

aliongea,

"Eeeh, makubwa, amekwambiaje?" Mama Kayoza aliuliza,.

"Ooh Mara mnyonya damu namjua, alikuja kanisa kwetu na kuombewa,

ooh Mara sijui nini, yaani inaonekana anamjua vzuri Kayoza" Sajenti

Minja aliongea,

"Ikawaje sasa?" Mama Kayoza akauliza,

"Aisee nimemuwasha mabanzi, sijui hata kama atarudia tena kusema"

Sajenti Minja aliongea huku akicheka,

"Usiseme hivyo, anaweza kwenda kituoni yule, maana ameshaonekana

sio mtu mzuri" Mama Kayoza aliongea,

" hata akienda atakuwa hana Maelezo ya kutosha" Sajenti Minja

aliongea kwa dharau,

"Tatizo lako wewe ni mpuuzi" Mama Kayoza aliongea kwa hasira baada

ya kumuona Sajento Minja ana dharau

"Sasa Dada mbona unanitukana tena?" Sajenti Minja aliuliza,.

"Mpuuzi sio tusi, mtu anayepuuza jambo ndio huitwa mpuuzi" Mama

Kayoza alimjibu ndugu yake,

"Sijapuuza hill jambo, mimi bado namfuatilia huyo binti ila sidhani

kama ataenda kutoa taharifa polisi" Sajenti Minja aliongea,

"Haya bwana" Mama Kayoza aliongea kinyonge,

"Jana niliangusha kitambulisho changu, alafu hata sijui

nilipokiangushia" Sajenti Minja aliamua kubadilisha mada,

"Kipo ndani, ulikiangushia hapa" Mama Kayoza alijibu,

"Afadhali, maana nilishapatwa na wasiwasi wa kukipoteza" Sajenti

Minja aliongea.

Baada ya kukichukua kitambulisho chake aliaga na kwenda moja kwa

moja hospitali kwa ajili ya kwenda kumuona Msaidizi wa Mganga.

Alifika mapema na moja kwa moja akaenda kumjulia hali Msaidizi wa

Mganga, baada ya kumjulia hali mgonjwa wake, Sajenti Minja

alifarijika kumuona mgonjwa wake amepata nguvu na anatembea kama

kawaida.

Bila kupoteza muda, sajenti Minja akamtafuta daktari, kisha akapewa

ruhusa ya kuondoka na mgonjwa wake, akamchukua hadi nyumbani kwake.

Kisha akampa taharifa mkuu wa polisi kuwa yule msaidizi wa mganga

ametoka hospitali na anakaa nae nyumbani kwake, mkuu akafurahi

kusikia hivyo.

Kayoza na Omari walijua sababu kubwa ya binti wa mchungaji kutaka

kwenda polisi ni kutokana na kukataliwa na Kayoza kuwa mpenzi wake,

Omari akaamua amchukue yeye, ikawa kila siku ni lazima aende kwa

mchungaji, tena gia aliyokuwa anaenda nayo ni kununua maziwa,

taratibu mazoea yakaanza hadi wakazoeana kabisa, mwisho kabisa

Omari akamtongoza binti wa mchungaji, bila iyana alikubaliwa kwa

roho safi, na sasa Omary na Binti Mchungaji wakawa Wapenzi rasmi.

Siku moja mkuu wa polisi alikuwa anafungua mlango wa ofisini kwake,

ndio akawaona askari watatu wakiwa wameongozana na babu aliyefungwa

pingu. Alikuwa ni yule Babu wa monchwari, akawaita, kisha akaingia

ofisini, wale askari na yule babu nao wakaingia,

"hii kesi ya huyu mzee mbona mnaiendesha pole pole sana". Mkuu wa

polisi aliwauliza wale askari.

"ushaidi ndio unatuchelesha mkuu" Askari mmoja alijibu

"niambieni katika uchunguzi wenu mmefikia wapi" Mkuu wa Polisi

akawatupia swali jingine,

"hakuna mwanga wowote tuliopata" yule askari akamjibu tena mkuu wa polisi.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
60 Kijijini kwa Bibi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni