Notifications
  • THE NIGHTMARE (7)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SABAILIPOISHIA...“kha!!!!”Ulikua mshangao mkubwa kwa watu karibu wote baada ya kumuona Sharji akiwa na taulo akitoka chumbani kwa Balqis.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wengine walicheka na kaka yake alionekana kutoifurahia hali ile.“sasa wewe unatutia wasi wasi bure, si ungesema tu kama unaenda kulala kwa huyu dada?” aliongea kaka yake na kukirudia kile chumba alichompangia…
  • THE NIGHTMARE (6)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SITAILIPOISHIA...“toa loud speaker bwana.”Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya…
  • THE NIGHTMARE (5)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TANOILIPOISHIA...Alijikuta outomatic akijisemea kwa mshangao baada ya kumuona dada mmoja mrembo mwenye asili ya kiarabu akiingia mule ndani. Hakuvaa ushungi kama alivyowazoea kuwaona waarabu wengi ambao alikutana nao. Huyu alivaa suruali ya jeanz nyeusi na juu akiwa na kikoti chake cheusi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Kati kati kulikua na nguo Fulani nyeupe iliyonakshiwa…
  • THE NIGHTMARE (4)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NNEILIPOISHIA...Aliongea Khalidi na kuufungua mkanda wa suruali yake na kuanza kumtandika Karim.“unanipiga mimi?...utaona!”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Aliongea Karim na kuondoka huku analia.*****************************Zilipita wiki mbili bila ya Karim kuonekana nyumbani kwao. Sabra alisikitika kidogo kutokana na kuwapenda sana watoto wake japokuwa huyo mtoto mkubwa hakuwa…
  • THE NIGHTMARE (3)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TATUILIPOISHIA...Akiwa hewani akikata mawingu kurudi Tanzania, kichwa chake kilikua na mawazo mengi sana juu ya mume wake. Aliikumbuka siku waliyofunga ndoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Pia alijua kwanini mume wake alipendelea kufanya kazi uingereza na yeye kumfungulia ofisi huku huku Tanzania. Hakujua kuwa kazi anayoifanya mumewe ni ile ya kutembea na tajiri mkubwa…
  • THE NIGHTMARE (2)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA PILIILIPOISHIA...Khalidi alishangaa kuitwa na mtu asiyemfahamu. Alitoka na kwenda kumuangalia huyo mtu maana kiukweli hakua na ndugu aishie hapa Dar hata mmoja anayemfahamu..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Alipigwa na butwaa baada ya kumuona Sabra pale.“ahsante mungu.” Aliongea Khalidi baada ya kumuona tu yule binti pale.“pole sasa kaka yangu, nisamahe mie.” Aliongea Sabra kwa…
  • THE NIGHTMARE (1)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA KWANZANi kipindi cha mvua za masika. Upepo mkali, na mvua kubwa iliendelea kunyesha kwa kasi kila kona ya nchi ya Tanzania.Ipo mikoa iliyofurahia mvua hizo kwa kuwa walikua wanaisubiria kwa hamu kwa ajili ya kilimo. Lakini ipo mikoa iliyokua inapata shida kwa uharabifu wa mazingira na mengineyo mengi.Moja ya miko hiyo ni Dar-es-salaam. Watu wanaoishi katika mkoa huo walichukia mvua mfululizo kutokana na sababu mbalimbali. Biashara nyingi…
  • MY DIARY (50)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA HAMSINITULIPOISHIA...Nilimnongo’oneza kuwa atumie kinga ili nisimwambukize ukimwi akanijibu kwa sauti ya mahaba nisiwe na hofu yeye yupo tayari kufa kwa ajili ya penzi langu hivyo hawezi kutumia kinga kwa mke wake aliyemoa tena siku muhimu kama hiyo.Sikutaka kumbishia yeye ndo muaamuzi wa mwisho kuhusu afya yake hivyo nilimuacha aendelee kufanya yake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kumbe na…
  • MY DIARY (49)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TISATULIPOISHIA...Baada ya maneno ya kusilimu ambayo waliambiwa wayatamke kiongozi huyo alisema neno ya mwisho kabla hajashuka.” Kila alie na akili timamu, mwenye busara naa anaetaka haki, na kusimama pamoja na haki, basi akiangalia dunia ilivyo na jinsi inavyokwenda basi lazima kutakuwa na nguvu kuuu nayo ni mwenyezi mungu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuna vitu vingi sana…
  • MY DIARY (48)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA NANETULIPOISHIA...Familia yangu haikukubali kabisa mimi kuolewa na rangi nyeusi hivyo walinitenga na kusema hawanitambui kuwa mimi ni ndugu yao.Lakini kutokana na mapenzi mazito niliyokuwa nayo kwa baba yake na Leah nilijikuta nipo tayari kwa lolote hivyo nikahama na kwenda kuishi Tanzania.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Katika miaka hiyo tuliyokaa nilibahatika kupata mtoto huyu…

KIJIJINI KWA BIBI (24)

Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
TULIPOISHIA...
"Mahakamani tena?, si nitafungwa jamani mie?" Babu wa monchwari

aliuliza huku akilalamika,

"Sasa sisi hatutaki ufungwe, na ndio maana tunaendelea kukuhifadhi

ili utusaidie kumpata huyo aliyeichukua hiyo maiti" Polisi

alimwambia Babu wa monchwari,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"Sasa mbona sioni juhudi zozote ukizifanya kumtafuta huyo mtu na

nilishawahi kumuona eneo hili huyo mtu mwenyewe" Babu wa monchwari

aliongea na kumfanya Mkuu wa polisi ashtuke kidogo,

"Alikuwa anafanya nini na kwa nini hukuwaambia Askari?" Mkuu wa

polisi aliuliza huku akimshangaa,

"Kitu ninachokishangaa ni kwamba alipotea ghafla, inawezekana

kabisa yule bwana si mtu wa kawaida, atakuwa mshirikina tu" Babu wa

monchwari aliongea,

"Kumbe ukimuona kwa sura unamjua vizuri tu?" Mkuu wa polisi

aliuliza,

"Vizuri sana tu, hata akiwa mbali namtambua" Babu wa monchwari

aliuliza,

"Ulivyomuona alivaaje, au alivaa kiaskari?" Mkuu wa polisi

alimdadisi Babu wa monchwari,

"Hajavaa kiaskari, na kwanza hawezi kuwa askari yule, ana ndevu

kabisa" Babu wa monchwari alijibu,

"Basis usijali babu, tunaendelea kufuatilia" Mkuu wa Polisi

aliongea,

Kisha yule askari aliepigiwa simu aliingia na kisha akamchukua Babu

wa mochwari na kumrudisha rumande.

Wakina kayoza walipofika kwa Mchungaji Wingo, walimkuta Binti wa

mchungaji anafagia fagia

"karibuni", Binti wa mchungaji aliwakaribisha alipowaona,

"asante, za hapa?", Omari alijibu alafu akamjulia hali,

"poa my husband, Kayoza mambo?", baada ya kujibu salamu ya Omari,

binti wa mchungaji akamgeukia Kayoza,

"poa, kuna maziwa ya mtindi?" Kayoza akamjibu kwa mkato, kisha

akasema kilichompeleka,

"yapo, mnataka kiasi gani?" Binti Mchungaji akauliza,

"nusu lita" Kayoza alijibu huku akimpatia pesa, Binti wa mchungaji

akachua hela kisha akaingia ndani kuwapimia maziwa.

"kaka uko siriazi, hutaki hata kucheka nae", Omari alimwambia

kayoza huku akijichekesha

"boya sana huyu demu", Kayoza aliongea akiwa na chuki za wazi kwa

binti wa mchungaji.

Baada ya dakika tano binti wa mchungaji alitoka, akawapa maziwa

,"Omari baki, kuna kitu kizuri nataka kukwambia", Binti wa

mchungaji alisema,

"nibaki?, kwani ndani uko na nani?", Omari alimuhoji Binti wa

mchungaji,

"niko peke yangu, wote wameenda mjini, ila baba kaenda kanisani",

ndivyo alivyojibu,

"Boy we tangulia, mimi ninakuja" Omary alimwambia Kayoza,

"Sasa nikifika peke yangu mama si ataniuliza?" Kayoza alihoji,

"Utajua namna ya kumdanganya, ila hata sitochelewa" Omary aliongea,

"Poa, jitahidi kuwahi bwana" Kayoza aliongea huku akianza kuondoka.

"Twende ndani basi" Binti Mchungaji alimwambia Omary huku akimvuta

mkono,

"Huogopi?" Omary aliuliza huku akijatahidi kutosogea zaidi ya pale

alipo,

"Twende ommy, utaniudhi ujue" Binti Mchungaji aliongea sauti ya

kudeka na kumfanya Omary alegeze msimamo,

"Una hatari sana" Omary aliongea huku akipiga hatua kumfuata binti

mchungaji

"Twende usiogope, awa hawarudi sasa hivi" Binti Mchungaji aliongea

huku akifungua mlango wa chumbani kwake,

"Bora ungenipeleka sebuleni, huku ndio pabaya kabisa" Omary

aliongea huku akiingia katika chumba cha Mchungaji,

"Kelele bwana, kaa hapo mimi nakuja sasa hivi" Binti Mchungaji

aliongea huku akimkalisha Omary kitandani,

"Uwahi basi" Omary aliongea wakati Binti Mchungaji akitoka,

"Nakukuja sasa hivi, kuna kazi naenda kuimalizia chap chap" Binti

Mchungaji aliongea na kisha akatoka nje baada ya kuurudishia

mlango, Omary akabaki chumbani peke yake huku macho yake yakitalii

katika kila kona ya chumba kile cha Binti Mchungaji.

Baada ya Binti mchungaji kumaliza kazi, akaenda kujisafi mwili,

kisha akarudi chumbani kwake na kufunga mlango kwa ndani,

"we mtoto huogopi?, Omari alimuuliza huku akiwa na sura ya

wasiwasi, Binti wa mchungaji badala ya kujibu, yeye akaitoa ile

khanga aliyotokanayo kuoga na kubaki mtupu kama alivyozaliwa, Omari

akili ilimruka na uoga wote ukamtoka, bila kutarajia akamvuta binti

wa mchungaji kitandani, na kuamia katika ulimwengu mwingie.

Mchungaji Wingo aliporudi nyumbani kwake, akakuta mlango wa mbele

uko wazi, video sebuleni inawaka, akamuita binti yake, lakini

hakupata jibu, akaamua aende akamuangalie chumbani kwake,

alipokaribia mlango wa chumba cha binti yake, alisikia mlio wa

kitanda cha binti yake kikilalamika kwa fujo,

"mh..", mchungaji Wingo aliguna…

…mh", mchungaji aliguna, kisha akagonga mlango, mlio wa kitanda

ukakoma, kisha ukimya ukatawala,

we happy", Mchungaji Wingo akamuita binti yake,

"abee baba", happy akaitika,"una shughuli gani umo ndani?",

Mchungaji Wingo akamuuliza, kimya kikatawala tena, ila cha sasa

hivi kilikuwa kirefu kidogo,

"mbona hujibu?", Mchungaji Wingo akauliza baada ya ukimya,

"nilikuwa naa…naa…naa.., sijakusikia ulichosema baba", Happy

akashindwa kujibu akawa anajiuma uma tu,

"nimekuuliza una shughuli gani umo ndani, mbona kitanda kinapiga

kelele hivyo?", Mchungaji Wingo akarudia swali katika sauti ya

ukali,

"nafunga neti baba", happy akajibu huku sauti ikiwa na

wasiwasi,"neti tu, ndo kitanda kipige kelele namna hiyo?",

Mchungaji Wingo aliongea huku akiwa anarudi sebuleni, pia

alionekana hakuridhishwa na jibu la binti yake

.*

Ndani baada ya kusikia mtu anagonga hodi, wote walishtuka, ila

hawakukurupuka, wakatulia tuli, baada ya kugundua kuwa anaegonga ni

mchungaji, happy aliteremka chini taratibu kisha akavaa kanga yake,

akawa anamjibu baba yake, kipindi hicho chote, Omari alikuwa

anajing'ang'aniza kupita dirishani bila mafanikio, baada ya

majibizano ya muda mfupi, kati ya happy na baba yake, Mchungaji

aliondoka mlangoni kwa happy, hapo ndipo Omari akapata sauti,

"Sasa nitatokaje nje?", Omari alimuuliza happy kwa sauti ya chini

sana,

"subiri kidogo, sasa hivi anaenda kuoga", Happy alimtoa Omari hofu.

"Happy umeniponza mwenzio" Omary aliongea huku akitaka kulia,

"Acha ujinga wewe, kwani baba amejua kinachoendelea?" Happy

aliuliza kwa ukali,

"Hata kama hajui, wewe unadhani nitatokaje nje?" Omary aliuliza

huku akiwa anafunga vifungo vya shati yake,

"Si nimekwambia ataenda kuoga muda si mrefu" Happy aliongea,

"Sasa mimi nitaaminije?" Omary alijikuta anauliza swali la kipuuzi,

"Mimi hapa ni kwetu, najua ratiba za watu wote hapa, ebu niamini

acha ujinga" Happy alimuelewesha Omary.

"Dah, tamaa nyingine mbaya sana" Omary aliongea peke yake huku

akijifuta jasho ingawa ndani hakukuwa na hali ya joto,

"Unasemaje" Happy alimuuliza Omary baada ya kumuona akiongea ingawa

hakumuelewa,

"Sijasema kitu bwana" Omary alijibu huku akionekana ana hasira I

logic hang any in an a na hofu.

"Mwenzangu ushaanza kuwa chizi" Happy aliongea huku akimcheka Omary

chinichini.

Mchungaji Wingo alipotoka mlangoni kwa binti yake, alienda

sebuleni, kisha akazima luninga, alafu akamuita happy,

"Umeshamaliza kufunga chandarua?" Mchungaji Wingo alimuuliza binti

yake,

"Tayari, alafu sijisikii vzuri" Happy alimwambia baba yake,

"Kwa hiyo umehisi itakuwa malaria na ndio maana ukafunga

chandarua?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akitabasamu,

"Ndio hivyo, mimi nadhani itakuwa ni malaria tu" Happy alijibu huku

nae akitabasamu,

"Kuna maji ya moto?" Mchungaji Wingo aliamua kubadili mada,

"Ndio, yapo…yatakosaje wakati najua watumiaji mpo?" Happy

aliuliza,

"Ebu niandalie nikaoge mie" Mchungaji Wingo aliongea huku

akinyanyuka,

"Sawa mzee" Happy alijibu,

"Mama bado hajarudi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akisimama,

"Wakiendaga mjini wanawahigi kurudi kwani?, hiyo ni mpaka saa kumi

na mbili jioni" Happy alijibu baba yake,

"Huyu nae bwana, si ahache kwenda uwage unaenda wewe?, yeye

ameshaanza kuzeeka" Mchungaji Wingo aliongea kwa kulalamika,

"Wivu tu huo, muache aendage yeye, maana ndio anajua mahitaji ya

watoto" Happy aliongea wakati baba yake anaelekea chumbani.

Happy akaenda bafuni akachukua ndoo na kwenda nayo jikoni ambapo

aliiwekea maji ya moto na kuirudisha tena bafuni.

"Maji yapo tayari baba" Happy alipaza sauti kumwambia baba yake

aliyekuwepo chumbani,

"Oooh nakuja, umeshayachanganya na maji ya baridi?" Mchungaji Wingo

aliuliza huku bado akiwa ndani,

"Utachanganya mwenyewe, maana Jana nilivyokuchanganyia ulilalama

nimezidisha ubaridi" Happy alimwambia baba yake,

"Bora hujachanganya, maana Sikh hizi nahitaji maji ya uvugu vugu

mkali kidogo" Mchungaji Wingo aliongea huku bado akiwa chumbani,

"Umeshaanza kuzeeka ndio maana unataka maji yenye joto Kali" Happy

alimwambia Baba yake huku akiwa bado amesimama mlangoni,

"Kweli aisee, naona umri unanitupa mkono" Mchungaji Wingo aliongea

huku akitoka ndani akiwa amejifunga taulo lake kiunoni na moja kwa

moja akanyoosha mpaka bafuni.

Alipoingia, akatoa taulo lake mwilini,

"mh..kumbe sabuni imeisha?", mchungaji aliongea peke yake, baada ya

kuangalia sehemu ya kuwekea sabuni ikiwa tupu mule bafuni,

Mchungaji Wingo akakata shauri la kurudi kutoka bafuni na kurudi

chumbani ambapo ndipo huifadhi sabuni nyingine.

Happy Binti Mchungaji alipoona kuwa baba yake kaingia bafuni,

akaingia chumbani haraka,

"Tayari baba ameingia bafuni, twende nikutoe nje" Happy aliongea

kwa sauti ya chini ambayo ilisikika vyema masikioni mpwa Omary,

''Sasa njia tunayotokea si ndipo lilipo bafu, akisikia hatua za

watu wawili zinatembea si atagutuka?" Omary alimuuliza happy Binti

Mchungaji,

"Hawezi kugundua bwana, twende acha uoga" Happy aliendelea

kumwambia Omary,

"Sasa si bora nisubiri Stoke bafuni aende chumbani?" Omary

aliuliza,

"Acha ujinga, mama anarudi sasa hivi na wadogo zangu, wakikukuta

humu, je itakuwaje?" Happy nae aliuliza,

"He!!!! Leo kweli siku yangu, haya twende" Omary aliongea kinyonge

huku akisikitika.

Happy akamshika mkono Omary, kisha akaanza kutoka nae nje kwa

mwendo wa kunyata, yaani mwendo wa taratibu usiokuwa na vishindo.

Walipofika usawa wa mlango wa baf na ndio muda huo Mchungaji Wingo

alikuwa anafungua mlango ili akachukue sabuni chumbani.

Ghafla tu Omary na Happy binti Mchungaji wakashuhudia mlango wa

bafu ukifunguliwa na wote macho yakawatoka pima mithili ya mtu

aliekwamwa na kitu kooni…

Happy akauwai mlango wa bafuni, akaushikilia, tena kwa kuwa mlango

wenyewe ulikuwa unafunguka kwa nje akaamua aulalie kabisa, Omari

kuona hivyo akahisi kitakachomsaidia ni nduki tu. Akatoka mbio

kuelekea nje,

"we happy vipi, una nini leo?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti

yake kwa sauti yenye mshangao huku akiusukuma mlango kwa utaratibu

mzuri ili asimdhuru binti yake aliyekuwa amelala,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
60 Kijijini kwa Bibi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni