SORRY MADAM (65)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA SITINI NA TANO
ILIPOISHIA...
Sauti ya Mzee Godwin iliendelea kusikika kwenye simu akizungumza kwa sauti iliyo jaa dharau
“Do you know, who will be the next to die?”(Je una unajua, ni nani atafwata kufa?)
“Hhahaahaaaa is your Sheila, na leo nimepata tunda lake kwa mara nyingine tena, Yupo so mwaaaaaaaaaa”(Hhahaahaaaa ni Sheila wako, ........)
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
“Enjoy your day, mr Eddy”(Furahia siku yako, bwana Eddy)
Simu ikakatwa, nikashindwa kuyazuia machozi yangu, kwa mara nyingine Mzee Godwin anawateka watu wangu wa karibu.Dorecy akanishika mkono na kunikalisha kwenye sofa, hasira taratibu ikaanza kupanda na kujikuta mwili wangu wote, ukianza kunitete, Dorecy akanitazama kwenye macho yangu.Mlango wa kuingilia ndani ukafunguliwa na kujikuta nikichomoa bastola yangu na kumuelekezea mlinzi aliye fungua mlango
“Ohooo, ni mimi kaka”
Alizungumza huku akiinyanyua mikono yake juu, huku mkononi akiwa ameshika gazeti
“Unataka nini?”
Nilimuuliza kwa sauti ya ukali
“Ka..ka kuna hili gazeti hapa.....”
“La nini?”
“Kukuuu.....”
“Nitolee kigugumizi chako, kabla sijakuua”
Mlinzi akaanza kutoka ndani
“Wee kaka samahni, hembu hilo gazeti”
Dorecy akanyanyuka na kwenda kulichukua gazeti, akalifungua na kuanza kulisoma huku akipiga hatua za taratibu akirudi sehemu ambayo alikuwa amekaa.Akakaa sehemu yake, sikuwa na haja ya kulitazama gazeti lake.
“Eddy”
Dorecy aliniita na kunifanya nimtazame, nikaikuta sura yake ikiwa imejaa mikunjano akionekana kuna habari iliyopelekea sura yake kuwa katika sura kama hii,Akanyanyuka na kukaa kwenye sofa nililopo mimi.
“Soma, hii habari”
Macho yangu yakatua kwenye maandishi meusi yaliyo andikwa kwa herufi kubwa zinazo onekana vizuri pasipo na shida yoyote
‘MTOTO WA WAZIRI WA AFYA (EDDY GODWIN), ANATAFUTWA NA JESHI LA POLISI KWA MAUAJI YA KIKATILI YA MFANYA BIASHARA WA MADINI JIJINI ARUSHA BWANA DERICK LAMBART NA MWILI WA DERICK KUWA CHAKULA CHA MBWA WAKE’
Chini ya maandishi haya makubwa kuna picha yangu, ya mama na Derick Lambart zikiwa zimeambataishwa kwenye mstari mmoja
“Eddy ni kweli?”
Dorecy alizungumza huku akinitazama machoni, sikumjibu zaidi ya kunyanyuka kwenye sofa, kabla sijamjibu Dorecy nikasikia mlio wa gari ukisimama nje ya geti.Cha kwanza nikazima taa za sebleni na kufungua pazia kidogo la dirisha linalo tazama kwenye geti,Nikawaona askari wawili wakizungumza na mlinzi huku wakionekana kulazimisha kuingia ndani kwa nguvu.
Dorecy akanyanyuka katika kochi alilo kaa na kunifwata nilipo simama,
“Shiit, wamejuaje kama upo humu?”
“Hata mimi sifahamu”
“So, inakuwaje?”
“Tuwauoe?”
“Eddy, usiongeze dhambi nyingine juu ya kuua.Uliyo yafanya yanatosha kwa sasa”
“Sasa wewe unanishaurije?”
“Ngoja nikuonyeshe”
Dorecy, akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine hadi akabakiwa na nguo za ndani(sidiria na chupi), na nguo zake akazificha nyuma ya masofa.Mlinzi alishindwa kuwazuia askari hao kuingia, Dorecy akaniomba nijifiche nyuma ya mlango wa kuingilia.Nikafanya kama alivo niagiza Dorecy, maaskari wakaanza kugonga mlango taratibiu.Dorecy akaisogelaa swichi ya kuwasha taa za sebleni, akaiwasha na kwenda kusimama ulipo mlango
“Fungua”
Nilizungumza kwa sauti ya chini sana, huku nikiwa nimeishika bastola yangu vizuri mikononi mwangu.Dorecy akafungua mlango akiwa katika hali ya nguo zake za ndani, zilizo ufanya mwili wake kuonekana vizuri na kuwa kivutio kizuri mbele ya wanaume marijali.
“Habai zenu maafande?”
Dorecy aliwasalimia, ila salamu yake haikujibiwa kwa sekunde kdhaa, kwa kupitia uwazi wa mlango nikwashuhudia askari wakiwa wamemtumbulia mimacho Dorecy
“Aha....aahaa Salama tu”
“Mmmm, labda niwasaidie nini?”
“Ahaaa”
Askari walibabaika, hawakujua hata wajibu kitu gani
“Karibuni ndani”
“Haya....haya”
Mmoja alizungumza huku akijilamba lamba mdomo wake, wakaingia ndani na Dorecy akaurudishia mlango, na kunnifanya niweze kuonekana vizuri na askari walio ingia ndani.Hawakuweza kufanya kitu chochote kwa sababu, nimeshika bastola, huku nikiwa sina masihara kabisa na kitu ambacho ninakifanya
“Nyoosheni mikono yenu juu”
Niliwaamrisha, wakatii huku wakitetemeka, Dorecy akaanza kuwapapasa na kuwachomoa bastola zao walizo zificha kwenye miguu yeo,Dorecy akawavua mikanda yao ya suruali
“Unawafanyaje?”
“Subiri uone”
Dorecy akaichukua mikanda yao ya suruali, nikawaamrisha waende kukaa kwenye masofa
“Nyinyi, mumekuja kufanya nini?”
Niliwauliza kwa sauti ya ukali
“Tu..lik..uku..ja, kukutaf...uta wewe”
Mmoja alizungumza huku akibabaika sana,
“Nani amewatuma?”
Dorecy alizungumza
“Eheee?”
“Nani amewatuma, au swali langu ni gumu kulijibu?”
Dorecy alizungumza, huku akiizungusha bastola ya mmoja wa polisi
“Ni..ni....nimzee Dodwin”
“Nilijua, tuu”
Dorecy alizungumza, huku akinitazama usoni.
“Simameni kwanza”
Niliwaamrisha na wakasimama, nikawaamrisha tena kuvua nguo zao, wakatii bila ya ubishi.Wakabakiwa na kaptula zao za ndani, nikaamrisha kulala chini, nikachukua pingu zao na kuwafunga mikononi, walio irudisha nyuma, Dorecy akachukua mikanda yao na kuwafunga miguuni kisha akaikutanisha miguu na mikono kwa mamoja na kuwafunga,
“Sasa ninahitai munijibu swali moja baada ya jengine?”
“Munaweza kuniambia ni wapi alipo mama yangu?”
Wakaa kimya, hakuna aliye nijibu hata mmoja.
“Ninarudia tena na tena kuwauliza hili swali.Ni wapi alipo mama yangu?”
“Si hatujuii”
“Hamujui eheee?”
“Ndio”
“Waangalie hawa”
Nikaondoka na kuingia jikoni, nikachukua ndoo ndogo na kuijaza maji mengi, kisha nikachukua fimbo moja ya fagio la kusimama na kurudi navyo sebleni, nikaanza kuwanyunyizia maji ya makalio
“Sasa, hapo utawachapaje?”
Dorecy aliniuliza
“Wafungue huo mkanda nilio wafunga na mikono”
Dorecy alizungumza huku akiendelea kuwanyooshea bastola aliyo ishika, nikamfungua mmoja mkanda ulio fungwa na pingu yake, nilipo hakikisha nimeiachanisha miguu na mikono, nikamvuta pembeni na kumwagia maji ya makalio.Nikaivunja fimbo, ya fagio kugawanyika katika vipende viwili nilivyo viona vinatosha
“Ninakuuliza ni wapi alipo mama yangu?”
“Sijuii mimi?”
Nikamchapa fimbo nne za nguvu kwenye makali, yenye bukta iliyo lowa maji mengi.Jamaa akawa amejikaza makalio yeka, nikamtandika fimbo nyingine nne kwenye mapaja yake, kidogo akaanza kutoa miguno ya maumivu
“Sijuii mimi?”
“Utajua tuu”
Nikaanza kumchapa fimbo zisizo na idadi maalumu ambazo ninajua ni lazima zitampa maumivu ya kusema ni wapi alipo mama yangu, japo mzee Godwin ameniambia kuwa mama amesha fariki, ila sikutaka kuamini kama ni kweli, hadi niuone mwili wa mama yangu ndio nitaamini kwambe amefariki dunia.Fimbo zisizo na idadi nikazidi kuzishusha kwenye makalio ya ya polisi huyu, na akazidi kumwaga machozi ya maumivu
“Huwa mimi ninawashangaa sana nyinyi, kazi yenu ni kulinda mali za raia.Huku kwenye matatizo mengine kama haya munafwata nini?”
“Sijuii,”
“Mimi leo nina wahakikishia kuwa mutajua”
Nikaendelea kumatindika fimbo zisizo na idadi hadi, sehemu ambazo nilizichapa zikaanza kuvimba na kuweka maalama ya fimbo
“Eddy, huyo kakataa kusema bwana, hamishia zoezi kwa huyu”
Dorecy alizungumza, nikamuacha ninaye mchapa na kumfwata mwenzake, nikamuandaa kama nilivyo muandaa mwenzake kabla sijamchapa Dorecy akanizuia
“Lete hiyo fimbo”
Nikamabidhi Dorecy fimbo moja, akamuweka askari vizuri, kwa nguvu zake zote akaishisha vimbo kwenye makalio ya askari na kumfanya atoe ukelele huku akiliita jina la mama yake.Dorecy akashusha fimbo nyingine mbili za nguvu na kumzidisha askari kutoa kelele
“Nasemaa, nasemaa”
“Sema sasa”
Dorecy alizungumza, huku akimwagikwa na jasho jingi,
“Yupo, kwenye mikono ya Mzee Godwin”
“Hilo tunalijua, tunacho kitaka sisi ni kujus ni sehemu gani ambayo yeye yupo?”
“Kule kwenye ule msitu”
Dorecy akanitazama usoni
“Napajua”
Dorecy alizungumza, akamtandika fimbo nyingine ya makalio na kuzidi kumliza askari huyu anaye onyesha bado ni kijana sana.
“Hawa dawa yao ni kuwafungia stoo”
Nilizungumza, huku nikikiondoa kindoo cha maji na kukipeleka jikoni, nikarudi sebleni na kumkuta Dorecy akimalizia kuvaa nguo zake.Nikatoka nje ya nyumba na kumfwata mlinzi getini
“Hawa wehu wamekuja na nini?”
“Kina nani?”
“Hawa askari?”
“Na gari yao ndogo, ipo hapo nje”
“Sasa ilikuwaje ukaacha waingie ndani?”
“Walinionyesha vitambulisho vyao”
Nikatoka nje ya geti na kukuta gari aina ya Corola ikiwa imesimama nje ya geti, nikarudi ndani na kuwaamrisha wanipe funguo za gari lao,
“Ipo kwenye hiyo suruali yangu”
Nikaiokota funguo ya askari aliyechapwa na Dorecy, nikatoka nje na kumuomba mlizi aniungulie geti, nikaingia ndani ya gari lao walilo jia na kuliingiza ndani ya geti na kwenda kulisimamisha nyuma ya yumba yetu pembezoni mwa ‘swimming pool’.Nikamuita mlinzi na kumuomba asaidiane na mimi kuwabeba askari hawa
“Tunawapeleka wapi bosi?”
“Nyuma ya nyumba huko”
“Ila kablwa hatujawapeleka, wavue viatu vyao”
Mlinzi akaanza kuwavua viatu kisha, tukamuanza yule niliye mchapa, kumbeba.Nikaingia kwenye nyumba ya nyuma, kwenye chumba ambacho chini kina handaki.Hata mlinzi mwenyewe akashangaa kwani hakuamini kama chumba hichi kina handaki, lenye ukumbi mkubwa.Tukamuingiza askari wa kwanza na kumfwata askari wa pili na kumuingiza, huku wote wakiwa wamefungwa miguu na mikono yao
“Hakikisha, hawatoki.Pia hakikisha unawapatia chakula mchana na jioni”
“Sawa bosi nimekuelewa”
“Pia hakikisha haingii, mtu yoyote akidai kuwa yeye ni askari au mpelelezi”
“Sawa”
Nikaachana na mlinzi yeye akarudi zake getini na mimi nikaingia ndani, nikamkuta Dorecy akimwalizia kuyafuta maji yaliyo tapakaa chini kwa tambaa.
“Eddy, uhisi njaa”
“Kwa mbali ninajihisi njaa”
“Kwenye friji, jikoni niliona nyama na soseji ngoja nipiki chakula”
“Powa, upendavyo wewe, mimi ninaingia chumbani huku juu”
“Sawa”
Nikaingia ndani kwangu, mazingira ya chumba changu kwa jinsi nilivyo yaacha, hapakuwa na tofauti sana.Nikaingia nikainama chini ya mvungu wa kitanda changu na kulikuta begi lenye madini, niliyo yatoa kwenye handaki.Nikakifungua na kukuta madini yapo kama yalivyo.Nikakirudisha kibegi chini ya mvungu, nikaingia bafuni na kuvua nguo zangu zote, nikasimama mbele ya kioo kikubwa kiichomo humu ndani ya bafu langu
Mwili wangu mzima umejaa, majeraha mengi, yaliyo tokana na mateso niliyo pitia siku chache za nyuma, nikajikuta machozi yakinimwagika kwani hata ule uzuri ambao Mungu aliniumba nao umetoweka kwa kiasi fulani.
“Kwa nini mimi?”
Nilijiuliza swali huki nikitokwa na machozi,
“Nimekuwa, hivi na roho ya kinyama”
“Gereza au kifo ndio mwisho wangu”
Nilizungumza huku nikiendea kumwagikwa na machozi mengi, malengo yangu yote niliyo jiwekea kuja kuwa daktari bingwa nchini Tanzania yametoweka kabisa, hapa ndipo nikaanza kuamini kwamba pesa haitimizi malengo ya mtu, kwani tangu nimezaliwa sikuwahi kuishi maisha ya shida kwani baba anapesa na mama ndio tajiri kupindukia, ila kwa sasa ndio wamekuwa maadui sana.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni