Notifications
  • MY DIARY (22)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILITULIPOISHIA...Alitumia vizuri umbo lake la kimiss kutembea kimiss na kuweka mapozi ya maana. Na baada hapo alilala kwenye kile kigodoro na akachojoa vyote isipokuwa kufuli jeupe ambalo nalo alipewa hapo hapo kwa ajili ya kazi hiyo. IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi sikumpa nafasi Joyce niliingilia nafasi yake na kuchukua ule uume wa bandia nikamfuta yule dada.…
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…
  • MY DIARY (20)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINITULIPOISHIA...Nikamwambia kuhusu namba zangu za simu amuombe aliyemtuma anisaidie na kuhusu hilo la pili je hatuwezi kufanya kesho kwa sababu kuna mahali nilikuwa nikienda? Alifikiria kwa sekunde kadhaa na kuniambia kuwa hapana anaomba nimsaidie leo kama yeye alivyonisaidia mimi kwa sababu ningekuwa kwenye foleni nisingeweza kuondoka kirahisi hivyo kama ninavyofikiria.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (19)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TISATULIPOISHIA...Baada ya hapo niliendelea kumdadisi juu ya tukio lile lakini hakuwa tayari kufunguka zaidi ya kusema aliumia sana. Hapo nikaamua kuutafuta ukweli kwa kutumia mbinu za kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilimwekaa mikono begani na kumwambia pleaee dear naomba uniambie ukweli ili nijue nakusaidiaje? Basi Ramadhani akaanza kulalamika kuwa baba yake amekuwa akimwingilia…
  • MY DIARY (18)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA NANETULIPOISHIA...Halafu eti akawasha simu na kuonesha zile picha alizotupiga kweli huyu rafiki yangu alikuwa hamnazo sio picha tu alituchukua video kabisa na sauti. Akanambia ngoja ampigie paparazi mmoja hivi aje ili atengeneze habari tupate hela. Kauli hiyo ilinikosesha amani na kunikera sana akanmabia eti kuna namna ya kufanya ili sura yangu isitokee.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (17)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SABATULIPOISHIA...Nilijifikiria mara mbili nikajikuta namkubalia kwani alionekana ni mpole na mstaarabu sana.Basi tukaenda hadi kwake ambapo haikuwa mbali na hapo tulipokuwa na kweli alikuwa na chumba na sebule na sebuleni kwake niliona picha ya ukutani akiwe yeye na mke wake nahisi ilikuwa siku ya harusi yao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikasema huyu kijana atakuwa amefunga ndoa…
  • MY DIARY (16)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SITATULIPOISHIA...Mwanamke akaamua kuingia jikoni na kukarangiza viazi na nyama rosti na kilipoiva kililetwa mezani tukaendelea kujenga afya. Sikuaamini kama Joyce alikuwa anakumbuka hata kupika kwa sababu alibadilka sana na alikuwa akiishi maisha ya starehe.. Lakini aliniprovu wrong kwa kutoa rost ya hatari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baada ya kula alinambia kuwa alikuwa amechoka…
  • MY DIARY (15)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TANOTULIPOISHIA...Hapo mzungu wa watu hakuweza kuvumilia tena aliichomeka yote.Mmmmmh mmmmmh ishiiiiiiiiiiii yeaaaaaahhhhhhhh yeaaaaaaah ni miguno niliyoitoa mara baada ya kusikia joto tamu la kiungo hicho.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Ikabid nijivute kwa nyuma ili lengo likiwa ni kukaa vizuri ili kichwa cha nyoka kiwe juu juu ya pango langu ili niweze kukisugua sawa sawa na pia…
  • MY DIARY (14)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA NNETULIPOISHIA...Nikamuuuuliza hivi wewe haugopi maradhi? Akanijibu kuwa angekuwa haogopi basi angeshakufa. Sikiliza Leah hapa nipo na vile vipimo vya ukimwi hivyo usiwe na wasiwasi tutapima wote wanne kama wapo fresh tutaingia kazini wewe si unatafuta hela ya kujiunga na chuo au?IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kabla sijajibu akanambia nitakupa na dawa ya kumeza ya kuzuia mimba na pia…
  • MY DIARY (13)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TATUTULIPOISHIA...Joyce akaanza kujimiminia mwenyewe, kweli dunia ina mambo wakati wenzake wakichanganya nay ale maji makubwa yeye alikuwa akinywa kavu kavu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi mimi sikuwa na jinsi zaidi ya kuaagiza ile bia yangu ambayo alinifundisha yaani savanna. Safari hii hakusubiri ili ifike mwisho ili anitambulishe bali tulivyoanza tu kunywa akawaambia wale…

DHAMANA (22)

Jina: DHAMANA

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
TULIPOISHIA...
"Khaa! Kumbe tupo hapa kwa ajili ya kumuangalia firauni huyo, sina muda huo muache afe  maana huyo ni zaidi ya shetani" Ally aliongea maneno ambayo yalizidi kumshangaza sana Mzee Buruhan na akajikuta  akimtazama  mzee Mahmud akionekana kutoelewa kafanya nini, Ally alinyanyuka ili aondoke lakini mzee Mahmud alimuita akamuomba aketi akakaa chini.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA CnZ Media APP INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"Ally tambua undugu ni kovu na halifutiki usifanye hivyo, najua unaumia kwa kile alichokifanya kaka yako lakini kumbuka ndugu ni ndugu tu" Mzee Mahmud aliongea kwa ustarabu wa hali ya juu akitegemea ataeleweka na Ally lakini haikuwa hivyo.

"Baba zangu mngejua alichokifanya huyo firauni mnayekuja kumuangalua wala msingethubutu kukaa hapa, na sijui hata ni kwasababu gani nilikuwa nikimpenda kwa kipindi chote hicho nahisi aliniroga yule maana miale ya mkufu wake sielewi hata imemifanyaje wakati nilikuwa nikimchukia" Ally aliongea  huku akionesha kumchukia  kaka yake.

"Ally unaongea nini wewe?" Mzee Buruhan aliuliza akionekana kushangaza na maneno anayoyaongea mwanae.

"Mzee mwenzangu kama nilivyokuambia hili tatizo linajulikana ila huyu hatakiwi kulisema na akilisema atakuwa kiziwi kama mwanzo muache huyo Shafii aeleze kila kitu. Unajua..." Mzee Mahmud aliongea maneno yaliyomfanya Mzee Mahmud atulie kimya na alishindwa kumalizia kauli yake baada ya mke wa Hamis kurudi akiwa amebeba chombo cha chakula kwenye mfuko wake.

"Vipi mgonjwa jamani tayari ameshaamka?" Mke wa Hamis aliongea baada tu ya kuwasili na alimuonesha Ally tabasamu kisha akampa mkono akampa mkono ili amsalimie akijua kuwa Ally hawezi kuongea.

Ally hakuupokea mkono wa Mke wa Hamis zaidi ya kusonya kwa nguvu kisha akanyanyuka akasema, "shetani jike mkubwa wewe".

Ally alinyanyuka kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akaelekea mahali akimuacha wazee wake na mke wa Hamis wakimshangaa sana, mke wa Hamis alipotaka kumfuata nje Mzee Buruhan alimshika akamzuia.

"Salma mama naomba unisikilize kwa umakini, achana na Ally kwa sasa kaa hapo usubiri muda wa kumuona mgoniwa akizinduka tukamuone" Mzew Buruhan alimuambia Salma mke wa Hamis.

"Lakini Ally kapatwa na nini wazee wangu kwani alikuwa hawezi kuongea na kusikia ila sasa hivi anaongea na kusikia  ila amekuwa kama akili haziko sawa hadi ananisonya mimi" Salma aliongea huku akishangazwa na hali ya Ally yule aliyekuwa anamsikiliza na kumtii na kumuheshimu ameamua kuonesha dharau.

"Hebu mama kuwa muelewa achana na habari za Ally sasa hivi, tufikirie kuhusu mgonjwa tu" Mzee Mahmud aliongea kwa msisitizo huku  akionekana kutopendezwa na maneno ya Salma.

"Sawa baba zangu nimewaelewa" Salma alijibu kwa shingo upande ili tu asiwaudhi  wazee ambao anawaheshimu.

****

 Wakati Ally akifunguliwa na kuanza kumuoneshea dharau upande wa himaya ya Majichungu Zalabain ndiyo alikuwa amerejea muda huo na aliamua kupitia chumbani walipo mama yake na dada yake ili awaone kutokana na upendo alionao kwao, alibisha hodi kwa adabu ingawa alitambua hata akiingia muda huo asingewakuta wakiwa bila stara. Alipokaribishwa aliingia kwa adabu  na akaenda hadi walipokuwa wamekaa kitandani na akawasalimia, halafu naye  akaketi kitandani jirani yao.

"Mwanangu kila nikikutazama namuona baba yako kwa jinsi wote mlivyokuwa na sura zilizofanana, haya niambie unatoka wapi?" Bi Farida aliongea kisha akamuuliza Zalabain.

"Nilikuwa Tanga kwenye  hospitali ya SBN nilienda kuongea na mzee Mahmud" Zalabain alimuambia mama yake.

"Mh! Huyo mzee huko hospitalini anafanya nini?" Bi Farida aliuliza.

"Amekuja kumuangalia mumeo amelazwa" Zalabain alimuambia mama yake.

"Jamadin sina mume kama huyo mimi tena sitaki kumsikia ukimtaja, mume aliyetakiwa kunioa mimi ni Faimu tu na sijui ilitokea nini mpaka nikamkana na nikamsababishia matatizo makubwa sana akahama kijijini akiwaacha jamaa zake. Nampenda Faimu na natamani nimuone hata leo ili nimuombe msamaha maana yeye ndiyo kila kitu kwangu" Bibi Farida aliongea na  mwishowe akalia kutokana na kujutia aliyoyafanya ya hapa zamani, Zalabain ilimbidi amkumbatie mama yake ambembeleze kutokana na upendo alionao kwake.

"Samahani mama kwa kukupa taarifa smbayo hutaki kuisikia,  sipendi uhuzunike nakupenda sana" Zalabain alimuambia mama yake baada ya kunyamaza.

"Nakupenda pia mwanangu" Bi Farida alisema huku akitabasamu kwa mbali, waliendelea kuongea maongezi mengine kwa furaha wakiachana na suala ambalo lilionekana kutomfurahisha kabisa Bi Farida.

****

 Baada ya masaa mawili Shafii aliamka kutoka usingizini akiwa yupo vizuri kiafya kuliko awali, hali yake iliendelea kutengemaa na ilipofika muda wa alasiri aliruhusiwa na daktari na alirudi nyumbani akiwa ameongozana ns wote waliokuja  kumuona hospitali kasoro Ally tu ambaye hakurudi tangu aondoke pale hospitali. Shafii alipelekwa moja kwa moja chumbani kwake na akaachwa apumzike na kisha wazee wake wakakaa sebuleni hadi ilipoingia jioni ndiyo mzee Buruhan na mzee Mahmud waliingia chumbani kwa Shafii wakamkuta akiwa ameamka ameegemea mito kitandani kwake,  Shafii alipoona ujio wa wazee wale alihisi kuna jambo ila alikaa kimya ili apate uhakika wa wasiwasi wake.

"Shafii" Mzee Buruhan alimuita

"Naam Baba" Shafii aliitikia

"unajua kama wewe ndiyo nguzo kuu kati ya nguzo zangu nne zilizobakia?" Mzee Buruhan alimuuliza

"nafahamu hilo baba" Shafii alijibu.

"Hussein hatunaye, Hamid hatunaye, Hassan ni mdogo kwako, Falzal ni mdogo kwako na Ally pia ni mdogo kwako. Wewe pekee ndiyo mkubwa ndiyo kiongozi wao ingawa wote wana maisha yao na hata wanajisomesha wakitaka kujiendeleza kielimu. Nadhani unatambua hilo" Mzee Buruhan alisema.

"Ndiyo baba natambua hilo" Shafii alijibu.

"Sasa basi inapotokea tatizo lenye kuhitaji kuelezewa ili lisizidi zaidi inabidi lielezewe mwanangu ikiwa utakaa kimya haitasaidia chochote" Mzee Buruhan aliongea.

"Baba sijakuelewa unachomaanisha" Shafii aliongea.

"Shafii najua unatambua suala la upotevu wa mke wako na hata mwanao linalokufanya uwe na matatizo kila kukicha, sasa mwanangu ukilificha itakusaidia nini ikiwa unalifahamu chanzo chake. Kumbuka mficha maradhi kifo humuumbua mwanangu, mwanangu ni bora uitoe aibu mbele ya daktari ili utibiwe kuliko kuficha tatizo halafu ufe na ugonjwa. Ongea chanzo cha  haya ni nini?" Mzee Buruhan alimsihi mwanae.

"Baba kusema ukweli sijui wala sitambui suala hili linasababishwa na nini?" Shafii alikataa.

"Shafii vuta kumbukumbu zako vizuri umefanya nini mpaka yote haya yatokee au hutaki  familia yako uione tena ikiwa na upendo" Mzee Buruhan alizidi kumsihi.

"Baba napenda sana familia niione tena ikiwa ina upendo lakini sikukumbuki chochote kilichosababisha haya ninayofanyiwa"  Shafii alikana kabisa juu ya suala hilo.

"Jirani na mashine ya kusaga unga kule Mpirani miaka ishirini na moja iliyopita unakumbuka kilitokea nini pale kwenye  nyumba yako uliyokuwa unaishi  baada ya wewe kuhama tena ilikuwa majira ya saa sita usiku?" Mzee Mahmud aliongea kwa mara ya kwanza na kumfanya Shafii ashtuke kwa jambo alilotajiwa, lilikuwa ni jambo ambalo alishalisahau kabisa katika ubongo wake na sasa alikumbushwa na mzee huyu ambaye ni mganga mtaalam.

"Shafiii unakumbuka nini hiyo siku" Mzee Buruhan naye aliunganisha maelezo ya rafiki yake ingawa hakuyaelewa kabisa, maneno ya mzee  Mahmud  yalimfanya anyamaze ghafla huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini.

"Shafii si nakuuliza" Mzes Buruhan aliongea huku akimtikisa bega baada ya kuona yupo kimya, Shafii alikurupuka baada ya  kutikiswa bega kama alikuwa yupo  katika usingizi mzito.

"Ha..hapana  si....sikumbuki chochote" Shafii aliongea kwa kubabaika baada ya kuhisi moja ya jambo baya alilolifanya linakaribia kugundulika.

"Una uhakika?" Mzee Mahmud aliuliza.

"ndiyo baba zangu nina uhakika wa kile ninachokiongea" Shafii alijikaza akajibu kwa kujiamini.

"mzee mwenzangu sisi twende tukanywe kahawa si unaona muda huu na kiubaridi cha kipupwe kimeanza, Shafii kama hujui juu  ya hilo basi inakupasa utambue kuwa maisha ya mkeo  na binti yako yapo kwenye kinywa chako kueleza unachojua na ukikaa kimya jua kinachofuata ni kama kilichowapata wadogo zako ia utambue umebaki peke yako" Mzee  Mahmud huku akiwa tayari amesimama na Mzee Buruhan naye akasimama, wote kwa pamoja walianza kutembea kuelekea ulipo  mlango ili waondoke lakini sauti ya Shafii ikiwaita iliwafanya wasimame na kugeuka wakamtazama.

"Nipo tayari kuwaambia kilichotokea wazee wangu naomba mnisaidie" Shafii aliongea baada ya kuona maji yamemfika shingoni na maneno ya mzee Mahmud ndiyo kabisa yalimfanya akubali. Mzee Mahmud alimtazama Shafii kwa tabasamu hafifu halafu akamuambia, "kesho muda kama huu pale ulipokuwa unaishi kule mpirani ndiyo kutakupa ahueni ya  tatizo lakokwa familia yako"

Mzee Mahmud aliposema maneno hayo alitoka humo ndani bila hata kumuangalia Shafii kwa mara nyingine, Mzee Buruhan naye alifuata akiwa nyuma yake.

****

Maneno ya Ally baada tu ya kupewa mkono na Salma yalimfanya Salma karibia siku nzima akiwa anajifikiria kwani Ally alikuwa amepatwa na nini mpaka awe vile, ilipofika jioni aliamua kutoka na kwenda kumtafuta Ally bila ya kumueleza mtu ili aongee naye tu kwani Ally alikuwa ni mmoja kati ya wanaume aliokuwa anawapenda na kipindi cha nyuma alipokuwa msichana alishajaribu kujivika ujasiri na kumueleza Ally yaliyo moyoni mwake lakini aliishia kukataliwa baada ya Ally kuwa anamuheshimu sana Hamis ambaye alikuwa na mahusiano na Salma kabla hajamuoa.

Baada ya mpango ambao ndiyo chanzo cha balaa lote lililowakumba watoto wa  mzee Buruhan, Ally alifungwa akili na akawa anasikiliza wote waliofanya mpango ule bila hata kuwapinga na alifungwa akili baada ya kuujua mpango huo akawa  amekasirishwa nao. Baada ya kufungwa akili ndipo Salma alipompata Ally kutokana na yeye pia ni mmoja kati ya watu walioshiriki huo mpango, alimtumia Ally vyovyote atakavyo baada ya Ally kutopinga kauli yake. Sasa akili ya Ally ilipofunguliwa na Mzee Mahmud na Salma kujibiwa vile alijikuta roho ikimuuma akijua Ally amepatwa na tatizo hivyo  aliamua kumtafuta.  Hakukujua kama Ally wa leo siyo wa jana alichokuwa anakijali yeye ni penzi lake  haramu alilolianzisha kwa Ally hata alipokuwa yupo ndani ya ndoa.

Tamaa za kutamani kingine wakati akiwa tayari ana kingine mkononi ndiyo zilimfanya Salma afanye jambo hilo ambalo lilipelekea afiche siri nzito sana ambayo laiti ingaligundulika mapema basi angekuwa ameleta matatizo makubwa sana kwa Hamis na Ally.

Juhudi za Salma kumtafuta Ally ziliendelea kwa usiku huo akiwa yupo ndani ya gari yake na hatimaye alimkuta akiwa amekaa kwenye matairi yaliyochimbiwa katika uwanja wa mpira  uliopo mkabala na shule ya sekondari ya Usagara, Salma alimfuata hadi hapo akaegesha gari pembeni kisha akashuka akaenda kumkumbatia Ally akitegemea atapokelewa lakini alijikuta akisukumwa hadi akaanguka chini akaumia.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
58 Dhamana Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni