SORRY MADAM (59)
Zephiline F Ezekiel
5 min read
SEHEMU YA HAMSINI NA TISA
ILIPOISHIA...
“Tuachane kwanza na hayo,mume wako yupo?”
“Nimeachana naye?”
“Umeachana naye,kisa ni nini kilicho wafanya muachane?”
“Wee acha tuu.Ila kila kitu wewe unakijua?”
“Mimi,mbona kama sikumbuki?”
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
“Eddy usinikumbushe ya nyuma”
“Kweli? Ok labda nikutokana na kupoteza kwangu kumbukumbu”
Nilizungumza kwa sauti ya upole kwa kumtega Madam Mery. Ukimya wa dakika kama tatu ukapita huku kila mmoja akiwa atamtazama mwenzake
“Mery”
“Una nipenda?”
“Ehee?”
“Unanipenda?”
“Mimi?”
“Wewe,ndio?”
“Ndio”
“Kwa nini umeamua kutembea na rafiki yangu?”
“Ehee.....ahaaa uun....ajua”
“Najua nini?”
“Wewe.....wewe ulikuwa umepotelea wapi sijui?”
“Hujanijibu swali langu”
“Ahaa Eddy tuachane na hilo bwana”
“Sawa. Nataka kuliona kaburi la mwanangu”
“Eheee”
“Hivi hizo Eheee zako ni za nini, Mimi sizipendi bwana”
“Eddy, Sikumzika mwanao”
Nikakaa kimya nikimtazama ni nini anataka kuniambia
“Ila ile siku nilikuwa nimechanganyikiwaa,na nilipomuwahisha mfanyakazi hospitalini.Nilipo rudi nilikuta mbwa wanamalizia kumla mwanao,huku wewe ukiwa umelaa pembeni”
Nikamtazama Mery kwa macho makali yaliyo anza kuchuruzikwa na machozi ya uchungu
“Wewe ni mama wa aina gani,Hujui dhamani ya utu wa kiumbe ulicho kiweka tumboni miezi tisa.Unaacha kinaliwa na mbwaa?”
“Eddy nilichanganyikiwa,Niliucha mlango wa ndani wazi.Na mbwa ile siku msichana wa kazi aliwafungulia na siku zote mchana wanashinda kwenye banda lao”
“Merry nidanganye kwa kingine ila sio kwa hili”
“Eddy ni kweli.Hata mimi ninauchungu moyoni mwangu kuona kiumbe changu kina.....”
Niliunyanyua mkono wangu kwa kasi na kutaka kumpiga madam Mery kofi la shavuni ila nikajizuia kabla halijatua shavuni mwake na kumfanya afumbe macho.Nikaushusha mkono wangu taratibu na kumtazama Madam Mery kwa macho makali nikaachia msunyo mkali,kabla sijazungumza kitu chochote Manka akaingia na akabaki akiwa anatutizama.Nikajifuta machozi na kutoka jikoni na kuwaacha wao wawili
“Naona umeamua kuniridhi kabla sijafa?”
Sauti yangu ilimstua John ambaye nimemkuta akiwa anapiga hatua za kunyata akielekea kwenye mlango wa kutokea huku nguo zake akiwa ameziweka begani
“Mbona unaondoka bila kuaga?”
John hakunijibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kubaki akiwa amesimama kama mlingoti wa bendera.Kwa ishara nikamnyooshea mkono arudi sehemu alipo kuwa amekaa.Akabaki akiwa amesiama asijue nini afanye,Nikaichomoa bastola kiunoni hapo ndipo nilipo mafanya John,kuanguka chini kama mzigo.Akajizoa zoa na kunipigia magoti
“Eddy....ni shetani amenipitia tu,ila sikukusudia mimi kulala na madam Mery”
John alizungumza huku akimwagikwa na machozi
“John,mimi sina ugomvi na wewe.Tutabaki kuwa marafika hadi mwisho wa maisha yetu.Hawa ni wanawake hawawezi kutugombanisha”
Maneno yangu yakamfanya John kuunyanyua uso wake na kunitazama machoni,akayashusha macho yake hadi shehemu ilipo bastola kisha akayarudisha macho yake usoni mwangu.Nikatambua kuwa anaihofia bastola niliyo ishika,Nikaichomeka bastola yangu kiunoni mwangu.Wasiwasi wa John kidogo ukapugua.Nikaunyuosha mkono wangu na kumpa John,akanipa na yeye mkono wake kisha nikamnyanyua na kumvuta juu na kukumbatiana naye.
“Eddy sijaamini ndugu yangu kama nitakuona tena”
“Hata mimi”
“Asante ka.....”
Sikumpa John nafasi ya kuzungumza chochote,kigoti cha mguu wangu wa kulia kikatua tumboni mwake na kumfanya ajikunje na kutoa ukulele mkoali.Nikamsukuma pembeni kwa nguvu,kwa haraka nikamfwata na kuanza kumpiga mateke ya mbavu.
“HIVI UNAJUA UCHUNGU WA MWANAMKE ALIYE BEBA KIUMBE CHANGU?”
“JOHN UNANIJUA MIMI VIZURI,UNAJUA NI KITU GANI AMBACHO NINAKIFANYA KWA WALE WANAO JARIBU KUNIIBIA KITU CHOCHOTE KUTOKA KWANGU”
Nilizungumza kwa sauti ya juu huku nikiendelea kumpiga John mateke ya mbavu.Kelele za John zikawatoa kwa kasi jikoni Madam Mery na Manka
“Eddy mu......”
Manka alizungumza kabla hajaimalizia sentesi yake,niliichomoa bastola yangu na kumnyooshe na kusimama sehemu alipo.Madma Mery kwa haraka akarudi nyuma ya Manka na kujificha mgongoni mwake.
“Eddy kuwa mpole mpenzi wangu.Kwa nini unafanya hivyo?”
“Manka mimi sio mpenzi wako”
Manka akakaa kimya akinitazama kwa umaki akishindwa cha kuzungumza.Nikamtazma John ambaye amejikunja chini huku akilia.Nikairudisha bastola yangu kiunoni nikampiga John teke jengine la mbavu
“USIRUDIE”
Nikampa John mkono,akabaki akinitazama kwa woga.Nikainama na kuushika mkono wake kwa nguvu na kumyanyua na kumkumbatia
“Wanaume huwa ahtulii”
Nikamuachia John na kumkalisha kwenye sofa.Nikawageukia Manka na Madam Mery,tukatizamana kwa muda
“Mbwa wako wapo wapi?”
“Huko nyuma”
Nikatoa funguo na kufungua mlango na kutoka nje.Nikazunguka nyuma ya gari na kufungua biti ya gari na kutoa turubai lenye mwili wa Derick.Manka akatoka na kusimama mlangoni na akabaki akiwa amenitazama
“Umebeba nini?”
“Unataka kuona?”
“Ndio.”
“Muite huyo mwenzako”
“Nani?’
“Huyo Mery”
Manka akamuita Madam Mery,Madam Mery akatoka akiwa katika hali ya kiunyonge
“Shosti umeniambia umbwa wako wapo wapi?”
“Huku nyuma”
“Nimewaletea chakula,twende basi ukanionyeshe”
Madam Mery akashuka kwenye kibaraza na kuongoza kwenda nyuma ya nyumba yake kwenye mabanda ya mbwa.Kwa uzuri wa yumba ya madam Mery imezungushiwa ukuta ulio mrefu na si rahisi kwa mtu wa nje kuweza kuona chochote kinacho endelea ndani.Nikakuta mabanda manne nyenye mbwa wengi wakubwa kwa haraka ninaweza kuwafananisha na mbwa wa jeshi la polisi kitengo cha kutuliza ghasia(F.F.U)
“Mbwa walio mla mwanagu ni wapi?”
“Hao kwenye hilo banda kubwa”
“Mbona una mbwa wengi hivi”
“Huwa ninawauzia wachina,mbwa mmoja naweza akafka hata dola elfu tatu”
Madam Mery alizungumza kwa sauti ya unyonge.Nikaliweka turubai chini kabla sijalifungua,Manka akaniita
“Eddy naomba funguo za gari,kuna kitu nataka nikachukue ndani ya gari”
Nikaanza kujipapasa mfukoni,wakati ninatoa funguo simu ya mume wa madam Mery ikaanguka.Manka akataka kuiokota ila nikamzuia,Nikamkabishi Manka funguo
“Hakikisha John aondoki”
“Sawa”
Manka akaondoka na kumfanya Madma Mery kubaki kimya akiitazama simu ya mume wake kwa umakini hadi sura yake ikatengeneza mikunjo.Nikaiokota simu na kumpa Madam Mery
“Naomba unishikie hii simu”
“Eddy,hii simu kama ya mume wangu?”
“Ahaaa...wewe si umesema umeachana naye?
“Ahaaaa eheeee”
Madam Mery akabaki akinitazama,Nikalifungua turubai,nikamtazama machoni madam Mery na akastuka kuona viungo vya mwili wa mtu kwenye turubai nililo lifungua.
“Mbwa yupi likuwa mmero kwa kumtafuna mwanangu?”
Madam Mery akabaki akiwa anashangaa shangaa,nikaokota kipande cha mkono na kukirushia ndani ya banda la mbwa wakakivamia na kukigombania kwa haraka na kuanza kukila
“Kwa msosi huu lazima mbwa mmoja utamuuza hata kwa dola elfu kumi”
Madam Mery akabaki akiwa ameuziba modomo wake kwa kiganja cha mkono wake wa kulia.Nikachukua vipande viwili na kuvidumbukiza kwenye banda
“Ed.....si ni mume wangu?”
“Shiiiii,mume wako yupi? Wewe si umeachana naye?”
“Eddy mtu wako nimemfunga kamba,nilimkuta anataka kukimbia”
Manka alizungumza huku akisimama na kujishika kiuno na macho yake yakiwa kwenye turubai
“Eddy si mwili wa mtu huo.....!!?”
Manka alizungumza kwa mshangao
“Kwani vipi?”
“Umeutoa wapi?”
“Wee acha tuu”
“Ni mume wangu”
Madam Mery alizungumza huku akikaa chini,Gafla akaanza kutapika baada ya kuona ninatoa kipande cha utumbo ulio kauka na kuingiza kwenye banda la mbwa.Nikavirusha vipande vyote vya mwili wa Derick kwenye mamanda yote ya mbwa.
“Hichi kichwa Madma utachemsha kama supu ya mbwa wako”
Manka akanitazama kuanzia chini hadi juu,Madam Mery akazidi kutapika.
“Eddy you’re a Mouster”
Manka alizungumza huku akinitazama kwa macho makali.Akamnyanyua Madam Mery.Wakanza kuelekea ndani,Kichwa cha Derick nikakirudisha ndani ya turubai na kulibebe turubai langu na kulirudisha ndani ya buti la gari.Nikaingia sebleni na kumkuta madam Mery akiwa amelazwa kwenye sofa kubwa huku mwili mzima ukimtetemeka
“John yupo wapi?”
Nilimuuliza Manka,ila akakaa kimy akabaki akinitazama kwa hasira.
“Manka si ninaungumza na wewe?”
“Kamtazame huhko jikoni”
Nikaichukua simu ya Derick ambayo Madam Mery ameiweka pembeni ya sehemu aliyo lala
“Sory madam,nilifanya hivi kwa ajili ya damu yangu”
Nikaingia jikoni na kumkuta John akiwa amefungwa kama za mkono na miguuni huku amelazwa chini kifudifudi.Nikakaa pembeni yake
“John shule kunasemaje?”
Nilizungumza kwa dharua,huku taratibu nikimshika shika kichwa chake
“Eddy mbona umekuwa katili kiasi hichi,Unamtuma huyu mwanamke wako kunifunga hivi kama mwizi”
“Wewe unajionaje,Si ni mwizi.Laiti kama ungekuwa hujaniibia madam Mery haya yote yasinge tokea”
“Sawa Eddy,najua kama nimekuumiza ila si kunifanyia hivi.Laiti kama ungejua wema nilio kufanyia wala usinge nifanyia hivi”
“Wema gani?”
“Eddy mimi nimekufanyia mitiahani yako ya kuingia kidato cha sita na umefaulu vizuri”
“Kivipi,wakat wewe una mitihani yako?”
“Eddy mimi nilimuhonga mwalimu wa academy.Aliniruhusu nikufanyie mitihani.Sasa jana wakati ninakuja kumuuliza Madam Mery kuwa anataarifa yoyote kuhusiana na wewe ndipo alipo nishawishi hadi nikalala naye.Halikuwa kusudio langu mimi kufanya hivyo.Kwa bahati mbaya leo wewe ukaja na kutukuta katika mazingira kama hayo”
John alizungumza kwa upolenhadi roho ya huruma ikaanza kunijaa moyoni mwangu
“Eddy,wewe ni zaidi ya ndugu yangu.Kumbuka wapi tulipo toka.Kuanzia kidato cha kwanza tupo pamoja.Hadi sasa hivi,kwa nini lakini ndugu yangu”
“Ila John...wewe tangu kidato cha kwanza.Unajua jinsi nilivyo,mtu yoyote anaye jaribu kuniibia mimi kitu changu chochote nilazima akilipe kwa njia yoyote”
“Ndio ninalijua hili,Na madam aliniambia kitendo cha yeye kufanya hivi ni juzi,alimpigia mumuwe na akapokea mwanamke na akatukanwa sana ndio maana akaamu kunishawishi mimi”
“John.....”
“Naam”
“Nakuomba unisamehe kaka”
Nilizungumza huku machozi yakinimwagika
“Usijali kwa hilo kaka,ninatambua umefanya hivi kwa ajili ya hasira tuu”
“Ni kweli”
Nikaanza kumfungua John kama moja baada ya nyingine.Nikasimama na kumsaidia kumyanyua.
“Mbavu zinaniuma sana”
“Pole,nikupeleke hospitalini”
“Ahaa wee acha tuu nipo vizuri”
Jinsi John anavyo zungumza nilijihisi vibaya moyoni mwangu,nikaanza kujilaumu ni kwa nini nimempiga John pasipo kumuuliza chanzo cha yeye kunisaliti.Tukarudi sebleni na kumkuta madam Mery akiwa amelala na Manka akiwa pembeni yake.Manka akanyanyuka na kunishika mkono na tukatoka nje
“Eddy,japo mimi ni katili ila wewe umezidi”
“Manka naomba hiyo mada uiache”
“Eddy hata kama.Mwili wa binadamu mwenzako unaukausha kama nyama nya ng’ombe”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni