KIJIJINI KWA BIBI (24)
Zephiline F Ezekiel
5 min read
Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Mahakamani tena?, si nitafungwa jamani mie?" Babu wa monchwari
aliuliza huku akilalamika,
"Sasa sisi hatutaki ufungwe, na ndio maana tunaendelea kukuhifadhi
ili utusaidie kumpata huyo aliyeichukua hiyo maiti" Polisi
alimwambia Babu wa monchwari,
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
"Sasa mbona sioni juhudi zozote ukizifanya kumtafuta huyo mtu na
nilishawahi kumuona eneo hili huyo mtu mwenyewe" Babu wa monchwari
aliongea na kumfanya Mkuu wa polisi ashtuke kidogo,
"Alikuwa anafanya nini na kwa nini hukuwaambia Askari?" Mkuu wa
polisi aliuliza huku akimshangaa,
"Kitu ninachokishangaa ni kwamba alipotea ghafla, inawezekana
kabisa yule bwana si mtu wa kawaida, atakuwa mshirikina tu" Babu wa
monchwari aliongea,
"Kumbe ukimuona kwa sura unamjua vizuri tu?" Mkuu wa polisi
aliuliza,
"Vizuri sana tu, hata akiwa mbali namtambua" Babu wa monchwari
aliuliza,
"Ulivyomuona alivaaje, au alivaa kiaskari?" Mkuu wa polisi
alimdadisi Babu wa monchwari,
"Hajavaa kiaskari, na kwanza hawezi kuwa askari yule, ana ndevu
kabisa" Babu wa monchwari alijibu,
"Basis usijali babu, tunaendelea kufuatilia" Mkuu wa Polisi
aliongea,
Kisha yule askari aliepigiwa simu aliingia na kisha akamchukua Babu
wa mochwari na kumrudisha rumande.
Wakina kayoza walipofika kwa Mchungaji Wingo, walimkuta Binti wa
mchungaji anafagia fagia
"karibuni", Binti wa mchungaji aliwakaribisha alipowaona,
"asante, za hapa?", Omari alijibu alafu akamjulia hali,
"poa my husband, Kayoza mambo?", baada ya kujibu salamu ya Omari,
binti wa mchungaji akamgeukia Kayoza,
"poa, kuna maziwa ya mtindi?" Kayoza akamjibu kwa mkato, kisha
akasema kilichompeleka,
"yapo, mnataka kiasi gani?" Binti Mchungaji akauliza,
"nusu lita" Kayoza alijibu huku akimpatia pesa, Binti wa mchungaji
akachua hela kisha akaingia ndani kuwapimia maziwa.
"kaka uko siriazi, hutaki hata kucheka nae", Omari alimwambia
kayoza huku akijichekesha
"boya sana huyu demu", Kayoza aliongea akiwa na chuki za wazi kwa
binti wa mchungaji.
Baada ya dakika tano binti wa mchungaji alitoka, akawapa maziwa
,"Omari baki, kuna kitu kizuri nataka kukwambia", Binti wa
mchungaji alisema,
"nibaki?, kwani ndani uko na nani?", Omari alimuhoji Binti wa
mchungaji,
"niko peke yangu, wote wameenda mjini, ila baba kaenda kanisani",
ndivyo alivyojibu,
"Boy we tangulia, mimi ninakuja" Omary alimwambia Kayoza,
"Sasa nikifika peke yangu mama si ataniuliza?" Kayoza alihoji,
"Utajua namna ya kumdanganya, ila hata sitochelewa" Omary aliongea,
"Poa, jitahidi kuwahi bwana" Kayoza aliongea huku akianza kuondoka.
"Twende ndani basi" Binti Mchungaji alimwambia Omary huku akimvuta
mkono,
"Huogopi?" Omary aliuliza huku akijatahidi kutosogea zaidi ya pale
alipo,
"Twende ommy, utaniudhi ujue" Binti Mchungaji aliongea sauti ya
kudeka na kumfanya Omary alegeze msimamo,
"Una hatari sana" Omary aliongea huku akipiga hatua kumfuata binti
mchungaji
"Twende usiogope, awa hawarudi sasa hivi" Binti Mchungaji aliongea
huku akifungua mlango wa chumbani kwake,
"Bora ungenipeleka sebuleni, huku ndio pabaya kabisa" Omary
aliongea huku akiingia katika chumba cha Mchungaji,
"Kelele bwana, kaa hapo mimi nakuja sasa hivi" Binti Mchungaji
aliongea huku akimkalisha Omary kitandani,
"Uwahi basi" Omary aliongea wakati Binti Mchungaji akitoka,
"Nakukuja sasa hivi, kuna kazi naenda kuimalizia chap chap" Binti
Mchungaji aliongea na kisha akatoka nje baada ya kuurudishia
mlango, Omary akabaki chumbani peke yake huku macho yake yakitalii
katika kila kona ya chumba kile cha Binti Mchungaji.
Baada ya Binti mchungaji kumaliza kazi, akaenda kujisafi mwili,
kisha akarudi chumbani kwake na kufunga mlango kwa ndani,
"we mtoto huogopi?, Omari alimuuliza huku akiwa na sura ya
wasiwasi, Binti wa mchungaji badala ya kujibu, yeye akaitoa ile
khanga aliyotokanayo kuoga na kubaki mtupu kama alivyozaliwa, Omari
akili ilimruka na uoga wote ukamtoka, bila kutarajia akamvuta binti
wa mchungaji kitandani, na kuamia katika ulimwengu mwingie.
Mchungaji Wingo aliporudi nyumbani kwake, akakuta mlango wa mbele
uko wazi, video sebuleni inawaka, akamuita binti yake, lakini
hakupata jibu, akaamua aende akamuangalie chumbani kwake,
alipokaribia mlango wa chumba cha binti yake, alisikia mlio wa
kitanda cha binti yake kikilalamika kwa fujo,
"mh..", mchungaji Wingo aliguna…
…mh", mchungaji aliguna, kisha akagonga mlango, mlio wa kitanda
ukakoma, kisha ukimya ukatawala,
we happy", Mchungaji Wingo akamuita binti yake,
"abee baba", happy akaitika,"una shughuli gani umo ndani?",
Mchungaji Wingo akamuuliza, kimya kikatawala tena, ila cha sasa
hivi kilikuwa kirefu kidogo,
"mbona hujibu?", Mchungaji Wingo akauliza baada ya ukimya,
"nilikuwa naa…naa…naa.., sijakusikia ulichosema baba", Happy
akashindwa kujibu akawa anajiuma uma tu,
"nimekuuliza una shughuli gani umo ndani, mbona kitanda kinapiga
kelele hivyo?", Mchungaji Wingo akarudia swali katika sauti ya
ukali,
"nafunga neti baba", happy akajibu huku sauti ikiwa na
wasiwasi,"neti tu, ndo kitanda kipige kelele namna hiyo?",
Mchungaji Wingo aliongea huku akiwa anarudi sebuleni, pia
alionekana hakuridhishwa na jibu la binti yake
.*
Ndani baada ya kusikia mtu anagonga hodi, wote walishtuka, ila
hawakukurupuka, wakatulia tuli, baada ya kugundua kuwa anaegonga ni
mchungaji, happy aliteremka chini taratibu kisha akavaa kanga yake,
akawa anamjibu baba yake, kipindi hicho chote, Omari alikuwa
anajing'ang'aniza kupita dirishani bila mafanikio, baada ya
majibizano ya muda mfupi, kati ya happy na baba yake, Mchungaji
aliondoka mlangoni kwa happy, hapo ndipo Omari akapata sauti,
"Sasa nitatokaje nje?", Omari alimuuliza happy kwa sauti ya chini
sana,
"subiri kidogo, sasa hivi anaenda kuoga", Happy alimtoa Omari hofu.
"Happy umeniponza mwenzio" Omary aliongea huku akitaka kulia,
"Acha ujinga wewe, kwani baba amejua kinachoendelea?" Happy
aliuliza kwa ukali,
"Hata kama hajui, wewe unadhani nitatokaje nje?" Omary aliuliza
huku akiwa anafunga vifungo vya shati yake,
"Si nimekwambia ataenda kuoga muda si mrefu" Happy aliongea,
"Sasa mimi nitaaminije?" Omary alijikuta anauliza swali la kipuuzi,
"Mimi hapa ni kwetu, najua ratiba za watu wote hapa, ebu niamini
acha ujinga" Happy alimuelewesha Omary.
"Dah, tamaa nyingine mbaya sana" Omary aliongea peke yake huku
akijifuta jasho ingawa ndani hakukuwa na hali ya joto,
"Unasemaje" Happy alimuuliza Omary baada ya kumuona akiongea ingawa
hakumuelewa,
"Sijasema kitu bwana" Omary alijibu huku akionekana ana hasira I
logic hang any in an a na hofu.
"Mwenzangu ushaanza kuwa chizi" Happy aliongea huku akimcheka Omary
chinichini.
Mchungaji Wingo alipotoka mlangoni kwa binti yake, alienda
sebuleni, kisha akazima luninga, alafu akamuita happy,
"Umeshamaliza kufunga chandarua?" Mchungaji Wingo alimuuliza binti
yake,
"Tayari, alafu sijisikii vzuri" Happy alimwambia baba yake,
"Kwa hiyo umehisi itakuwa malaria na ndio maana ukafunga
chandarua?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akitabasamu,
"Ndio hivyo, mimi nadhani itakuwa ni malaria tu" Happy alijibu huku
nae akitabasamu,
"Kuna maji ya moto?" Mchungaji Wingo aliamua kubadili mada,
"Ndio, yapo…yatakosaje wakati najua watumiaji mpo?" Happy
aliuliza,
"Ebu niandalie nikaoge mie" Mchungaji Wingo aliongea huku
akinyanyuka,
"Sawa mzee" Happy alijibu,
"Mama bado hajarudi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akisimama,
"Wakiendaga mjini wanawahigi kurudi kwani?, hiyo ni mpaka saa kumi
na mbili jioni" Happy alijibu baba yake,
"Huyu nae bwana, si ahache kwenda uwage unaenda wewe?, yeye
ameshaanza kuzeeka" Mchungaji Wingo aliongea kwa kulalamika,
"Wivu tu huo, muache aendage yeye, maana ndio anajua mahitaji ya
watoto" Happy aliongea wakati baba yake anaelekea chumbani.
Happy akaenda bafuni akachukua ndoo na kwenda nayo jikoni ambapo
aliiwekea maji ya moto na kuirudisha tena bafuni.
"Maji yapo tayari baba" Happy alipaza sauti kumwambia baba yake
aliyekuwepo chumbani,
"Oooh nakuja, umeshayachanganya na maji ya baridi?" Mchungaji Wingo
aliuliza huku bado akiwa ndani,
"Utachanganya mwenyewe, maana Jana nilivyokuchanganyia ulilalama
nimezidisha ubaridi" Happy alimwambia baba yake,
"Bora hujachanganya, maana Sikh hizi nahitaji maji ya uvugu vugu
mkali kidogo" Mchungaji Wingo aliongea huku bado akiwa chumbani,
"Umeshaanza kuzeeka ndio maana unataka maji yenye joto Kali" Happy
alimwambia Baba yake huku akiwa bado amesimama mlangoni,
"Kweli aisee, naona umri unanitupa mkono" Mchungaji Wingo aliongea
huku akitoka ndani akiwa amejifunga taulo lake kiunoni na moja kwa
moja akanyoosha mpaka bafuni.
Alipoingia, akatoa taulo lake mwilini,
"mh..kumbe sabuni imeisha?", mchungaji aliongea peke yake, baada ya
kuangalia sehemu ya kuwekea sabuni ikiwa tupu mule bafuni,
Mchungaji Wingo akakata shauri la kurudi kutoka bafuni na kurudi
chumbani ambapo ndipo huifadhi sabuni nyingine.
Happy Binti Mchungaji alipoona kuwa baba yake kaingia bafuni,
akaingia chumbani haraka,
"Tayari baba ameingia bafuni, twende nikutoe nje" Happy aliongea
kwa sauti ya chini ambayo ilisikika vyema masikioni mpwa Omary,
''Sasa njia tunayotokea si ndipo lilipo bafu, akisikia hatua za
watu wawili zinatembea si atagutuka?" Omary alimuuliza happy Binti
Mchungaji,
"Hawezi kugundua bwana, twende acha uoga" Happy aliendelea
kumwambia Omary,
"Sasa si bora nisubiri Stoke bafuni aende chumbani?" Omary
aliuliza,
"Acha ujinga, mama anarudi sasa hivi na wadogo zangu, wakikukuta
humu, je itakuwaje?" Happy nae aliuliza,
"He!!!! Leo kweli siku yangu, haya twende" Omary aliongea kinyonge
huku akisikitika.
Happy akamshika mkono Omary, kisha akaanza kutoka nae nje kwa
mwendo wa kunyata, yaani mwendo wa taratibu usiokuwa na vishindo.
Walipofika usawa wa mlango wa baf na ndio muda huo Mchungaji Wingo
alikuwa anafungua mlango ili akachukue sabuni chumbani.
Ghafla tu Omary na Happy binti Mchungaji wakashuhudia mlango wa
bafu ukifunguliwa na wote macho yakawatoka pima mithili ya mtu
aliekwamwa na kitu kooni…
Happy akauwai mlango wa bafuni, akaushikilia, tena kwa kuwa mlango
wenyewe ulikuwa unafunguka kwa nje akaamua aulalie kabisa, Omari
kuona hivyo akahisi kitakachomsaidia ni nduki tu. Akatoka mbio
kuelekea nje,
"we happy vipi, una nini leo?", Mchungaji Wingo alimuuliza binti
yake kwa sauti yenye mshangao huku akiusukuma mlango kwa utaratibu
mzuri ili asimdhuru binti yake aliyekuwa amelala,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni